Generation ya pili ya Mercedes Benz AMG GT 63 ni kali aisee!

Mad Max

JF-Expert Member
Joined
Oct 21, 2010
Posts
26,961
Reaction score
77,890
Hawa Mercedes Benz sio wa kuwachukulia kitoto. Sasa wametoa hii 2nd gen ya AMG GT (GT 63 to be specific) aisee ni kali. Usichanganye na SLS kwa leo.

Tukumbuke AMG GT ni coupe yenye arrangements ya seat 2+2.


Tukijirudisha nyuma mwaka 2014, hawa Benz ndio walianza kutoa 1st Gen za GT ambazo kwa wadau wa movie wameiona kwenye Justice League ambapo Batman alikua anampa lift The Flash.



Na wadau wa F1 wameiona kwenye Safety car mwaka 2015, 2016 na 2017 GP.

Sasa hawa jamaa wameiupgrade, ndani na nje hii 2nd gen.


Mbwle imekua aggressive, na aerodynamics imeimprove. Cheki hidden door handles izo.



Kwanza GT63 imepunguzwa ukubwa wa engine displacement, sasa hivi tuna 4.0L V8 twin turbo M177 engine, top speed 315 km/h, acc 3.2 sec from 0 to 100kph, ikiwa na 9 speed gear Auto (AMG speed shift) na ni AWD.



Kupunguza displacement haina maana wamepunguza horsepower, kwasababu sasa GT63 version ina horsepower 577.


Ndani wameimprove technology, kuanzia kwenye cluster gauge na infotainment screen.



Kama kawaida steering ina options kibao. Sema ndio ivyo wadau uwa mna mind tukisema gari lazima liwe na buttons za kutosha kwenye steeling.



Bei sio kali sana, $178,000/= najua matajiri hamshindwi.
 

Attachments

  • Mercedes-AMG_C192_1X7A0832.jpg
    311.4 KB · Views: 36
Hili la zamani alikuwa nalo jirani yangu wa next door. Aki li park tu nje nyumba inapanda heshima 🤣🤣🤣
 
Tafuta pesa dogo
 
Hivi ni kweli Mafuta yataacha kutumika kwenye magari hivi karibuni? nafikiri ni jambo la muda mrefu kidogo mpaka wakubwa waamue kwa nguvu zao.
Inawezekana maana hii inategemeana pakubwa na jinsi nchi za kiarabu ambao ni supplier wakubwa wa mafuta wana interract na USA maana alternatives zipo nyingi sana ila kwa sababu bado nchi za kiarabau zinamtumikia USA ili kujiendeleza kiuchumi in return USA anazidi pia kutajirika sioni kama itakuwa karibuni bado bado sana .

Imagine kuna mtu kama Stanley Mayer huyu jamaa alivumbua gari ambalo lilikuwa linauwezo wa kutumia maji kama chanzo cha nishati na by product ni oxygen gas wakati Hydrogen inatumika kufanya mlipuko(combustion) jamaa alitaka kuli patent taarifa ambazo hazikuwa nzuri kwa oil moguls ikabidi waongee na USA kuomba kikao na jamaa USA akatuma secret services wakamuita jamaa ku bagain na moguls
condition ya kwanza ilikuwa watamlipa awauzie uvumbuzi wake na waingie mkataba wa kutotengeneza tena kitu kama hicho jamaa akakataa , condition ya pili ilikuwa basi alitumie mwenyewe ila pia akakataa.

Baada ya hapo akawa anapewa vitisho sana na mara ya pili alipoitwa tena kwenye kikao ndiyo ikawa mwisho wake , alipewa sumu na alipokufa tu wasiojulikana wakajaa nyumbani kwake na kuchukia documents zote zinazohusu ubunifu wa jamaa pamoja na gari ila kaka yake akaipambania hadi ikarudishwa ili ibaki kama kumbukumbu ya mdogo wake.

Ukisoma articles nyingi mtandaoni utagundua kwamba maji kutumika kama nishati (ukiondoa kwenye kutengeneza mzunguko wa prime mover kwenye Hydro power plant) ni teknolojia ambayo ilishaanza kuwa perfected muda sana ila nadhani kwa sasa hawataki kuitumia maana haitowafaidisha wawekezaji wakubwa na USA kwa ujumla .
 

Attachments

  • images.jpeg
    49.6 KB · Views: 6
  • images-1.jpeg
    43.4 KB · Views: 10
  • images-3.jpeg
    46.9 KB · Views: 8
  • images-2.jpeg
    46.7 KB · Views: 11
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…