Geita: Chuo Kikuu cha Utumishi wa Umma kujenga Kampasi yake Wilayani Chato

Geita: Chuo Kikuu cha Utumishi wa Umma kujenga Kampasi yake Wilayani Chato

Serikali isijenge tawi la chuo cha utumishi wa umma - kama inataka kuwasaidia watu ijenge tawi la chuo cha SUA (umuhimu wa kada hii ktk maendeleo ya kilimo ni mkubwa sana hasa kuchochea ukuaji wa sekta binafsi, uchumi, uwekezaji na huduma za kitafiti kwa wakulima)

Tusiharibu fedha za umma
Yes!
 
Kujipendekeza Ili tumbo lishibe ni janga la taifa. Tunakamuliwa Kodi ukichelewa tu riba inakuhusu siku hizi Kodi ni sawa na mkopo ni lzm ulipe na riba. Halafu wa chache Wana mis use Kodi zetu kutafutia sifa kulinda utumbuzi.
Then wanawadanganya watu eti umasikini wetu sababu mabeberu awapendi tuendelee.
 
Kampasi ya Chuo cha Utumishi wa Umma tawi la kanda ya ziwa kitajengwa wilayani Chato, amethibitisha waziri wa utumishi wa umma George Mkuchika.

Kwa mujibu wa Mkuchika ni kuwa amejiridhisha kuwa Chato inazo sifa zote zinazoiwezesha kujenga chuo hicho ikiwemo ukubwa wa eneo unaoridhisha.

=======

TPSC KUJENGA KAMPASI CHATO KUKIDHI KIU KANDA YA ZIWA

CHUO cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) kiko mbioni kujenga kampasi wilayani Chato, mkoani Geita itakayotoa fursa ya mafunzo kwa Watumishi wa Umma na wananchi wa Kanda ya Ziwa.

Akikagua eneo litakalojengwa Kampasi hiyo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Kapteni mstaafu George Mkuchika alisema ameridhika na eneo lililotengwa kwani ni rafiki kwa usalama na utoaji wa elimu.

Kampasi itajengwa eneo la Rubambangwe lenye ekari 41.66 na itahudumia mikoa ya Geita, Mwanza, Kagera, Shinyanga, Simiyu na Mara.

Waziri Mkuchika alisema Kanda ya Ziwa pekee ndiyo ilikuwa haijabahatika kuwa na Kampasi ya Chuo cha Utumishi wa Umma, hivyo fursa hii ni muafaka na itakuwa na manufaa kwa watumishi wa umma na wakazi wa eneo la Kanda hiyo.

Akizungumzia uamuzi wa kujenga Kampasi hiyo wilayani Chato, Mkuchika alifafanua kuwa halmashauri ya wilaya ya Chato imetoa kiwanja hicho bure tofauti na maeneo mengine ya Kanda ya Ziwa ambayo yangekigharimu chuo fedha nyingi kununua kiwanja.

Aliishukuru halmashauri kwa kutoa kiwanja na kumhimiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chato kuharakisha mchakato wa upatikanaji wa hati kwani chuo kiko tayari kuanza ujenzi mapema iwezekavyo.

Mtendaji Mkuu na Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, Dk Emmanuel Shindika aliwathibitishia wakazi wa Kanda ya Ziwa kuwa fedha za kuanza ujenzi zimeshapatikana, hivyo kinachosubirikiwa ni hati.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Chato, ambaye pia ni Waziri wa Nishati, Medard Kalemani alimtaka Mtendaji Mkuu na Mkuu wa Chuo kuwasilisha maombi ya kupatiwa umeme katika eneo hilo ili kuharakisha ukamilishaji wa ujenzi wa kampasi hiyo.

Akizungumzia eneo ambalo chuo kitajengwa, Mkuu wa Mkoa wa Geita, Robert Gabriel alisema ujenzi wa kampasi hiyo ukikamilika itakuwa ni chachu ya maendeleo kutokana na muingiliano wa watu kutoka maeneo mbalimbali watakaokuja kupata mafunzo na utavutia uwekezaji.
Sitashangaa, ule Mradi wa Bandari ya Bagamoyo ukihamishiwa Chato...
 
Shida ndiyo inaanzia hapo vyuo kibao vina branch kila mahali sijwahi ona watu wanahoji sasa hapo kujenga branch tu unaona maneno kibao. Pale maana yake watahudumia mikoa kama minne mitano kwa hiyo ni sawa
 
chato CHATO chato CHATO
Mhe Dkt John Pombe Magufuli, usikubali, kataa Serikali yako isijenge tawi la chuo cha Utumishi wa Umma Chato

Kama inataka kuwasaidia wananchi basi ijikite kwa (wakulima ambao ni tabaka kubwa) basi ijenge tawi la Chuo cha Kikuu cha Kilimo SUA (umuhimu wa kada hii ktk maendeleo ya kilimo ni mkubwa sana hasa kuchochea ukuaji wa sekta binafsi, uchumi, uwekezaji na huduma za kitafiti kwa wakulima) nk

Dkt John Pombe Magufuli tafadhali pamoja na kuwa Cpt John Mkuchika ni mtu mnayeheshimiana sana lkn ktk hili mkatalie - tufanye miradi ambayo mutiplier effect yake inagusa moja kwa moja ukuaji wa uchumi ktk Kaya, Halmashauri, na Taifa.

Tusiharibu fedha za umma
 
Shida ndiyo inaanzia hapo vyuo kibao vina branch kila mahali sijwahi ona watu wanahoji sasa hapo kujenga branch tu unaona maneno kibao. Pale maana yake watahudumia mikoa kama minne mitano kwa hiyo ni sawa
Nadhani tuna shida ktk kuamua kipi kiwe kipaumbele cha kwanza, pili, tatu, nne nk

= Hivi kama ni muhimu kuwa na tawi la Chuo Kikuu hapo Chato kipi kilitakiwa kuanza (a). Cha Utumishi wa Umma, au (b). Cha Kilimo "SUA"?

= Sasa kama kuna hitaji la kuwa na tawi hapo basi tawi hilo liwe kwanza lile linalogusa maisha ya takriban watu zaidi ya 10M (Geita 1M, Kagera 3M, Mwanza 4M, Shinyanga 2M) nk nk

= Baada ya kukamilika kwa Chuo hicho cha Kilimo basi vifuate vyuo ambavyo huandaa mafundi (Engineers) hawa watakuwa kada muhimu kwenye sekta ya viwanda - hatujawa na mafundi ya kuunda gari, meli, ndege, mabomba nk - kwa maana kwamba sekta binafsi na za umma bado tunaagiza vitu hivyo toka nje kwa wingi - magari ya ofisini, magari ya washawasha, vifaru, nyambizi bahari kuu vyote hivi lzm tuangalie jinsi ya kujitengenezea nchini ili ikiwezekana tuwauzie hata wengine.

= Jana niliandika kwa sekta binafsi za Tanzania hazijafanya vizuri kwa msingi kwamba Kenya makampuni 600 yameomba fedha toka AfDB, Uganda 300, na Tanzania 8 tu - tushajiuliza kwa nini tuwe nyuma au chini? Majibu yako wazi kwamba waliomtangulia Dkt John Pombe Magufuli waliwekeza sana ktk mambo mengi yasiyosaidia ukuaji wa sekta binafsi ie kuanzisha Chuo cha Serikali za Mitaa Hombolo, Chuo cha kumbukumbu ya Mwl Nyerere, Chuo cha Uhazini nk

Sasa muda huu tusiutumie kujenga vyuo vya aina hiyo - tujenge vyuo vyenye tija.
 
Back
Top Bottom