Gamboshi

Weka stori yako katika uzi mmoja na si kila kipande unakianzishia uzi.
Je, unapata shida yoyote kwenye utafutaji wa episode za story hii,? Ningependa kukujulisha kuwa story hii itapatikana kila siku kwenye jukwaa kuu la "entertainment" kama unapata changamoto kwenye utafutaji wa episode nijulishe kwa msaada zaidi
 


>>>>>>>EPISODE : 05<<<<<<<<<
JINA LA STORY: GAMBOSHI
(Malkia wa wachawi)
MTUNZI: MOSSES AGREY
SEASON : 01
EPISODE: 05
Whatsapp
call/Text: +255687409189
(Audio version ya story coming soon)

ILIPOISHIA,,,,,,,,,
kwa ujasiri wa kiaskari, aliusogelea ule mwili na kuugeuza kwa mguu na aliuona mwili wa dereva taxi Hamisi ukiwa mkono mmoja umeshikilia Irizi kubwa iliyokatika kutoka kiunoni, na mkono mwingine akiwa ameshika noti zake mbili za elfu kumikumi zikiwa zimejaa damu. Akiwa anaendelea kuupekua pekua mwili ule, ghafla alisikia "pah - pah - pah - pah" milio ya risasi ikitokea katikati ya pori lile kwenye giza totoro.
Inspecta Dotto alisimama na kushikilia bunduki yake kwa ujasiri, lakini kabla hajapiga hatua, lahaulaa!!!, Dereva taxi Hamisi alikurupuka na kumdaka mguu,
"WACHAWI, kimbi.... Ki-ki-mbia...kim..." Ni maneno aliyotoa dereva taxi Hamisi kabla ya kuanguka chini na kukata roho palepale.
******

SEHEMU YA 05

SASA ENDELEA,,,,,,
Nyangeta alizinduka huku bado akisikia maumivu kisogoni mwake huku akiwa hajui kilichomtokea,
alifumbua macho na alijikuta amekaa chini huku akiwa ameegamizwa kwenye ule mti mkubwa, kwa pembeni umbali kama wa mita nne na nusu aliiona bastola yake ikiwa imeanguka na pembeni ya ile bunduki aliwaona watu wawili mvulana na msichana wakiwa wanajadili jambo fulani. Kwa mbali kidogo upande wa kulia kwake alikaa fisi mkubwa aliyekua anaangalia pembeni. kwa akili ya haraka
Nyangeta aliendelea kujifanya amezimia huku akipiga hesabu za kuipata bastola yake bila wale watu kutambua.
"Nilikwambia usipende kupiga watu vichwani, umeona sasa umemuua tutamueleza nini Mama?!?" aliongea yule msichana aliyekua pembeni
"Aaaagh... Mbona nimemgusa kidogo tu, tatizo hawa makabeth ni walaini sana" alijielezea yule mvulana huku akitumia mikono kuonyesha ishara kwa maelezo aliyoyatoa.
" ameamkaaa...!" Ilisikika sauti ya binti mdogo wa umri kati ya miaka 12 mpaka 14 aliyekua amemuinamia Nyangeta, wote pamoja na yule fisi waligeuka na kumsogelea Nyangeta
" we Minza unauhakika ameamka?" Aliuliza yule msichana mkubwa ambaye alionekana ndio kiongozi wao.

"Ndio nimemuona amefumbua macho akawa anaangalia kile kitu chake kilichopiga kelele muda ule, "alijibu yule msichana mdogo huku akionyeshea kidole ile bastola ya Nyangeta, yule mvulana aliifuata ile bunduki na kuiokota nyuma mbele, mbele nyuma huku akionekana fika kuwa hafahamu ni kitu gani, wakati hawajatahamaki, Nyangeta aliamka kwa judo kutokana na mafunzo ya ukomando aliyopewa kutoka jeshini huwezi amini ndani ya sekunde tu, na kumpora ile bunduki yule kijana, alibiringita kininja na kuwageukia huku akiwanyooshea bastola kwa ustadi mkubwa,
"Tulieni hivyohivyo," alisema nyangeta huku akihema kwa kasi,
"Samahani sitochukua tena" aliongea yule kijana huku akionekana kuswa na simanzi na kujutia kushika bunduki ya Nyangeta
"Samahani Nyangeta, hatochukua tena hiyo kitu yako" aliongea yule msichana mkubwa kwa upole huku akimsogelea Nyangeta,
"Simama hapohapo usipige hata hatua moja," aliongea Nyangeta kwa ukali, huku akijiuliza kichwani kwake mbona watu wale wanaonekana hawafahamu maana ya bunduki, na wala hawaiogopi!!!??
" mikono juu, ...wote!" Aliongezea Nyangeta huku akiwa anawaonyesha kwa ishara na kuikamatilia bunduki yake sawa sawa.
wote watatu walinyoosha mikono juu huku yule fisi akiwa anaangalia pembeni, yule msichana akamwambia yule fisi,
"Mbiti..!!! Hujasikia au kiburi?!?" Yule msichana mkubwa alimuuliza yule fisi kwa ukali, yule fisi alimgeukia nyangeta na ghafla alikaa na kunyoosha mikono yake juu, basi yule binti alimgeukia Nyangeta na kutabasamu,

Nyangeta alikuwa kama anaota na hakuamini alichokiona, alijikaza huku akishikilia bastola yake sawasawa akiwa amewalenga wale watu wa ajabu ambao hakuwaelewa.
" haya sema umejuaje jina langu na nyie ni wakina nani?!?"
"Jina lako tunalifahamu muda mrefu, na kuhusu sisi ni wakina nani hilo itabidi tukuelezee tukifika maana hapa muda umeisha, ila kwa ufupi sisi ndio tuliokutumia ule ujumbe" alijibu yule msichana huku akiangalia huku na kule,
"Mikono inauma dah, mwambie tushushe" aliongea yule binti mdogo,
"Shhhhhh" yule msichana mkubwa alimnyamazisha mwenzie.,
" uamuzi ni wako Nyangeta ukitaka kujua ukweli unaweza kwenda na sisi ila unatakiwa ufanye maamuzi haraka maana dawa aliyoweka minza imekaribia kuishiwa nguvu na Makabedon wakitukuta hapa hatutoweza kukulinda." Aliongezea yule msichana huku akimuangalia usoni Nyangeta
"Makabedon ndio wakina nani?" aliuliza Nyangeta
"Naomba uniamini usiombe watukute hapa maana itabidi utoe ile silaha uliyosema mwanzo na uwapige nayo la sivyo watatumaliza wote" alijibu Yule msichana huku akiendelea kumkodolea macho Nyangeta.

Nyangeta alifikiria kwa sekunde kadhaa huku akiiangalia bunduki yake akaamua kuishusha chini, lakini kabla hajaifikisha chini aliinyoosha tena kuelekea kwenye ule mti ambako kulikuwepo na yule mtu mwenye macho mekundu yanayowaka huku akiwa na yeye amenyoosha mikono juu,
" na yule ni nani?" Aliuliza Nyangeta huku akiogopa na kujikaza kisabuni
" aagh yule ni Kangina, kaka yetu" alijibu yule msichana huku akitabasamu,

Nyangeta alishusha bunduki yake na kuiweka kiunoni kimachale machale huku akiwatazama kwa umakini watu wale waliomstaajabisha, japo alikua na hamu ya kutaka kujua ni kitu gani kinaendelea ili kumamilisha upelelezi wa ajali za ajabu ajabu, zinazotokea gamboshi, hivyo aliamua kujifanya anakubaliana nao kwa maana wahenga walisema, 'mtaka cha uvungu...'.

"Shusheni mikono" aliongea Nyangeta kwa upole, na wote walishusha kwa pamoja
"Aaah afadhali" aliongea yule binti mdogo ambaye alionekana kuchoka kwa kunyoosha mikono juu,
" kabla hatuja fanya chochote, ni kwa nini mlinitumia ujumbe wenye kutisha, na isitoshe kwa nini hamkuja hotelini na kuniita, tena pale kuna sehemu nzuri ya kuongelea? na hao wanaotaka kuniua ni wakina nani?" aliuliza nyangeta huku akiwasogelea,
"Nyangeta, tunajua unamaswali mengi, ila nakuahidi utapata majibu yake, hapa sio mahala pa kuongelea" alijibu yule msichana huku akimtazama usoni nyangeta na yule fisi alianza kumsogelea Nyangeta.,

"haya twendeni, ila mkijaribu kufanya jambo lolote baya, nawaahidi, mimi ni askari polisi, na kitakachowakuta mtajuta kuzaliwa na pia naomba huyu fisi asinisogelee"Aliongea Nyangeta kwa msisitizo ,huku kauoga kakiwa kamemuingia kwa maana sio kawaida kwa binadamu kukaa na wanyama mwitu kama wale kwa ukaribu.
Yule msichana mkubwa alitikisa kichwa ishara kukubali maneno aliyoongea Nyangeta na kisha alimuangalia yule mvulana mkubwa na kumpa ishara fulani huku akimgeukia yule Fisi na kumpa ishara ya kumkataza, ili waondoke eneo lile kwa usalama, yule mvulana alitoa kibuyu kikubwa na kumimina kwenye kiganja chake unga mweusi ambao ulikua kama vumbi la mkaa uliosagwa sagwa na kuanza kupulizia hewani,
"Nya- nge-taaaaaa lala chini" ilisikika sauti ya inspecta Dotto akitokea kwa nyuma huku akipiga risasi kadhaa,,,ITAENDELEA


USIKOSE EPISODE 06

©Copyright "haki zote zimehifadhiwa"
 
>>>>>>EPISODE : 06<<<<<<<<
JINA LA STORY: GAMBOSHI
(Malkia wa wachawi)
MTUNZI: MOSSES AGREY
SEASON : 01
EPISODE: 06

Whatsapp
call/Text:+255687409189
(Audio version ya story coming soon)

*************************************
Previously on GAMBOSHI...

ILIPOISHIA,,,

"Nya- nge-taaaaaa lala chini" ilisikika sauti ya inspecta Dotto huku akipiga risasi,,,,,,

Sehemu ya 06


Sasa endelea,,,,,
kadhaa kuelekea upande wa Kangina( yule mtu mwenye macho mekundu)
Wote waligeuka ghafla na kumuona inspecta Dotto akija mbio huku akiendelea kumimina risasi ambazo zilikua zinadunda tu kwenye mwili wa Kangina na haikuonyesha kuleta madhara yeyote kwenye mwili wake, risasi moja ilidunda vibaya na kumrudia na kumpiga inspecta Dotto kwenye bega la kushoto na kuanguka chini huku damu zikianza kumbubujika, Nyangeta alimfuata mbio na kumshika mkono, huku akijaribu kumkalisha chini
"Dotto umefikaje huku?!?"
"Nilikuona muda unaondoka so nilikuja kama back up yako, ila ... Inaonekana kila kitu umekicontrol!" Aliongea Inspecta Dotto kwa shida huku akitokwa na damu nyingi,
"Nyangeta inabidi twende muda umeisha" aliongea yule msichana huku akichuchumaa alipo inspecta Dotto,
"Siwezi kumuacha hapa akiwa katika hali hii, inabidi aende Hospitali haraka wacha nipigie ambulance" aliongea nyangeta huku akishika simu yake ambayo ilikua kwenye mfuko wa koti lake,
"Nyangeta hawa ni wakina nani?" mbona wanamavazi ya ajabu?" aliuliza Dotto huku akijikongoja kutaka kuamka
"daah, ni story ndefu na yaajabu" alijibu nyangeta huku akimshikilia.
Nyangeta alijaribu kupiga simu yake lakini ilishindikana kutokana na ubovu wa mtandao katika eneo lile,
"Acha mimi nimpeleke hospitali" aliongea yule msichana mdogo.
"Nyangeta ...hawa ni wakina nani?, usiwaamini... wamemuua Dereva Taxi wako...koh ..koh!" Aliongea inspeta Dotto huku akikohoa.
"Nini!?" Aliuliza nyangeta kwa hasira huku akimgeukia yule msichana,
"Ohoo Kumbe, tunatakiwa tuondoke haraka, Minza mpeleke" aliongea yule msichana huku akisimama,
"Ampeleke wapi!!!??? Wauaji wakubwa nyie, !?!" Alihamaki Nyangeta huku akisimama, na kushika bastola yake tena, kabla hajafyatua risasi,
Yule mdada alinyoosha vidole viwili juu na kufanya ishara kama anamuita nyangeta, palepale Nyangeta alijikuta ananyanyuka juu na kuvutwa hewani bila kushikwa na kitu chochote kuelekea alipo yule msichana ambaye kwa sasa alionekana hataki mzaha kwa wakati huo, Nyangeta alikua anapiga kelele kwa nguvu huku hofu ikiwa imemjaa moyoni mwake, akiwa hewani alianza kuishiwa nguvu taratibu na alianza kuona giza na kupoteza fahamu palepale.
******
Nyangeta alifumbua macho na kujikuta amelala kwenye kitanda kikubwa kizuri, aliamka na kuketi kitandani huku akishangaa sehemu aliyokuwepo, ndani ya chumba kile kikubwa kwa pembeni kushoto kulikua na meza yenye kioo kikubwa cha kujitazama, juu ya ile meza kulikuwa na bunduki yake pamoja na waleti yake pembeni ya ile meza kulikuwa na kiti kidogo chakwa mbao, kwa upande mwingine wa chumba kile kulikua na madirisha makubwa yaliyokua yamefunikwa na mapazia meupe ambayo yalipepea taratibu, chumba kile kilirembwa vizuri upande wa juu kwa marumaru za dhahabu na sakafu yake ilikua kama kioo kwa jinsi ilivyokua inang'ara.
Nyangeta alijiangalia na kujiona akiwa kwenye mavazi tofauti na alivyovaa mwanzo, alikua amevalishwa gauni zuri kama la mtoto wa kifalme, gauni hilo la silk likiwa na rangi nyeupe lilikua limedariziwa vizuri kwa vito vya dhahabu, hakika gauni lile lilionekana ni zuri sana na pia lilikua linaonekana ni la gharama kubwa.
Akiendelea kushangaa na kupepesa macho kwenye kile chumba, macho yake yalitua moja kwa moja kwa msichana mrembo ambae alikaa kwenye kiti mbele yake huku akiwa anatabasam.
"Hatimaye umeamka... Pole sana kwa uchovu wa usingizi" aliongea msichana yule akiwa anatabasamu
"Asante, wewe ni nani? Na hapa niko wapi!?" Aliongea nyangeta kwa shauku huku akimuangalia yule msichana kwa wasiwasi,
"Usiogope Nyangeta, uko katika mikono salama kabisa" alijibu msichana yule huku akisimama na kumsogelea Nyangeta.
"Alafu... Nakujua wewe nilishawahi kukuona sehemu" aliongea nyangeta huku akimuangalia kwa makini yule msichana
"Hahahhaha" yule msichana alicheka kidogo kicheko cha kistaarabu,
"Ndio tulionana jana asubuhi"
Aliongezea yule msichana
"Yes nimekumbuka, nilikuona kituoni ulienda kuulizia kuhusu ajali iliyotokea"
"Haswaa tulionana pale mlangoni, na tulisalimiana vizuri sana"
"Ok, bila shaka wewe ndio uliniandikia ule ujumbe, haya naomba uniambie hapa niko wapi? Nimefikaje? Wewe ni nani, na wale walio niteka ni wakina nani.... Alafu! Dotto yuko wapi na anaendeleaje?" Aliuliza nyangeta maswali mengi kwa mfululizo huku akikaa kwenye kitanda
"Sasa nianze kujibu lipi maana dah! maswali mengi!" Alijibu yule msichana huku na yeye akikaa kitandani,
"Dotto yuko wapi?"
"Aliwahishwa hospitali, hali yake ni nzuri na nafikiri ataishi!"
"Wewe ni nani na hapa ni wapi?"
"Mimi naitwa Marietukan Ti Ng'wana Ng'humbu, japo watoto wangu wananiita Mariet au Mama" alijibu yule msichana kwa upole huku akimpa
Mkono Nyangeta
Nyangeta na yeye alimpa mkono kama ishara ya kusalimiana, Mariet aliamka na kusogea dirishani na kusimama
"Samahani watoto wangu walikubeba bila ridhaa yako lakini ni kutokana na muda wa kuwepo kwenye ulimwengu wa binadam wa kawaida uliwaishia na pia hatari ilizidi baada ya wewe kuja na mpenzi wako wakati ujumbe ulisema usije na mtu" aliongea Mariet huku akimgeukia Nyangeta huku akitabasamu kidogo,
"Dotto sio mpe.... Anyway, umesema ulimwengu wa kawaida kwani huku ni wapi?" Aliongea nyangeta kwa kuhamaki na uoga ulianza kumuingia, huku akishuka kitandani na kumsogelea Mariet,
"Haha... Nyangeta ...karibu GAMBOSHI" aliongea Mariet huku akifungua mapazia ya dirisha na kuonyesha taswira ya nje,
Kupitia dirishani pale Nyangeta aliweza kuona mji wa Gamboshi ambao ulikua ni mji mzuri ambao hajawahi kuuona maishani mwake, wakazi wa Gambioshi walionekana kuwa na furaha, barabara nzuri zilizojengeka vizuri za lami juu na chini (Fly Over), watu mbalimbali wakiwa wamepanda fisi wakubwa walipita ikiwa kama moja ya usafiri barabarani, kwa juu angani aliona watu wakiwa wamepanda nyungo za aina tofautitofauti wakipaa, huku wameshikilia singe kama usukani wa kuendeshea nyungo zile. Kwa mbele kidogo aliona magorofa makubwa kama yale yaliopo New york cit marekani, na nyumba nyingi nzuri zilizojengwa vizuri, ama kwa hakika mji ule ulipendeza sana ijapokua mambo mengi yalikua yakistaajabisha.
"Watoto watakupeleka ukatembee baadae " aliongea Mariet kwa ukarimu mkubwa baada ya kumuona nyangeta akiduwaa kuutazama uzuri wa mji ule,
"Oooh no...Nipo kuzimu...!!!" Aliongea nyangeta kwa sautimaana ndogo, huku akiwa anaendelea kuduwaa akiushangaa ule mji
" hahahah... Hapana, Haupo kuzimu Nyangeta, kuzimu ni kulee... barabara ile ndio umeiona? ukiifuata ile barabara ndio inakupeleka huko, japo usije ukaenda kule sio pazuri! ... Hapa ni Gamboshi" aliongea Mariet kwa msisitizo huku akimuonyesha nyangeta barabara iliyopo nje kidogo ya mji,
"Uko tayari nikakutambulishe kwa familia?!?" Aliuliza marieta huku akimgeukia Nyangeta
"Hebu niambie kwa nini nipo hapa?" Aliuliza Nyangeta huku akihamaki
"Hilo tutakueleza ila kwanza inabidi ukutane na familia nzima"
"Ok sawa," alijibu nyangeta huku akitikisa kichwa
Mariet alimshika mkono nyangeta na kuongozana nae, wakatoka nje ya mlango.
Walipotoka kwenye kile chumba Nyangeta akiwa na wasiwasi mkubwa moyoni mwake, walipita kwenye korido kubwa iliyokua imepambwa vizuri, huku kukiwa na milango ya vyumba vingine, walikwenda bila kuongea neno lolote mpaka mwisho wa korido ile, ambapo mwishoni kulikua na ngazi za kisasa zilizokuwa zinaelekea chini ambapo ilionekana kama ni sebule ya nyumba ile ambayo ilikua ni nzuri sana na kubwa sana kama hekalu la kifalme,
Walishuka zile ngazi huku Mariet akimuangalia usoni Nyangeta huku akitabasamu kwa mbali,
"Polepole Nyangeta hizi ngazi huwa zinateleza"
Nyangeta hakujibu kitu na kuendelea kushuka mpaka mwisho wa ngazi na kutokezea kwenye ile sebule ambapo kulikua na watu kama watatu waliokua wamekaa kwenye makochi mazuri makubwa , Nyangeta alisimama kwa kusita sita huku akiwaangalia wale watu ambao kila mmoja alikua Anafanya mambo yake.
"Usiogope Nyangeta" Mariet alimwambia huku akimuangalia usoni kwa ukarimu, akawageukia wale watu waliokaa,

"Jamani mgeni wetu ameamka mje mumsalimie." Aliongea Mariet akiwaambia wale watu huku akienda kwenye yale makochi,
"karibu ukae, mbona unasimama mbali," aliongezea Mariet huku akimuangalia Nyangeta,
Nyangeta kwa taratibu alienda na kukaa kwenye moja ya makochi yale yaliyowekwa kwa utaratibu mzuri,
Nyangeta baada ya kukaa aliwaangalia wale watu na kumtambua mmoja wao ambaye alikua ni yule kijana mkubwa aliyemuona kule kwenye mti wa mbuyu, mwingine alikua ni bibi mzee kikongwe akionekana kama ana umri wa miaka 70 hivi, yule mtu wa tatu alionekana ni mvulana mdogo mwenye umri kati ya miaka 12 mpaka kumi na 14.
"Wengine wako wapi? " Mariet alimuuliza yule kijana mkubwa huku akiketi,
"Minza atakua chumbani kwake, kangina alikua jikoni, ....Kanginaaaa" alijibu yule kijana huku akimuita kwa nguvu Kangina,
"Naaaaam!, namalizia nakuja" ilisikika sauti kutokea kwenye chumba kingine karibu na sebule ile.
Yule kijana mdogo alimuangalia Mariet huku akifanya ishara za mikono kama bubu akimwambia mariet jambo fulani.
"Haaaa kumbe ndio anachofanya!" Aliongea mariet huku akionekana kukasirika,
"Joram hebu muite... Na umwambie aje nacho" Mariet aliongea huku akiwa amekasirika,
Yule kijana alinyanyua vidole viwili akashika kichwa chake na kufumba macho, alionekana kama anawasiliana na mtu kwa kutumia fikra zake (telepathicaly).
Ghafla kwa kasi kama ya risasi alikuja msichana mdogo na kusimama katikati yao huku akiweka mikono nyuma,
Nyangeta alistuka sana akataka kukimbia lakini alijizuia kutikana na hakujua wapi pa kukimbilia, alimuangalia yule binti mdogo na kumkumbuka, wale watu wengine walionekana kuwa hawana wasiwasi huku yule bibi akimuangalia nyangeta bila ya kupepesa macho na kumfanya akose amani,
"Unaficha...!!!?!? Si nilikukataza kushika vitu vya watu?" Aliongea Mariet huku akimuangalia yule msichana
"Haraka rudisha kitu cha watu" aliongea Mariet huku akionekana kukasirika,
Yule msichana akatoa simu ya Nyangeta huku ikiwa inaonyesha alarm ya low betry, aliitoa na kumpa nyangeta huku akiwa na wasiwasi,
"Na uombe msamaha" aliongezea Mariet
"Samahani" aliongea yule binti kwa sauti ya uoga, Nyangeta aliipokea huku akijibu,
"Usijali mwaya....!" Yule msichana aligeuka na kwenda kukaa kwenye kiti, kwa upande ule wa ngazi kwa pembeni kidogo alitokea mvulana mwingine mkubwa akiwa na mwili uliojazia kama anafanya mazoezi ya kutunisha misuli huku akiwa ameshika sahani iliyojaa nyama iliyokua inanukia vizuri, akiwa ameongozana na yule binti ambaye na yeye alikuwako kwenye mti wa mbuyu, yule kijana alimsogezea Nyangeta stuli ndogo na kuiweka ile sahani juu kishana alimkaribisha kwa sauti ya upole na ukarimu,
"Karibu chakula, najua unanjaa, ... Huyu nilimuua mwenyewe na kumchuna mwenyewe, nimekuchagulia mguu alikua na mafuta kwelikweli" aliongea yule kijana akijisifia huku akimsogezea Nyangeta,
"aaah...! Asante sana...!!!" Alijibu huku akirudi nyuma kwa woga,
Watu wote walikua wakimuangalia,
"Haina sumu, si unaona..." Aliongea yule kijana huku akichukua kipande kimoja na kukitia mdomoni.
"Anahisi ni nyama ya mtu ndio maana anaogopa" aliongea Joram yule kijana mwingine
"Ooh...! hapana sio nyama ya mtu, sisi hatuli nyama za watu, hii ni nyama ya ng'ombe na Kangina alikua anampenda kweli huyo ng'ombe wake ila amemtoa kwa ajili yako" aliongea yule binti mkubwa.
"Hebu ngoja kwanza...! Mbona siwaelewi naona mnanifanyia vituko tu... Ukarimu mwingiii ambao sielewi mwisho wake ni nini..! " aliongea nyangeta kwa kuhamaki,
" hebu niambieni nyie ni wakina nani na kwa nini mmenileta huku,,,,,,,ITAENDELEA

USIKOSE EPISODE 07


©Copyright "haki zote zimehifadhiwa"

 
>>>>>>EPISODE : 07<<<<<<<<<
JINA LA STORY: GAMBOSHI
(Malkia wa wachawi)
MTUNZI: MOSSES AGREY
SEASON : 01
EPISODE: 07


ILIPOISHIA,,,,,,,,,,

" aliongea yule kijana akijisifia huku akimsogezea Nyangeta,
"aaah...! Asante sana...!!!" Alijibu huku akirudi nyuma kwa woga,
Watu wote walikua wakimuangalia,
"Haina sumu, si unaona..." Aliongea yule kijana huku akichukua kipande kimoja na kukitia mdomoni.
"Anahisi ni nyama ya mtu ndio maana anaogopa" aliongea Joram yule kijana mwingine
"Ooh...! hapana sio nyama ya mtu, sisi hatuli nyama za watu, hii ni nyama ya ng'ombe na Kangina alikua anampenda kweli huyo ng'ombe wake ila amemtoa kwa ajili yako" aliongea yule binti mkubwa.
"Hebu ngoja kwanza...! Mbona siwaelewi naona mnanifanyia vituko tu... Ukarimu mwingiii ambao sielewi mwisho wake ni nini..! " aliongea nyangeta kwa kuhamaki,
" hebu niambieni nyie ni wakina nani na kwa nini mmenileta huku"

SASA ENDELEA,,,,,
Nyangeta aliongea huku akijipapasa kiunoni na kugundua bunduki yake aliiacha chumbani,
"Usiogope nyangeta" aliongea Mariet huku akiwaonyesha ishara ya kwenda kukaa Wale waliosimama,
" uko katika mikono salama kabisa," aliongezea Mariet huku akikaa vizuri na wote wakiwa wameketi wakimuangalia Nyangeta.
"Mimi kama nilivyojitambulisha awali, ninaitwa Marietukan, na huyu ni Mama yangu, Ng'humbulian, au unaweza ukamuita Nyanya," aliongea Mariet huku akimuonyeshea kidole yule bibi mzee,
"Yani wewe ni mzuri kama mama yako, masikini aliondoka mapema sana"aliongea yule bibi mzee kwa huzuni huku akipigapiga kofi chini kwenye sakafu kwa mkono wake wa kulia na wakushoto akiuweka kifuani, Na wote walifanya hivyo,
Nyangeta alimuangalia yule bibi huku akishangaa
"huyu ndio binti yangu mkubwa anaitwa Pagilian.." Aliongea mariet huku akimuonyesha yule binti mkubwa,
"Samahani kwa kukuchukua bila ridhaa yako sikua na njia nyingine" aliongea yule binti,
Nyangeta alitikisa kichwa ishara ya kukubali,
"Na huyu ni Kangina ndio mpishi wetu hapa ndani, najua ulikutana nae kabla akiwa katika ile hali yake nyingine" aliongea Mariet akimuangalia yule mvulana aliyekua anamkaribisha chakula Nyangeta,
"Karibu sana japo umegoma kula chakula changu" aliongea Kangina,
Kwa kutabasamu, Nyangeta aliangalia ile sahani ya nyama na kuchukua kipande kimoja na kuanza kukitafuna, hakika nyama ile ilikua tamu ajabu,
"Mmh, mbona tamu sana unajua kupika!" Aliongea nyangeta,
"Asante sana..." Alijibu kangina huku akiinamisha kichwa chake ishara ya kukubali pongezi zile,
"Haya tuendelee, huyu anaitwa Joram, anawafuatia hawa wawili, halafu hawa wawili ni mapacha huyu Anaitwa Minza na huyu anaitwa Mbitian, nae pia ulikutana nae japo kwa hali tofauti... Huyu ni Bubu hana uwezo wa kuongea hivyo anaongea kwa ishara" aliongea Mariet huku akiwaonyesha kwa vidole , Joram na Minza walinyanyua mikono na kumpungia Nyangeta huku wakitabasamu,
Mbitian alinyoosha mikono yake na kufanya ishara fulani, wote wanaangua kicheko kasoro yule bibi mzee ambae muda wote alimkodolea macho Nyangeta.
"Mbona mnanicheka..!" Aliuliza nyangeta akiwa haelewi kinachoendelea,
"Hahaha, Mbiti anasema wewe ni mzuri na anataka kukuoa!" Aliongea Mariet huku akiendelea kucheka,
Nyangeta alimgeukia Mbiti na kutabasam.
"Ngoja kwanza, uliniambia hapa ni mji wa wachawi kwa hiyo nyie wote ni wachawi!?!" Aliuliza nyangeta kwa ujasiri, huku akiwa na wasiwasi moyoni mwake,
"Ndio, huu mji haingii mtu yoyote kama sio mchawi au hana chimbuko la kichawi.. Sisi wote ni wachawi" alijibu Mariet huku akimuangalia usoni,
"Sisi ni wachawi lakini wote tuna uwezo tofauti, sisi ni wachawi wa asili kabisa yani uchawi tumezaliwa nao ni tofauti kabisa na wachawi unaowafahamu wewe au uliowahi kuwasikia, uwezo nilio nao mimi ni tofauti na wengine yani kila mmoja anauwezo wake ambao haufanani na mwingine
Kwa mfano,
Mbitian anauwezo wa kubadilika kuwa kiumbe chochote ambacho kina uhai, na ndio maana ulipomuona alikua kwenye umbo la fisi, anapenda sana umbo hilo" aliongea huku akimuonyesha kidole Mbitian ambae ghafla alibadilika na kugeuka kuwa Fisi mkubwa, kisha alirudi tena kua binadamu.

"Minza uchawi wake yeye ni anauwezo wa kukimbia kwa kasi sana na bila kuchoka, ndio alimpeleka mpenzi wako hospitali," aliongezea mariet huku akimuangalia minza ambae aliondoka kwa kasi ya ajabu, kama sekunde mbili alikua amerudi na kumkabidhi nyangeta bunduki yake ambayo aliiacha chumbani, nyangeta alipigwa na butwaa mdomo ukiwa wazi,
"Sio mpenzi wangu"aliongea Nyangeta
"Joram anauwezo wa kujua mawazo yako yani anaona unachokifikiria pia ana uwezo wa kukuamrisha ufanye kitu bila ridhaa yako na ukafanya kwa kutumia mawazo yake"Mariet aliongezea huku akimuonyesha Joram ambaye alishika kichwa chake kwa vidole viwili na kufumba macho, hapohapo mkono wa Nyangeta ulinyanyuka ukiwa umeshika ile bunduki na kuelekezea kwenye kichwa chake, Nyangeta alijaribu kuurudisha lakini hakuaa na mamlaka kwenye mkono wake.
" hey joram tafadhali.... Basi nimeshajua uwezo wako" aliongea Nyangeta huku akitoa macho na kutetemeka kwa hofu, ghafla mkono wake ulirudi chini.
"Hahaha, haya na huyu Kangina yeye nafikiri unajua uwezo wake anabadilika kuwa kama ulivyomuona na pia ananguvu za ajabu sana" aliongezea Mariet huku akimkazia macho kangina, ambaye ghafla macho yake yaligeuka kuwa mekundu yanayowaka kama taa alafu yakarudi kuwa kawaida,
"pia anauwezo wa kuongezeka umbo na kuwa futi kama kumi na nane au ishirini hivi" aliongezea Mariet,
"Pagiliana anauwezo wa kuongoza kila kitu, na pia anauwezo wa kuwa zaidi ya mtu mmoja...ya..." kabla hajamaliza alitokea pagilian mwingine akishuka kutoka kwenye ngazi huku akiwa na walet ya Nyangeta ambayo nayo aliiacha chumbani, yule pagilian alikuja na kumletea ile walet Nyangeta na kumpa mkononi kisha akaenda akasimama kando na kupotea kama hewa.
"Wewe je !?" Aliuliza nyangeta huku akimuangalia Mariet
"Subiri mbona unaharaka" aliongea mariet huku akinyoosha mkono wake wa kushoto kuelekea jikoni, ambapo mkono ule ulirefuka moja kwa moja na kwenda mpaka jikoni, ulibeba jagi la maji na mkono ule ukarudi ukiwa na jagi mkononi., nyangeta alifumba macho huku akistaajabu aliyoyaona,
"Na mama yangu yeye pia uwezo wake ni kuona hatari zote ambazo zinakuja yani anaweza kuona jambo kabla halijatokea. Pia anaweza kukuonyesha mambo yaliyopita na pia yajayo. Na pia anauwezo wa kukuonyesha kitu chochote anachotaka yeye," aliongeza Mariet,
Yule bibi alinyanyua mkono wake huku akitetemeka kwa uzee huku akumuonyesha Nyangeta,
"Nenda ukajaribu anataka kukuonyesha kitu" aliongea Mariet,
Nyangeta aliamka na kwenda kumshika mkono yule bibi.
Alipo mshika hakuna kitu chochote kilichotokea, wote walikaa vizuri Na kushangaa,
"Nini kimetokea?" Aliuliza Kangina kwa mshangao,
"Mama uko sawa!?" Aliuliza Mariet huku akisimama na kwenda kumshika mabegani yule bibi,
"Yuko sawa ila kuna kitu kina mzuia kufanya uchawi wake kwenye mwili wa Nyangeta" aliongea Joram
"Kweli kuna kitu kina nizuia, kuna kitu umevaa shingoni" aliongea bibi Ng'humbulian, huku akimuangalia Nyangeta kifuani,
Nyangeta alibaki ameduwaa, mariet alimfunua kidogo maana ile nguo aliyovaa ilimfunika mpaka shingoni,
Nyangeta alikua amevaa rozali ambayo yeye alikua anaona ni rozali ya kawaida lakini kwa upande wa wale wachawi ilikua inang'aa kama jua na ilikua inawachoma macho,
" hili ni nini!?!" Aliongea Mariet huku akiangali pembeni,
"Ni Rozali" alijibu nyangeta huku akiiangalia,
Mariet alimsogelea huku akijikaza alitaka kuishika na kuitoa shingoni mwa Nyangeta, ilimuunguza kwa moto mkali sana na kumuachia Jeraha kubwa sana, aliiachia na kuanguka chini.
Wote walimkimbilia mama yao huku wakimsogeza Nyangeta pembeni,
"Mama..."
"Mama..."
"Mariet..." ,,,,,,,ITAENDELEA


SIKOSE SEHEMU YA 08


©Copyright "haki zote zimehifadhiwa"


 
Mbona haiendelei??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…