Gaza: Makombora ya Israel yashambulia kituo cha mpakani upanda wa Misri

Gaza: Makombora ya Israel yashambulia kituo cha mpakani upanda wa Misri

Jeshi la Israel limetoa salamu za Pole baada ya kombora lake kupiga kituo cha mpakani cha RAFAH upande wa Misri. Mara nyingi Israel hushambulia kituo hicho lakini upande wa GAZA. Kituo hicho ndio njia pekee ya kutoka na kuingia GAZA ambacho hakidhibitiwi na Israel.

Hata hivyo, Misri bado haijatoa tamko lolote mpaka sasa. Hayo yanajiri baada ya msafara wa pili wa Malori 18 ya msaada wa kibinadamu yakiingia Gaza kutokea upande wa Misri. Hata hivyo Israel imesema Malori hayo yaliingia bila Israel kujulishwa na hivyo kukiuka Usalama wake. Malori ya Msaada 20 ya kwanza yaliingia Gaza baada ya Marekani kuishawishi Israel ikubali msaada huo kuingia GAZA.


View: https://youtu.be/ZB2SqgnkbP0?si=DkmQokKOD6KUwsZ3View attachment 2789569

Israel= USA 51 th state (located in middle east).

Israel= USA foot soldier in middle east.

Israel= last remaining apartheid country.
 
Kuna fix hapo😃

Israel inasema haikujulishwa juu ya kuingizwa kwa malori hayo ya misaada huko Gaza 😃

Israel inasema imepiga kwa bahati mbaya😃 Hapa ni fix Tupu.

Ukweli ni kwamba Israel haijapiga kwa bahati mbaya,
Isipokuwa ,Kwa kuwa haikujulishwa juu ya kuingia kwa malori hayo huko Gaza, Israel ikajua misri inapeleka vifaa vya kivita kwa HAMAS ndo maana ikapiga.


Na inawezekana kabisa Israel ilijua hiyo ni misaada ya chakula kwa kuwa haitaki HAMAS wapewe chakula ikatumia ujanja ngoja tuyapige hayo maroli ya chakula halafu tuje tuseme tulikosea😃😃
 
Atakutana mkoko wa USA, hapo Egypt lazima afunike kombe yaishe
Nadhani unachukulia kuwa kuanzisha vita ni jambo rahisi, hapana haya mambo ya vita unaweza kuyaingia na usijue njia ya kutokea, vita ni maafa na gharama kubwa kabisa inaweza kukurudisha nyuma miaka 20 na miaka 20 ku recover. Angalia mfano vita vya Russia na Ukraine kuna mtu anajuwa njia ya kutokea? hakuna mwisho nchi tajiri tu zinachoka resource na kusupply. Egypt na Israel wana mkataba wa amani hawa wote wanajuwa maafa makubwa kuingia katika kupigana na hata kama USA ila majanga yake tutasimuliana mpaka kizazi kijacho. kwanini? History inatufundisha tunajuwa nini mpaka leo Iraq kilitokea au Afghanistan. unaweza kushinda vita sasa kuleta amani au kusimamia amani hapo sasa ndio majanga.

Tusiwe washabiki wa haya mambo ndio maana USA hakuna kitu kitu anaogopa vita hivi kutoka nje ya Israel na Ghaza sababu wanajuwa ni maafa makubwa yatatokea duniani na athari zake ni kubwa kupita maelezo. Hata nchi kama sisi ambao tuko mbali lakini tutaisoma number. Tuombe huu moto mdogo waweze ku control na kuzima sio kuusambaza.
 
So,kumbe ni vita ya USA against Palestine siyo?

Sasa hiyo nguvu ambayo mnaisifu nayo Israel kumbe bila kusaidiwa hawawez?

Cha ajabu zaidi wakiona Hezbollah na nchi kama Iran zinaside na Palestine wanakasirika na kulalama wanataka vipi Sasa.
Wewe kijana kama hujui kwa sasa Israel ndio Marekani na Israel ndio Israel
 
Mimi sijui kiarabu mkuu...nmeandika navyosikia wanavyosema mzee kwani vipi? Mbn kama unamind vitu vidogo sana, Wewe mwarabu nini?
Wewe unaona kunywa na kunya ni neno moja? Na kosa hilo la kiuandishi unaona ni kitu kidogo tu? Uoni kama umepotosha maana nzima ya neno ulilokusudia?
 
Wewe unaona kunywa na kunya ni neno moja? Na kosa hilo la kiuandishi unaona ni kitu kidogo tu? Uoni kama umepotosha maana nzima ya neno ulilokusudia?
Mimi sijali maana sio lugha yangu na wala nilikuwa siandiki kitabu kinachohitaji uhakiki wa fasihi
 
Back
Top Bottom