Fursa haionekani kwa Macho bali kwa akili

Sijui watu huwa tunachukuliaje/fafanuaje tukisikia neno biashara/ujasiliamali!mleta mada sina nia kukupinga but hapa inabidi ujue jambo moja.

Hizo nyumba za kupanga siyo wote wanaoshinda majumbani,pia hata wale wanaobaki nyumbani ni kina mama na watoto ambapo hawa kile kiporo kilicholala jana ndo wataamkia kama kitafunwa cha chai huku wakiitafuta saa sita wale chakula shibe.

Ingekuwa rahisi hivyo kila mama mtaani angefanya hii kazi,20K siyo ndogo hii biashala ina changamoto zake.

Sent from my Redmi Note 5 using Tapatalk
 
Ivi wewe unawajua wabongo kwa kukopi na kupaste. Hiyo biashara utaifanya wiki 2 tu ikilipa wiki ya 3 mtajikuta mko 6 mtaani hapo ndipo utakapoanza kuuza maamdazi 10:kwa Siku.
 
Uswazi kaanga mihogo, weka kachumbali. Kipande 100, utapiga sana hela. Tegesha sehemu ya njiani inayopita watu wengi kwenda au kutoka kwenye shughuli mbalim ali.


2015 nilienda Mwanza, jamaa yangu alinipeleka sehemu inaitwa mabatini. Pembeni ya lile daraja la waenda kwa miguu kunajamaa anakaanga pumbu za mbuzi, ng'ombe na kondoo. Vile vidude ni vitamu sana aisee.

Nb: zingatia usafi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu wewe una tazama kwa Macho tatizo Lako fikiria boss upya

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sawa boss lakini uzi hatuzungumzii kutazama kwa Macho ni akili tu.. Neno akili Lina uwanja mpana Sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa upande mwingine wa shilingi hiyo survey yako haijakaa vyema,umesema ukipita kwenye nyumba ya kupanga hapo tayar ni uswahilini, na ki uhalisia ni nadra sana kwa mtu wa uswahilini kununua kitafuno kimoja kwa sh.500. Nawasilisha
 
Ni ubunifu tu kwa kutumia akili Mungu aliyokupa kama haijachakaliwa na binadanu . Mf. Mwalimu ukionekana unauza maandazi kwa wasioelewa watamcheka eti biashara uchwara ! Kwa mwenye busara atapiga mzigo bila kuangalia makunyanzi . Kwa mf . uliotoa wa maandazi kwa kuzingatia kauli nzuri na kanuni za biashara utamuacha mtu aliyeajiriwa mbali .

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni wazo zuri,kwa kupanga inawezekana ila ukiingia field ndio changamoto zinaonekana.leo utauza,kesho hautauza utayapeleka wapi?
 
Ishu hapo yanatoka maandazi mangapi kwa kilo moja ya ngano?,
kwa bei hiyo ya sh 100 ni wazi kuwa yatachangamkiwa sana tu na mji kama dar mfano sidhani kama nyumba hapo hazizidi 50,
lakini sasa unatoa mangapi katika kilo ili faida tuione?
 
Let say unatoa 20 kwa kilo,hapo utahitaji mfuko mmoja wa kg 25 kutengeza maandazi 500,
mfuko mmoja tsh 28000,
mafuta ya kukaangia hata uweke lita 5,hiyo ni tsh 15000,hapo tayari inahesabu 43,000,
ukiweka na mkaa wa 2000,tayari gharama ni 45,000,
unauza unapata 50,000,faida 5000,

hujaweka gharama za hamira,ha ha ha,na umetembea kinondoni nzima kwa miguu kwa faida chini ya 5000,
cost benefit analysis imegoma kutick hapa
 
Nimecheka kdogo....nyumba wapngaj 7 kila 1 akinunu a mandaz 5= 35 apo umeassume bt mambo hayapo hvyo.

Wapangaji WA uswaz huwajui mkuu labda hyo hesabu iwe ya mkopo,
 
Mh hesabu zako mkuu hakuna ambae angefanya hizo biashara

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Binafsi nilishafanya biasha kama hizo..cha msingi ni kutafta eneo lenye watu wengi.mm nilianzia mtaani nikajikuta nipo shuleni..nilikuwa natengeneza chapati 100,maandazi 200,sambusa 200,ndizi mzuzu 200,mihogo roba LA kg 50,na ndoo mbili za chips per day..nilitumia kachumbari za aina tofauti ,ukwaju na rosti la mifupa nililokuwa nanunua 2000 kwa kilo katika kunogeshea vitafunwa.
 
kutengeneza vitu tofauti tofauti kuna push sana biashara..ila changamoto yake in wasaidizi..na kitu kingine ni kusimamis recipe yako isiweze kubadilika
 
Biashara za whatssap groups huwa ni nyepesi njoo katika uhalisia ujionee tofauti
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…