Gazeti la Mwananchi online lafungiwa miezi sita na kulipishwa faini milioni 5 kwa kupotosha

Bia yetu,
Mkuu hili si suala linalohusu mabeberu wala nini. Itazame hoja yangu beyond hizo sentiments. Media ndo namna pekee ya umma kupaza sauti. Serikali inayofanya kufungia media kuwa jambo rahisi inakuwa inajinyima yenyewe haki na uwezo wa kuwatumikia wananchi kikamilifu.
 
Gazeti la Mwananchi online content limefungiwa na TCRA kwa muda wa miezi sita (source: The Citizen). Online ni njia ya kuzuia au kupunguza maambukizi ya Coronavirus 2, sasa njia hiyo inafungiwa na ile ya karatasi inayotunza virusi kuendelea.

Leo ninatembelea gazeti online ninakutana na ujumbe huu 'www.mwananchi.co.tz Pole! We are unavailable.'

Hivi faini bila kufungiwa isingetosha? Ni vyema mahakama ndio iwe inaamua kesi kama hizi.
 
Sio kila kitu ni ufipa na ufupa.Tazama msingi wa hoja yangu.Kufungia chombo cha habari haipaswi kuwa rahisi hivyo.Kuna mambo hata viongozi wa serikali watakosa kuyafahamu kwa sababu ya vyombo vya habari kuwa na hofu ya kufungiwa.
Nani kasema limefungiwa kirahisi wakati sheria imefatwa kulifungia?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hata ikiwa hivyo media bado media haiko juu ya sheria

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hli ni jambo ambalo limefanya nikose majibu kabsa ni kutokana na Gazeti la MWANANCHI Kupgwa faini hvyo nkahisi kuwa TCRA kama wameingilia jukumu la Posta.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…