Gazeti la MwanaHALISI lafungiwa kwa miaka miwili, wahukumiwa kwa kuandika habari za uzushi kuhusu Mwakyembe na Makinikia

Gazeti la MwanaHALISI lafungiwa kwa miaka miwili, wahukumiwa kwa kuandika habari za uzushi kuhusu Mwakyembe na Makinikia

Ufungiaji huu ungefanyika na kwa gazeti la Uhuru...ingekuwa vizuri!:-
Maana huwa linaandika mashudu sana!
 
weledi kwa waandishi wa habari hapa nchini ni jambo la muhimu sana kuzingatiwa. magazeti mengi yamekua yakiandika habari mbali mbali zisizo na vyanzo vya kueleweka au za kuzusha tu kwa minajili ya kuuza kopi nyingi, lakini wanasahau kwamba wanao wajibu muhimu sana wa kuwapa wananchi taarifa sahihi.
Screenshot_20170919-111438.png

Tambua picha hiyo!
 
Miaka miwili ?Uhuru wa vyombo vya habari upo Wapi ?Tanzania kama Uturuki.

Usijali kuna siku wataamka na watakapoamka nadhani itakuwa nilifanya haya kwa sababu huyu aliniamuru nifanye.Anyway toleo la jana sijaona chochote cha uchochezi labda habari za Lissu kuwa front page.

Na gazeti zima hakuna aliyeongelewa zaidi ya Lissu.
 
Uwiiii, habari za Ben saa 8 tutazipata wapi sasa!!! si hawa ndio walisema wanajua alipo Ben saa Nane?!!
ahahaaa wanaudhi sana wale jamaa.wana story zinachafua roho vibaya kumbe uongo tu. eti jm ana account ya euro million mia tano.ataifanya chato kuwa Dubai 2018
 
weledi kwa waandishi wa habari hapa nchini ni jambo la muhimu sana kuzingatiwa. magazeti mengi yamekua yakiandika habari mbali mbali zisizo na vyanzo vya kueleweka au za kuzusha tu kwa minajili ya kuuza kopi nyingi, lakini wanasahau kwamba wanao wajibu muhimu sana wa kuwapa wananchi taarifa sahihi.
Swadakta mkuu, [emoji16][emoji16][emoji16]
 
Wangelifungia na lile la Uhuru ingekuwa poa sana,maana lile gazeti kwa kuandika shudu halijambo.."
 


Msemaji wa serikali: Mfano tarehe 30 Januari lilichapisha habari yenye kichwa cha habari 'Ufisadi ndani ya ofisi ya JPM' ilhali ndani linazungumzia ufisadi ndani ya shirika la elimu Kibaha, ni kiwango cha juu sana cha sensetionalism. Tuliwaita wakaona udhaifu wao na kuomba Radhi na tukawasamehe.

Miezi miwili baadae April 27 wakaja na habari kubwa Mwakyembe: Maisha yangu yako hatarani. Hii stori ilikuwa ya kutunga, Mwakyembe hakuzungumza popote na mhariri wa Mwanahalisi wala mwandishi yoyote, wakaomba radhi kwenye gazeti lao la Mei kwa mheshimiwa Mwakyembe kwa kuomba Radhi, wakaahidi kwenye gazeti kuchukua hatua za kinidhani kwa mhandishi aliezusha, hatua hatujazisikia hadi leo na bado wameendelea na uandishi huo.

September 4 walikuwa na habari nyingine kubwa 'Makinikia yakwama'. Ni mfano mwingine wa habari ya kutunga, tukawapa muda wasahihishe lakini wakakataa kwa maana hawaoni kosa kisheria. Msingi wa kwanza kwenye uandishi wa habari ni ukweli, kamati ya makinikia imekwama wapi na lini, hata ukisoma Miga ina msingi wa confidentiality, sasa katikati ya mazungumzo gazeti kuibuka na kusema mazungumzo yamekwama.

Ila kwa uelewa wangu mtu akiweka maneno ktk wuotation hamaanishi literal meaning of it, unatakiwa kung'amua anamaanisha nini!
 
kama taarifa haikua na ukweli, haikuhusu serikali ya huyo kiumbe wangewashauri waandike ile ya mpwa, au ya mv dar es salaam, au ya nyumba..
au hilo gazeti lingepigwa risasi.
 
weledi kwa waandishi wa habari hapa nchini ni jambo la muhimu sana kuzingatiwa. magazeti mengi yamekua yakiandika habari mbali mbali zisizo na vyanzo vya kueleweka au za kuzusha tu kwa minajili ya kuuza kopi nyingi, lakini wanasahau kwamba wanao wajibu muhimu sana wa kuwapa wananchi taarifa sahihi.

image.jpg
 
Siku hizi ili uuze gazeti lazima iwe na kichwa cha Lisu;
Mfano:
1. Lisu aonyesha sura ya tabasam
2. Lisu akohoa hodini
4. Lisu amelalia ubavu wa kushoto Leo
5. Lisu anadai kikombe cha uji mapema Leo
6. Lisu apiga stori na waliomtembelea Leo
7. Nk

Sasa bwana, huku mtaani tutasikia maneno ya wajuaji...Mara Lisu kakohoa Leo!!, mara kaomba uji Leo!!! Ilimradi kila mmoja aonekane mfuatiliaji wa karibu.
Hilo gazeti walifungue tu maana soko ni baya kwasasa
 
Back
Top Bottom