Fumanizi ni lazima, labda...

Fumanizi ni lazima, labda...

Sipo

JF-Expert Member
Joined
Jul 25, 2008
Posts
2,139
Reaction score
95
Wataalamu wa masuala ya mahusiano wanadai kuwa mtu anapotoka nje ya ndoa ni lazima atafumaniwa. Na kama hatafuniwa mwaka wa tatu tangu aanze uhusiano na huyo hawara yake basi kuanza basi lazima atafumaniwa kabla ya mwaka wa sita wa uhusiano huo haramu.

Sababu za lazima ufumaniwe ni hizi:-
  • Kujisahau na kuweka ngao ya kujikinga chini mfano badala ya kwenda mbali kufanya mapenzi basi watafanyia karibu,

  • Kumwambia rafiki wa karibu wa kufa na kuzikana akiamini taficha siri,


  • Dhana ya kumilikiana uanza kuingia kati ya hawa wawili na kuanza kuuona kila mmoja ni mali ya mwingine,

Unaweza kuamini kwamba wewe una maarifa sana na ni mjanja sana na una maarifa mengi ya kukanusha kuwa una nyumba ndogo na kuteleza husifumaniwe. Lakini kwasababu ni nguvu mbovu unazopanda ni lazima utazilipia kwani zitakurudia tu, utake husitake.

Unapotoka nje ya ndoa jiandae kunaswa siku isiyokuwa na jina. Kama utaacha kabla hujanaswa, siyo kwasababu ni mjanja, bali ni kwasababu hiyo nguvu uliyoipanda ilikuwa haijakamilisha mzunguko wake.

Unapoonywa na mpenzi/mke wako, au anapoonyesha wasiwasi kuwa unatoka nje, kama ni kweli inabidi uache. Kama utaendelea jua tu kwamba utapata shida, utaumia baadaye.

Nawasilisha
 
Wataalamu wa masuala ya mahusiano wanadai kuwa mtu anapotoka nje ya ndoa ni lazima atafumaniwa. Na kama hatafuniwa mwaka wa tatu tangu aanze uhusiano na huyo hawara yake basi kuanza basi lazima atafumaniwa kabla ya mwaka wa sita wa uhusiano huo haramu.

...te he heee 😀 hao wataalamu bana,.... watu mpaka wanasomesha sekondari fumanizi zero!
 
...te he heee 😀 hao wataalamu bana,.... watu mpaka wanasomesha sekondari fumanizi zero!

hiyo mpaka mtoto yuko sekondari ina mambo mawili:-
1. Ni mke mdogo ambaye hata mke mkubwa anafahamu
2. Ni mume alizaa nje ya ndoa kabla au baada ya ndoa lakini hakuna mhusiano tena baina ya wazazi wawili
 
Back
Top Bottom