Fursa ya mboga mboga na matunda Dodoma

Fursa ya mboga mboga na matunda Dodoma

mwagito25

JF-Expert Member
Joined
Aug 11, 2013
Posts
633
Reaction score
352
Habarini wana jamvi.

Kutokana na kukua kwa kasi ya kuridhisha kwa jiji la Dodoma, kuna mahitaji yanayoongezeka kutokana na umuhimu wake kwa maisha ya binadamu ya kila siku.

Uhitaji wa mboga mboga na matunda unakua kwa kasi kubwa.

Uhitaji huu ni wa wote, yaani wauzaji na wazalishaji.

Kwa wale waliopo au watakaopata mazingira mazuri kwa mjini katikati hii ni biashara nzuri saana endapo huduma yako itakuwa ina ubora mkubwa, yaani mboga zako ziwe katika ubora wa kumvutia mlaji. Mfano kuna sehemu kama majengo sokoni kando ya njia akina mama wanauza mchicha, figili na mnafu ambao hata kama hukuwa na wazo la kununua utanunua.

Upande wa mkulima, nimeona pale magereza (isanga) wanajitahidi kuzalisha mboga nzuri inayopendwa na walaji kwa kuzingitia viwango hasa matumizi ya samadi kwa wingi kuliko mbolea za dukani. Pamoja na jitihada zao lakini hawakidhi mahitaji hata kwa mbali, ukizingatia pamoja na wimbi la wakazi lakini pia uwepo wa wanafunzi wa vyuo mbalimbali nao ni chachu katika hili.

Maoni yangu ni kwamba kwa mtu ambaye anaweza kutatumia maeneo yenye maji ya kutosha yaliyopo karibu na Dodoma mjini mfano Hombolo kutokana na uwepo wa bwawa hii yaweza kuwa fursa nzuri katika kujipatia chochote kitu.

Kila la kheri kwa wapambanaji.

1624959179369.png

 
Habarini wana jamvi.

Kutokana na kukua kwa kasi ya kuridhisha kwa jiji la Dodoma, kuna mahitaji yanayoongezeka kutokana na umuhimu wake kwa maisha ya binadamu ya kila siku.

Uhitaji wa mboga mboga na matunda unakua kwa kasi kubwa.

Uhitaji huu ni wa wote, yaani wauzaji na wazalishaji.

Kwa wale waliopo au watakaopata mazingira mazuri kwa mjini katikati hii ni biashara nzuri saana endapo huduma yako itakuwa ina ubora mkubwa, yaani mboga zako ziwe katika ubora wa kumvutia mlaji. Mfano kuna sehemu kama majengo sokoni kando ya njia akina mama wanauza mchicha, figili na mnafu ambao hata kama hukuwa na wazo la kununua utanunua.

Upande wa mkulima, nimeona pale magereza (isanga) wanajitahidi kuzalisha mboga nzuri inayopendwa na walaji kwa kuzingitia viwango hasa matumizi ya samadi kwa wingi kuliko mbolea za dukani. Pamoja na jitihada zao lakini hawakidhi mahitaji hata kwa mbali, ukizingatia pamoja na wimbi la wakazi lakini pia uwepo wa wanafunzi wa vyuo mbalimbali nao ni chachu katika hili.

Maoni yangu ni kwamba kwa mtu ambaye anaweza kutatumia maeneo yenye maji ya kutosha yaliyopo karibu na Dodoma mjini mfano Hombolo kutokana na uwepo wa bwawa hii yaweza kuwa fursa nzuri katika kujipatia chochote kitu.

Kila la kheri kwa wapambanaji.
Yaani dodoma naitamani sana kwa kuuza mboga mboga, ningekua naweza safirisha hadi dom tokea iringa ningepeleka
 
Mbona Iringa dodoma ni karibu kabisa
Kama unasafirisha kutoka Iringa, ili uwe na tija lazima uwe na stock ya kutosha. kwenye uchumi tunaita economies of scale. Pia, uwe na soko la uhakika ili mzigo usikudodee. Utaumia mwanzoni lakini baadaye utakaa sawa.
 
Kama unasafirisha kutoka Iringa, ili uwe na tija lazima uwe na stock ya kutosha. kwenye uchumi tunaita economies of scale. Pia, uwe na soko la uhakika ili mzigo usikudodee. Utaumia mwanzoni lakini baadaye utakaa sawa.
Maana nina mboga nyingi sanaaaa na za aina takribani zote, ningempata mwenyeji wa dodoma tufanye bihashara
 
Upo Iringa sehemu gani ndugu?njoo PM tujadili hilo,nina gari Toyota Noah hapa Dodoma halina kazi limepark tu,pengine linaweza kufanya kazi hiyo ya kubeba kutoka Iringa kuleta Dodoma
 
Upo Iringa sehemu gani ndugu?njoo PM tujadili hilo,nina gari Toyota Noah hapa Dodoma halina kazi limepark tu,pengine linaweza kufanya kazi hiyo ya kubeba kutoka Iringa kuleta Dodoma
Weka picha nilinunue nije kusombea Mpunga huku Meatu Simiyu
 
Back
Top Bottom