King Kong III
JF-Expert Member
- Oct 15, 2010
- 56,205
- 79,515
Wewe msifie tu kisha weka namba tu kesho yake unatupiwa Q7.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Habarini za nyakati hizi wapendwa,
nimepata wasaa wa kufuatilia baadhi ya video za chaneli ya YouTube yake na nimekuwa nikiona akitoa hela kwa wasanii, waandishi wa habari mpaka magari.
Je, kuna injili ya kweli hapo au? Wanaomfahamu tafadhali taarifa zaidi tunaomba.
Mie na washikaji zangu watatu tuliwahi kuingia na kurekodi ktk studio ya pale majengo juu yeye ndie alikuwa studio engineer, namfahamu sana na alikuwa akipenda kutembea na gitaa (box guitar) mtaani.Huyu ndugu jina lake halisi ni George David Kasambale ni mwenyeji wa Singida mi nlianza kumfahamu miaka ya tisini alikuwa tarishi pale world vision, Arusha alikuwa pia mwanamziki wa nyimbo za injili ktk mikutano mbalimbali na alikuwa anasali ktk kanisa la Siloam Gospel Assembly lililokuwa linasali ktk shule ya msingi Uhuru Arusha.
Kwa kipindi hicho mi nlikuwa mwanafunzi wa primary tulikuwa tunamuita Nyakizanya kwa sababu ya wimbo wake maarufu ''Nyakizanya umeokoka'' ila alikuwa kijana wa kipindi kile na alikuwa ana mambo yake ya ujana ka kuvaa mabagi na kunyoa pushback kitu kilichomfanya asikubalike na wachungaji wengi wa kiroho hapa Arusha.
Si kumsikia tena hadi miaka ya kuanzia tisini na sita hivi alikuwa na studio ya nyimbo za injili iliyoitwa supreme na baadae ikawa radio station ila ilikuwa inasikika baadhi ya sehemu za Arusha. Ila kutokana na ujanja ujanja wake na ambitions yake aliweza kukutana na wazungu na kufungua kituo cha watoto wa mitaani ingawa alikuwa anao ka watano hivi wa kuzugia.
Kituo hichi kilikuwa majengo karibia na Sacon Opposite na kanisa la KKKT Burka, baadaye alihamia Kisongo baada ya kuwa na fedha, aliwaondoa wale watoto kwa namna mbaya sana mmojawapo ni rafiki yangu ni fundi TV, ndio ghafla tukasikia Nabii GeoRDavie, kanisa lake liko kisongo mnadani na ofisi zake ziko huko ktk mashamba yake maarufu ka ''mji wa Daudi'' kwa kweli huduma yake imejaa contrervasial saana maisha yake pia yana utata.
Means jinsi anavyiobehave pamoja na family life yake kwa ujumla watu wanaomfahamu tangu kitambo hawamuelewi. Ila hatuwezi kusema sana tusije tukakufuru ila kwa upande wangu mmhh.
Simkubali na hii ni kutokana na matunda yake yaani tabia huwezi kuwa na upako kiasi hicho afu matendo ni design ka yake ila sijui? Siwezi sema ni mtume wa Mungu au la ila kuna maswali mengi sana kuliko majibu.
FafanuaMimi lile jicho juu kwenye ghorofa yake lilinishtua Sana.
Angalia hapo vizuri utaona pembe tatu na jicho.Fafanua
Sasa hiyo ni hotel au nyumba yake ya kuishi?! Anyway kuna watu wanatumia nguvu za giza machoni pa watu bila kujulikana na wengine wanaamini ni watumishi wa Yesu Kristo.Angalia hapo vizuri utaona pembe tatu na jicho.View attachment 2435876
Ebwanainaonekana we ni ndugu yangu hatujuani. aliye vunjiwawa ndoa ni ndugu yangu sakina kibanda maziwa,saiv jama yetu ana mke mchungaji from kenya au sio mwanangu
Hukujifunza somo la mwandiko primary? Hata kuacha nafasi huwezi [emoji35][emoji35][emoji35][emoji35]Kitu kinachonishangaza ni vile watumishi wa Mungu wanasakamwa kila kona! Ni kama watu wote walioandika wana uadui na huyu mtu! Ina maana huyu jamaa hajawahi kufanya jema hata moja! Ni kama yeye kuwa Mtumishi wa Mungu kimekera sana watu. Yeye ni mwanadamu tu kwani yeye ni Mungu! Watumishi wote, Mungu anawatumia kama punda au lorry! hivyo yeye kuanguka au kusimama hakuwahusu! Ikiwa anamwakilisha Mungu, wagonjwa wanapona, Mapepo yanatimuka, wachawi wanatupa vibuyu, watu wanafanikiwa na Mungu anainuliwa shida iko wapi! Msimwangalie mtumishi mwangalieni Mungu! Shida watu hawaamini kama Mungu anaponya wamezoea waganga hivyo wamemweka Mungu chini na kumwinua shetani. Hivi shetani anaponya? Mapepo yangekimbia? wachawi wangejisalimisha? kwa kweli mimi ninatamani kumwona huyu jamaa kama kwa Jina la Yesu mambo makuu yanatokea huyu ndio mganga ninayemtaka kwani hakuna mganga kama Yesu Kristo. Nimemfuatilia sana huyu mtu ndio maana nimeandika yote haya! Mengi mliyoandika ni uongo mtupu, mpaka jina lake, ametokea wapi, cheo chake, mambo anayoyafanya, hilo limenihakikishia wengi hawamjui na wengi hapa ni maadui wanachafua kazi anayoifanya. Tangu lini adui yako akakusifia! au akakusema vizuri! Kama haumwamini achana naye! Acha wale wanaoamini wakamwabudu Mungu na kupokea miujiza yao. Kweli wivu ni mbaya mlitaka awagawie hizo sadaka? Jamani Mungu akimwinua mtu kubalini!!! Mnafikiri Mungu amelala haoni yeye??? angeacha watu wote wapotee?? tena kwa taarifa yenu lol! watu wamejaa full j2 nilienda kuchungulia na ndio kwanza wanazidi kwenda!!! Hawa watumishi wanaojiona wema na wananguvu za Mungu si waombe ache basi! Mwacheni komandoo wa Yesu apige kazi kama mmeshindwa kuruka kwa ungo mseme!!
Mambo vipi Joji Devidi KasambaleWajameni Mimi ninamfahamu Nabii GeorDavie vilivyo! Mimi ni mtumishi ninayempenda Yesu kupita maelezo na nimekombolewa kwa damu ya YESU!! Ninataka niwatoe duku duku zenu. Maswali yote niulizeni nitawajibu moja baada ya lingine! Ila kwa wale wenye chuki binafsi, wivu na waongo na wale wanaoamini shetani ana nguvu kuliko Mungu nisingependa kupoteza muda! Ila wale wanaohitaji kweli kufahamu kwa kina kuhusu Mhe. Nabii GeorDavie niko tayari kuwaelezeni! Ninakaribisha maswali yenu. Imenishangaza sana jinsi mwanadamu anavyoweza kutunga uongo kisa tu ameona tunguri zake zikishindwa kufanya kazi. Wanadamu maisha haya yanapita tujipange sawasawa!
Kwema ndugu jo devie?Mhe. Nabii GeorDavie ni mtumishi wa Mungu. Anaijua kazi yake, anajiamini, ni shujaa, anajitambua na anaielewa kazi yake. Anamwakilisha Mungu ipasavyo. Anamwelewa boss wake vizuri na hana mashaka naye. Hajali maneno wala haogopi vita kwa kuwa anamwelewa Mungu aliyemwita na kumtuma. Kama tujuavyo shetani ni mpinzani wetu hivyo kurusha makombora ni kitu cha kawaida.
Maelfu ya watu yameshuhudia matendo makuu ya Mungu. Mara nyingi shuhuda zimekuwa zikiwekwa kwenye Radio ya ya Ngurumo FM Hata hao wakina Channel na watumishi wote waliokengeuka kwa sababu zao wanazojizua walishuhudia, tena walikuwa hawamjui Mungu lakini wamefungua makanisa. Ikiwa wanakufuru matukufu ya Mungu na kusema ni Nguvu za giza je wao wanatumia nini na wamejifunzia pale.
Tena channel alishuhudia na kusema upako huu ni mtaji kwangu! Wivu ni wa nini watu wa Mungu??? Mara ooh kuna mwanamke Alifunga macho na alipofungua akaona nyoka mara akafa.... Inaingia akilini??? Tunaomba kumjua huyo mwanamke ayelikufa na ushahidi....ni uongo wa ibilisi jamani nendeni mkajionee matukufu ya Mungu...shetani anaharibu kazi ya Mungu lakini ameshindwa.... Kazi ya Mungu inasonga mbele!!!
Mnashangaa misafara na magari ya kifahari, Mungu ni tajiri atumie hata ndege za angani kumtukuza Mungu!!! Eti anaitwa mheshimiwa sasa kama mafisadi wanaitwa waheshimiwa vipi watumishi wa Mungu!!! Mimi ninasema GeorDavie amemwelewa Yesu na ndiye mtumishi anayemwakalisha Mungu ipasavyo. Hivi mimi kama ninatembea peku na ninakuambia Mungu ni tajiri anaweza kukusaidia kiuchumi utanielewa kweli!!! unajua mtu ajionavyo ndivyo alivyo.
Ukimwona Mungu unayemwamini hawezi kuponya, kwako kitu kama hicho kitabaki kuwa story, ukiona Mungu unayemwamini anatawala mbinguni na kumiliki duniani na mamlaka alishatupatia ndivyo itakavyokuwa kwako. Wengi hapa wamebaki kumuhukumu na kumkatisha tamaa kwa kazi anayoifanya, na kupakaza mambo ambayo hayana maana. Ila kwa muelewa inaonyesha wazi ni maadui, wivu, chuki kwani sielewi kwanini kinawauma sana.
Kama kweli mnampenda Mungu na mnamjua Mungu kwanini msimwombee mnampiga vita yeye ni mwanadamu kama wanadamu wengine. Wengi walisema anatumia nguvu za giza wakafunga na kukemea na kuharibu ikaishia GeorDavie kuinuliwa nao wakashushwa! Mwacheni Mungu aitwe Mungu! Mungu akimpenda mtu na kumchagua afanye kazi yake atamtumia mpaka atakapomaliza haijalishi chochote!
Yeye ndiye atakayemhukumu na wala sio mwanadamu! Mungu anaweza kumtumia mtu yeyote kwani anaangalia utayari wa mtu alionao, Kweli GeorDavie ni shujaa katika mashujaa otherwise angekuwa mtu wa kawaida katika vita zote alizopitia angekimbia na kumwaibisha Mungu. Lakini yeye anasonga mbele akicharaza mapepo. Mungu anawapa watu karama tofauti, Na maandiko yako wazi, alisema wengine ni Manabii,
mitume, wachungaji, waalimu na wainjilist kama yeye amepewa upako wa Kinabii wivu niwa nini wanadamu??? hamna jema.
Mtumishi asipotembea na Nguvu za Mungu mnasema hajaitwa, akiwa na nguvu za Mungu mnasema anatumia nguvu za giza lipi jema kwenu! Acheni kumnyoshea mtumishi wa Mungu kidole, angekuwa hajatumwa tangu mmeanza kumpiga vita ametikisika??!! Huduma imekufa???
Kitu cha Kimungu hata upambane vipi huwezi kukiharibu! Hamtamweza Nabii huyu mpaka Mungu akamilishe kusudi lake aliloweka ndani yake. Haijalishi punda amechafuka au amelowana lazima safari aimalize na kusudi la Mungu litimie! Lakini ole wake yule ambaye hakumsaidia punda kukamilisha kusudi la Mungu kwa wanadamu! je umehusika kufanya nini?? kumchafua, kumwangusha, ulimlisha, ulimtemea mate, ulimpaka marashi?? ulishiriki vipi kuhakikisha kazi ya Mungu inasonga mbele??
Mungu kumtumia mwanadamu hamaanishi ni malaika! Shida watu hawasomi maandiko na kuelewa neno la Mungu. Nchi yetu hii inanishangaza, kazi kupinga watumishi wa Mungu na kuwaombea mabaya huku wakiwainua watumia mizizi waliojaa udanganyiifu! Nabii akiwaambia huko siko wanakimbilia hawamtaki Yesu! sasa wanaanza kulalamika ooh tulidanganywa...Tafuteni uso wa Mungu wanadamu na kumwabudu yeye pekee dunia hiini ubatili mtupu.
Ikulu? Kweli imanii ni kitu chengine kabisaWw ndo husikiki,yupo Ariusha Kisongo,ukitaka kuijua radio ya huduma inaitwa Ngurumo ya Upako Fm,na Ikulu yake iko Njiro..any question???na huduma yake Tawi la Dar ipo Kawe Tanganyika packers,Morogoro,Moshi,Babati,Mwanza..una swali lingine???
Tuondolee ujinga hapa(Al islam dinul hak)
Uislam ndio.dini ya ukweli...hakuna hizi propaganda zakudanganyana
Wajinga ndio waliwao...Yani kuna maskini wa hela...ila hawa wenzetu wa mlengo wapili ni maskini wa akili....manabiii na mutume hahahahaha huyo bado kugeuka kibwetele...na mtakufa bila kelele
Umeeleza vizur angalau nmemjua kidogoHuyu ndugu jina lake halisi ni George David Kasambale ni mwenyeji wa Singida mi nlianza kumfahamu miaka ya tisini alikuwa tarishi pale world vision, Arusha alikuwa pia mwanamziki wa nyimbo za injili ktk mikutano mbalimbali na alikuwa anasali ktk kanisa la Siloam Gospel Assembly lililokuwa linasali ktk shule ya msingi Uhuru Arusha.
Kwa kipindi hicho mi nlikuwa mwanafunzi wa primary tulikuwa tunamuita Nyakizanya kwa sababu ya wimbo wake maarufu ''Nyakizanya umeokoka'' ila alikuwa kijana wa kipindi kile na alikuwa ana mambo yake ya ujana ka kuvaa mabagi na kunyoa pushback kitu kilichomfanya asikubalike na wachungaji wengi wa kiroho hapa Arusha.
Si kumsikia tena hadi miaka ya kuanzia tisini na sita hivi alikuwa na studio ya nyimbo za injili iliyoitwa supreme na baadae ikawa radio station ila ilikuwa inasikika baadhi ya sehemu za Arusha. Ila kutokana na ujanja ujanja wake na ambitions yake aliweza kukutana na wazungu na kufungua kituo cha watoto wa mitaani ingawa alikuwa anao ka watano hivi wa kuzugia.
Kituo hichi kilikuwa majengo karibia na Sacon Opposite na kanisa la KKKT Burka, baadaye alihamia Kisongo baada ya kuwa na fedha, aliwaondoa wale watoto kwa namna mbaya sana mmojawapo ni rafiki yangu ni fundi TV, ndio ghafla tukasikia Nabii GeoRDavie, kanisa lake liko kisongo mnadani na ofisi zake ziko huko ktk mashamba yake maarufu ka ''mji wa Daudi'' kwa kweli huduma yake imejaa contrervasial saana maisha yake pia yana utata.
Means jinsi anavyiobehave pamoja na family life yake kwa ujumla watu wanaomfahamu tangu kitambo hawamuelewi. Ila hatuwezi kusema sana tusije tukakufuru ila kwa upande wangu mmhh.
Simkubali na hii ni kutokana na matunda yake yaani tabia huwezi kuwa na upako kiasi hicho afu matendo ni design ka yake ila sijui? Siwezi sema ni mtume wa Mungu au la ila kuna maswali mengi sana kuliko majibu.
Ukitaka kukosana na Mheshimiwa,Mtukufu,Nabii Mkuu,Askofu Mkuu Dr George David Kassambale mwite Kassambale George.Ni shemeji yangu, mdogo wake wa kiume amezaa na dada yangu..
Mdogo wake Yona David Kasambale sasa ni marehemu.
Hawezi kumaindi hata kidogo.Ukitaka kukosana na Mheshimiwa,Mtukufu,Nabii Mkuu,Askofu Mkuu Dr George David Kassambale mwite Kassambale George.
Laana itakuwa juu yako milele na milele.