Gari yangu inaoverheat ikiwa kwenye foleni au low speed

Ingekuwa thermostat inge overheat muda ukiwa kwenye mwendo maana kama thermostat haifungua maji hayawezi kuzunguka kwenye radiator.
Ushauri: Epuka mafundi wa mtaani, tafuta wa mzuri akusaidie kuondoa hilo tatizo, ni tatizo ndogo sana kama utapata mzuri.
 
Pia nilichogundua feni ikifungua hata kama gari iko stationary temperature haipandi kabisa hata ikae masaa mangapi, so yes nikajiridhisha shida ni feni
basi kama shida ni feni ,inawezekana hiyo switch alokubadilishia nayo sio nzima ,hawa mafundi sio wa kuaminika ,mimi nimeunga yangu direct maana nilishapasua rejeta mfuniko wa chini ,natembea na gari kumbe feni haifungui vizuri ,inafungua dakika chache inazima ,
 


Yupo sahihi kwa kiwango flani..

Hio dhana ambayo unaipinga (nchi za baridi/ nchi za joto) ni dhana sahihi kabisa na kisayansi ipo.. unaweza pitia kwenye automotive blogs mbalimbali utaikuta.

Thermostat imewekwa kuhakikisha engine ina operate kwenye kiwango cha joto kinachotakiwa (85c - 110 deg celcius). hili unalifahamu......sasa hapa ndo panahitaji akili ya ziada. Uliponunua wewe gari used kutoka japan ambako wanaamka Asubuhi wanakuta gari imefunikwa na snow ukubali kuwa ukija huku kwetu ambako Jua la saa nne asubuhi linaivisha Sausage hutatumia baadhi ya vitu.. pengine hutavihitaji kabisa..

Gari lako lina switch ya ku warm seat.. binafsi hii switch sijawahi itumia hata siku moja. mtu akiniambia hii ichomolewe siwezi kuhamaki na kusema ooh ni mjapani kaweka... ndo mana nikasema panahitaji akili ya kujiongeza.

kwa Dar.. naamini kabisa 98% ya magari yenye thermostat bado.. yanapowashwa asubuhi ndani ya safari husika hakuna wakati wowote ambao thermostat itajifunga (kuzuia mzunguko wa maji kwamba engine ni ya baridi mno) nadhani umeelewa.
Naamini pia endapo Wajapani wangekua wanaunda magari specifically kwa kila eneo basi wasingeweka thermostat kwa magari yanayoenda kutumika nchi zenye joto kali. cha msingi ni kutambua kua asilimia karibia 80% ya magari tunayotumia hayakulenga soko la nchi kama zetu.. huo ndo ukweli kwahio ukitambua hili haupati shida kuskia mtu anataka ku deactivate kitu flani. magari yalolenga soko la africa yanafahamika kabisa na wenyewe wauzaji wanasema.. na utalikuta limekaa kiafrica kwelikweli ma springs, shockabs n. k
 
Unataka watu waharibu magari yao
 
Gari ikileta usumbufu wa hivyo anza kwanza kwa kubadilisha radiator cap, pili kagua kama temperature sensor ile inayochomekwa kwenye radiator ipo vizuri
 
Reactions: Cyb
Haupo sahihi. Na nitakuelekeza
 
Story za vijiweni.

Hata hizo LC200 zinazoletwa brand new kwa ajili ya serikali na taasisi zinawekwa thermostat.

Thermostat sio kwaajili ya nchi za baridi au joto. Yenyewe kazi yake ni ku-control joto la engine ya gari yako hata uwe Dubai au Antartica.
 

Kwa hiyo Dar ukiwasha gari saa 6 mchana thermostat inakuwa iko wazi?
 
Kwa hiyo Dar ukiwasha gari saa 6 mchana thermostat inakuwa iko wazi?
Lol... ndo mana nasema inahitajika akili ya ziada, Ukiwasha gari saa sita mchana si engine ilikua imepoa thermostat inakuaje wazi bro?? Thermostat itafunga wakati umeliwasha namna ambayo inatakiwa kua ILA baada ya kutembea kidogo hakuna wakati mwingine wowote katika safari yako ambapo ETI thermostat itabidi ifunge tena kwa sababu engine imepoa mno (katika Nchi zetu hizi za Tropic), huko kwa wenzetu themorstat inaweza kufungua na kufunga mara nyingi sana ndani ya safari moja.

Kama umenisoma vizuri.. Point yangu kiufupi ni kua Kuondoa Thermostat kwa nchi zetu za joto hakuna adhari yoyote katika matumizi ya gari lako..

Sent from my CLT-L09 using JamiiForums mobile app
 
Reactions: Cyb
ILA baada ya kutembea kidogo hakuna wakati mwingine wowote katika safari yako ambapo ETI thermostat itabidi ifunge tena kwa sababu engine imepoa mno

Mfano, Thermostat za engine za Toyota huwa zinaandikwa namba fulani.

Mfano 82 C. Umeshawahi kujua maana yake?

Hiyo Tropical ya huku mnayoizungumzia ni joto la ngapi?

Na joto la nchi za wenzetu kwenye baridi ni ngapi?

Hayo majoto mawili yanaathiri vipi kufungua na kufunga kwa thermostat katika joto ambalo ni above 80 C?
 
Kumiliki gari bila kuwa na fundi mzuri ni msalaba wa chuma.Mtu anakuambia kuwa anataka aitoe thermostat na bado unamwita kuwa ni fundi,hii maana yake ni kwamba wewe ndiye tatizo namba moja.

hii hata mi imenifanya nistuke aisee , sasa unatoa thermostat hapo nin kitaregulate engine temp, huyu fundi atakua hajui kitu
 
Kufanya kitu kwa mazoea pasipo kufuata maelekezo ya watengenezaji na kupata matokeo chanya haimaanishi ni sahihi. Mara nyingi huwa na madhara yanayokuja kuonekana baadae sana (long term effect)

MTAZAMO BINAFSI kuendana na research ndogo tu.
Sio kila kitu anachoelekeza mtengenezaji ni cha kufuata. Vitu vingine ni kujiongeza kulingana na mazingira. Mfano siku hizi wamekuja na lifetime fluids, kama za gearbox. Sasa fuata hayo maelekezo usibadili uone kama hutanunua gearbox kila mwaka.
 
Ulipata solution ya hili tatizo?
 
Mara nyingi thermostat huwa zinajam..zikijam inakua haifungui kuruhusu coolant kuzunguka..hapo lazima uchemshe maindi ndani ya gari.. mafundi huwa wanapima kujua kama imejam au lah kwa kuidumbukiza kwenye maji ya moto..
 
 
kama ulibadili switch angalia feni inavuta upepo kwa ndani au inatoa ilisha nikuta kumbe inatoa
 
Hiyo switch inafanya kazi vema kweli na umecheki relay kama ipo vema?!
 
Kama haujui vitu ni vema kukaa kimya ili kujiepusha na aibu ndogo ndogo na kudhalilisha ukoo wako.

Ipo hivi, kutoa thermostat katika gari kuna madhara makubwa sana kadiri unavyoendelea kuitumia hiyo gari isiyo na thermostat kwasababu engine inakiwango chake cha kupozwa lakini ikizidi sana inakuwa na madhara ndani ya block ya engine kwenye oil kutokuwa katika joto linalotakiwa ili iweze kuzunguka vema.

Kwa mfano ukiamka asubuhi ule muda unawasha gari tu cooling ina anza sekunde chache zijazo na inakuwa ni constant process hakuna regulation ya coolant katika system.

Shida inaanzia hapo. Gari inaanza kuchapa Pistons huku oil ikiwa katika jotoridi la chini kuzidi namna inavyotakiwa.

Zile pistoni unanazoziona ndani ya block zina a very soft surface ambayo ikikosa lubrication wakati wa friction then kulika huanzia hapo na kuleta madhara katika kuta za ile combustion chamber ya kila pistoni.

Ndio unaanza shangaa gari baada ya muda fulani inaanza kutoa moshi mweupe au mweusi kwa wingi, unashangaa gari inakula oil, kesho piston rings hazifai, mara matatizo ya nozels kutema mafuta mengi sababu ya kulika rubber,mara engine inatakiwa kufanyiwa overhaul.

Kwa kifupi kitendo cha kutoa kifaa nyeti na muhimu kama thermostat kwenye gari yako tayari unajiandaa kuzalisha magonjwa makubwa baade ambayo ni ngumu kuwa reversible in their damaging rate. Na hayo magonjwa yataua engine haitafaa tena kwa matumizi ya yako na hautaenjoy gari.

Gari inapokuwa inadisplay tabia ambazo si za kawaida au tunasema ina malfunctioning kwenye eneo lolote unatakiwa kulipa attention ya kitaalamu na kiufundi na sio kupiga ramli na kuchukulia mambo kirahisi na kwa shortcut ili kukwepa kuwajibika na kuzikwepa gharama.

Gari ni kama mke,unatakiwa kuishi nalo kwa akili kupitia ishara linazokupatia.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…