Gari la IST linapokuwa na mlio kama lori na moshi kunuka kama Petroli mbichi

Gari la IST linapokuwa na mlio kama lori na moshi kunuka kama Petroli mbichi

kapuchi

JF-Expert Member
Joined
Oct 8, 2008
Posts
268
Reaction score
163
Wadau hebu nisaidieni, gari yangu ya IST ya mwaka moja tu toka niagize inatoa mlio kama lori huku moshi ukiwa una harufu kama Petroli mbichi.

Kuna baadhi ya watu wameniambia huenda wajanja wameniibia platinum ambayo ni aina ya madini ambayo hupatikana katika kiungio ambacho huwa kinachakata mafuta yanapotoka kwenye engine.

Mwenye ujuzi anisaidie
 
Mkuu tuongee biashara, niuzie nikusaidie matatizo hayo
 
Wadau hebu nisaidieni, gari yangu ya IST ya mwaka moja tu toka niagize inatoa mlio kama lori huku moshi ukiwa una harufu kama Petroli mbichi.

Kuna baadhi ya watu wameniambia huenda wajanja wameniibia platinum ambayo ni aina ya madini ambayo hupatikana katika kiungio ambacho huwa kinachakata mafuta yanapotoka kwenye engine.

Mwenye ujuzi anisaidie
Pole mkuu

Tatizo linaweza kuwa kama ifuatavyo kutokana na kama gari yako itakuwa inafanya kama ninavyodhani

(Kama gari inatetemeka na mlio unakuwa kama wa kumiss n unasikia harufu ya petrol kutoka kwenye exhaust)

Kama ni hivo tatizo linaweza kuwa moja katika vitu viwili..
1: ignition coil ( coil spark kibongo)
2: spark plug

1
Ignition coil ikifa huwa cylinder ambayo inahusika na kuchomwa na hiyo coil spark huwa haichomi kiwango cha mafuta na hupelekea yale mafuta kutoka moja kwa moja kwenye exhaust ( ndio maana unasikia harufu ya pure petrol kwenye exhaust)

Solution ni kutambua ni coil spark ipi imekufa kwa kuchomoa connector moja moja gari ikiwa imewaka, ukiona gari kama inataka kuzima ujue hiyo ni nzima, chomeka hamia nyingine mpaka uone ukichomoa connector gari haibadili mlio wala mtetemo hiyo itakuwa ndio coil mbovu.

2
Unaweza dhani ni coil ila ikawa ni spark plug ya hiyo cylinder ndio mbovu,

Chomoa na spark plug ikague kama ni nzima au kama huna ujuzi ihamishie kwenye cylinder iliyoonesha kuwa coil yake ni nzima, kama isipobadili hali basi spark plug ni nzima na coil ulipoitoa spark plug mwanzo ndio mbovu


Lilinukuta hili janga nikitokea musoma kwenda mwanza na ist na nikadhani ni coil spark, nilipochukua nyingine nzima na kuiweka nikaona bado na nikawa na uhakika kabisa kuwa coil mpya ni nzima.
Nilipofungua sparkplug nikagundua kale kakichuma cha chini ya ule mkunjo wa plug kalikuwa hakapo yane kameungua kabisa na kutoka. Nilipoweka sparkplug nyingine nikakuta kumbe coil yangu ni nzim kabisa nikasave 45k yangu ya ile coil mpya.

Nawakilisha.
 
Wadau hebu nisaidieni, gari yangu ya IST ya mwaka moja tu toka niagize inatoa mlio kama lori huku moshi ukiwa una harufu kama Petroli mbichi.

Kuna baadhi ya watu wameniambia huenda wajanja wameniibia platinum ambayo ni aina ya madini ambayo hupatikana katika kiungio ambacho huwa kinachakata mafuta yanapotoka kwenye engine.

Mwenye ujuzi anisaidie
Hahahahah Platinum sio, mkinunua magari muhakikishe mna watu wazoefu katika cycle yenu 😂😂😂!

Hicho anachoita platinum kinaitwa catalyic converter. Ni chujio maalum la kuchuja moshi baada ya combustion kutokea ili kuondosha zile sumu zitokanazo na compounds zinazozalishwa after combustion cycle completes.

Kuhusu wizi ni kweli hii inaibiwa sana sababu ni aghali sana kuinunua so ni dili kwa mafundi na wizi huu ufanyika kama unaachaga gari gereji bila kulisimamia au kulialaza kabisa gereji.

Madhara:
-Increased gas consumption.

-Increased noise from the muffler
ambazo zinaingia hadi kwenye cabin mda mwengine. Gari inapiga
bunda kama Altezza...Buuuuuuuuh!

- Kusambaza sumu ambayo ilikuwa
ichujwe mwanzoni ila haichujwi tena.
 
Hahahahah Platinum sio, mkinunua magari muhakikishe mna watu wazoefu katika cycle yenu [emoji23][emoji23][emoji23]!

Hicho anachoita platinum kinaitwa catalyic converter. Ni chujio maalum la kuchuja moshi baada ya combustion kutokea ili kuondosha zile sumu zitokanazo na compounds zinazozalishwa after combustion cycle completes.

Kuhusu wizi ni kweli hii inaibiwa sana sababu ni aghali sana kuinunua so ni dili kwa mafundi na wizi huu ufanyika kama unaachaga gari gereji bila kulisimamia au kulialaza kabisa gereji.

Madhara:
-Increased gas consumption.

-Increased noise from the muffler
ambazo zinaingia hadi kwenye cabin mda mwengine. Gari inapiga
bunda kama Altezza...Buuuuuuuuh!

- Kusambaza sumu ambayo ilikuwa
ichujwe mwanzoni ila haichujwi tena.
Mkuu kwani ndani ya catalyst converter kuna madini gani?
 
Hahahahah Platinum sio, mkinunua magari muhakikishe mna watu wazoefu katika cycle yenu 😂😂😂!

Hicho anachoita platinum kinaitwa catalyic converter. Ni chujio maalum la kuchuja moshi baada ya combustion kutokea ili kuondosha zile sumu zitokanazo na compounds zinazozalishwa after combustion cycle completes.

Kuhusu wizi ni kweli hii inaibiwa sana sababu ni aghali sana kuinunua so ni dili kwa mafundi na wizi huu ufanyika kama unaachaga gari gereji bila kulisimamia au kulialaza kabisa gereji.

Madhara:
-Increased gas consumption.

-Increased noise from the muffler
ambazo zinaingia hadi kwenye cabin mda mwengine. Gari inapiga
bunda kama Altezza...Buuuuuuuuh!

- Kusambaza sumu ambayo ilikuwa
ichujwe mwanzoni ila haichujwi tena.
Tatizo ni kuwa wabongo wengi wananunua magari bila kuwa na uwezo. Sikatai kuwa usafiri hasa kwa jiji kama Dar ni muhimu lakini kwanini ulazimishe? Wengi utakuta anataka na yeye aonekane kuwa ana gari!
 
Tatizo ni kuwa wabongo wengi wananunua magari bila kuwa na uwezo. Sikatai kuwa usafiri hasa kwa jiji kama Dar ni muhimu lakini kwanini ulazimishe? Wengi utakuta anataka na yeye aonekane kuwa ana gari!
Hapo kwenye uwezo ndiyo sijaelewa, bila uwezo wa kifedha au ufundi.

Maana kama ni uwezo wa kifedha, sioni alipoandika hivyo, na kama ni uwezo wa kiufundi, sidhani kama wameliki wengi wa magari hata huko, kwenye nchi zingine wamiliki wa magari pia ni mafundi. Sema kuna mambo muhimu dereva wa gari anapaswa kujua.
 
Back
Top Bottom