Gazeti la MwanaHALISI lafungiwa kwa miaka miwili, wahukumiwa kwa kuandika habari za uzushi kuhusu Mwakyembe na Makinikia

Gazeti la MwanaHALISI lafungiwa kwa miaka miwili, wahukumiwa kwa kuandika habari za uzushi kuhusu Mwakyembe na Makinikia

Kuna watu humu hata ilo gazeti hawajawahi kulisoma lakini wako fasta kusema limeonewa. kama umewahi kulisoma hata mara mbili tu utajua style yao ya uandishi na wala Serikali haijakosea.
 
hivi ben saanane yupo wapi jamani shosti wangu yule acha tu yaani kanyamazishwa mazima kabisa
 
Poti nimetoka mara ya mwisho ' Uzanakini ' mwaka 2009 na mpaka sasa bado sijaenda na najua kabisa kwamba ' mizimu ' yetu ile mikali ya ' Kizanaki ' itakuwa imekasirika mno na Mimi. Hata hivyo namalizia ' michakato ' fulani ili angala ndani ya miaka mitatu au mitano ijayo niweze kwenda ' nikatambike ' kwani naona kama vile ' Betri ' zangu zimeisha ' chaji ' Poti.

Ukienda nisalimie sana Wazanaki wenzangu wote wa kuanzia Butuguri, Buhemba na Butiama waambie Kijana wao GENTAMYCINE a.k.a The Brain of Zanaki nipo, nawakumbuka na ninawawakilisha vizuri sana katika mambo mbalimbali kama vile ambavyo ' naturally ' Wazanaki ni Watu very intelligent, humble, committed, brave, daring, visionary, hardworking, philosopher Kings and fearless.

Mkuu leo umenifanya niwakumbuke sana Ndugu zangu ' Wazanaki ' na Mkoa wangu mzuri wa Mara ( Musoma )

Najua kwa ' bandiko ' hili ' Washamba ' wa kutoka Kagera, Kigoma, Singida na Dodoma kwa Warangi ' watanuna ' ile mbaya kwani walitamani mno GENTAMYCINE nitokee katika hiyo Mikoa yao ili na wao basi angalau ' waringe ' na Mtu ambaye kiukweli ni ' Purely Talented and Charismatic Fella '.

Kila la kheri Poti wangu.
Poti chaji imeisha? Hata mie nadhani imeisha. Nikienda nitawasalimia butuguri, buhemba! Kila LA kheri poti
 
Rudi kwenye hoja yako. Hata hivyo, ili nikusaidie staili za uhariri za Mwanahalisi na Mwananchi au Tanzania Daima ni tofauti. Kama umeisoma taarifa ya Dk Abbas ungeona haraka kwamba sababu ya kufungia Mwanahalisi ni moja tu-kuchapisha makala inayoonyesha kwamba Lissu ni mzalendo kuliko mkuu, period!

chapisha tu mkuu
 
Dictatorial regime, kwa nini wasingepeleka shitaka mahakamani?
 
Mimi nilitegemea baada ya kuonywa kwa mara kadhaa hatua inayofuata ni kulishitaki kwa kufungua kesi mahakamani kwa mujibu wa sheria husika. Maana tofauti na hivyo haki haipatikani kwa kuongea na waandishi wa habari na kutoa hukumu kupitia press conference au siku hizi press conference ndiyo imekuwa mahakama.
Hapa sasa mamlaka imeonyesha udhaifu kwa maana ya kutokufuata sheria, kuogopa, na kukwepa kwenda kwenye chombo cha kutafsiri sheria.
Kwa maana hiyo nikisema MwanaHalisi wameonewa nitakuwa ninakosea? Yaani nchi hii ni vituko tuuuuuu mpaka kero.
 


Msemaji wa serikali:
Mfano tarehe 30 Januari lilichapisha habari yenye kichwa cha habari 'Ufisadi ndani ya ofisi ya JPM' ilhali ndani linazungumzia ufisadi ndani ya shirika la elimu Kibaha, ni kiwango cha juu sana cha sensetionalism. Tuliwaita wakaona udhaifu wao na kuomba Radhi na tukawasamehe.

Miezi miwili baadae April 27 wakaja na habari kubwa Mwakyembe: Maisha yangu yako hatarani. Hii stori ilikuwa ya kutunga, Mwakyembe hakuzungumza popote na mhariri wa Mwanahalisi wala mwandishi yoyote, wakaomba radhi kwenye gazeti lao la Mei kwa mheshimiwa Mwakyembe kwa kuomba Radhi, wakaahidi kwenye gazeti kuchukua hatua za kinidhani kwa mhandishi aliezusha, hatua hatujazisikia hadi leo na bado wameendelea na uandishi huo.

September 4 walikuwa na habari nyingine kubwa 'Makinikia yakwama'. Ni mfano mwingine wa habari ya kutunga, tukawapa muda wasahihishe lakini wakakataa kwa maana hawaoni kosa kisheria. Msingi wa kwanza kwenye uandishi wa habari ni ukweli, kamati ya makinikia imekwama wapi na lini, hata ukisoma Miga ina msingi wa confidentiality, sasa katikati ya mazungumzo gazeti kuibuka na kusema mazungumzo yamekwama.
========

View attachment 591506
View attachment 591504

Mwananchi , Tanzania Daima na Mwananchi yote ni magazeti ya Udaku tupu.
 
Je serikali haiwezi kuyafungia magazeti ya Fahari Yetu na Tanzanite kwa ku "cite judgment" hii baada ya Takukuru kukanusha vikali tuhuma zilizotelewa na magazeti hayo kupitia taarifa yao kwa vyombo vya habari ya terehe 17.06.2019?
 
Je serikali haiwezi kuyafungia magazeti ya Fahari Yetu na Tanzanite kwa ku "cite judgment" hii baada ya Takukuru kukanusha vikali tuhuma zilizotelewa na magazeti hayo kupitia taarifa yao kwa vyombo vya habari ya terehe 17.06.2019?
Hayo magazeti ni untouchable nagwaaa

Ova
 
Back
Top Bottom