Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mbegu ni ULE MCHE kama ulivyo kwenye mboga aina ya MATEMBELE. Kile ndiyo kinapandwa ardhini. Siyo jani!Mbegu sio jani, mbegu ni shina
Mbegu sio jani, mbegu ni shina
Sijaelewa unanielezea au kunisahihisha??Mbegu ni ULE MCHE kama ulivyo kwenye mboga aina ya MATEMBELE. Kile ndiyo kinapandwa ardhini. Siyo jani!
Vile viazi vya Songea si viazi lishe ni viazi tu vya kawaidaDemand take ni majanga bora mihogo,songea kule yangu miaka ya2000s vinalimwa tumekula sana tukiwa shule na njiani along songea njombe road wakulima walikuwa wanapanga magunia kutafuta Wateja kwa bei chee sijui kwa sasa
mkuu tunaomba kamrejesho kidogonimepanda hizi mbegu nasikilizia kama hisabati zako ni sahihi baada ya kuvuna
Mavuno hayakuwa mazuri, wataalaam wakaniambia nilichelewa kupanda na mvua za mwisho. Nimeandaa mbegu nitawahi mvua za awali mwaka huu.mkuu tunaomba kamrejesho kidogo
Mna mawakala mikoa mingine? Maana sisi huku huu ndo msimu wa mvua.KULA VIAZI LISHE, LIMA VIAZI LISHE
Mzigo huo. Hivi ndivyo viazi lishe vyenye matumizi kedekede katika mwili wa mwanaadamu. Unaweza kutumia viazi hivi katika utengenezaji wa cake, maandazi, ungalishe, ugali, biscut, crisps, ama kula vyenyewe kwa kuchomwa, kukaangwa au kuchemshwa.
Viazi lishe ni katika vyakula vyenye vitamin A kwa wingi. Vinawafaa sana akina mama wajawazito, wanaonyonyesha, watoto pamoja wazee.
Kazi kubwa ya vitamin A katika mwili wa Binaadamu ni pamoja na kusaidia katika utengenezaji na uimarishaji wa meno na mifupa. Pia husaidia katika uchocheaji wa uonaji wa macho hasa kwenye mwanga hafifu.
Vitamin A inasaidia vilevile kwenye ukuaji wa kitoto kichanga kiwapo tumboni mwa mama yake, inasaidia pia kwenye uumbikaji wa miguu na utengenezaji wa moyo, macho na masikio. Kwa hiyo ulaji wa viazi lishe una manufaa makubwa kwetu sote bila kujali umri. Viazi lishe ni katika vyakula bora sana.
Unga wa viazi lishe kwa siku za hivi karibuni umekuwa hitajio kubwa kwa akinamama wajawazito, watoto wanaonyonya na wezee wenye Kisukali. Lakini pia chanzo kikubwa cha kipato kwa wadau waliyojitumbukiza kwenye mnyororo mzima wa thamani wa kilimo hiki.
Kula viazi lishe, Lima viazi lishe, hii ndiyo kuuli mbiu yetu.
Ukitaka kula viazi lishe tuone tutakuuzia viazi hivyo na ukitaka kupanda viazi hivyo halikadhalika tutakuuzia mbegu za viazi hivyo zitakazokuwezesha kuwa mdau wa kilimo hicho. Na hii ndiyo kazi moja wapo ya Kinasoru East Africa Tanzania Ltd
Aman Ng'oma
0767989713
Dodoma
Aiseh calculator ni tamu sana kwakuiangalia ikiwa na mahesabu ya makisio matharani ma figure ya sufulisufuli yakigeuka kuwa reality basi unaweza ukaamka ukizani umekuwa tajiri kumbe ilikuwa ni makisio ya JF uliokuwa umeota ndotonimkuu tunaomba kamrejesho kidogo
Nilikuwa natoa msisitizo ZAIDI kwa ajili ya muuliza swali!Sijaelewa unanielezea au kunisahihisha??
Maana nami nilikua namsahihisha mtu nimeona wewe tena umeni quote
Poa poa MkuuNilikuwa natoa msisitizo ZAIDI kwa ajili ya muuliza swali!
Ninavyo hivi ,mbegu ilitoka Dar,pia niliona Nakumat wakiuza bidhaa zake,wengine huita viazi vya Msumbiji,tatizo ni kuwa wengi hawajui manufaa na utofauti wa viazi hivi na hivyo vingineViazi lishe ni aina ya viazi vitamu vyenye mwonekano wa rangi ya njano kwa ndani vikimenywa. Viazi lishe ni biashara mpya katika kilimo biashara ambacho hakijamulikwa vyema na wakulima wetu. Hii ni fursa muhimu na ya kipekee kwa wakulima wanaolenga utajiri kutokana na kilimo. Kwa kifupi huku kuna pesa kuliko kawaida. Ni muhimu tukaichangamkia fursa hii. Kilimo cha viazi lishe ni kama ilivyo kwa viazi vingine vitamu ni rahisi sana ukilinganisha na aina nyingine ya kilimo.
Viazi lishe hutumia muda wa miezi mitatu toka kupandwa hadi kuvunwa. Na kama vikilimwa kwa ajili ya mbegu, vyazi hivyo hutumia miezi miwili tu na vinakuwa tayari kuvunwa na kupelekwa shambani.
Viazi lishe vina beta karotini ambayo ni chanzo muhimu cha vitamini A. Viazi lishe vinatengeneza bidhaa mbalimbali zikiwemo Chipsi, Kripsi pamoja na Unga ambao hutumika kutengenezea bidhaa mbalimbali kama vile Mikate, Keki, Maandazi, chapati, Biskuti na vitafunwa vinginevyo. Kwa kifupi, kwa kutumia viazi lishe, tunaweza kutengeza bedhaa zote ambazo unga wa ngano unatengeneza. Majani ya viazi lishe hutumika kama mboga.
Ekari moja huitaji mbegu elfu 12 na kila mbegu moja tunaiuza kwa tsh 60/= kwa mteja anayechukua mbegu kuanzia elfu 12 na kuendelea lakini chini ya hapo mbegu moja inauzwa kwa tsh 100/=. Tunatoa huduma ya kukusafirisha hadi ulipo kwa kukupostia mzigo kwenye gari na huduma yetu ni bora sana .
Katika ekari moja una uwezo wa kuvuna tani 19 hadi 24 kutegemeana na matunzo yako. Kwa kawaida mbegu moja ya viazi lishe iliyopandwa inatoa kilo 2 za viazi. Kadiri unavyoweka matuta makubwa ndivyo unatakavyovuna viazi vikubwa zaidi. Upandaji wa viazi lishe kati ya shina moja na jingine ni futi moja moja na kati ya tuta moja na tuta jingine pia ni futi moja.
Viazi lishe ni vitamu sana. Vina unga wa kutosha na mwonekano wake huwavutia wateja wengi sokoni ukilininganisha na viazi vitamu vya kawaidi. Lakini vilevile viazi hivi vimepewa chapuo kubwa na wenzetu wataalam wa lishe kwa ajili kuboresha afya ya watoto, akina mama wajawazito pamoja na wazee.
Kilo moja ya viazi lishe inakwenda kwa tsh 1000/= sokoni. Na shina moja linatoa wastani wa kilo mbili na ekari moja ina mashina 12,000. Kwa haraka haraka ekari moja ikiwa utafuata na kuzingatia masharti yote muhimu utaweza kuvuna tani hadi 24. Sasa wewe rudisha nyuma hiyo hesabu, fanya utavuna tani 20 tu ambayo ni sawa na kilogramu 20,000. Je wajua kwa hiyo ekari moja utaweza kutengeneza tsh ngapi? Hapa utachukua 1000/= X 20,000KGS itakuwa sawasawa na tsh. 20 milioni. Hebu niambie kuna biashara gani unaweza kufanya kwa miezi michache tu ukaibuka na kiwango hicho cha pesa. Fursa ni nyingi mtaani tuzichangamkieni.
Hapo hatujaongealea biashara ya mbegu za viazi hivyo. Navyo ni hela pia. Ukiamua kuzalisha mbegu za viazi lishe kama nilivyosema hapo awali vyenyewe huchukua miezi miwili tu hadi kuvunwa. Katika ekari moja inatoa mbegu laki moja 1,046,000 na kila mbegu kwa mkulima shambani inanunuliwa kwa tsh 30/= na sokoni kwa wale wateja wakubwa kabisa wanaochukua kuanzia mbegu 360,000 zinauzwa kwa tsh 50/=. Sasa ukichukua mbegu 1,046,000 x 30/= mkulima ataweza kupata jumla ya tsh 31,380,000/= . Je kuna biashara yeyote unayoweza kufananisha na kilimo hiki cha uzalishaji wa mbegu na viazi vyake?
Ni muhimu kukumbuka viazi ni miongoni mwa mazao yanayostahimili sana ukame hivyo vinamuhakikishia mkulima chakula cha uhakika. Vilevile kilimo hiki cha viazi lishe, hakina usumbufu kama ilivyo kwa aina nyingine ya kilimo. Ukipitisha trakta likavuruga ardhi, ukapanda mbegu kitakachofuata ni palizi tu. Kwa baadhi ya maeneo huhitaji mbolea lakini kuna baadhi ya maeneo mengine kama vile Morogoro hayahitaji hata mbolea, ukivichomeka tu basi utasubiri palizi kisha kuvuna.
Viazi lishe hustawi katika maeneo mengi ya nchi yetu lakini hustawi zaidi katika maeneo ya joto kwa mfano maeneo yote ya mikoa ya Pwani na Morogoro, maeneo yote ya Kanda ya ziwa na mikoa ya magharibi kama vile Tabora na Kigoma, Mikoa ya Kanda ya kati Singida na Dodoma pamoja na mikoa ya nyanda za juu kusini hasa Ruvuma, Rukwa na Katavi. Kwahiyo wakulima waliyo kwenye maeneo hayo wana fursa zaidi ya kuendesha kilimo hiki cha viazi lishe pamoja na mbegu zake.
Hii ndiyo fursa niliyoona niwashirikishe siku ya leo.
Kwa mahitaji yako ya Viazi lishe au Mbegu zake tafadhali wasiliana nami
Aman Ng'oma
Mkurugenzi Mtendaji
Kinasoru East Africa Tanzania Ltd
0767989713/0786989713
amanngoma@gmail.com
Dodoma.
View attachment 486804 View attachment 486805 View attachment 486806 View attachment 486807 View attachment 486810 View attachment 486811