Mhe. Nabii GeorDavie ni mtumishi wa Mungu anaijua kazi yake, anajiamini, ni shujaa, anajitambua na anaielewa kazi yake, anamwakilisha Mungu ipasavyo, anamwelewa boss wake vizuri na hana mashaka naye! Hajali maneno wala haogopi vita kwa kuwa anamwelewa Mungu aliyemwita na kumtuma! Kama tujuavyo shetani ni mpinzani wetu hivyo kurusha makombora ni kitu cha kawaida! Maelfu ya watu yameshuhudia matendo makuu ya Mungu, mara nyingi shuhuda zimekuwa zikiwekwa kwenye Radio ya ya Ngurumo FM Hata hao wakina Channel na watumishi wote waliokengeuka kwa sababu zao wanazojizua walishuhudia, tena walikuwa hawamjui Mungu lakini wamefungua makanisa. Ikiwa wanakufuru matukufu ya Mungu na kusema ni Nguvu za giza je wao wanatumia nini na wamejifunzia pale. Tena channel alishuhudia na kusema upako huu ni mtaji kwangu! Wivu ni wa nini watu wa Mungu??? Mara ooh kuna mwanamke Alifunga macho na alipofungua akaona nyoka mara akafa.... Inaingia akilini???tunaomba kumjua huyo mwanamke ayelikufa na ushahidi....ni uongo wa ibilisi jamani nendeni mkajionee matukufu ya Mungu...shetani anaharibu kazi ya Mungu lakini ameshindwa.... Kazi ya Mungu inasonga mbele!!! Mnashangaa misafara na magari ya kifahari, Mungu ni tajiri atumie hata ndege za angani kumtukuza Mungu!!! Eti anaitwa mheshimiwa sasa kama mafisadi wanaitwa waheshimiwa vipi watumishi wa Mungu!!! Mimi ninasema GeorDavie amemwelewa Yesu na ndiye mtumishi anayemwakalisha Mungu ipasavyo, hivi mimi kama ninatembea peku na ninakuambia Mungu ni tajiri anaweza kukusaidia kiuchumi utanielewa kweli!!! unajua mtu ajionavyo ndivyo alivyo. Ukimwona Mungu unayemwamini hawezi kuponya, kwako kitu kama hicho kitabaki kuwa story, ukiona Mungu unayemwamini anamiliki mbinguni na kutawala duniani na mamlaka alishatupatia ndivyo itakavyokuwa kwako. Wengi hapa wamebaki kumuhukumu na kumkatisha tamaa kwa kazi anayoifanya, na kupakaza mambo ambayo hayana maana. Ila kwa muelewa inaonyesha wazi ni maadui, wivu, chuki kwani sielewi kwanini kinawauma sana. Kama kweli mnampenda Mungu na mnamjua Mungu kwanini msimwombee mnampiga vita yeye ni mwanadamu kama wanadamu wengine, Wengi walisema anatumia nguvu za giza wakafunga na kukemea na kuharibu ikaishia GeorDavie kuinuliwa nao wakashushwa! Mwacheni Mungu aitwe Mungu! Mungu akimpenda mtu na kumchagua afanye kazi yake atamtumia mpaka atakapomaliza haijalishi chochote! Yeye ndiye atakayemhukumu na wala sio mwanadamu! Mungu anaweza kumtumia mtu yeyote kwani anaangalia utayari wa mtu alionao, Kweli GeorDavie ni shujaa katika mashujaa otherwise angekuwa mtu wa kawaida katika vita zote alizopitia angekimbia na kumwaibisha Mungu!!! Lakini yeye anasonga mbele akicharaza mapepo!! Mungu anawapa watu karama tofauti, Na maandiko yako wazi, alisema wengine ni Manabii, mitume, wachungaji, waalimu na wainjilist kama yeye amepewa upako wa Kinabii wivu niwa nini wanadamu??? hamna jema. Mtumishi akitembea na Nguvu za Mungu mnasema hajaitwa, akiwa na nguvu za Mungu mnasema anatumia nguvu za giza lipi jema kwenu!!! Acheni kumnyoshea mtumishi wa Mungu kidogo, angekuwa hajatumwa tangu mmeanza kumpiga vita ametikisika??!! huduma imekufa??? kitu cha Kimungu hata upambane vipi huwezi kukiharibu!!! Hamtamweza Nabii huyu mpaka Mungu akamilishe kusudi lake aliloweka ndani yake!!! haijalishi punda amechafuka au amelowana lazima safari aimalize na kusudi la Mungu litimie! Lakini ole wake yule ambaye hakumsaidia punda kukamilisha kusudi la Mungu kwa wanadamu! je umehusika kufanya nini?? kumchafua, kumwangusha, ulimlisha, ulimtemea mate, ulimpaka marashi?? ulishiriki vipi kuhakikisha kazi ya Mungu inasonga mbele?? Mungu kumtumia mwanadamu hamaanishi ni malaika! Shida watu hawasomi maandiko na kuelewa neno la Mungu. Nchi yetu hii inanishangaza, kazi kupinga watumishi wa Mungu na kuwaombea mabaya huku wakiwainua watumia mizizi waliojaa udanganyiifu! Nabii akiwaambia huku siko wanakimbilia hawamtaki Yesu! sasa wanaanza kulalamika ooh tulidanganywa...Tafuteni uso wa Mungu wanadamu na kumwabudu yeye pekee dunia hii haina maana na ni ubatili mtupu!! Mwangalie GeorDavie amemwinua Yesu na Yesu akamwinua sasa mnatatanika!! kwakuwa mlijua waganga ndio wanaweza kutajirisha mara ooh ni mnaigeria!! Aibu kwetu! Mimi ninamwinua Mungu na Mungu wangu yuko juu na mimi niko juu! Nitasimulia habari zake nikiwa ndani ya Helikopta!!