Zainab Tamim
JF-Expert Member
- Jan 15, 2015
- 1,293
- 583
- Thread starter
-
- #141
Katika jambo jema na lenye tija vikwazo na mapingamizi hayakosekani. Kama anashindwa kuthibitisha utapeli wenu asiwasumbue sana kujibishana nae, mwenye kutaka kuwekeza atawatafuta tu, msipoteze muda na nguvu kujibishana nao.
Hasbunna Llahu wa Neema L'wakil. (FaizaFoxy )
Nimefurahishwa sana na wazo lenu na jinsi unavyojibu maswali kwa ufasaha, hiyo peke yake imanifanya nianze kuwaamini kabla hata ya kuwatembelea miradi yenu. Naomba kuuliza, mmefanya insurance yoyote kwa asset zenu ili hata kama inatokea chochote mali zenu na wawekezaji wenu wasipate hasara?
Muundo/Mfumo wa kampuni ukoje, ni formal organization au ni biashara ya familia tu? Nauliza hivyo sio kwa lengo baya, ni kujua sustainability ya kampuni, ikitokea wewe haupo kwa sababu moja ama nyingine, uhakika wa wawekezaji kupata pesa zao. Nafikiri utanielewa na natanguliza shukrani zangu.
Mungu awabariki
Zainab Tamim , Mungu awabariki sana, kikubwa zaidi nimependa jinsi mnavyojibu hoja na maswali yanayoulizwa.
Binafsi nimeridhika, kama ulivyosema hayo mengine tunamwachia Mungu, kikubwa ni kuomba uzima na baraka zake atujalie heri.
Kingine, natamani watu wangejaribu kujifunza kwenu namna ya kuangalia fursa na kujiongezea kipato huku mkisaidia wengine kama mnavyofanya ninyi. Niseme kwli mko vizuri kwenye kubuni miradi na kufikiria mawaz ya biashara.
Mungu akinijalia ntakuwa miongoni mwa washiriki wa awamu ya pili, natamani sana nikamilishe mipango yangu kabla ya mwezi wa tatu na endapo bado nafasi zitakuwepo, Inshallah.
Kudos Bi Zainab Tamim, keep it up.
In sha Allah nafasi zitakuwepo na fursa hazitakwisha, Muhimu ni nia safi.
Karibu sana kwetu ujionee.
Naomba mniwie radhi kwa maswali mengi, nafasi za awamu ya pili bado zipo? Kama zipo, bado kiasi gani kufikia 30M? Nakumbuka 10M ilishapatikana kama sikosei. Itanisadia kufanya maamuzi.
Biashara ya pesa ogopa sana, ina maneno matamu, utajiri unakuja mpaka usoni daaah..!
Na hata ukipigwa uhamini kama umepigwa kwa jinsi walivyo kunyenyekea na maneno matamu.
Ukiliangalia jina mume wangu, ushirikina upo, maneno matamu yapo na kudanganywa uku unaona kupo, kama vile mume kwa mke wake.
Ukienda kwenye hii biashara lazima ukawe mke, na mke lazima azae kwa maumivu.
Tafakali chukua hatua upo tayari kuzaa kwa maumivu?
Pesa pesa ogopa naneno yanayo husu pesa maana ni matamu na mwisho ni uchungu.
Biashara ya pesa ogopa sana, ina maneno matamu, utajiri unakuja mpaka usoni daaah..!
Na hata ukipigwa uhamini kama umepigwa kwa jinsi walivyo kunyenyekea na maneno matamu.
Ukiliangalia jina mume wangu, ushirikina upo, maneno matamu yapo na kudanganywa uku unaona kupo, kama vile mume kwa mke wake.
Ukienda kwenye hii biashara lazima ukawe mke, na mke lazima azae kwa maumivu.
Tafakali chukua hatua upo tayari kuzaa kwa maumivu?
Pesa pesa ogopa naneno yanayo husu pesa maana ni matamu na mwisho ni uchungu.
Ndugu yangu tunakuomba ututembelee kabla hujaanza kutupakazia.
Hii ni fursa tunayoitengeneza kwa wenye mitaji midogo, tunatamani sana ungetuunga mkono na si kutupakazia.
Sisis hatuamini kabisa katika ushirikina na ushirikina hauna nafasi katika uwekezaji wetu.
Tunakuomba sana tena sana ututembelee ili ujionee mwenyewe uwekezaji wetu na baada ya hapo upo huru kuandika chochote kuhusu sisi.
Mikataba ikiwepo ni rahisi,kwa sababu hata Contractors wa barabara huwa wanafanya hivyo kwenye tenda za barabarani.duh cjui nijitose