fungua moyo!

Kuanzia siku ile sikupenda tena....na kila niliyemuona mbele yangu nilimuona kama mbwa, katili au kitu kisichokuwa na maana, baada ya so many sleepless night imagining how they are hanging out somewhere, wakipinduana hivi na vile....roho iliuma sana hasa pale nilipokumbuka zile siri zetu kwene mechi, iliniongezea uchungu wa hali ya juu na nikatamani niue au nijiue, nisimwone tena, kwa nini aniache? kwani nimemkosea nini? nimemnyima nini? mbona tulifanya hata yale ambayo jamii isingeyaruhusu, Mimi ndie niliyejua kupenda kuliko hata baba yangu alivyompenda mama yangu hadi kunizaa, maana hawakunizaa kwa bahati mbaya, kwanini alinifanyia vile? Nikatamani niende kwa kiongozi wangu wa kiroho nikatubu na kumrudia Muumba, mmmh eti sasa ndio nilikua naona kuwa nilichokuwa nakifanya ni makosa! Mapenzi jamani. Lakini nashangaa tu eti nimekupenda ghafla, nahitaji kuwa nawe, daima na milele nisahau maumivu yale, nimsahau kiumbe katili yule........Haya ni maneno ya Kiumbe fulani wakati wa MTONGOZANO. Haya niambie formula ya kupenda iko wapi hapa
 


Pretense if anything...
 
Usha anza utundu wako.... am telling you don't repeat... i repeat... Don't repeat...lol..
naona MTM alitakiwa anipe ushauri wa under the carpet before.. :A S 39:
Ahaaa ahaaa namuona Kaizer hapo kati
 
Elliiii!??? Pole mwali eeee ndio maisha yalivyo fungua moyo wako uwe happy tena
 
Mbu yuko wapi? au anafunga mwezi ofisini
 
Hii umenifanya nifikirie vitu vingi lakini hata hivyo ni maisha kila kitu kina sababu ila inauma sana
Nimeacha bwana siku hizi
:dance::dance:
 
Hapa MJ1 nadhani unaongelea gentlemen and gentle-ladies 🙂biggrin1🙂, Otherwise ukikutana na nyang'au kama mimi (joke) umeumia manake ni fix juu ya fix and by the time u realise I was lying it is too late.
 
Upendo una definition pana sana, Lakini huu unaozungumzwa hapa ni ule ule unaokata mioyo yetu. Inategemeana unampandaje MJI au TF ! Kama rafiki? au Mwenza? Na pia hata hao wapenzi wetu hatuwapendi katika kipimo sawa, Wengine wanachukua nusu ya mioyo yetu! wengine robo na wengine uchukua moyo wote. Na ndiyo maana wale wanaochukua moyo wote wakiumega tunaumia.Inachukua muda mrefu kuponya kitu kizima kuliko kuponya nusu au robo.
Katika mapenzi kila mtu anakujaza katika moyo wake hivyo inategemeana wewe au yeye amechukua sehemu gani ya moyo wako, aliyechukua sehemu kubwa huyo bila shaka amezidi.
 
Halafu huyu Mbu mchokozi sana sijui kaleta hii thread ili iweje, haya banaa Mbu:dance::dance::biggrin1::biggrin1:

ha ha ha,....pheeeeewwwww! nimesoma comments zenu nyoooote,....mnh!
Balaaa.,....!

The Finest. Unajua kwanini nimeileta hapa? Maneno Mkuki, aliyokuwa analalamika
huyu besti, ndio ulikuwa msimamo wangu.... moyo wangu ulikuwa umekufa ganzi
kabisa bana,...cha ajabu,...few weeks ago ametokea soulmate kayeyusha kila kitu...

Sasa hata sijielewi elewi kaja na anti-numb injection? ...akili yangu yote ni kwake/kapangisha kichwani mwangu bila kodi!
Mbaya zaidi, kila nikijaribu kupiga mabreki ninavyompenda...naona hazishiki...
Lyrics za 'Lets Wait A while!' hapo chini...ndio dua yangu..

Mbu yuko wapi? au anafunga mwezi ofisini

Gaga, Mbu is In-Love, breathing it, inhaling and exhaling love :mwaaah: 'in and out...'
 

Chimala na BelindaJacob naomba ni Quote posting zenu, kwani zimenigusa pale nilipoikuwa napataka.


Swali ambalo ningewauliza, au wachangiaji wengine nao wanaweza kuchangia ni;
  • Je, Ungependa mpenzi wako mpya afanye nini ili aweze kuziba pengo lililojitokeza?
  • Je, utakuwa tayari kumwambia the truth, nothing but the truth yote yaliyokukwaza kwenye relationship yako iliyopita ili mwenzio ajue wapi penye kovu, na wapi penye kidonda?
  • Je, Wewe mwenyewe (binafsi,) unachukua jitihada gani kuhakikisha unakubaliana na maisha na mapenzi mapya?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…