SAYVILLE
JF-Expert Member
- Mar 25, 2010
- 7,895
- 12,975
Kitendo alichofanya kocha wa Yanga Gamondi cha kuchanganya nafasi za wachezaji hasa kipindi cha pili katika ile mechi dhidi ya Red Arrows kwanza kilikuwa na nia ya kupunguza pressure kwa mashabiki waliokuwa wameshaanza kupagawa na matokeo ya mchezo. Lile lilifanyika ili mchezo msiuchukulie serious sana.
Pia baada ya mipango ya nyuma ya pazia kufanyika wakati wa mapumziko yaliyowahakikishia walau kupata sare, akaamua kubadili nafasi za wachezaji eti wanavyosema wachambuzi ili benchi la ufundi la Simba wasiweze kuisoma vizuri Yanga.
Mbinu za mchezo zinatofautiana kati ya mchezo na mchezo, hakuna mtu atakayeangalia jinsi mnavyocheza dhidi ya timu moja ategemee utakuja vile vile. Style ya uchezaji wa Yanga inajulikana, ni counter attacks, speed na kutumia penetration passes hadi kwenye box la mpinzani.
Walichobadili siku ile ni kujaribu sana kufunga magoli ya mbali ili kuyafunika magoli ya kina Fernandez, jambo lililoshindikana.
Makocha wa Simba bado wameweza kuona uwezo wa wachezaji mmoja mmoja wa Yanga na style zao za uchezaji. Wameiona Yanga kule Afrika Kusini ambapo katika mechi mbili dhidi ya Kaizer Chiefs na wale Wajerumani, hamu ya ushindi ilikuwa kubwa kwa hiyo ilikuwa rahisi kuwasoma wachezaji mmoja mmoja.
Bado wana hazina kubwa ya video za Yanga za msimu uliopita, ukichukulia kikosi hakijabadilika sana. Hapo unaficha nini sasa?
Tuambieni mapema, ngao mnaitaka au hamuitaki maana mkifungwa mtakuja na maneno yenu ya kuidharau wakati mlienda kushangilia airport kupokea kombe la bonanza tena la timu mbili tu.
Tunajua waliokuwa wanalilia sana kuiona live Simba ikicheza kule Misri si mashabiki wa Simba bali watu wa Yanga. Hakuna anayeenda kwa tahadhari na hofu kubwa katika mchezo huu wa kesho kama mashabiki, benchi la ufundi, viongozi na wachezaji wa Yanga. Mpaka sasa hawajui wanaenda kukutana na nini.
PS. Robertinho alimfunga Nabi akamfunga na Gamondi.
Pia baada ya mipango ya nyuma ya pazia kufanyika wakati wa mapumziko yaliyowahakikishia walau kupata sare, akaamua kubadili nafasi za wachezaji eti wanavyosema wachambuzi ili benchi la ufundi la Simba wasiweze kuisoma vizuri Yanga.
Mbinu za mchezo zinatofautiana kati ya mchezo na mchezo, hakuna mtu atakayeangalia jinsi mnavyocheza dhidi ya timu moja ategemee utakuja vile vile. Style ya uchezaji wa Yanga inajulikana, ni counter attacks, speed na kutumia penetration passes hadi kwenye box la mpinzani.
Walichobadili siku ile ni kujaribu sana kufunga magoli ya mbali ili kuyafunika magoli ya kina Fernandez, jambo lililoshindikana.
Makocha wa Simba bado wameweza kuona uwezo wa wachezaji mmoja mmoja wa Yanga na style zao za uchezaji. Wameiona Yanga kule Afrika Kusini ambapo katika mechi mbili dhidi ya Kaizer Chiefs na wale Wajerumani, hamu ya ushindi ilikuwa kubwa kwa hiyo ilikuwa rahisi kuwasoma wachezaji mmoja mmoja.
Bado wana hazina kubwa ya video za Yanga za msimu uliopita, ukichukulia kikosi hakijabadilika sana. Hapo unaficha nini sasa?
Tuambieni mapema, ngao mnaitaka au hamuitaki maana mkifungwa mtakuja na maneno yenu ya kuidharau wakati mlienda kushangilia airport kupokea kombe la bonanza tena la timu mbili tu.
Tunajua waliokuwa wanalilia sana kuiona live Simba ikicheza kule Misri si mashabiki wa Simba bali watu wa Yanga. Hakuna anayeenda kwa tahadhari na hofu kubwa katika mchezo huu wa kesho kama mashabiki, benchi la ufundi, viongozi na wachezaji wa Yanga. Mpaka sasa hawajui wanaenda kukutana na nini.
PS. Robertinho alimfunga Nabi akamfunga na Gamondi.