Gari yangu inaoverheat ikiwa kwenye foleni au low speed

Gari yangu inaoverheat ikiwa kwenye foleni au low speed

318horses

Member
Joined
Jul 7, 2020
Posts
7
Reaction score
15
Habari za saa hizi wakuu, poleni na majukumu, gari yangu (corolla spacio) ilipata majanga iligongwa mbele vitu vyote vya mbele vikaharibika including fan, radiator na vyote vya mbele pale, so ikabidi iwe fitted with a new nosecut, baada ya hapo gari ikawa sawa, sasa kurudi barabarani gari inaenda nikifika tu kwenye foleni, geji ya temperature inaanza kupanda so inanibidi nipark nizime gari kwa muda kidogo then niendelee, badae nikaja kugundua feni ndo shida kwamba haifungui kwa wakati, lakini pia kuna kitu kikawa kinanitatiza kwasababu kuna muda ilikua inafungua, so ni kama ina mawenge kuna muda inafungua muda haifungui, nikampelekea fundi akasema ni switch ya feni akaweka nyingine, tatizo bado liko pale pale, kuongea na fundi tena anasema niende watoe thermostat gari iende bila thermostat, hapo sasa ndo nikawa na doubts, sasa sijajua nini shida nalileta kwenu wakuu tufunguane mawazo angalau, natanguliza shukrani

NB: sio kama feni haifungui kabisa, kuna muda inafungua kuna muda inafeli kufungua na hapo ndo overheat inapokuja
 
mkuu tafta fundi umeme mzuri hiyo shida ishawahi nipata

Mkuu kwanza Unahakika hiyo switch iliyobadilishwa nayo ni nzima ? maana hawa mafundi wetu wengi miyayusho sana maana spea zao nyingi anatoa kibovu kwenye gari fulani unafungiwa ww ,yani hapo lazima uchukie gari ,
Pia inawezekana kuna Liley labda nayo imekufa ,
Pata fundi umeme mzuri ujuwe tatizo liko wapi ,Au jaribu kwanza kuunga feni direct uwone ,ukitembea na gari temp ina panda na kama inapanda ,safisha rejeta na kama haipandi ,tambua tatizo liko katika Switch hiyo ilowekwa sio nzima au kuna Liley imekufa
 
mkuu tafta fundi umeme mzuri hiyo shida ishawahi nipata

Mkuu kwanza Unahakika hiyo switch iliyobadilishwa nayo ni nzima ? maana hawa mafundi wetu wengi miyayusho sana maana spea zao nyingi anatoa kibovu kwenye gari fulani unafungiwa ww ,yani hapo lazima uchukie gari ,
Pia inawezekana kuna Liley labda nayo imekufa ,
Pata fundi umeme mzuri ujuwe tatizo liko wapi ,Au jaribu kwanza kuunga feni direct uwone ,ukitembea na gari temp ina panda na kama inapanda ,safisha rejeta na kama haipandi ,tambua tatizo liko katika Switch hiyo ilowekwa sio nzima au kuna Liley imekufa

shukran mkuu
 
mkuu tafta fundi umeme mzuri hiyo shida ishawahi nipata

Mkuu kwanza Unahakika hiyo switch iliyobadilishwa nayo ni nzima ? maana hawa mafundi wetu wengi miyayusho sana maana spea zao nyingi anatoa kibovu kwenye gari fulani unafungiwa ww ,yani hapo lazima uchukie gari ,
Pia inawezekana kuna Liley labda nayo imekufa ,
Pata fundi umeme mzuri ujuwe tatizo liko wapi ,Au jaribu kwanza kuunga feni direct uwone ,ukitembea na gari temp ina panda na kama inapanda ,safisha rejeta na kama haipandi ,tambua tatizo liko katika Switch hiyo ilowekwa sio nzima au kuna Liley imekufa

Pia nilichogundua feni ikifungua hata kama gari iko stationary temperature haipandi kabisa hata ikae masaa mangapi, so yes nikajiridhisha shida ni feni
 
Badili sensor ya ECU utakuja kunishukuru

sent from HUAWEI
 
Kumiliki gari bila kuwa na fundi mzuri ni msalaba wa chuma.Mtu anakuambia kuwa anataka aitoe thermostat na bado unamwita kuwa ni fundi,hii maana yake ni kwamba wewe ndiye tatizo namba moja.

mkuu hivi vitu ndo vinatutokea mara ya kwanza wengine na hatuna ujuzi navyo, kwaio hatuna clue na tunaemwamini hapo ni fundi tu, na fundi ndo kama hivyo hamna kitu
 
Habari za saa hizi wakuu, poleni na majukumu, gari yangu (corolla spacio) ilipata majanga iligongwa mbele vitu vyote vya mbele vikaharibika including fan, radiator na vyote vya mbele pale, so ikabidi iwe fitted with a new nosecut, baada ya hapo gari ikawa sawa, sasa kurudi barabarani gari inaenda nikifika tu kwenye foleni, geji ya temperature inaanza kupanda so inanibidi nipark nizime gari kwa muda kidogo then niendelee, badae nikaja kugundua feni ndo shida kwamba haifungui kwa wakati, lakini pia kuna kitu kikawa kinanitatiza kwasababu kuna muda ilikua inafungua, so ni kama ina mawenge kuna muda inafungua muda haifungui, nikampelekea fundi akasema ni switch ya feni akaweka nyingine, tatizo bado liko pale pale, kuongea na fundi tena anasema niende watoe thermostat gari iende bila thermostat, hapo sasa ndo nikawa na doubts, sasa sijajua nini shida nalileta kwenu wakuu tufunguane mawazo angalau, natanguliza shukrani

NB: sio kama feni haifungui kabisa, kuna muda inafungua kuna muda inafeli kufungua na hapo ndo overheat inapokuja

Ukitembelea AC Gari ina overheat?
 
Ukitoa tu thermostat Hilo tatizo linaisha na hakuna madhara yoyote ni kwamba tu maji yanaflow saa zote gari ilishapigwa moto

Ila kama hutaki kuitoa Thermo
Kagua utendaji kazi wa cooling Timer na fen zote mbili ziwake

Usafi wa Radiator yako

Water pump kama Iko sawa.

NB. Kutoa thermo hakuna madhara kwenye nchi za kwetu
Mabadiliko tu ni kwamba temperature gauge haitakuwa inakuwaga pale katikati kama siku zote
Ukiitoa hii saa gari Iko silent au ikishuka kwende mteremko ( I mean saa injini imerelax basi na gauge Inaweza ikashuka chini kabisa
Gari ikishakuwa Mzee kutoa thermo ni sahihi kabisa
 
Aisee! Niliposoma post yako nilihisi unailezea gari yangu. Ghafla ilipandisha joto nikiwa stationary au low speed ila nikiongeza mwendo joto linashuka.
Nilimuita fundi akaniambia switch imekufa kwa hiyo akainganish feni direct yaani muda wote inazunguka. Na hapa muda wote taa ya low temperature ikawa inawaka kwa ku-blink.

Nilienda kwa fundi mmoja pale Mawasiliano akaniambia switch imekufa. Nikaagiza switch ikafungwa. Akasema feni inawaka kwa kususua kwa sababu brush za feni zimeisha.

Alisema kitendo cha brush kuisha kilisababisha switch kufa.

Niliweka brush mpya na gari imetulia na haijasumbua.

Kwa hiyo fanya utafiti kuhusu brush za feni.
 
Ukitoa tu thermostat Hilo tatizo linaisha na hakuna madhara yoyote ni kwamba tu maji yanaflow saa zote gari ilishapigwa moto

Ila kama hutaki kuitoa Thermo
Kagua utendaji kazi wa cooling Timer na fen zote mbili ziwake

Usafi wa Radiator yako

Water pump kama Iko sawa.

NB. Kutoa thermo hakuna madhara kwenye nchi za kwetu
Mabadiliko tu ni kwamba temperature gauge haitakuwa inakuwaga pale katikati kama siku zote
Ukiitoa hii saa gari Iko silent au ikishuka kwende mteremko ( I mean saa injini imerelax basi na gauge Inaweza ikashuka chini kabisa
Gari ikishakuwa Mzee kutoa thermo ni sahihi kabisa

Nahisi hauko sahihi katika kutoa thermostat.

Sio sahihi kwa injini kufanya kazi chini ya kiwango cha joto stahiki. Geji ya joto ikiwa chini inamaanisha injini inafanya kazi chini ya kiwango cha joto kinachotakiwa.

Na katika sheria za kifizikia maji au coolant yakipita muda woto huwa hayachukui joto na kulitoa sahihi. Inabidi maji au coolant yanyonye joto kwa kutulia kisha hiyo coolant au hayo maji yaliyobeba joto yatolewe kisha yaingie yaliyopoa kuanza kunyonya joto tena. Mzunguko huo ndio sahihi na sio ya maji kupita muda wote. Hayatochukua joto ipasavyo.

Kufanya kitu kwa mazoea pasipo kufuata maelekezo ya watengenezaji na kupata matokeo chanya haimaanishi ni sahihi. Mara nyingi huwa na madhara yanayokuja kuonekana baadae sana (long term effect)

Joto ni muhimu sana kwa injini na mtazamo wa “NCHI ZA JOTO / NCHI ZA BARIDI” hakihusiani na wewe kutoa thermostat maana joto la uendeshaji wa injini halihusiani na joto la hali ya hewa kama mfumo wako wa rejeta (radiator) ni msafi hauna vizuizi na unapooza sawasawa.

MTAZAMO BINAFSI kuendana na research ndogo tu.
 
Nahisi hauko sahihi katika kutoa thermostat.

Sio sahihi kwa injini kufanya kazi chini ya kiwango cha joto stahiki. Geji ya joto ikiwa chini inamaanisha injini inafanya kazi chini ya kiwango cha joto kinachotakiwa.

Na katika sheria za kifizikia maji au coolant yakipita muda woto huwa hayachukui joto na kulitoa sahihi. Inabidi maji au coolant yanyonye joto kwa kutulia kisha hiyo coolant au hayo maji yaliyobeba joto yatolewe kisha yaingie yaliyopoa kuanza kunyonya joto tena. Mzunguko huo ndio sahihi na sio ya maji kupita muda wote. Hayatochukua joto ipasavyo.

Kufanya kitu kwa mazoea pasipo kufuata maelekezo ya watengenezaji na kupata matokeo chanya haimaanishi ni sahihi. Mara nyingi huwa na madhara yanayokuja kuonekana baadae sana (long term effect)

Joto ni muhimu sana kwa injini na mtazamo wa “NCHI ZA JOTO / NCHI ZA BARIDI” hakihusiani na wewe kutoa thermostat maana joto la uendeshaji wa injini halihusiani na joto la hali ya hewa kama mfumo wako wa rejeta (radiator) ni msafi hauna vizuizi na unapooza sawasawa.

MTAZAMO BINAFSI kuendana na research ndogo tu.
Ndiyo maana serikali inasisitiza Sana watu wasome VETA kwasabb huku kuna mambo mengi yanafundishwa tofauti na mtaani ambapo mafundi wengi wamekariri kutoa thermostat... baadhi ya mafundi wa mtaani ni wazuri Ila hawako updated
 
Ndiyo maana serikali inasisitiza Sana watu wasome VETA kwasabb huku kuna mambo mengi yanafundishwa tofauti na mtaani ambapo mafundi wengi wamekariri kutoa thermostat... baadhi ya mafundi wa mtaani ni wazuri Ila hawako updated

Uko sahihi mkuu.
 
sio kama feni haifungui kabisa, kuna muda inafungua kuna muda inafeli kufungua na hapo ndo overheat inapokuja

Pole sana, tatua tatizo hilo...
 
Kumiliki gari bila kuwa na fundi mzuri ni msalaba wa chuma.Mtu anakuambia kuwa anataka aitoe thermostat na bado unamwita kuwa ni fundi,hii maana yake ni kwamba wewe ndiye tatizo namba moja.
ishu ya umeme hiyo mzee tafuta tu fundi mzuri wa umeme
 
Back
Top Bottom