Fursa ya kuuza mahindi Congo

Fursa ya kuuza mahindi Congo

Ton 1 sawa na kg 1000.
Kwaivo ni sawa ton 1 kuwa usd 350: unajua ni sh ngapi hiyo in Tsh?
Songwe gunia la kg 100 sh 47,000×10 = 470,000 ton 1
So kwa usd 350×2300 sh ngapi?
Rekebisha hapo kwenye
Tani 1 ni USD 350
Nadhani ni
Kilogram 1 ni USD 350
 
Jamani hii fursa sana me napendekeza Michele ndio upatikanaji wake nimrahisi sana maana huku kwetu kwajumla kilo moja haizidi elfu elfu moja namia tano kwahiyo kama kuna mtu anajua jinsi yakuanza hii biashara atwambie jamani yaani unaanzaje mpaka kufika huko kongo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wadau, chekini taarifa ya fursa hiyo hapo chini kutoka TCCIA;

Ndugu Viongozi wa TCCIA,

Tunapenda kuwajulisha kuwa tumepokea barua kutoka Wizara ya Viwanda,Biashara na uwekezaji kwamba Ofisi ya RAS-Songwe kwa kushirikiana na TCCIA walifanyia kazi fursa ya kuuza mazao ya chakula huko DRC kwa upendeleo maalum na kufanikiwa.

Kufikia makubaliano na Uongozi wa Jimbo la Haut-Katanga umetoa Kibali cha miezi minne(4) kuanzia tarehe 1 Desemba,2018 hadi Machi31,2019 kwa wafanyabiashara wa Tanzania kuuza chakula katika jimbo hilo kwa kiwango chochote walichonacho pasipo kulipa ushuru.

Makubaliano hayo yameeleza kuwa,baada ya kipindi hicho hawataruhusiwa kuuza kwa utaratibu wa kawaida ikiwa ni pamoja na kulipa ushuru.

Hivyo kwa makubaliano hayo,Tani moja(1) ya mahindi itauzwa kwa USD350,Unga wa Mahindi USD 400,Maharage na Mchele USD1,120.Bei hizi ni pamoja na gharama za uchukuzi.

Hivyo wafanyabiashara wote mnashauriwa kutumia fursa hii.

Asanteni sana kwa ushirikiano.

For more enquiries

hq@tccia.com

TCCIA
Tatizo ni uvamizi wa vikundi vinavyopigana na serikali.
 
Bei zinakata sana mahindi kwa rate ya $1=2280tsh gunia la kg100 ni 80,000.
Unga kg 1= 912 tsh
Mchele na maharage kg 1=1430 tsh. Hapa bado hujaweka gharama za usafiri mpaka ufike huko

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Safi watafute soko Nchi zilizo na usalama pia huko vitani na biashara Mara sijui uchaguzi haueleweki unaweza ukakimbia mzigo wako ili kuokoa nafsi yako...
Siku zote kwenye maeneo hatarishi ndio kuna pesa, hujiulizi kwa nini biashara haramu ndio zenye utajiri.!
 
Siku zote kwenye maeneo hatarishi ndio kuna pesa, hujiulizi kwa nini biashara haramu ndio zenye utajiri.!
Mkuu nimeenda Angola enzi za Savimbi kupeleka jean Luanda niliuza 150 mpaka 200 kwa jean moja wakati Cape Town nilikua nachukua rand 200 mpaka 400 ilikua haifiki hata 30 USD wakati huo unatoka na Gari unaenda kuuza huko Risk yake ni kubwa sana baada ya kuuza ilibidi niache Toyota raider kwa alienipokea kisa wasijue kuwa naondoka na nilipita bara bara ya kuitafuta Zambia wakati wao wanajua ntarudi njia ya kuitafuta Windhoek nilifanikiwa kwa ile tripu ila Risk ni muhimu sana kuzingatia kuliko muda wote kuangalia mambo ya pesa tuu...
Johannesburg yenyewe tunayoishi ni hatari kama watu wako vitani muda wote ila kuna maeneo huwezi kwenda au kufanya biashara ingawaje ukiwa na biashara huko utauza...Waethiopia na Wasomari wanakufa sana kwa sababu wanafungua maduka sehemu hatarishi bila kuangalia Risk kwanza hapa Johannesburg...
 
Back
Top Bottom