Fursa za kibiashara zilizopo Comoro

BABA TUPAC

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2015
Posts
1,527
Reaction score
3,811
Habari zenu wakuu,

Mara kadhaa nimekuwa nikisikia sikia kuwa Comoro kuna fursa nyingi za kibiashara lakini sijafahamu hasa ni fursa zipi zilizopo. Kwa wale watafutaji wanaozunguka sehemu mbalimbali, ningependa kufahamu fursa za kibiashara zilizopo Comoro.

Natanguliza shukrani
Cc: Zanzibar Spices
 
Ni kweli kuna fursa nyingi shida ni usafiriiii ni majahazi au anga
 
Kule ni kisiwani hivyo kunafikika kwa njia mbili tu bahari na anga basi , na si unazijua changamoto za baharini?
Tufafanulie changamoto za usafirishaji bahalini kupinduka,muda mwingi mzigo kuwa bahalini ,kupolwa na wahalamia au?
 
Yani acha tu thread kama hii watu tunakaa kuona majibu ya watu lakini holaa..ingekua thread ya ngono hapa reply zingekua zimetapika humu
 
Yani acha thread kama watu tunakaa kuona majibu ya watu lakini holaa..ingekua thread ya ngono hapa reply zingekua zimetapika humu
Hii inaonesha kuwa watz wengi tunatumia nguvu kubwa katika masuala ya ngono kuliko masuala mengine muhimu kama haya.

Ndio maana hata asilimia kubwa ya sanaa zetu zinabeba dhamira ya mapenzi tu.
 
Hii inaonesha kuwa watz wengi tunatumia nguvu kubwa katika masuala ya ngono kuliko masuala mengine muhimu kama haya.

Ndio maana hata asilimia kubwa ya sanaa zetu zinabeba dhamira ya mapenzi tu.
Kweli kabisa yani inasikitisha
 
jamani wengi tunataka kuwenda huko visiwa vya comoro vipi changmoto zipi zitatupata
 
Nazi
Nguo
Vitu vya umeme
Nyama ya ng'ombe na mbuzi
Changamoto ni jinsi ya kufika huko! Usafiri rahisi kibiashara ni kwa njia ya bahari
Hivi hua kuna umbali gani kutoka hapa kwetu?ila mtu mmoja afisa mifugo aliwahi kuniambia kua mbuzi wa kule ni dili sana.ni wakubwa na wanauzwa kwa mpunga mrefu
 
Hivi hua kuna umbali gani kutoka hapa kwetu?ila mtu mmoja afisa mifugo aliwahi kuniambia kua mbuzi wa kule ni dili sana.ni wakubwa na wanauzwa kwa mpunga mrefu
Hakuna umbali wa kutisha changamoto ni usafiri
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…