Lord denning
JF-Expert Member
- Jun 3, 2015
- 15,819
- 33,255
JWTZ
Najua mnafahamu kuwa endapo lolote likitokea Uganda hata leo, Rais anayefuata wa Uganda ni Generali kichaa Muhoozi Kainerugaba.
Najua mnafaham kuwa Muhoozi na Mjomba wake Kagame wanaamini sana kwenye theory ya Expansionism! Kwa Kagame na Muhoozi maeneo ya Afrika Mashariki yanapaswa kuwa nchi moja (imaya moja) na wao kuwa Viongozi wa hiyo nchi.
Sote tunafaham, miaka ya hivi karibuni Kagame na Muhoozi wamekuwa wakiyaimarisha sana majeshi yao. Uimarishaji huu unaenda sambamba na kununua vifaa vya kisasa vya teknolojia ya Juu sana.
Taarifa zinasema kwenye ziara ambazo Kagame amekuwa akizifanya UAE, Uturuki na nchi zingine, amekuwa akinunua vifaa vya kisasa kwa ajili ya majeshi yake ikiwemo Drones, Makombora ya kutungulia ndege na Silaha nyingine za teknolojia mpya na za kisasa.
Wito wangu kwenu!
1. Kuanza sasa wekezeni heavily kwenye mafunzo ya kutumia silaha za kisasa za teknolojia mpya. Mf. Drones makombora ya kisasa na nyinginezo.
2. Kuanzia sasa wekezeni sana kwenye kununua silaha za kisasa za teknolojia mpya. Kuanzia Vifaru, Makombora, Ndegevita na hata Ndege zisizotumia rubani (UAV/Drones)
3. Imarisheni sana Kamandi yenu ya Wanamaji. Nadhani mmejifunza namna Rwanda na M23 walivyoingia Goma na Lubavu kupitia Ziwa Kivu. Kuna haja kubwa sasa kuwa na Kambi Kubwa za Kijeshi za Wanamaji kwenye Maziwa ya Victoria na Tanganyika. Kambi hizi ziwekewe vifaa vya kisasa na bora kabisa vya kivita na Wanajeshi wetu wapewe mafunzo bora kabisa kuhudumu kwenye silaha hizo.
4. Imarisheni sana Uhusiano na Mataifa yenye uwezo mkubwa wa kijeshi hasa Marekani na China. Ingawa mnafanya vizuri kwenye hili, ila ongezeni sana ushirikiano kwenye eneo hili. Pelekeni maofisa wengi kwenye mafunzo vyuo vya nje vya kijeshi wachukue utaalam na waje kuwafundisha wenzao.
5. Mwisho ingawa sio kwa umuhimu, wekezeni basi hata kwenye mavazi mazuri na nadhifu kwa wanajeshi wetu pamoja na other protective gears (Mabuti mazuri na viatu vizuri vya kiaskari). Hivi karibuni naona Askari wetu wanavaa nguo kuu kuu zilizochoka sana. Wafanyeni askari wetu wawe proud kuvaa nguo zao. Watengenezeeni nguo na mavazi mazuri ya kijeshi yanayowafanya sio tu wawe vizuri ila wapendeze na kuonekana askari nadhifu wanaojaliwa vizuri. Kwenye hili mjifunze kwa wenzenu wa Rwanda.
Najua mnafahamu kuwa endapo lolote likitokea Uganda hata leo, Rais anayefuata wa Uganda ni Generali kichaa Muhoozi Kainerugaba.
Najua mnafaham kuwa Muhoozi na Mjomba wake Kagame wanaamini sana kwenye theory ya Expansionism! Kwa Kagame na Muhoozi maeneo ya Afrika Mashariki yanapaswa kuwa nchi moja (imaya moja) na wao kuwa Viongozi wa hiyo nchi.
Sote tunafaham, miaka ya hivi karibuni Kagame na Muhoozi wamekuwa wakiyaimarisha sana majeshi yao. Uimarishaji huu unaenda sambamba na kununua vifaa vya kisasa vya teknolojia ya Juu sana.
Taarifa zinasema kwenye ziara ambazo Kagame amekuwa akizifanya UAE, Uturuki na nchi zingine, amekuwa akinunua vifaa vya kisasa kwa ajili ya majeshi yake ikiwemo Drones, Makombora ya kutungulia ndege na Silaha nyingine za teknolojia mpya na za kisasa.
Wito wangu kwenu!
1. Kuanza sasa wekezeni heavily kwenye mafunzo ya kutumia silaha za kisasa za teknolojia mpya. Mf. Drones makombora ya kisasa na nyinginezo.
2. Kuanzia sasa wekezeni sana kwenye kununua silaha za kisasa za teknolojia mpya. Kuanzia Vifaru, Makombora, Ndegevita na hata Ndege zisizotumia rubani (UAV/Drones)
3. Imarisheni sana Kamandi yenu ya Wanamaji. Nadhani mmejifunza namna Rwanda na M23 walivyoingia Goma na Lubavu kupitia Ziwa Kivu. Kuna haja kubwa sasa kuwa na Kambi Kubwa za Kijeshi za Wanamaji kwenye Maziwa ya Victoria na Tanganyika. Kambi hizi ziwekewe vifaa vya kisasa na bora kabisa vya kivita na Wanajeshi wetu wapewe mafunzo bora kabisa kuhudumu kwenye silaha hizo.
4. Imarisheni sana Uhusiano na Mataifa yenye uwezo mkubwa wa kijeshi hasa Marekani na China. Ingawa mnafanya vizuri kwenye hili, ila ongezeni sana ushirikiano kwenye eneo hili. Pelekeni maofisa wengi kwenye mafunzo vyuo vya nje vya kijeshi wachukue utaalam na waje kuwafundisha wenzao.
5. Mwisho ingawa sio kwa umuhimu, wekezeni basi hata kwenye mavazi mazuri na nadhifu kwa wanajeshi wetu pamoja na other protective gears (Mabuti mazuri na viatu vizuri vya kiaskari). Hivi karibuni naona Askari wetu wanavaa nguo kuu kuu zilizochoka sana. Wafanyeni askari wetu wawe proud kuvaa nguo zao. Watengenezeeni nguo na mavazi mazuri ya kijeshi yanayowafanya sio tu wawe vizuri ila wapendeze na kuonekana askari nadhifu wanaojaliwa vizuri. Kwenye hili mjifunze kwa wenzenu wa Rwanda.