Nikiwa kama mmoja ya watz walioishi miaka mingi katika hii nchi nawezakusema yafuatayo:-
1. China ina viwanda vya kila aina(state owned, watu binafsi na wageni)
2. Viwanda hivi ni vipo vinavyotoa bidhaa za ukweli na copy.
3. Viwanda vimejaa hadi kwenye majumba ya watu hasa nje ya miji mikubwa.
4. Kwa wale wenye mitaji mikubwa USD 100,000 na zaidi nawashauri wanunue mashine za bei nafuu then waanzishe viwanda vidogo vidogo katika mikoa ya Tanzania na si kutazama Dar pekee yake. Viwanda hivi vitasaidia kukua kwa soko la ajira na hata uchumi wetu kwa ujumla.
5. Wale wanaotaka kuanzisha viwanda msiogope, chukueni mashine ndogo ndogo tuu, zinauzwa kuanzia USD5000 na kuendelea hapa uchina. Kwa kufanya hivyo tutapunguza kuwa wategemezi wa ku import kila kitu kutoka nchi za watu. Yes, nimekutana na wafanyabiashara wa kitanzania wana hela nyingi balaa lakini wananua tshirt, jinsi na viatu kutoka china badala ya kununua mashine au kuingia ubia na viwanda vinavyozalisha bidhaa hizo hapa china. Wapo ambao wanaingiza hadi toothpick wakati mbao zimejaa africa.
6. China ime over produce, hawana soko la bidhaa zao, incase africa ikagoma kuchukua bidhaa za china basi mchina lazima achanganyikiwe. Tusisahau kwamba hawa watu wako 1.3 billion, 0.5 billion ya hii population inafanya kazi ile mbaya, kila leo wanatoa kitu kipya.
7. wale wenye mitaji midogo endeleeeni kuchukua mizigo yenu kama kawaida kutoka uchina na kwingineko ili retail market ya hapo tz isikose bidhaa muhimu. Pia nawashauri ninyi wenye mitaji midogo, mpange sehemu kubwa then mfanye biashara kama kikundi. mnawezachukua jengo kubwa somewhere,in tz, mkawagawana space kila mmoja akawa anaweka bidhaa zake hapo. mnaweka sheria zenu zitakazolinda ubora wa bidhaa zenu ili mjenge imani kwa wananchi ambao ndio wateja wenu. huku china wanafanya sana hizi biashara za makundi. kama kikundi, mnaweza weka service za ku deliver mizigo kwa wateja, service za matangazo, mnasfairisha makontena yenu kwa umoja kwa msimu mtakaojiwekea wenyewe. Pia kama kikundi mtapata fursa ya kupewa msamaha wa kodi kwa asilimia fulani na serikali kwakuwa mpo kwaajili ya nchi yenu. watz wengi hampendi kuungana, hapa mjini wengine hawataki hata kusalimia wakishajua wewe ni mtz, huu ni ugonjwa mbaya sana, lazima upewe tiba mapema.
Ndugu zangu, hakuna muda au kipindi ambacho tz kama nchi inawezakujenga uchumi mzuri hasa wa viwanda kama huu. Siku uchina wakifunga access kwenye products zao za ndani, tutakuwa tumechelewa sana.
Nasisitiza tena, nunueni mashine ndogo ndogo toka uchina, then anzishe viwanda, hatua za mwanzo ni ngumu lakini ipo siku mtatambua umuhimu wa kufanya hivyo.
Ndugu zangu, jiulizeni, ngozi ya ng'ombe ipo tz, mtz analeta china anauza kwa shidaaaa hiyo ngozi, mchina ana process ngozi hiyo then inatumika kutengeneza kiatu, sofa na viti vya magari. Mtz huyo huyo anakuja tena uchina kubeba kiatu , sofa na viti vilivyotengenezwa na ngozi yake mwenyewe, tena anauziwa kwa gharama kubwa ajabu.
Jee inaingia akili hii process. Kwanini tusinunue mashine za kutosha, tukaprocess hiyo ngozi wenyewe then wao wachina wakaja africa kubeba kwenda kwao kutengeneza viatu? Kwani kipi kigumu hapa ndugu zangu? Tena tungekuwa na jeuri, na tungeweka mkataba kabisa kwamba ukichukua ngozi yetu, bidhaa unayotoa isizidi gharama X kwa kila Y inch za ngozi unazotumia, Yeah, ni swala la kukubaliana tuu. Hapa tunge serve kiasi kikubwa cha fedha, na taifa lingekuwa na ajira nzuri tuu.
Ndugu zangu, furnture karibu zote zinatoka uchina. mbao za mchina ni dhaifu kuliko zote duniani nawezasema. Hivi kweli tumeshindwa kuanisha viwanda vidogo vidogo vya ku process mbao na kumuuzia mchina processed mbao kama anavyofanya m marekani na brasil? ni kweli tumeshindwa kuingiza mashine nzuri za furniture zilizopo hapa uchina, then tukawapa vijana wetu wafyatue furnture za nguvu?
Ndugu zangu, serikali haiwezileta maendeleo kama wananchi hatujaamua kubadilisha maisha yetu na uchumi wetu wenyewe. Hivyo basi kila mmoja wetu kwa uwezo na nafasi yake achukue hatua.
Muda umenitupa, nitatafuta siku nyingine niandike kwa ufasaha zaidi ili tuweze shiriki pamoja katika mijadala ambayo ina lengo la kututoa kiuchumi kama Taifa.
Nawakilisha