RugambwaYT
JF-Expert Member
- Jan 11, 2014
- 1,397
- 1,899
Gari hilo maarufu lililopewa jina la BEAST (mnyama mkali) kutokana na kusheheni mifumo mbalimbali ya kujilinda dhidi ya jaribio la mashambulizi kwenye msafara wa rais wa Marekani, limeonekama likipita Manhattan na viunga vya mji wa New York wakati rais Trump akihudhuria Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa uliohudhuriwa na viongozi wa mataifa mbalimbali duniani.
Awali rais huyo alikuwa akitumia gari lililokumwa likitumiwa na rais Obama, amabalo halijabadilishwa tangu lilipoundwa mwaka 2009 wakati Rais Obama akiingia madarakani. Gari hilo lenye nembo ya Cadillac la mwaka 2018 ni moja kati ya magari kadhaa ya aina hiyo yanayotarajiwa kuundwa na kampuni ya General Motors kwa gharama ya takribani dola za kimarekani millioni 15.8.
Gari hilo lenye muonekano wa kisasa zaidi kuliko lile lililotumiwa na rais Obama, limezinduliwa majuma machache baada ya gari jipya la rais Putin wa Urusi na lile la rais Xi Jiping wa China kuonekana hadharani.
Taarifa kuhusu mifumo ya gari hilo bado ni siri kubwa, japo linasemekana kuwa na uwezo wa kujikinga dhidi ya mashambulizi mbalimbali ya risasi na makombora, pia lina vifaa vya huduma ya afya kwa rais ikiwemo machine ya hewa ya oxygen na damu ya rais. Picha hapo chini iliyowekwa na afisa wa habari wa Ikulu ya White House kwenye mtandao wa Twitter inaonesha mlango wa nyuma wa gari lilo wenye upana wa karibu futi moja.