Geita: Mkoa "tajiiri" usiokuwa tajiri

Geita: Mkoa "tajiiri" usiokuwa tajiri

Leo, ikiwa ni siku ya mapumziko, nimetembelela eneo lililoanzishwa machimbo mapya ya dhahabu hivi karibuni hapa Geita. Pichani ni mwanamke akiokota mawe anayodai yana dhahabu kwa lengo la kwenda kuyauza.
 

Attachments

  • IMG_20230629_131859.jpg
    IMG_20230629_131859.jpg
    1,016.3 KB · Views: 13
  • IMG_20230629_131851.jpg
    IMG_20230629_131851.jpg
    1.3 MB · Views: 13
  • IMG_20230629_131845.jpg
    IMG_20230629_131845.jpg
    1.3 MB · Views: 12
Sipajui sana Geita, lakini napafahamu, alau kidogo. Habari zake zimevuma ndani na nje ya Tanzania, hasa kwa shughuli za "uvunaji" dhahabu!

Hivi karibuni, nimesimuliwa kuwa baada ya Mzungu mmoja huko ughaibuni kukutana na dhahabu iliyodaiwa kuwa ilichimbwa na kampuni ya Geita Gold Mine (GGM), iliyopo Geita, aliamua kufungua safari hadi Geita nchini Tanzania. Alitaka kwenda kujionea ustawi wa mji ulikotoka hiyo dhahabu! Alichokiona ni tofauti na alichokitarajia.

Kwa "madhahabu" yanayozalishwa Geita, alitarajia kukuta maskycraper ya maana, kumbe hakukuwepo hata na ghorofa lenye lifti.

Alitarajia kukuta maflyover mengi, lakini kumbe hata barabara zenye lami ni chache mno.

Alitegemea kukuta mji uliojengwa ukajengeka, matokeo yake alikuta kuna mpaka nyumba za nyasi.

Alifikiri, kama vile Almasi ilivyosaidia kuijenga Afrika Kusini, na dhahabu nayo itakuwa imeisaidia Geita kuwa jiji la kipekee sana.

Geita ina "madhahabu" mengi mno. Ni kati ya mikoa ambayo machimbo ya dhahabu yanaendelea kuibuliwa na raia wa kawaida. Si mara moja wala mbili, mtu amebadili "plan" ya kuchimba shimo la choo baada ya kukutana na mwamba wenye dhahabu, na kupelekea shimo lililokusudiwa kuwa la choo kugeuka kuwa mgodi wa dhahabu.

Takwimu za mwaka 2020 zinaonesha kuwa Geita, mkoa "mtajiri" wa dhahabu, unazidiwa na mkoa wa Lindi kwa utajiri. Sijui hilo limekaaje! Labda Wachumi watanisaidi.

Geita, mkoa "mtajiri" kiasi hicho, unakosaje kuwa na stendi ya kisasa?

Geita, mkoa "mtajiri" wa dhahabu, unapitwaje kwa utajiri na mkoa wa Iringa ambao Mhe. Dr. J. K. Msukuma aliuita ni mkoa wa walima nyanya?

"Nimepita" Iringa, na nimekaa kwa muda mkoani Geita. Naam, hata sasa ninapouandika huu uzi, nipo Mkoani Geita. Kwa mwonekano tu, Iringa panaonekana pameendelea sana ukipalinganisha na Geita.

Kwa nini Geita mkoa "mtajiri" siyo tajiri?
upo geita sehemu gani?? karibu uje uchome nyama hapa bever night club
 
Sipajui sana Geita, lakini napafahamu, alau kidogo. Habari zake zimevuma ndani na nje ya Tanzania, hasa kwa shughuli za "uvunaji" dhahabu!

Hivi karibuni, nimesimuliwa kuwa baada ya Mzungu mmoja huko ughaibuni kukutana na dhahabu iliyodaiwa kuwa ilichimbwa na kampuni ya Geita Gold Mine (GGM), iliyopo Geita, aliamua kufungua safari hadi Geita nchini Tanzania. Alitaka kwenda kujionea ustawi wa mji ulikotoka hiyo dhahabu! Alichokiona ni tofauti na alichokitarajia.

Kwa "madhahabu" yanayozalishwa Geita, alitarajia kukuta maskycraper ya maana, kumbe hakukuwepo hata na ghorofa lenye lifti.

Alitarajia kukuta maflyover mengi, lakini kumbe hata barabara zenye lami ni chache mno.

Alitegemea kukuta mji uliojengwa ukajengeka, matokeo yake alikuta kuna mpaka nyumba za nyasi.

Alifikiri, kama vile Almasi ilivyosaidia kuijenga Afrika Kusini, na dhahabu nayo itakuwa imeisaidia Geita kuwa jiji la kipekee sana.

Geita ina "madhahabu" mengi mno. Ni kati ya mikoa ambayo machimbo ya dhahabu yanaendelea kuibuliwa na raia wa kawaida. Si mara moja wala mbili, mtu amebadili "plan" ya kuchimba shimo la choo baada ya kukutana na mwamba wenye dhahabu, na kupelekea shimo lililokusudiwa kuwa la choo kugeuka kuwa mgodi wa dhahabu.

Takwimu za mwaka 2020 zinaonesha kuwa Geita, mkoa "mtajiri" wa dhahabu, unazidiwa na mkoa wa Lindi kwa utajiri. Sijui hilo limekaaje! Labda Wachumi watanisaidi.

Geita, mkoa "mtajiri" kiasi hicho, unakosaje kuwa na stendi ya kisasa?

Geita, mkoa "mtajiri" wa dhahabu, unapitwaje kwa utajiri na mkoa wa Iringa ambao Mhe. Dr. J. K. Msukuma aliuita ni mkoa wa walima nyanya?

"Nimepita" Iringa, na nimekaa kwa muda mkoani Geita. Naam, hata sasa ninapouandika huu uzi, nipo Mkoani Geita. Kwa mwonekano tu, Iringa panaonekana pameendelea sana ukipalinganisha na Geita.

Kwa nini Geita mkoa "mtajiri" siyo tajiri?
Upo sahihi kabisa,halafu njoo shangaa Tanzania ilinganishae na Quatar,halafu baada ya hapo ishangae Africa,ilinganishe na Australia.
 
Leo, ikiwa ni siku ya mapumziko, nimetembelela eneo lililoanzishwa machimbo mapya ya dhahabu hivi karibuni hapa Geita. Pichani ni mwanamke akiokota mawe anayodai yana dhahabu kwa lengo la kwenda kuyauza.
Jirani na machimbo ya dhahabu yajulikanayo kama Tembo Mining, nimewakuta watoto wadogo wametoka kuvua samaki kwenye mto mdogo pembezoni mwa barabara. Walio hai wamewatengea kwa ajili ya kwenda kuwafuga na waliokufa wanaenda kuwatumia kwa mboga.

Ila nimeshangazwa pia kuwakuta wanaume watu wazima wakioga mtoni pembezoni mwa barabara Mchana kweupe bila kujali watoto na wanawake wanaopita jirani na wanakoogea. Kama huo ni ujasiri, basi wanastahili pongezi. Wengine wasingethubutu.
 

Attachments

  • VID_20230629_140553.mp4
    48.7 MB
Upo sahihi kabisa,halafu njoo shangaa Tanzania ilinganishae na Quatar,halafu baada ya hapo ishangae Africa,ilinganishe na Australia.
Nahisi Geita imeonewa ama imejionea. The region is so rich!

Kama dhahabu za kuokotwa zipo, zilizokwisha kuchimbwa, zinazochimbwa na zinazosubiri kuchimba ni nyingi kiasi gani?
 
Mkuu mikoa ya bara inasaidia kuijenga dar. Utaidharau Geita Leo lakini kutokana na mifumo yetu,kinachopatikana kinaingia serikali kuu kwenda kuijenga dar na Dodoma. Tukisema kila mkoa ujitegemee, ndani ya mwaka geita utaufuta huu Uzi.
Japo uzi una muda mrefu lakini hili ndiyo jawabu sahihi!.

Hii nchi kuna mikoa inanyonya rasilimali za maeneo mengine na kujisifu wana maendeleo huku mikoa inayotoa ikiwa kwenye hali mbaya

Mkoa wa Geita ukitoa hiyo highway ya Mwanza Bukoba hakuna barabara yoyote ya lami inayozidi 5km

Ukitaka kwenda mkoa wowote tofauti na Mwanza Musoma au Kagera unapita barabara ya Vumbi.
 
Sipajui sana Geita, lakini napafahamu, alau kidogo. Habari zake zimevuma ndani na nje ya Tanzania, hasa kwa shughuli za "uvunaji" dhahabu!

Hivi karibuni, nimesimuliwa kuwa baada ya Mzungu mmoja huko ughaibuni kukutana na dhahabu iliyodaiwa kuwa ilichimbwa na kampuni ya Geita Gold Mine (GGM), iliyopo Geita, aliamua kufungua safari hadi Geita nchini Tanzania. Alitaka kwenda kujionea ustawi wa mji ulikotoka hiyo dhahabu! Alichokiona ni tofauti na alichokitarajia.

Kwa "madhahabu" yanayozalishwa Geita, alitarajia kukuta maskycraper ya maana, kumbe hakukuwepo hata na ghorofa lenye lifti.

Alitarajia kukuta maflyover mengi, lakini kumbe hata barabara zenye lami ni chache mno.

Alitegemea kukuta mji uliojengwa ukajengeka, matokeo yake alikuta kuna mpaka nyumba za nyasi.

Alifikiri, kama vile Almasi ilivyosaidia kuijenga Afrika Kusini, na dhahabu nayo itakuwa imeisaidia Geita kuwa jiji la kipekee sana.

Geita ina "madhahabu" mengi mno. Ni kati ya mikoa ambayo machimbo ya dhahabu yanaendelea kuibuliwa na raia wa kawaida. Si mara moja wala mbili, mtu amebadili "plan" ya kuchimba shimo la choo baada ya kukutana na mwamba wenye dhahabu, na kupelekea shimo lililokusudiwa kuwa la choo kugeuka kuwa mgodi wa dhahabu.

Takwimu za mwaka 2020 zinaonesha kuwa Geita, mkoa "mtajiri" wa dhahabu, unazidiwa na mkoa wa Lindi kwa utajiri. Sijui hilo limekaaje! Labda Wachumi watanisaidi.

Geita, mkoa "mtajiri" kiasi hicho, unakosaje kuwa na stendi ya kisasa?

Geita, mkoa "mtajiri" wa dhahabu, unapitwaje kwa utajiri na mkoa wa Iringa ambao Mhe. Dr. J. K. Msukuma aliuita ni mkoa wa walima nyanya?

"Nimepita" Iringa, na nimekaa kwa muda mkoani Geita. Naam, hata sasa ninapouandika huu uzi, nipo Mkoani Geita. Kwa mwonekano tu, Iringa panaonekana pameendelea sana ukipalinganisha na Geita.

Kwa nini Geita mkoa "mtajiri" siyo tajiri?
Kwa kuwa wewe mi mjanja kuliko wana Geita, njoo uchimbe utajirike uoneshe mfano.
 
Japo uzi una muda mrefu lakini hili ndiyo jawabu sahihi!.

Hii nchi kuna mikoa inanyonya rasilimali za maeneo mengine na kujisifu wana maendeleo huku mikoa inayotoa ikiwa kwenye hali mbaya

Mkoa wa Geita ukitoa hiyo highway ya Mwanza Bukoba hakuna barabara yoyote ya lami inayozidi 5km

Ukitaka kwenda mkoa wowote tofauti na Mwanza Musoma au Kagera unapita barabara ya Vumbi.
sera ya majimbo ya chadema ilikuwa na maana
 
Back
Top Bottom