Fursa ya kuwekeza kwa msingi mdogo

Wapiga Dili


Si tuhuma nzuri hizo.

Tunakukaribisha uje kujionea kazi zetu kwa macho yako na ufanye utafiti japo kidogo ili ujiridhishe kabla hujatuchafua na huku hautujui.

Njoo ujionee na unaweza kuwa mgeni wetu kujiridhisha na shughuli zetu ili uje kutusafisha hiyo tuhuma nzito ulioturushia ambayo nafikiri uliitoa bila ya kufikiri.
 
Zainab Tamim vipi maendeleo ya biashara/mradi ..ulipata watu wa kutosha?

Nashukuru, tumepata watu wa kutosha kwa phase 1, kazi inaendelea na hivi karibuni tunaanza phase nyingine nategemea leo baadae kuwaletea mpango mwingine wa kuwekeza kwa atakae jaaliwa.
 
Nashukuru, tumepata watu wa kutosha kwa phase 1, kazi inaendelea na hivi karibuni tunaanza phase nyingine nategemea leo baadae kuwaletea mpango mwingine wa kuwekeza kwa atakae jaaliwa.
Asante. Tunasubiri huo mpango mwingine.
 
Hawa matapeli tuu kama mnatoa hiyo riba si wekezeni wenyewe mpaka mchangiwe? Eti tunataka watu 20 wa Kwanza biashara eti zipo kwa nn msifanye wenyewe. Hatutaki matapeli humu, riba watoe benki na nyie mtoe! Acheni UJUHA wenu ndani ya JF
 
Hawa matapeli tuu kama mnatoa hiyo riba si wekezeni wenyewe mpaka mchangiwe? Eti tunataka watu 20 wa Kwanza biashara eti zipo kwa nn msifanye wenyewe. Hatutaki matapeli humu, riba watoe benki na nyie mtoe! Acheni UJUHA wenu ndani ya JF

Walikutapeli nini? Walikwambia wanatowa riba?

Sema roho inakuuma huna ubunifu alionao Bi Zainab na mumewe.

Sisi tumewekeza na AlhamduliLlah, mambo safi kabisa, twala faida kwa sasa.

Kati ya watu nnaowaheshimu ni Bi Zainab na mumewe. Hawana longo longo za kijinga kabisa, si juu hapo wanawakaribisha watu wakajionee wenyewe shughuli zinazofanyika, ulikwenda kwao ukajionea?

Bi Zainab yupo JF tena verified user kwa takriban miaka miwili sasa na anaweka nyuzi mara kwa mara humu za ujasiriamali, hatujasikia hata mmoja aliye deal nao akilalamika kwa chochote.

Watu kama wewe ndiyo mahasidi na wachawi na chuki tu za kijinga.

Kama haujuwi maana ya uwekezaji kaa kimya.

Punguani wahed.
 
Walikutapeli nini? Walikwambia wanatowa riba?

Sema roho inakuuma huna ubunifu alionao Bi Zainab na mumewe.

Sisi tumewekeza na AlhamduliLlah, mambo safi kabisa, twala faida kwa sasa.
Haya usisahau kutujuza hali ya matanga tuje tuanue vilago
 
Kumbe na wewe ni dalali kwa hawa matapeli, dunia ishajua

Walikutapeli nini? Hasidi mkubwa.

Mimi licha ya udalali ni muwekezaji kwao na ni silent partner.

Ukiwa unadhani unawaharibia basi umechelewa jamvini, karamu imeshaliwa. Watu wameitikia mwito, wakawekeza na sasa wanakula faida tu, AlhamduliLlah mimi mmojawapo.

Umemsoma Bi Zainab juu hapo, anasema anakuja na phase II, subiri ailete uwahi kuponda.

Hasbunna Llahu wa Neema L'wakil.
 
Hawa matapeli tuu kama mnatoa hiyo riba si wekezeni wenyewe mpaka mchangiwe? Eti tunataka watu 20 wa Kwanza biashara eti zipo kwa nn msifanye wenyewe. Hatutaki matapeli humu, riba watoe benki na nyie mtoe! Acheni UJUHA wenu ndani ya JF


Kwanza ninashukuru sana Mwenyezi Mungu kwa kukuwezesha wewe kuja kifua mbele na kuturushia tuhuma nzito ya utapeli.

Napenda kukutoa hofu kuwa sisi si matapeli ma kama kuna chochote tulichokutapeli au kuna yeyote unaemjua kuwa tumemtapeli utueleze.

Sisi ni binadamu na kaa binadamu mwengine yeyote yule, hatujakamilika, labda katika kazi zetu kuna ambayo tuliifanya na wewe na haukuridhika ukafikia tamati ya kutushutumu kuwa ni matapeli?

Kazi zetu zote kuanzia ile ya udongo, hadi leo hii ya kuwekeza tunaziwekea Guarantee ya money back au hii ya kuwekeza tunaweka guarantee ya investment yako na faida tuliyoitangaza kwa muda tuliouweka, utaipata iwe au isiwe mradi umeingiza faida au la. Tumesema juu huko, assets zetu nje ya huu mradi zunatuwezesha ku guarantee kiasi tutachokubaliana kuwekeza na sisi. Kama ni uwekezaji mkubwa na hatuwezi ku u gurantee basi hatupokei.

Ndugu yangu ninakuomba sana tena kama kuna sehemu unafahamu au unahisi tumekutapeli wasiliana na sisi aidha kwa njia hii ya wazi kama ulivyorusha tuhuma au kwa njia za kisheria ili usiendelee kutupakaza mavi ambayo hayatuhusu.

Utapeli ni jinai na polisi zipo wazi saa 24, kama tumekutapeli wewe au mwengine yeyote kwanini usitushitaki?
 


Cool down, please.
 
Kumbe na wewe ni dalali kwa hawa matapeli, dunia ishajua


Ndugu yangu bado unaendelea tu kutuita matapeli? Tumekutapeli nini?

Sisi tumeweka ID zetu wazi, namba zetu za simu wazi, anuani ya kwetu ipo wazi, kuna wana JF wengi sana wameshafika kwangu na wananijua, kama unasema kweli tunaomba jiweke na wewe wazi utueleze tumekutapeli nini?

Pia tungependa sana tuwasiliane na wewe ili tuyatatue haya ya kutuita matapeli kisheria.
 
Asante. Tunasubiri huo mpango mwingine.


Mpango mwingine ni very simple isipokuwa uwekezaji wake ni mkubwa kidogo. Huu unaanzia millioni tano na unapanda kwa millioni tano tano, yaani unaweza kuwekeza millioni tano au kumi au kumi na tano au ishirini.

Kwa sasa tunahitaji wawekezaji au muwekezaji wa millioni 30 kama ni mmoja tu, au kama ni 6 kila mmoja atatoa millioni 5 (tumeshapata wawili wa millioni 5 kila mmoja kwa hiyo tuna nafasi ya millioni 20 tu kwa sasa).

Tunawekeza kwenye mgodi wa michanga ya kujengea ambayo ipo kihalali kabisa. Tuna guarantee faida ya 50% kwa miezi mitatu mpaka sita tu.

Maana yake, itakapotimia miezi 6 tunahakikisha kuwa kiasi ulichowekeza na faida ya 50% ipo kwako tayari. Na mambo yakienda vizuri basi ndani ya miezi mitatu itakuwa tumeshamaliza phase hii.

Kulipwa ni kila wiki mpaka uwekezaji wako na faida ziwe zimesharudi.


Msingi ulikuwa unatakiwa wa millioni 30 lakini tayari tumeshapata millioni 10 za kuwekeza. Kazi hii tunatarajia itaanza mwanzo wa mwezi March.

Karibu sana.
 
Naomba kujua progress ya miradi hii.


Mradi wetu wa awali unaenda vizuri sana, tunashukuru.

Tulikamilisha kupata wawekezaji tuliotarajia na sasa wanarudisha pesa zao.

Unakaribishwa kujionea mwenyewe shughuli zetu.

Hivi karibuni tunaanza phase mpya ya uewekezaji mweingine, nimeuelezea kwenye posti namba 115, tafadhali ipitie.

Kaaribu sana.
 
km ikaja kutokea risk yoyote mtaturudishia pesa yetu 500,000 tutakayotoa? au itakuwa imekwenda hiyo?

je mmejiandaaje na wimbi la vibaka watakaowapora hizo pesa pindi wakijua mnapopwekeza ?


Ndiyo. Uwekezaji wetu kwako unakuwa "risk free", risk tunazibeba sisi kwani tunatumia pesa zako na za wengine kuwekeza kwenye miradi tofauti tofauti ili kupunguza risks.

Mara nyingi huwa hatubebi cash. Tunatumia sana mitandao ya simu kulipana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…