Zanzibar-ASP
JF-Expert Member
- Nov 28, 2013
- 11,550
- 40,697
Ni wazi kuwa Spika Ndugai imejiuzuru uspika wa bunge la Tanzania kwa shinikizo la chama chake cha CCM baada ya kutofautiana kimtazamo na Rais Samia Suluhu ambaye ndio mwenyekiti wa CCM taifa.
Upande wa pili pia, utendaji wa Ndugai akiwa spika wa bunge la Tanzania kwa sehemu kubwa ulikuwa umelenga kukibeba chama chake cha mapinduzi (CCM) kwa hila, hali na mali kwa sababu ya mashinikizo ya chama chake.
Yaani CCM ilimuweka Ndugai kuwa spika pale bungeni ili kuibeba serikali na CCM, na ghafla alipokuja na msimamo tofauti na serikali na CCM ikamshinikiza kuachia ngazi.
Kwa kuwa bunge ni mali ya wananchi, na spika wa bunge ni kiongozi wa chombo hicho kimamlaka, ni vyema na busara kuwa na sheria itakayohakikisha Spika wa bunge hakishinikizwi na mamlaka nyingine yoyote ya nje ya bunge katika utendaji wake wa kila siku ikiwemo chama cha siasa. Na njia rais, spika asiwe mwanachama chochote cha siasa.
Haya ya Ndugai yatuamshe sasa kuwaza mbali, maana yataendelea kujirudia tena na tena ikiwa tutaendelea na utaratibu huu wa sasa wa kuwa na spika anayetokana na chama cha siasa.
Katiba mpya ni jambo la lazima kwa sasa.
Upande wa pili pia, utendaji wa Ndugai akiwa spika wa bunge la Tanzania kwa sehemu kubwa ulikuwa umelenga kukibeba chama chake cha mapinduzi (CCM) kwa hila, hali na mali kwa sababu ya mashinikizo ya chama chake.
Yaani CCM ilimuweka Ndugai kuwa spika pale bungeni ili kuibeba serikali na CCM, na ghafla alipokuja na msimamo tofauti na serikali na CCM ikamshinikiza kuachia ngazi.
Kwa kuwa bunge ni mali ya wananchi, na spika wa bunge ni kiongozi wa chombo hicho kimamlaka, ni vyema na busara kuwa na sheria itakayohakikisha Spika wa bunge hakishinikizwi na mamlaka nyingine yoyote ya nje ya bunge katika utendaji wake wa kila siku ikiwemo chama cha siasa. Na njia rais, spika asiwe mwanachama chochote cha siasa.
Haya ya Ndugai yatuamshe sasa kuwaza mbali, maana yataendelea kujirudia tena na tena ikiwa tutaendelea na utaratibu huu wa sasa wa kuwa na spika anayetokana na chama cha siasa.
Katiba mpya ni jambo la lazima kwa sasa.