Mkuu...Mkuu naskia gemstones huko zinauzika vizuri,kuna wa thai huwa nawauzia nkiwabana wanipe soko la huko hawataki,wananunua mzigo mkubwa huku inamana kwao soko ni kubwa.
Ntawezaje kupata link za soko la tanzanite huko ili niwe napeleka mwenyewe
Mkuu...
Kuhusu gemstone sikufanya tafiti na mimi sasa hivi sipo huko, labda kama utaweza kwenda ni vyema poteza hela kidogo uende ukaangalie soko. Kama utashindwa mimi ntakuwepo huko mwezi wa kumi mwishoni hivyo nitajaribu kukuangalizia then ntakupa mrejesho. Aksante sana na ubarikiwe
Visa mkuu unaipata nairobi, 8000Kshs..(100USD), single entry. tickets ukibook mapema ni around 1200USD return ticket. kwa msaada zaidi nicheki mkuu kama nafahamu ntakusaidia. Thanks againNaweza kwenda mwez huo ila viza ni wapi nagonga,wathai wananunua sana tanzanite huko so kwao kuna soko,thx kwa info
Kama ukifika nairobi city centre chukua matatu inayoeleke NGONG halafu shukia YAYA, toka yaya mpaka embassy ya Thai sio mbali unatembea kwa miguu ni mtaa karibu na embassy ya South africa. Wanapokea Kshs, hivyo change kabisa au ukifika YAYA kuna sehemu za kubadilishia hela. Kihalali visa inachukua siku tatu kuprocess ila ukiongea nao unapeleka leo kesho unachukua. (kama unaenda kwa ndege, ukifika airpot ya Jomo kenyata chukua matatu mpaka city centre sababu Tax wanagonga sana ). Hope hapo hutasumbukaNaweza kwenda mwez huo ila viza ni wapi nagonga,wathai wananunua sana tanzanite huko so kwao kuna soko,thx kwa info
kaka msumeno please naomba utumbukize hiyo link tena ya DRC maana nimesearch na kusearchua sijaiona....
Hilo ndo tatizo la watanzania wako ki negative... ohhhh usalama ooohhhh ubaguzi.... nitafikia wapi ,,, sina ndugu kule..... unataka uwe na ndugu thailand?? umeshaambiwa hoteli sh 21000 ndo ndugu yako huyo...... kuna wakati niliwahi post fursa za biashara DRC du maswali ya kitoto ndo niliyapata.... oohhhh tufanyie mpango kabisa wa soko na pale boarder tumwge mzigo.. yaani watz wanataka umpe deal umpokee na soko umtafutie ,,, na baadae aje akunage kwamba mlikula ugali kila siku.... wakeup guys
huko si ndiyo wanaangalia value for money , mama wa feki ndiyo yupo hukoMkuu vipi kuhusu electronics kama Camera, LED tv , printers na vifaa vya studio vina unafuu?
Visa haina complication, ila Tanzania hakuna balozi ipo Nairobi. Mnaweza mkajipanga mkamtuma mmoja akaenda nairobi kuwagongea. Visa ni kama dola mia kwa single entry. Ticket sina hakika tokea dsm sababu mimi sitokei Tanzania(sianzii safari Tanzania) ila kama ukibook mapema means miezi hii itakugharimu USD 1,200 return ticket. (kwa ndege kama Kenya air ways, Ethiopia naTurkish air). Jipangeni wakuu
Mkuu nimeandika return ticket, means kwenda na kurudi kama unavyoita two way. Ila ukichelewa kubook usitegemee hiyo price. aksanteKaka hio USD 1200 ni kne way ticket au go and return?!
hhaha Mtalii wa MAMBO YETU, haw ahata bongo si wapo.viburudisho navyo vipo cheap tujuze mkuu
Ingefaa kwa sasa kufikiria zaidi pia upatikanaji wa zana za kuanzishia viwanda badala ya hizi biashara za kununua na kuuza tu. Tujaribu zana za processing ndizo zilizofikisha wenzetu kuwa na viwanda vingienvyo tubaendelea kuwa dampo la ejected.
Smile Money Stunna anakaa USA, labda tufuate ratiba yake; lkn kwa maelekezo nafikiri twaweza kwenda tu. Mimi nataka kuivaa hii fursa 100%. Twende pm kwa mipango zaidi, maana safari ya wawili si sawa na mmoja.
za leo wandugu..nimekua nikifatilia huu mjadala wa thai kwa kweli nimeona umekaa poa sana.ila sasa mbona hatupati mrejesho na cc tukiendelea kujipanga
Mkuu sisi bado tunajipanga, tutakwenda November. Sijui kwa walioenda huko.
C.C. Kaunga, ladyfurahia, amu na wengineo
Na mimi ntakuwepo huko kuanzia tarehe 25/10 kwa week mbili. Mungu akijaalia tutakutana huko. Kila la kheri na maandalizi mema.KWELI TUNAJIPANGA ILA BADO HATUJAJUA MAMBO MENGI HIVYO KUNA MDAU DIKEmba YEYE ANAJUA VIZURI CAUSE YEYE ALIKWENDA KULE NA OCTOBER ATAKWENDA PIA LABDA YEYE ATUPE MAMBO YALIYOKO KULE TUJUE TUSIKURUPUKE