Furaha yatoweka CCM, ushindi kama msiba, wapinzani washangilia. Rais ageuka kauli zake za awali kanisani Dodoma

Furaha yatoweka CCM, ushindi kama msiba, wapinzani washangilia. Rais ageuka kauli zake za awali kanisani Dodoma

Siasa za bongo ukifuatilia sana unakuwa chizi na masikini.
Hivi jamani naomba msaada kuku wangu kroiler chotara wameanza kutoa kinyesi chenye damu.
Msaada nipo serious.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mmmmh....mbona hata mimi sina furaha wakati ni mwanaCCM tena hai?? Uchaguzi ulivurundwa na kufanywa wa kidhuluma ya kidemokrasia na ubabe wa kidola kupitia wizara husika. Waliopitishwa hata wao hawana ujasiri wa kujisifia au kifurahia kupachikwa kwao.
Mambo yakiwa hivi kwa 2020, haina haja ya kufanya uchaguzi wowote bali ufanyike uteuzi tu tuache demokrasia ya kimaigizo na machukizo.
Vijiji vyote vya huku kwetu watu wanadai eti uchaguzi bado haujafanyika, viongozi waliopo hawatambuliki, wanaogopa kuitisha mukutano na kwenye misiba hawatoi matangazo kwa kuogopa kuzomewa. Furaha imetoweka!!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom