Ibrah
JF-Expert Member
- Mar 22, 2007
- 2,730
- 530
Siku ya Jumatatu ya juzi Magazeti ya Bongo yalisheheni kwa habari za Matokeo ya Uchaguzi wa Tarime yaliyokuwa yakisubiriwa kwa hamu na Watanzania.
Nilifuatilia kupitia kipindi cha "Watanzania Tuzungumze Magazeti" cha RFA. Katika kipindi hicho Magazeti yote yalisema CHADEMA walikuwa wakiongoza kwa kura kwa mujibu wa kura kztika vituo vya Uchaguzi; Ni gazeti la UHURU tu ambalo ni la propaganda la CCM ndilo liliripoti tofauti na magazeti yote (likiwemo Habari Leo ambalo lilisema CHADEMA wanaongoza).
UHURU walitoa taarifa kuwa CCM ilikuwa inaongoza katika vituo 11 kato ya 20 vya kupigia kura SIkubahatika kulisoma gazeti hilo lakini kwa udondozi ule wa RFA nilipata mawazo yafuatayo:-
Moja, UHURU lilitoa ripoti ya Uongo ambayo kwa hali ya Tarime wakati ule taaifa ile ingeweza kuleta machafuko makubwa maana CHADEMA na wafuasi wao waliamini kuwa wameshindwa na habari ile ilitosha kuwapa picha wapiga kura kuwa CCM wameiba kura.
Mbili, Kama kina cha habari kilikuwa hivyo, basi gazeti la UHURU liliudanganya umma wa WaTz.
Tatu, Inaelekea kulikuwa na njama za kupora ushindi wa WanaTArime na habari hizo za UHURU ziliandaliwa mapema kulingana na njama hizo ili kuwaondoa mashaka WaTZ juu ya matokea ambayo CCM walikuwa wameandalwa kushinda.
Naomba WanaJF waliopata gazeti hilo watubandikie hapa na ikithibitika kuwa kichwa cha habari walichokitumia kinaendana na maudhui ya habari hiyo basi namuomba Waziri Mkuchika alifungie Gazeti hilo kwa kutoa habari za uongo na za kuwagombanisha WaTZ na pia kuhatarihsa amani Tarime.
Nilifuatilia kupitia kipindi cha "Watanzania Tuzungumze Magazeti" cha RFA. Katika kipindi hicho Magazeti yote yalisema CHADEMA walikuwa wakiongoza kwa kura kwa mujibu wa kura kztika vituo vya Uchaguzi; Ni gazeti la UHURU tu ambalo ni la propaganda la CCM ndilo liliripoti tofauti na magazeti yote (likiwemo Habari Leo ambalo lilisema CHADEMA wanaongoza).
UHURU walitoa taarifa kuwa CCM ilikuwa inaongoza katika vituo 11 kato ya 20 vya kupigia kura SIkubahatika kulisoma gazeti hilo lakini kwa udondozi ule wa RFA nilipata mawazo yafuatayo:-
Moja, UHURU lilitoa ripoti ya Uongo ambayo kwa hali ya Tarime wakati ule taaifa ile ingeweza kuleta machafuko makubwa maana CHADEMA na wafuasi wao waliamini kuwa wameshindwa na habari ile ilitosha kuwapa picha wapiga kura kuwa CCM wameiba kura.
Mbili, Kama kina cha habari kilikuwa hivyo, basi gazeti la UHURU liliudanganya umma wa WaTz.
Tatu, Inaelekea kulikuwa na njama za kupora ushindi wa WanaTArime na habari hizo za UHURU ziliandaliwa mapema kulingana na njama hizo ili kuwaondoa mashaka WaTZ juu ya matokea ambayo CCM walikuwa wameandalwa kushinda.
Naomba WanaJF waliopata gazeti hilo watubandikie hapa na ikithibitika kuwa kichwa cha habari walichokitumia kinaendana na maudhui ya habari hiyo basi namuomba Waziri Mkuchika alifungie Gazeti hilo kwa kutoa habari za uongo na za kuwagombanisha WaTZ na pia kuhatarihsa amani Tarime.