Fundi Niyonzima sasa rasmi Simba SC, hongera mtani

Chirwa naye ameandika barua ya kuomba kuvunja mkataba, Ngoma haeleweki tangu katikati ya msimu, Tambwe eti naye anataka 80M ili asaini, daah hawa mapro hawana shukrani
Tuambatanishie Barua..

Maana mimi niko karibu na mlango wa jikoni. Kiingiacho & Kitokacho nakiona....
 
Yanga mwakani watashuka daraja
Tayari siasa za usajili wa timu yako zimeshabandiko ukoko kwenye macho na masikio yako....

Huoni wala husikii...

By the way! Washazoea kucheza psychology games na nyinyi mashabiki..

Nakuomba usisahau kwenda kumchagua tena Aveva...uchaguzi ujao.

Mkumbushe suala la Barua kwa FIFA, sijui ndege ya DHL imepotea njia...[emoji23]
 
Asante kwa huduma yako ya miaka sita Jangwani,kamalizie makombo kwa mnyama,ila tu wasije wakasema baadae kama bado una mapenzi na Yanga pindi pasi zako zikienda fyongo.
 
Yaan Simba mwaka huu ilichokifanya kama inachofanyavBayern Munich ligi ya Bundesliga nahisi ubingwa watachukua wakiwa na mechi 6 mkononi!!!!
 
Washamharibia bei itashuka maana hakuna competition tena
 
Sawa japo nimeumia ila hakuna namna ....kila la kheri uko aendako[emoji17] [emoji30] [emoji30] [emoji30] [emoji17] [emoji24] [emoji24] [emoji24] [emoji24]
 
Childish argument.
Unatumia Ku_comment kwa lugha ya kigeni ili point yako ionekane ni nzuri? Sasa wewe ungempa shilingi ngapi Niyonzima ili abaki Yanga? Tutajie thamani ya Niyonzima kwa sasa? Unajifanya mjuaji sanaaaa . Unavoaanza kukosoa uwe umeandaa jibu sahihi. Tutajie thamani ya Niyonzima .
# Msimu 2017/18 Yanga sc itashuka daraja au itapambana na kina Ndanda , Mbao.[emoji12]
 
ndani ya hiyo misitu 6 aliyo chezea Yanga, uongozi ulitaka kumuacha kama mara 2 hivi, mara ya mwisho ilibidi adi mwenyekiti aitwe 'ikulu' ya Rwanda kwenda ku-resolve issue za huyu dogo, leo hii amekuwa 'Precious' tuna mtakia kila raheli huko aendako, na huko ndiko 'kupiga hatua'
 
Vyura sc ngada sc aka kishika uchumba sc kama inauma chomoeni bas au mnaendekea kuikatikia
 
Eti nikutajie thamani... Kawaulize wakina Kaburu watakumbia...

Hiko kimombo ni cha kawaida xana...naona umepata shida kung'amua nilichosema.

Kuhusu kushuka daraja.

Najua umeanza shabikia simba miaka ya usoni.
Rekodi ninayoishikilia ya kutomaliza Ligi chini ya 2 hujawahi kuinawa hata chembe.
 
Hiyo ni ndoto mkuu,Yanga bingwa tena msimu ujao,Yanga inaendelea na usajili wake km kawaida ila ww endelea kusikiliza propaganda za viongozi wako
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…