Karibu katika ujasiliamali....sasa hiyo launch pad yenu pale jahazi itakuwaje katika kupromoti mamaa?
11.30.2010
CAPTAIN GARDNER G HABASH..........AMETANGAZA RASMI KUACHA KAZI RADIO CLOUDS NA KUANZA SAFARI MPYA YA UJASIRIAMALI
Baada ya muda wa takribani miaka 9 kuifanyia kazi Redio Clouds, Katika vipindi mbali mbali kikiwemo maarufu cha JAHAZI, sasa ameamua kuangalia maisha upande wa pili wa sarafu.
Tunakukaribisha ulimwengu wa kujiajiri. na tutakufanyia bonge la Party kwa uamuzi huo mgumu na mzuri ambao watu wengi wanaogopa kujaribu.
GARDNER G HABASH a.k.a Captain ametangaza rasmi kuacha kazi ya utangazaji Clouds FM
Na kuamua kuwa mjasiriamali wa kujiajiri mwenyewe
Posted by Jide at
7:56 AM
34 comments:
Anonymous said... Hongera Captain karibu kwenye ujasiriamali.
November 30, 2010 2:17 PM
Candy1 said... Surely going to miss him and his amazing voice I guess sometimes in life you just have to make the next step. Congratulations
🙂
November 30, 2010 5:32 PM
Jide's secret admirer said... This is the most brave movement. Congrats to Gadna and you too Jide kwa ushauri mzuri. Maisha ni popote
November 30, 2010 6:11 PM
Anonymous said... Mmhh Clouds vp tena? ila haina ukweli wowote hii statement,yenye ukweli ni ya Sophia kessy.
November 30, 2010 7:44 PM
Mama 2 said... Hongera Captaaaaiin! lakini wapenzi wa JAHAZI tutakumisijeeeee! kile kicheko chako ukiwa na Mtarajiwa Meya Kibonde wa mwaka 2015.
November 30, 2010 9:39 PM
sophia said... Hongera sana Captain kwakweli umeonyesha ujasiri mkubwa mmno kwa maamuzi ulioamua, Mie nina imani utaweza kwani umeoa mke mwenye uwezo mkubwa wa kuhangaikia pesa , kwahiyo safari yako mmpya ya ujasiriamali ikuwa salama na yenye amani na mafanyikio kila la kheri Inshaalah!
November 30, 2010 9:55 PM
Anonymous said... Hongera sana!! Ila naomba kuuliza hii inahusian na November noma?? Sasa ni serious au ndio mambo ya ubunifu wa Clouds halafu anarudi?? ni kweli sielewi naomba kueleweshwa.
November 30, 2010 10:05 PM
Anonymous said... U know Captain to be honest many of us we are going to mic u big as u know ur the captain of Jahazi show but all in all u did a gret decision and its a step of going further in life.
November 30, 2010 10:18 PM
Anonymous said... am some how happy for him,ila moyoni naumia.
yani jahazi ndo kushneiii...
anyways,all the best Gardner.May God be with you.
November 30, 2010 10:25 PM
Anonymous said... am some how happy for him,ila moyoni naumia.
yani jahazi ndo kushneiii...
anyways,all the best Gardner.May God be with you.
November 30, 2010 10:28 PM
bigtom said... hongera sana gardner.. kwa uamuzi mzito,mgumu ila wenye busara na hekima nyingi.. tunakukaribisha sana kwenye ujasiliamali.. ila cha msingi cha kuzingatia nikuongeza nguvu,uwezo kiutendaji kazi kwa sifa ya kutukuka na mungu atakuwezesha kwenye malengo yako yote..wahenga walisema kila jambo lina mwanzo!!!
November 30, 2010 10:39 PM
Rachel Temu said... KkakA karibu saana kwenye ujasiriamali
November 30, 2010 10:58 PM
rida said... du mkumbe kweli? mbona sitaki kuamini? nimesikia ila nilijua ni mambo ya utani wao. ok inabidi tukubali matokeo na pia hongera kwa mwanzo mpya wa maisha ya ujasiriamali!!!!!!!!
rida
November 30, 2010 11:07 PM
Anonymous said... jiondoke bwana kwanza radio yenyewe imejaa majungu fitina nakutakia kila lakheli katika maisha yako
November 30, 2010 11:09 PM
Mama B said... hongera kaka,
Uamuzi wa kuacha kazi yenye guarantee remunaration ni mgumu sana, na ninatumai utakuwa umechagua business idea itakayokutoa na umeshafanya research ya market na potential customers wako. mimi ninakuombea kwa Mungu akuonyooshee na utafanikiwa. Jide and Gardner ongezeni ubunifu na mtakuwa among Tycoon in tanzania. big up
Mama B
November 30, 2010 11:35 PM
Anonymous said... Utachekwaje mjini hapa? ndio huyo jd wako alivyokudanganya? angalia sasa atakavyopotezwa hewani maana wewe tu ndio uliebakia unambeba beba
November 30, 2010 11:42 PM
Anonymous said... Nasuburi kwa hamu kuona hiyo Restaurant ya haja mtakayofungua. Jina la restaurant mlishapata!!??
Otherwise, I am so happy for you. Umeitumikia Clouds vya kutosha, umewaingizia pesa vya kutosha, its time for you to make your own money.
Kudoz brother.
December 1, 2010 12:19 AM
Anonymous said... nyie hamjui kuwa ni uwongo huo<hii ni katika kuliendeleza gurugumu la clouds,huo ni msemo tuu
December 1, 2010 12:19 AM
Anonymous said... Nitakumiss Gardener, ila hongera sana ni uamuzi mgumu sana wengi tumeajiriwa tunaogopa kuanza kutoka na kujiajiri tunaogopa kuanguka tunawaza mshahara tu, ni mfano wa kuigwa, hongera sana Jide, kweli jide komando (hongereni wote kila la kheri mungu awazidishie zaidi kwani na nyie mnagawa mnachopatiwa na mungu) ina nasikitika Jahazi oh my God tume mtu mwingine like Gardener
December 1, 2010 12:39 AM
Anonymous said... Na dada JIDE Mazee alikuwa nakupa shavu sana pale clauds, sasa ni aje, au ndo mzimu wa MR TOO umeanza kuinuka.
December 1, 2010 1:21 AM
Bazizane said... Wazeee wetu walisema kidole kimoja .... sasa itakuwa nguvu mbili! MWENYEZI MUNGU AKUPE NGUVU NA UJASIRI ZAIDI. Hongera sana kaka, hiyo ni moja ya hatua kubwa katika maisha. SELF CONFIDENCE!
December 1, 2010 2:22 AM
Shy-Rose Bhanji said... uamuzi mzito sana huu lakini ni uamuzi wa kishupavu...hapa gadna ametoa bonge moja la somo ...ni mfano wa kuigwa kwa kweli!
December 1, 2010 3:33 AM
kai rooney said... Kweli kabisa kuna wakati inabidi kuangalia upande wa pili wa sarafu. kila la kheri captain
December 1, 2010 3:42 AM
Anonymous said... Duu!ebwanaeee mchizi umeamua kutoka solo sio!kweli mwanangu mwenyewe njaa unaiweza,umeona pale mjengoni unauweka sio..safi kaka,ila kaza buti uraiani kama una roho ndogo utajikuta unashika bunduki,kwakua nina kakipaji ka kutunga nyimbo japo sikatumii nimekutungia wimbo wenye maneno yafuatayo:
"mwenda kwao si mtoro kariiibu,karibu ndugu yetueeee..hapa ni nyumbani kwako tunakukaribisha soote kariiiibu"karibu sana kaka uraiani
December 1, 2010 3:42 AM
Sab said... Waau ni Huzuni lakini hapo hapo ni furaha sana kaka kila la kheri kwenye maisha mapya.na Hongera kwa utumishi wako clouds miaka 9 sio mchezo wao wenyewe watakukumbuka
December 1, 2010 3:46 AM
Anonymous said... kweli fani ya radio inaenda pabaya... watangazaj kama gardner si rahisi kuwapata hata kama watapatikana wenye degrees za utangazaji nk, kipaji na sauti ya gardner ni ingredients tofauti na adimu kuzipata katika radios.... majuzi kipaji na sauti nyingine adimu imezimika magic fm kutoka katika kipindi chao murua cha morning magic, sasa hivi jahazi hali ni hiyo hiyo japo gardner bado anaishi... ila ni pigo kwa radio zote mbili! wasikilizaji wa vipindi vya asubuhi na jioni kweli pigo limepatikana, hatujapona na pigo la morning magic (magic fm) sasa tunapata la jahazi (clouds fm) ..... kazi ipo!
ILA GADNER ULICHOFANYA SI KOSA KAKA ADICTION YETU ISIWE KIFUNGO CHAKO CLOUDS, KIUKWELI TUTAKUKOSA SANA HASA KILE KICHEKO CHAKO CHA BADO TUPOOOOO....KABAAAA!
December 1, 2010 3:49 AM
Anonymous said... KARIBU BWANA GARDNER,WENZIO MASUDI NA FINA WASHAZOEA MAISHA YA ULIMWENGU MWINGINE WA NJE YA CLOUDS,NA WAMESIMAMA KIVYAO SO HAKUNA CHA KUHOFIA,KWANI WAO WAMEWEZA WANA NINI NA WEWE UNA NINI MPAKA USHINDWE?JUDY WAMBURA PIA ALIWEZA KUTOKA CLOUDS LEO ANAMILIKI BENDI.SEMA WE KIJANA NAKUMBUKA ULIPOKUA UNAJIUNGA NA CLOUDS KINA MAREHEMU AMINA WANAKUKARIBISHA BAMBATAA...UNAANZA KUTANGAZA WANAKUTANIA BAADAE UKAJA KUWE BONGE LA MTANGAZAJI
December 1, 2010 3:51 AM
Anonymous said... No way! he can't be going, hii ni ubunifu wa clouds ya novemba nomer, let wait and see!
December 1, 2010 4:06 AM
MloMmoja said... Shy-Rose Bhanji bana, somo limetolewa vp wkt hatujui nini anaenda fanya na kama atafanikiwa au la?
Upande wangu mie naona nimpongeze tu, siwezi sema ni maamuzi magumu wala shupavu ila wadau tunapenda kupamba ata majengo ya kale. Kwa hapa mjini jamaa ata akifulia hawezi kosa mzigo, jiulizeni vituo vya redio na tv ni vngapi Bongo hii?Mbona Fina na Kipanya walimwaga lkn leo hii wapo njema tena sana.
Kiongozi najua umeneja wa Machozi Band unaleta tumaini la mafanikio ya maziwa na asali kwahy lazima izo nguzo uzitie zege, wana tupo pamoja kwenye kuchangiana chochote kitu na kwa pamoja tutashinda.
December 1, 2010 4:19 AM
GK said... Jamani Jahazi,aya lkn ndio maisha tena.Tunakutakia mafanikio mema kaka
December 1, 2010 4:31 AM
MwanaharakatiMpiganaji said... Clouds ilipoanzishwa ilikuwa na watangazaji/dj wanamziki kama Jide,Ray C,OJ,Ml Chris,Kibacha na wengineo. Uongozi ulipotoa tamko kwamba anaetaka kufanya kazi kama mtangazaji/dj afanye na anaetaka mziki aachie ngazi. Jide na Ray C waliachia ngazi, japo siwezi jua ndo ulikuwa mwanzo wa Smooth Vibe chini ya Ruge, huu ndo naweza kuita umamuzi mgumu coz kipindi icho Jide na Ray na bongoflava kwa ujumla ilikuwa ni burudani zaidi kuliko unavyolipa sana.
Maamuzi magumu ni yale yakina Fred Mpendazoe kuachia jimbo,posho na haki zake na kwenda kuendeleza vita vya ufisadi. Maamuzi magumu na ya kishujaa ni kama ya kina Sugu kuingia ndani ya siasa,Felix Mkosamali 24, mwanafunzi wa sheria pale SAUT Mwanza kugombea ubunge wa jimbo la Muhambwe na kushinda kwa kishindo.Heri kufa ukiacha fikra zilizo hai kuliko kubaki hai bila bila mchango wowote kwa jamii yako....kama una wengine ongezea hapo
December 1, 2010 5:02 AM
Anonymous said... safi sanaa. mi nimeipenda zaidi hii taiming - unachukua kabisa mshahara harafu mwanzo wa mwezi unatimuka! just kidding - congrats Gadna. Hii ndivyo inavyotakiwa you go for better pasture at the same time you create opening for new generation. Our politicians need to consult you for such wiosdom.
December 1, 2010 6:00 AM
Anonymous said... Seriously Gadna, mi najua ni ubunifu wa Clouds katika novemba noma. Unatangaza kipindi jioni, you have plenty of time to do any ujasiriamali you want to do.
Please dont go please......!
December 1, 2010 7:25 AM
Kemmy said... mi nimehuzunika sana...bt i wish him ol the best ktk ujasiriamali.
December 1, 2010 10:28 AM
Post a Comment