Gari ipi pasua kichwa kati ya hizi?

Gari ipi pasua kichwa kati ya hizi?

Sasa mkuu kama unasema haujui chochote then usibishe,ila jua brevis ziko aina 2 tu za cc2500 na cc3000 na kama ulinunua mkononi kwa mtu then jua alikudanganya tu ni Cc 2000 wkt ni cc2500.

Na case za brevis nilizosikia nyingi ni kuna wenye magari ya brevis ya cc 3000 yaliyoandikwa ai300 pale nyuma hua wanatoa hio lebel wanaweka ai250 kumdanganya mnunuzi kwamba hio gari ni ya cc2500 ila hii case yako ya cc2000 kwangu ni mpya mkuu.
Uko sahihi %100 mkuu inaweza ikawa 2500 ila nimepigwa danganya toto lkn haisumbui...iko poa tuu....
 
Kati ya:-

Brevis
Verossa
Gx 110
Xtrail

Kwenye Mafuta, Vipuli na matengenezo. Kwasisi tunaohitaji kununua kwa mtu, (mkononi)
Hakuna gari pasua kichwa ni USHAMBA wa mafundi tu...
Kana BREVENGA kitu 1jz fse ni bonge la injini kwa safari na mbio...
Gx 110 na verossa 110 zenye 1g fe nazo ni bonge la injini...
Mafundi ndo tatizo...
 
Brevis haziuzwi bei rahisi sababu ya ubovu,wanaziuza bei rahisi sababu wabongo especially madalali wameshaipa jina baya(Jini Mafuta) sababu ya kua na Cc 2500&Cc 3000.

Lkn ni gari makini sana na hainaga ubovu huo mnaoaminishwa.
Alafu wanavyoiponda kama wameshawahi kumiliki
 
Uko sahihi %100 mkuu inaweza ikawa 2500 ila nimepigwa danganya toto lkn haisumbui...iko poa tuu....
Gari ni matunzo mkuu....hao wanaosema shipa au jini hawajui magari.

Watu wanasukuma v8 za petrol, sembuse brevis.

Ni watu tu wameamua kuzichafua hizi gari.

Me si mpenzi wa magari ya Toyota lakini hili gari linaonewa sana.
 
Kwa bahati zuri nimeendesha gari zote hizo karoso Hiyo Verossa Kwangu mimi kama unataka gari zuri ya kutalii na kula raha nunua Brevis sema shida ni wakati wa kuuza tuuh unaweza kuuza kwa bei ya chini ila kama utapata brevis full option utakula pesa zuri wakati wa kuuza

Xtrail ni zuri sema unajua Nissan model na Tzania yetu vipuli plus ina body mbovu...

GX110 hii ni gari zuri sema ni old model na haiko confitable kama Brevis na haiko balance kwenye speed kama Brevis ila wakati wa kuuza utauza bei ya chini
 
Mkuu usitishe na hiki kijiwe...maana jf siku hizi imeshakuwa kijiwe cha kuchezea bao na draft.....
Ukisoma coment tu ya mdau, utagundua huyu ana gari au hana...
Utagundua huyu amesikia tu maneno ya kijiweni naye akayabeba akilini.

Hakuna gari pasua kichwa ukizingatia masharti yake.

Ubaya wa gari huwa unakuja toka kiwandani kuwa kuna baadhi ya model zinakuwa na shida mfano computer.

kama vile Nissan murano mwanzo zilikuwa na shida ya transmission, baadae Nissan wakafanya marekebisho kwenye model zilizofuata.

Toyota Rav 4 kill time kama sijkosea, nazo zilikija na matatizo ya Computer...computer yake inaonekana ilikiwa na shida ya programming toka kiwandani...ila baadae ilirekebishwa.

Ukikuta gari linatesa watu, hayo ni matatizo yake toka kiwandani kama vile mtoto anavyozaliwa mlemavu...

Sasa watanzania tunapenda bei rahisi.....mtu amezoea kununua wheel bearing ya starlet 3500/-
Akiambiwa ya Nissan ni 140000/- anaanza kusema hizi gari hazifai ni pasua kichwa..
Alafu wanavyoiponda kama wameshawahi kumiliki
 
Afadhali wewe umesema kuispoti hiyo gari, maana ndio nimeilipia juzi juzi tu sasa nikisikia vile watu wanaipondea huwa nawaza labda nimejichanganya kununua hilo gari.
Simu yangu ina shida ku upload picha ,ninge upload picha ya gari husika ili wanaoambiwa kuwa brevis ni magari ya chini ya bahari (majini) wakome ...
Na wajue tunaendesha tena kwa fujo za 4.5km/l
 
Brevis ni moja ya gari tamu sana ila wengi wanaonunua hawana uwezo wa kulimiki na kusingizia ubovu au ulaji wa mafuta hali inayopelekea kuuzwa bei ya chini.

Waswahili wanasema starehe gharama, huwezi kutaka comfot kwenye gari halafu itumie mafuta kama ya kwenye ist. Na hakuna gari inayoweza kukupa vigezo vyote unavyovitaka duniani.
Hujakutana na ford Everest 2020 ni balaa
 
Back
Top Bottom