Gentleman. . .

Na mimi nimefurahi pia Mjuni Lwambo Ila hii ID umebadili ama?

Those were the good days!🥴

Hata sijui alipotelea wapi wifi yangu na vipenzi vyangu!!🥺
Hapana sijawahi kubadili ID. Huo mwaka 2012 ndio niliojoin, wewe hatujakutana sana jukwaani,

Ila nawakumbuka akina AshaDii, WomanOfSubstance, kitila na akina mukandara, wote hawa wameadimika, umebaki wewe tu na Kichuguu,

Labda na ndugu yangu Kiranga cha Ngeda Kandumbwa. Wakongwe wengi wametupa kisogo.
 
Owwkey!🙂

Kuna wengine wengi bado wanatamba jamvini kama kawaida!

Wasioonekana nadhani baadhi walibadili ID zao, wengine wamebaki kuwa wasomaji wa kimya kimya na wengine wamekimbia kabisa kwa sababu tofauti tofauti. 😕
 
Mkuu umeibuka?

Unamkumbuka Field Marshall ES, Sauti ya Umeme, anakwambia "no research, no right to speak" na "kumkoma nyani giladi" ?

Ukitaka kumpiga nyani usimuangalie usoni, itamuonea huruma.

RIP FM ES.

Unamkumbuka jamaa mmoja alikuwa anaitwa GAME THEORY ? Jamaa alikuwa ana mavitabu yote kama Profesa wa Harvard, akiwakuta mnabishana anawatumia mavitabu tu.

Ukiqnza mjadala wa Israel na Palestina kama huu wa sasa basi anakwambia "Umemsoma Edward Said katika "Orientalism" wewe? Umemsoma Albert Hourani katika "A History of The Arab Peoples" wewe?"

Kisha anakuwekea ma cover ya vitabu kibao mpaka unaanza kuvitafuta vingine.
 
Mdakuzi
...Couldn't have said it any better!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…