Gairo: DC amtuhumu mwenyekiti wa CCM kuhongwa gari na mbunge Shabiby, mwenyewe akana asema amenunuliwa na Dkt. Mwigulu. Kesi iko Takukuru

Gairo: DC amtuhumu mwenyekiti wa CCM kuhongwa gari na mbunge Shabiby, mwenyewe akana asema amenunuliwa na Dkt. Mwigulu. Kesi iko Takukuru

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Mkuu wa wilaya ya Gairo amemtuhumu mwenyekiti wa CCM wa wilaya kwamba amehongwa gari na mbunge Ahmed Shabiby ili wambebe kwenye uchaguzi. Mkuu wa wilaya amewataka Takukuru wamshughulikie mwenyekiti huyo.

Naye mwenyekiti wa CCM amesema gari hilo hajahongwa na Shabiby kama inavyodaiwa bali amenunuliwa na waziri wa Katiba na sheria Dr Mwigullu Nchemba. Mwenyekiti amesema yeye pia ni msaidizi wa Dkt. Mwigulu jimboni Iramba akisimamia mahusiano ya mbunge na Waislamu hivyo amenunuliwa gari hiyo kama kitendea kazi.

Kuhusu kuchunguzwa mwenyekiti amesema ni kweli aliitwa Takukuru wilayani na wakamwambia tuhuma hizo ni za kisiasa hivyo jalada limepelekwa Dodoma ambako alihojiwa Ijumaa iliyopita na sasa anasubiri majibu.

Mwisho mwenyekiti amebainisha kuwa mkuu wa wilaya ni mtu mkorofi na kwamba anataka kugombea ubunge wa jimbo hilo na kila wakati amekuwa anawatisha kwamba yeye ana ulinzi wa kigogo aliye juu.

Chanzo: Clouds 360

Maendeleo hayana vyama!
 
Amenunuliwa yeye kama yeye ? au nafasi/cheo/ anachokitumikia ?
 
... kwa tuhuma hizo yeye DC, Shabiby, Mwigulu, na huyo Mwenyeki wa CCM (W) wanatakiwa "kuchinjiwa" mbali kabisa huko wafutwe kabisa uanachama. Akisimamia "mahusiano na waislamu"! Kuna cheo cha aina hiyo siku hizi hadi kununuliwa gari la kutekeleza jukumu hilo?
 
ccm ccm eeeeh, chama chama fisadi ccm namba wani...na shetwani anajua ccm mafisadi [emoji23]
 
Mkuu wa wilaya ya Gairo amemtuhumu mwenyekiti wa CCM wa wilaya kwamba amehongwa gari na mbunge Ahmed Shabiby ili wambebe kwenye uchaguzi. Mkuu wa wilaya amewataka Takukuru wamshughulikie mwenyekiti huyo.

Naye mwenyekiti wa CCM amesema gari hilo hajahongwa na Shabiby kama inavyodaiwa bali amenunuliwa na waziri wa Katiba na sheria Dr Mwigullu Nchemba. Mwenyekiti amesema yeye pia ni msaidizi wa Dkt. Mwigulu jimboni Iramba akisimamia mahusiano ya mbunge na Waislamu hivyo amenunuliwa gari hiyo kama kitendea kazi.

Kuhusu kuchunguzwa mwenyekiti amesema ni kweli aliitwa Takukuru wilayani na wakamwambia tuhuma hizo ni za kisiasa hivyo jalada limepelekwa Dodoma ambako alihojiwa Ijumaa iliyopita na sasa anasubiri majibu.

Mwisho mwenyekiti amebainisha kuwa mkuu wa wilaya ni mtu mkorofi na kwamba anataka kugombea ubunge wa jimbo hilo na kila wakati amekuwa anawatisha kwamba yeye ana ulinzi wa kigogo aliye juu.

Chanzo: Clouds 360

Maendeleo hayana vyama!
Hayo ndiyo marurupu ya viongozi wote wa Ccm.
 
Back
Top Bottom