Fursa ya kuwekeza kwa msingi mdogo



Ma sha Allah.

Sitaki kusema mengi kwa kuwa mimi pia ni muwekezaji wa awamu ya kwanza ya pili na ya tatu.

Ahsanteni sana Abdul na Zainab. Tunafurahi sana kwa kuwa fedha zetu tumewekeza mahali salama.

Count me in katika hiyo phase ya tatu b.

Mwenyeezi Mungu atuzidishie kila la kheri.
 
Nataka nije kuwatembelea site, nimepiga hiyo namba hapo haipatikani. Naomba unipe maelezo ili niweze kufika kwenye mradi wenu.

Asante.
 
Jaman acheni Roho Mbaya me naomba niwe mkweli na Mungu asimame kama shahidi katika haya kiukwel me Bi Zainab sijawahi kumuona face2face wala Mumewe mimi Niko Mwanza wao wapo Dar nimefanya nao business nyingi na hawajawai nitapel so sio kila mtu ni tapel jaman hawa ni watu wenye hofu ya Mungu kama kwel wahitaji kuwekeza fanyen nao kaz u won't regret
 
Nataka nije kuwatembelea site, nimepiga hiyo namba hapo haipatikani. Naomba unipe maelezo ili niweze kufika kwenye mradi wenu.

Asante.


Samahani sana, labda ni mtandao tu maana huku site kuna sehemu mtandao unakosekana.

Karibu sana, ukija njoo, Misugusugu shule, ukifika hapo chukuwa bodaboda yoyote atakuleta mpaka kwetu mwambie tu kwa Mzee Abdul Ghafur. Ukifika kwetu tutakupeleka site zetu ujionee mwenyewe.

Tutafurahi sana ukitutembelea. Ukiikosa namba 0625249605 jaribu 0656399856.
 


Asante sana kwa maneno mema.

Mwanza watu wanaulizia sana udongo, hatuna siku hizi mtu wa kuuza huko. Unaweza kututafutia?
 
Mimi niko jijini Mwanza, nawezaje kuingia kwenye huo uwekezaji?
 
Mimi niko jijini Mwanza, nawezaje kuingia kwenye huo uwekezaji?


Ni rahisi sana, unatutumia pesa zako unazotaka kuwekeza au tunakupa account namba unaziiingiza kwenye account yetu na inakuwa umeshawekeza.

Kwa upande wetu tunaanza kazi kwa tarehe kama tulizoziweka huko juu na kama kuna madiliko tunakujulisha, baada ya hapo tunakupa updates za mara kwa mara na tuna guarantee kuwa utapata 50% ya pesa ulizowekeza ndani ya miezi mitatu mpaka sita. Na huenda ikawa kabla ya hapo. Tunasema miezi mitatu mpaka sita ili tu kujiweka kwenye "safe side".

Mara tunapoanza mradi tunakutumia pesa kila wiki mpaka tunapohakikisha unapata kama tulivyoahidiana.
 
Leo tuna furaha kuwajulisha kuwa tumeanza test production ya phase 3 A.

Phase 3B tunatarajia itaanza April au May kutegemea na mwenendo wa mvua.

Abdul
 
Unajua kuhusu pato langu au wazungumza tu.

Ndugu yangu, ningependa uweke mbali au ufungue Uzi mwingine kuhusu wazo lako zuri. Aina ya biashara na uendeshaji wake iko tofauti sana na hii inayoongelewa hapa.

Hii itaepusha kuchanganya majibu na michango kuhusu hizo topic mbili tofauti.

Shukrani
 
Hivi inapoonza awamu ya pili na tatu na ikiwezekana nne awamu ya kwanza inakua inaendelea au inakuaje?


Inakuwa inaendelea.

Awamu ya kwanza ilikuwa ni uwekezaji wa 500,000 kwa wiki 52. Unaendelea kwa wale waliokwisha wekeza.

Tumeombwa na wengi tuanze tena ule uwekezaji mdogo, kuna watu wametutumia pesa zao, tunatarajia tutauanza tena mwezi huu wa nne. Tutawajulisha.
 
mnamali/asset zisizo hamishika?
mkipata hasara/any risk usalama wa pesa utakuwepo?
na je mkishindwa kunilipa naweza kuchukua asset mlizo nazo kufidia?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…