George Job: Al Ahly ni unga

George Job: Al Ahly ni unga

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Simba na Al Ahly zimetolewa kwenye mashindano ya African Football League (AFL) bila kushinda mechi hata moja. Baada ya Simba kushindwa kuifunga Al Ahly hata baada ya kutangulia kuifunga, mchambuzi wa michezo, Bw. George Job alisema Al Ahly imeshuka kiwango (unga) ndio maana alishindwa kuifunga Simba mbovu pia. Alisema kama simba ingekuwa nzuri ingeitoa Al Ahly (mbovu msimu huu) kwenye mashindano.

Baada ya kusema hivyo, wachambuzi wenzake walimjia juu na kusema anaikosea heshima Simba, wakimaanisha kuwa Simba bora imetoka sare Al Ahly bora. Lakini Al Ahly kutupwa nje ya mashindano ya AFL pia kunasadifu uchambuzi wa Mr. Job kuwa Al Ahly msimu huu imeshuka kiwango, imeshindwa kupata matokeo hata kwenye uwanja wake wa nyumbani tofauti na zamani.

Tumpe Job maua yake kwenye football, Simba msimu huu haina timu ya kushindana kimataifa.
 
Wafilipi 2:3
Msitende neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake
 
Simba na Al-Ahly zimetolewa kwenye mashindano ya African Football League (AFL) bila kushinda mechi hata moja. Baada ya Simba kushindwa kuifunga Al-Ahly hata baada ya kutangulia kuifunga, mchambuzi wa michezo, Bw. George Job alisema Al-Ahly imeshuka kiwango (unga) ndio maana alishindwa kuifunga Simba mbovu pia. Alisema kama simba ingekuwa nzuri ingeitoa Al-Ahly (mbovu msimu huu) kwenye mashindano. Baada ya kusema hivyo, wachambuzi wenzake walimjia juu na kusema anaikosea heshima Simba, wakimaanisha kuwa Simba bora imetoka sare Al-Ahly bora. Lakini Al-Ahly kutupwa nje ya mashindano ya AFL pia kunasadifu uchambuzi wa Mr. Job kuwa Al-Ahly msimu huu imeshuka kiwango, imeshindwa kupata matokeo hata kwenye uwanja wake wa nyumbani tofauti na zamani.

Tumpe Job maua yake kwenye football, Simba msimu huu haina timu ya kushindana kimataifa.
Katika CAF CL msimu uliopita wa 2022/2023, Ahly na Mamelodi walikuwa katika group moja, na Al Ahly alipoteza kwa Mamelodi 5-2 mechi ya kwanza na wakatoa sare ya 2-2 mechi ya pili, lakini wote wakaingia robo fainali. Huko mbele Mamelodi akaishia nusu fainali na Al Ahly akachukua ubingwa. Je, hapo nani ni unga, aliyeshindwa kupata ushindi walipokutana wenyewe kwa wenyewe ila akachukua ubingwa AU aliyepata ushindi walipokutana wenyewe kwa wenyewe ila akatolewa nusu fainali?
 
Wakati tukifikiria Al ahly ameshuka kiwango ukweli ni kuwa timu zimepanda viwango sana, mpira umebadilika sana hivyo kupanda ubora Kwa timu imefanya watu kuona kama Al ahly ameshuka ila Wala hajashuka kiwango kihivyo kama wengi wanavyofikiri, timu pinzani zimewaoutsmart tu,timu inayojichukulia ubingwa wa afrika kama wa kwake haiwez kushuka kama inavyodhaniwa,
 
Katika CAF CL msimu uliopita wa 2022/2023, Ahly na Mamelodi walikuwa katika group moja, na Al Ahly alipoteza kwa Mamelodi 5-2 mechi ya kwanza na wakatoa sare ya 2-2 mechi ya pili, lakini wote wakaingia robo fainali. Huko mbele Mamelodi akaishia nusu fainali na Al Ahly akachukua ubingwa. Je, hapo nani ni unga, aliyeshindwa kupata ushindi walipokutana wenyewe kwa wenyewe ila akachukua ubingwa AU aliyepata ushindi walipokutana wenyewe kwa wenyewe ila akatolewa nusu fainali?
Inazungumziwa mechi za msimu huu na sio msimu uliopita.

Binafsi kwa mtazamo wangu, naona safu ya umaliziaji ya Al Ahly ndio yenye shida msimu huu, sielewi wameshuka viwango au kuna mgomo au kuna nini.

Al Ahly imekutana na mitihani mitatu msimu huu, na mitihani yote imemshinda kuondoka na ushindi na ukiangalia namna ya uchezaji ni kwamba wanatengeneza nafasi nyingi sana ila zinapotea bure mpaka mtu unajiuliza hii ndio safu ya ushambuliaji ambayo imetumika mabilioni ya pesa kuwanasa.

Mechi dhidi ya USMA hakushinda
Dhidi ya Simba mechi mbili hakushinda
Dhidi ya Mamelod mechi mbili hakushinda
Mechi tano msimu huu pasipo ushindi.

Kama hili jambo litawekwa sawa, sidhani kama kuna timu inaweza furukuta kwa hawa waarabu. Ila kama ndio hali ndio itakuwa hivyo hivyo basi watakuwa na msimu mgumu safari hii.
 
Wafilipi 2:3
Msitende neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake
Nimeshangaa kwa mara kwanza leo hujatukana. Hii imekuwa ajabu kabisa. Maana hoja zako zote ni matusi
 
Simba na Al-Ahly zimetolewa kwenye mashindano ya African Football League (AFL) bila kushinda mechi hata moja. Baada ya Simba kushindwa kuifunga Al-Ahly hata baada ya kutangulia kuifunga, mchambuzi wa michezo, Bw. George Job alisema Al-Ahly imeshuka kiwango (unga) ndio maana alishindwa kuifunga Simba mbovu pia. Alisema kama simba ingekuwa nzuri ingeitoa Al-Ahly (mbovu msimu huu) kwenye mashindano. Baada ya kusema hivyo, wachambuzi wenzake walimjia juu na kusema anaikosea heshima Simba, wakimaanisha kuwa Simba bora imetoka sare Al-Ahly bora. Lakini Al-Ahly kutupwa nje ya mashindano ya AFL pia kunasadifu uchambuzi wa Mr. Job kuwa Al-Ahly msimu huu imeshuka kiwango, imeshindwa kupata matokeo hata kwenye uwanja wake wa nyumbani tofauti na zamani.

Tumpe Job maua yake kwenye football, Simba msimu huu haina timu ya kushindana kimataifa.
Ahly pale kwa madiba huwa anachezea za kutosha mno, this time alifungwa 1-0,
Ahly kwa mamelodi hata pale Cairo huwa anaitafuta sare kwa tochi, ila this time mamelodi ndio kaitafuta sare kwa tochi,

kama Ahly kiwango kimeshuka, basi hata Mamelodi pia kimeshuka......

wakati flani watanzania tujifunze kujikubali, na kuzikubali juhudi za watanzania wenzetu....... Simba hii sio mbovu ila ni ngumu mno kufungika, yani kuifunga hii simba goli zaidi ya 2 ufanye kazi ya ziada sana.......

anyway ndio watanzania wenzetu
 
Al Ahly imekutana na mitihani mitatu msimu huu, na mitihani yote imemshinda kuondoka na ushindi
Mechi dhidi ya USMA hakushinda
Dhidi ya Simba mechi mbili hakushinda
Dhidi ya Mamelod mechi mbili hakushinda

Mechi tano msimu huu pasipo ushindi.
Katikati ya mechi dhidi ya USMA na Simba, Ahly alitoka kuzishinda mechi tano mfululizo dhidi ya Al Masry (4-0), Saint George (0-3), Saint George (4-0), ENPPI (3-0) na Ismailiy (3-1)

NB: Ili kutoa tafsiri sahihi, si vizuri kuonyesha mechi alizoshindwa kupata ushindi tu na kuzificha ambazo alishinda
 
Inazungumziwa mechi za msimu huu na sio msimu uliopita.

Binafsi kwa mtazamo wangu, naona safu ya umaliziaji ya Al Ahly ndio yenye shida msimu huu, sielewi wameshuka viwango au kuna mgomo au kuna nini.

Al Ahly imekutana na mitihani mitatu msimu huu, na mitihani yote imemshinda kuondoka na ushindi na ukiangalia namna ya uchezaji ni kwamba wanatengeneza nafasi nyingi sana ila zinapotea bure mpaka mtu unajiuliza hii ndio safu ya ushambuliaji ambayo imetumika mabilioni ya pesa kuwanasa.

Mechi dhidi ya USMA hakushinda
Dhidi ya Simba mechi mbili hakushinda
Dhidi ya Mamelod mechi mbili hakushinda
Mechi tano msimu huu pasipo ushindi.

Kama hili jambo litawekwa sawa, sidhani kama kuna timu inaweza furukuta kwa hawa waarabu. Ila kama ndio hali ndio itakuwa hivyo hivyo basi watakuwa na msimu mgumu safari hii.
kwanini usiwapongeze simba, usm na mamelodi kwa ubora wa defence zao?....

ahly pale egypt katupia magoli mechi zote za ligi alizocheza, tena goli zaidi ya 1, kwenye CL kampiga mtu 7-0 agg,.......

kwa simba akatupia goli 2 kwa mkapa (a record), na 1 kwao...jumla 3, kwanini asipongezwe simba aliyetoka nae 3-3? hapo hapo mnasema safu ya ushambuliaji ya simba mbovu....!

ukiangalia kwa makini ni kwamba ahly bado ni bora, ana defence bora ndio mana kafungwa 1-0 na mamelodi, ana offense bora ndio mana katupia 3 dhidi ya simba
 
Katika CAF CL msimu uliopita wa 2022/2023, Ahly na Mamelodi walikuwa katika group moja, na Al Ahly alipoteza kwa Mamelodi 5-2 mechi ya kwanza na wakatoa sare ya 2-2 mechi ya pili, lakini wote wakaingia robo fainali. Huko mbele Mamelodi akaishia nusu fainali na Al Ahly akachukua ubingwa. Je, hapo nani ni unga, aliyeshindwa kupata ushindi walipokutana wenyewe kwa wenyewe ila akachukua ubingwa AU aliyepata ushindi walipokutana wenyewe kwa wenyewe ila akatolewa nusu fainali?
Huo ni msimu uliopita, timu zimesajili upya makocha na wachezaji wapya na wengine wameondoka. Tunaongelea msimu huu kuwa Al-Ahly ni unga kutokana na kushindwa kuifunga Simba na mamelod nje ndani.
 
Katika CAF CL msimu uliopita wa 2022/2023, Ahly na Mamelodi walikuwa katika group moja, na Al Ahly alipoteza kwa Mamelodi 5-2 mechi ya kwanza na wakatoa sare ya 2-2 mechi ya pili, lakini wote wakaingia robo fainali. Huko mbele Mamelodi akaishia nusu fainali na Al Ahly akachukua ubingwa. Je, hapo nani ni unga, aliyeshindwa kupata ushindi walipokutana wenyewe kwa wenyewe ila akachukua ubingwa AU aliyepata ushindi walipokutana wenyewe kwa wenyewe ila akatolewa nusu fainali?
Umeambiwa msimu huu sio msimu uliopita Mkuu
 
Katika CAF CL msimu uliopita wa 2022/2023, Ahly na Mamelodi walikuwa katika group moja, na Al Ahly alipoteza kwa Mamelodi 5-2 mechi ya kwanza na wakatoa sare ya 2-2 mechi ya pili, lakini wote wakaingia robo fainali. Huko mbele Mamelodi akaishia nusu fainali na Al Ahly akachukua ubingwa. Je, hapo nani ni unga, aliyeshindwa kupata ushindi walipokutana wenyewe kwa wenyewe ila akachukua ubingwa AU aliyepata ushindi walipokutana wenyewe kwa wenyewe ila akatolewa nusu fainali?
Ila Mamelodi watamuwezea Al Ahly, pia wako njema.
 
Katikati ya mechi dhidi ya USMA na Simba, Ahly alitoka kuzishinda mechi tano mfululizo dhidi ya Al Masry (4-0), Saint George (0-3), Saint George (4-0), ENPPI (3-0) na Ismailiy (3-1)

NB: Ili kutoa tafsiri sahihi, si vizuri kuonyesha mechi alizoshindwa kupata ushindi tu na kuzificha ambazo alishinda

Mechi tano nilizoongelea ni za CAF msimu huu sijazungumzia mechi za ligi yao.
Al Ahly kacheza mechi ngapi za CAF msimu huu?
Kashinda mechi ngapi?
Je St George ni kipimo cha timu ngumu?
 
kwanini usiwapongeze simba, usm na mamelodi kwa ubora wa defence zao?....

ahly pale egypt katupia magoli mechi zote za ligi alizocheza, tena goli zaidi ya 1, kwenye CL kampiga mtu 7-0 agg,.......

kwa simba akatupia goli 2 kwa mkapa (a record), na 1 kwao...jumla 3, kwanini asipongezwe simba aliyetoka nae 3-3? hapo hapo mnasema safu ya ushambuliaji ya simba mbovu....!

ukiangalia kwa makini ni kwamba ahly bado ni bora, ana defence bora ndio mana kafungwa 1-0 na mamelodi, ana offense bora ndio mana katupia 3 dhidi ya simba

Mpira uliangalia? Katika mpira kuna muda unatakiwa uipongeze safu ya ulinzi kama wanafanya blocking kuzuia on target ama kipa anapofanya saving. Lakini katika mechi zote tano Al Ahly wachezaji wao wameonesha hawana utulivu golini kwa kushindwa kuzitumia nafasi za wazi
 
Back
Top Bottom