Gari za umeme pasua kichwa gharama za uendeshaji

Nilidhani ni mimi tu nisiyependa yanavyokwenda bila sauti kama jongoo. Yaani siyakubali kabisa hata pale kwenye dashboard huwa naona ni kama jikoni.
 
Hizi gari za umeme bado sana hadi watakapogundua chanzo nafuu cha nishati kinachokaa muda mrefu zaidi then tunaweza kuzungumza biashara ila kwa sasa ni maigizo.

Halafu hizi gari zikiwaka moto hauzimiki hata gari ikitumbukizwa baharini inaendelea kuwaka. Aiseee.
 
Mi naona ni kwa sababu kibongo bongo hatutunzi record,utakuta hiyo miaka kumi ya kubadirisha betri
inakuwa ni nusu ya mafuta ambayo ungetumia kwa miaka hiyo kumi.
Battery za vitu muhimu kama hivyo zinadumu sana,sana suala la kupata ajali haliepukiki maana hata gari za mafuta
kuna wakati unapata mzinga wa maana gari haitengenezeki.
 
Gharama ya kuweka betri mpya haitokani na bei ya betri inatokana na muda wa kuiondoa bodi yote kwa sababu betri huwekwa kwenye sakafu ya gari, wengine watadhani betri inafanana na hizi za kawaida la hasha, wenzetu gharama za kazi hupimwa kwa muda unaotumia kutengeneza kitu, spea unanunua kwa sh. 20,000/= kuweka mpya unatozwa sh.100,000/= huku chombo kipya sh. 70,000/=, uamuzi ni wako ununue kipya au utengeneze unachokipenda.
 
Hizo gari wanazitupaje mkuu!?
 
Wapi huko wanauza battery ya prius kwa 2.5m mzee tukanunue maaana nmetoka kumfungia mteja wangu hata week haijapita kwa 4m tena hapo baada ya kupunguziwa toka 4.3m
Pale Japanese Car Service, Mtaa wa Shaurimoyo. Battery za Prius Generation 3 hadi 2m kasoro unapata.
 
Mie natumia full ev car na pia natumia hybrid car.....na nipo hapahapa bongo
 
Wapi huko wanauza battery ya prius kwa 2.5m mzee tukanunue maaana nmetoka kumfungia mteja wangu hata week haijapita kwa 4m tena hapo baada ya kupunguziwa toka wewe

Wapi huko wanauza battery ya prius kwa 2.5m mzee tukanunue maaana nmetoka kumfungia mteja wangu hata week haijapita kwa 4m tena hapo baada ya kupunguziwa toka 4.3m
Unatisha watu wewe prius hizi tunazotumia bongo gen 2 na gen 3 bei ya battery haifiki 4.3m.... mie natumia prius toka 2017 kwanza sijawai pata changamoto ya battery wala nini. Pia battery yake ukienda pale garage ya Yokohama ya wajapan pale shaurimoyo (price ni 1.5m-2m) unapata every healthy reconditioned battery packs ready to take you another 200,000km easily..

Tukumbuke kwa wale wanaotumia gari za hybrid kinacho ua battery prematurely ni temperature (yaan extreme cold or extreme heat) sasa kwa Tanzania joto ndo linaua battery but only kama uzingatii cooling performance ya feni inayopoza battery yako... hybrid car zinakua na separate cooling system ya kupoza battery yake ya high voltage.. system hii inakua na feni na filter ya kuchuja vumbi lisiingie huko kwenye battery, sasa unakuta mwamba ana hybrid car toka amenunua gari ajawahi fanya service ya feni au filter inayo husika na upozaji wa high voltage battery matokeo yake battery packs zina overheat na kuanza kupungua uwezo wake kuhold charge na battery kua weak...

Kingine hybrid hizi pia battery zake with time hutengeneza carbon kwenye terminal but carbon hizi hutokana na electrolyte kuvuja, so carbon zikijaa inafanya upitaji wa umeme uwe wa shida (yaan resistance inakua kubwa, so resistance ikiongezeka hufanya battery ku overheat na kupunguza life ya battery....so ni muhimu kufanya service ya kuondoa carbon kwenye terminal ya high voltage battery na service hii ni rahisi kiifanya kama wewe ni DIY mzuri ila kama ukienda kwa fundi pale kwa wajapan shaurimoyo wanafanya service hii kwa 50,000 tu..

Kwa mtu anaetaka hybrid yenye uwezo wa kuchaji kwenye umeme yaan (plug-in hybrid) anaweza akaaanza na prius gen 3 ambayo ni plug-in hybrid...hii itakupa pure range ya EV drive ya km 25-30km bila engine kuwaka...


Kwa wanao hitaji pure EV kwa bongo unaweza anza na Nissan leaf..japo hii inaenda km 200 ikiwa full charged ila charge iikiisha ndo safari inaishia hapo...ni nzuri kwa matumizi ya kutoka na kwenda kazini na huna misele mingi ila kama misele ni mingi si gari nzuri saana bora uchukue hybrid.
 
Sasa charger tu 25$ k hata ikienda 5000km lakini charger ikiharibika?

Ni mwendo wa Passo vitz na IST
Inategeana na gari..kwani service ya range rover ni sawa na paso?? Vivyo hivyo electric cars kuna betri za mil2 ya kibongo na kuna betri ya mil50
 
Hizo gari ni sahihi kununua used? Na gharama ya mpya ni kiasi gani?
 
30k kwa siku kwa mwezi ni laki 9 kwa mwaka ni 11.8mil..mbona ni hesabu ndogo sana
 
Subiri betrii likifa ndio utajua tofauti ya wewe wa bongo na mbele ni ipi
Mkuu, labda nikuambie ...hizi hybrid kwenye battery pack yake inakua na modules kadhaa mfano yangu inakuja na module (cell 28) zenye volts 7.2 zilizo ungwa in series na kutengeneza total voltages 201.6 (this is minimum voltage...na kuna kua na computer inayo monitor voltage ya every individual block ya cell, sasa what happens ikitokea battery inashida utakuta ni cell specific ndo inashida so unafungua battery pack yako unaondoa hiyo cell mbovu unaweka nyingine maisha Yana songa....cell moja inauzwa kati 50,000 to 100,000 but buying individual cell unaeza ona ni cheap ila ukinunua kwa cell zote 28 at individual price inakua ni cost kubwa kuliko kununua the entire pack at tzs 1.5m... so options ni zako wewe...ukiwa DYI person kama mimi service ndogo mdogo kama nafanya mwenyewe maana ni kazi nyepesi sana..

Pia kama nivotangulia kusema awali maintenance ya hybrid car ni rahisi ni vitu vichache ndo vinaongezeka kama filter ya feni ya kupozea hybrid battery packs, lakini pia kusafisha carbon in case zikiwepo kwenye terminal... Lakini other than that hybrid car has less maintenance costs kuliko gari ya kawaida in terms of fuel consumption, oil change interval, 12 v battery lasting duration, brakes hubaduri kama gari ya kawaida (mie nimeendesha gari tangu ikiwa na km 50000 mpaka sasa ina 195,000+km bila kubadili pads za brake, engine haichoki kama gari ya kawaida, sina stress za gearbox na kuchange transmission fluid kama Gari ya kawaida, fen belt, sijui kufa kwa compressor ya ac, etc...


Ukitaka nunua gari hybrid kwa mtu ni kuwa makini unatakiwa uwe na fundi wa umeme apime kujua system faults gari maana kuna faults ukizikuta kidogo ni expensive ku repair mfano mfumo wa brake wa gari ya hybrid ni kama uliopo kwenye brevis na land cruiser v8 na nyingine zinakuja na electronic brake system kumbuka hybrid car si muda wote engine inafanya kazi hivo ili brake system yake ipate assistance ilibidi waweke mfumo wa kielectonic (brake by wire) ambayo inafanya kazi pamoja na regenerative brake mechanism so brake system ikifa hata mota tu unanunu system nzima ya ABS kwasababu inakuja kama unit moja so price ni 700k to 800k.


NB: nime attach screen ya data kuka kwenye application moja inaitwa dr prius ambayo huwa naiunganisha obd2 dangle kusoma data za battery yangu ie kama internal resistance ya batteries, voltages ya kila module, temperature ya battery pack, Delta State ot charge (Delta SOC) pamoja na State of charge ya battery yangu, then najua health ya 12v battery ukumbuke gari hii haitumii battery ya 12volts kuwasha engine kama gari ya kawaida hivo incase ikitokea battery. Hii ipo down si rahisi kujua kamq gari nyingine ambayo utaona starter inashindwa kuwasha gari but kwa hybrid car issue ni tofauti kidogo kwakua gari haina stator ya 12v inayowasha engine bali battery ya voti 12 hutumika ku switch on and off hybrid battery relays na ku power 12 volts system ya Gari yako kama taa, radio, wiper, etc hivo kwakua ni ngumu kujua health ya battery hyo ndogo maana wamekuwekea hiyo feature kwenye app ya dr prius ili iwe rahisi kujua what is going on... Pia application hii inakiruhusu kujua battery/cell gani ipo weak na ipi ipo strong hii kitu ni muhimu ndo maana app ina monitor voltage difference so ikitokea voltage difference ikafika 0.3 between cells basi gari itawasha taa ya warning,,, lakini pia app hii inakuwezesha kuona charging rate na discharging rate... Niishie hapa ila ni gari tamu na ina instant power because of electric motor


A
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…