jogi
JF-Expert Member
- Sep 25, 2010
- 25,556
- 25,342
Kuna fani huwa haikosei?weledi kwa waandishi wa habari hapa nchini ni jambo la muhimu sana kuzingatiwa. magazeti mengi yamekua yakiandika habari mbali mbali zisizo na vyanzo vya kueleweka au za kuzusha tu kwa minajili ya kuuza kopi nyingi, lakini wanasahau kwamba wanao wajibu muhimu sana wa kuwapa wananchi taarifa sahihi.
Wahandisi wanaporomosha majumba, wanajeshi yanatokea ya mbagala na gongolamboto, madereva ndio kila siku, madaktari wengine hupasua kichwa badala ya mguu, mahakamani rufaa nyingi tu zinashinda ikimaanisha walihukumiwa kimakosa, mashuleni ndio usiseme! Kwa mfano "siasa ni kilimo"
Kwenye siasa, kwa mambo ccm inayoyafanya hayajawahi kuleta faida kwa nchi! Si mkukuta wala mkurabita.
Ugatuaji wa madaraka mikoani umemalizwa na pushup za jukwaani.
Boriti jichoni mwa nchi hii ni CCM, tusihangaike na vibanzi machoni mwa tasnia nchini.