Gari lilikuwa nyumbani siku 2, mfumo wa Trafiki Polisi unaonesha ilipigwa faini

Gari lilikuwa nyumbani siku 2, mfumo wa Trafiki Polisi unaonesha ilipigwa faini

mzeemzima

Senior Member
Joined
Apr 14, 2010
Posts
123
Reaction score
78
Nina gari langu dogo la mizunguko ya kazini na watoto shule, gari hii muda wote na hasa kipindi cha Desemba na Januari lilikuwa linaendeshwa na mimi au mke wangu.

Wiki ya kwanza ya Januari na hasa tarehe 3 na 4 hatukutoka na gari kabisa, kutokana na kuwa katika likizo ya mwaka mpya. Leo baada ya kugundua kuwa kuna website ya police, TMS CHECK - Tanzania Police Force, ambayo unaweza kuangalia kama gari lako linadaiwa au la

Nikaona ngoja niangalie na gari langu, lahaula nakuta system inasoma kuwa gari lilipigwa faini Tarehe 4 Januari 2019 kwa kosa la kutozingatia kivuko cha waenda kwa miguu.

Leseni ambayo inayoambatana na kosa si yangu wala ya mke wangu lakini zaidi sana kama nilivyosema katika tarehe hii, gari haikutoka ndani kabisa .

Je katika mazingira kama haya napeleka wapi malalamiko yangu kuhusu faini hii ya kubambikiwa kimakosa au kwa makusudi kabisa?

Na je kuna uthibitisho wowote naoweza kuutumia katika mazingira kama haya ?

Naomba msaada wenu.

Natanguliza Shukrani
 
Mkuu Wick

Kuna ofisi maalum ya tafiki wanaohusika na malalamiko ya namna hii ? Kama ni hivyo , ni trafiki office ipi?

Asante
Kila mkoa/wilaya ina makao ya trafiki. We nenda central police ya sehemu ulipo watakuelekeza tu!. Kwa dsm nenda Central Police Posta.
 
Hapa sasa ndio unapokuja umuhimu wa kumtoza faini mwenye leseni na sio gari kwa kupitia namba ya gari.
Waanzishe tu utaratibu kuwa mtu akitozwa faini basi ihusike leseni na iwapo asipolipia basi deni lake lihusike nae tu hata kama leseni ikiisha muda basi akienda kulipia alikute deni lake.

"To expect bad man not to do wrong is madness"
 
Hili linawezekana. Wakati anaingiza namba kupiga faini...badala ya 356 akaingiza 365 au DNA akaingiza DAN
Wadau nashukuru kwa ufafanuzi , nipo wilaya ya kinondoni , na kosa limerekodiwa kuwa lilifanyika Kigogo. Nitafuatilia suala hili ofisi za trafiki
 
Leo nimegombana na trafic mkoa fulani hivi, mvua ilikuwa inanyesha nikiwa naendesha gati mbele yangu kulikuwa na toyota Coaster ikapita sehemu ya watembea kwa miguu na mm nikapita tikasimamishwa mbele eti hatuja simama katika zebra hafu kulikuwa na mvua ya wastani inanyesha, nikamuuliza traffic kuna mtu alikuwa anataka kuvuka? Yeye akasema pameandikwa stop lazima usimame nikamuuliza kama nikisimama je alama ya go/drive ingeonekana pale chini? Tumesumbuana akaniacha ila polisi katika zebra wanauonevu sana.
Nina kagari kadogo ka mizunguko ya kazini na watoto shule , gari hii muda wote na hasa kipindi Cha December na January lilikuwa linaendeshwa na mimi au mke wangu. wiki ya kwanza ya January na hasa tarehe 3 na 4 hatukutoka na gari kabisa , kutokana na kuwa katika likizo ya mwaka mpya . Leo baada ya kugundua kuwa kuna website ya police , TMS CHECK - Tanzania Police Force , ambayo unaweza kuangalia kama gari lako linadaiwa au la , nikaona ngoja niangalie na gari langu , lahaula nakuta system inasoma kuwa gari , lilipigwa fine Tarehe 4 January 2019 , kwa kosa la kutozingatia kivuko cha waenda kwa miguu . Leseni ambayo inayoambatana na kosa si yangu wala ya mke wangu , lakini zaidi sana kama nilivyosema katika tarehe hii , gari haikutoka ndani kabisa . Je katika mazingira kama haya napeleka wapi malalamiko yangu kuhusu faini hii ya kubambikiwa kimakosa au kwa makusudi kabisa? Na je kuna uthibitisho wowote naoweza kuutumia katika mazingira kama haya ?

Naomba msaada wenu.

Natanguliza Shukrani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapa sasa ndio unapokuja umuhimu wa kumtoza faini mwenye leseni na sio gari kwa kupitia namba ya gari.
Waanzishe tu utaratibu kuwa mtu akitozwa faini basi ihusike leseni na iwapo asipolipia basi debi lake lihusike nae tu hata kama leseni ikiisha muda basi akienda kulipia alikute deni lake.

"To expect bad man not to do wrong is madness"
Hili ndo suluhisho
 
Leo nimegombana na trafic mkoa fulani hivi, mvua ilikuwa inanyesha nikiwa naendesha gati mbele yangu kulikuwa na toyota Coaster ikapita sehemu ya watembea kwa miguu na mm nikapita tikasimamishwa mbele eti hatuja simama katika zebra hafu kulikuwa na mvua ya wastani inanyesha, nikamuuliza traffic kuna mtu alikuwa anataka kuvuka? Yeye akasema pameandikwa stop lazima usimame nikamuuliza kama nikisimama je alama ya go/drive ingeonekana pale chini? Tumesumbuana akaniacha ila polisi katika zebra wanauonevu sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
Zebra hata kiongozi wao alitoa ufafanuai UNASIMAMA iwapo kuna mvukaji. Na huyo mvukaji asikurupuke tu na yeye anatakiwa afuate taratibu za kuvuka.
 
Nachokiona traffic wanafanya ubabe wakiona mnabishana sana mwenzo mmoja anajifanya kung'oa plate namba ila leo nimewapa hadi wakawa wapole. Nadhani nawao wamepewa malrngo ya kukusanya kodi kama TRA na taasisi zingine za serikali badala ya kuwapa malengo ya kupunguza ajari za kizembe
Zebra hata kiongozi wao alitoa ufafanuai UNASIMAMA iwapo kuna mvukaji. Na huyo mvukaji asikurupuke tu na yeye anatakiwa afuate taratibu za kuvuka.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Leo nimegombana na trafic mkoa fulani hivi, mvua ilikuwa inanyesha nikiwa naendesha gati mbele yangu kulikuwa na toyota Coaster ikapita sehemu ya watembea kwa miguu na mm nikapita tikasimamishwa mbele eti hatuja simama katika zebra hafu kulikuwa na mvua ya wastani inanyesha, nikamuuliza traffic kuna mtu alikuwa anataka kuvuka? Yeye akasema pameandikwa stop lazima usimame nikamuuliza kama nikisimama je alama ya go/drive ingeonekana pale chini? Tumesumbuana akaniacha ila polisi katika zebra wanauonevu sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwenye zebra ni wewe mwenyewe dereva unatakiwa ujiongeze, kama nyuma ulishakiona kibao cha watembea kwa miguu basi kabla ya kufika kwenye zebra yenyewe angalia pembeni je hakuna mtu anaetaka kuvuka. Ukifanya hivyo utakuwa mbali na makosa kama hayo.

"To expect bad man not to do wrong is madness"
 
Duh! Dhuluma zinaendelea katika mikakati ya kukusanya bilioni 60 kutoka kwa wenye magari.

Nina gari langu dogo la mizunguko ya kazini na watoto shule, gari hii muda wote na hasa kipindi cha Desemba na Januari lilikuwa linaendeshwa na mimi au mke wangu.

Wiki ya kwanza ya Januari na hasa tarehe 3 na 4 hatukutoka na gari kabisa, kutokana na kuwa katika likizo ya mwaka mpya. Leo baada ya kugundua kuwa kuna website ya police, TMS CHECK - Tanzania Police Force, ambayo unaweza kuangalia kama gari lako linadaiwa au la

Nikaona ngoja niangalie na gari langu, lahaula nakuta system inasoma kuwa gari lilipigwa faini Tarehe 4 Januari 2019 kwa kosa la kutozingatia kivuko cha waenda kwa miguu.

Leseni ambayo inayoambatana na kosa si yangu wala ya mke wangu lakini zaidi sana kama nilivyosema katika tarehe hii, gari haikutoka ndani kabisa .

Je katika mazingira kama haya napeleka wapi malalamiko yangu kuhusu faini hii ya kubambikiwa kimakosa au kwa makusudi kabisa?

Na je kuna uthibitisho wowote naoweza kuutumia katika mazingira kama haya ?

Naomba msaada wenu.

Natanguliza Shukrani
 
  • Thanks
Reactions: Aza
Hapa sasa ndio unapokuja umuhimu wa kumtoza faini mwenye leseni na sio gari kwa kupitia namba ya gari.
Waanzishe tu utaratibu kuwa mtu akitozwa faini basi ihusike leseni na iwapo asipolipia basi deni lake lihusike nae tu hata kama leseni ikiisha muda basi akienda kulipia alikute deni lake.

"To expect bad man not to do wrong is madness"

Wana taabu na wenye magari. Nia yao ni kuwakandamiza na kuwakamua wenye magari. Wenye leseni tu watatoa wapi bil. 29 za faini ndani ya mwezi mmoja.

Ama kweli maendeleo yana chama!
 
Back
Top Bottom