George Mpole endelea kubaki Geita Gold, hutajutia

George Mpole endelea kubaki Geita Gold, hutajutia

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Mwanangu George Mpole hongera sana kwa kuonyesha juhudi uwanjani katikati ya ligi iliyojaa wageni wengi, juhudi zako zinatamanisha wapenda soka wote duniani. Lakini lakini lakini bado unahitaji kuonekana tena tena kwa wadau wa mpira ukirudia kukifanya hiki ulichokifanya kwenye msimu huu ili kuwaaminisha wadau kuwa hivyo ndivyo ulivyo na sio mambo ya chance (bahati). Yaani watu wenye hela zao wananunua kipaji, juhudi, maarifa na nidhamu ndani na nje ya kiwanja. Na ili kuthibitisha kuwa unavyo hivyo vitu 4 kuna vitu wanaviangalia, kwa kimombo wanaviita precision, validity na specificity, KIFUPI wanaangalia consistence kwenye kufunga katika mazingira tofautitofauti ya mechi, aina ya wachezaji kwenye mechi, hali ya hewa, ukiwa na furaha, ukiwa na huzuni, nk. Hivyo lazima ubaki kwenye timu ambayo itakufanya ucheze mechi nyingi sana ili wadau wapate wasaa wa kutosha wa kukuangalia tena na tena na tena. Sehemu hiyo sio Simba na Yanga, lahsha.

Simba na Yanga ni timu ambazo hazina uvumilivu hata kidogo, zinataka matokeo leoleo. Ni timu ambazo zinasajili wachezaji wengi kutoka ligi nyinge kwa lengo la kupata matokeo viwanjani leoleo, hivyo kama utacheza mechi 3 mfululizo bila kufunga bao hawatakuvumila, utakaa benchi na kupisha wachezaji wenye majina yao na wanaolipwa pesa nyingi sana. Hivyo utarudi nyuma badala ya kwenda mbele. Kumbuka mle msemo maarufu wa makocha usemao "The wining team never change" kikosi kinachoshida uwanjani hakibadilishwi, hawataki kujaribu kumpunzisha mchezaji mwenye uhakika wa kufunga eti kwasababu ya kukupatia wewe uzoefu.

Kama malengo yako ni kupata hela kuliko unazopewa Geita Gold basi nenda Yanga na Simba, lakini kama malengo yako ni kupata hela nyingi zaidi kuliko utakazopewa na Yanga na Simba basi endelea kubaki Geita au kwenye timu nyingine ya kati angalau kwa msimu mwingine mmoja wa kucheza kikamilifu.

Tumia makosa ya wengine (Ayee, Yusufu Mhilu, Ali Yusufu, Waziri Juma, Adam Adam, Salamba, Raphael, Nkane, Ambundo, Ngushi, Ndemla.....) ambao walitoka kwao wakiwa heros na kuishia kuwa zeros walipofika Simba na Yanga.
 
Mwanangu George Mpole hongera sana kwa kuonyesha juhudi uwanjani katikati ya ligi iliyojaa wageni wengi, juhudi zako zinatamanisha wapenda soka wote duniani...
acha ujinga[emoji12][emoji12][emoji12][emoji12][emoji12][emoji12]
 
makollo watakubalia na hili wazzo lako kweli. kwa maana wao ndiyo wahalibifuu vya talents za wachezaji wazawa!
 
makollo watakubalia na hili wazzo lako kweli. kwa maana wao ndiyo wahalibifuu vya talents za wachezaji wazawa!
Waziri Juma "shemtembo" alikimbilia Yanga baada ya kung'ara kwenye msimu mmoja huko atokako, akaja kuishia kapuni. Hata akina Bocco hawakimbilia Simba na Yanga, alikuja wakiwa wamekomaa kabisa ndio wakapata nafasi. Huyu George Mpole atafanya kosa kubwa sana kama ataikimbia Geita Gold kwa kudanganywa na ufungaji bora wake kwenye msimu, hata huko timu ya taifa kwenyewe haja fanya ya kutosha.

Simuonei gere, lakini anaekwambia usikombe mboga anataka ushibe. Simba na Yanga hakuna mchezo, muulize Ndemla, Muhilu, chikwende, Yipe, shemtembo, Buswita
 
Mpira ni ajira na maisha kama zilivyo kazi zingine,sio mambo yakufurahisha watu au kujipatia maujiko.Nchi yetu bado haina uwekezaji wa maana kwenye ngazi ya vilabu vya mikoani kwahiyo kama kuna mchezaji anaweza kupata nafasi yakucheza simba au yanga akatengeneza maisha yake mapema ni vyema akafanya hivyo.Ni yanga na simba peke yake ndipo kwenye mfereji wa mafanikio kwa mchezaji,ikiwa ana ndoto zakua na maisha bora au kufika mbali kisoka.Ushauri wako umekaa kufurahisha watu zaidi badala yakumsaidia kimaisha.Soka halina guerentee,anaweza akakataa ofa nzuri leo then kesho akawa majeruhi kisha akapotea kabisa.Mpole awaze maisha sio kufurahisha watu,soka ni kazi soka ni maisha ya kesho hayajulikani.
 
Kweli ushauri murua kabisa..Anaweza kusaini Simba akabaki benchi tukamsahau
Unataka umkumbuke uku akiwa maskini.Huu sio muda wakuishi kwakuangalia unapata sifa kiasi gani kwa watu.Anatakiwa aangalie maisha.Ajifunze kwa kaka zake walioimbwa sana wakaondoka kwenye soka wakiwa hawana kitu.inawezekana huu msimu ndo msimu wake pekee nyota kung'aa na ndo msimu wakujenga maisha yake ya badae.Mimi naamini ikija ofa nzuri ataitumia kwa busara.
 
Waziri Juma "shemtembo" alikimbilia Yanga baada ya kung'ara kwenye msimu mmoja huko atokako, akaja kuishia kapuni. Hata akina Bocco hawakimbilia Simba na Yanga, alikuja wakiwa wamekomaa kabisa ndio wakapata nafasi. Huyu George Mpole atafanya kosa kubwa sana kama ataikimbia Geita Gold kwa kudanganywa na ufungaji bora wake kwenye msimu, hata huko timu ya taifa kwenyewe haja fanya ya kutosha.

Simuonei gere, lakini anaekwambia usikombe mboga anataka ushibe. Simba na Yanga hakuna mchezo, muulize Ndemla, Muhilu, chikwende, Yipe, shemtembo, Buswita
Tusiishi kwa kukariri maisha ya watu.mimi naamini wachezaji wote duniani wanatafuta kwanza maslahi bora,swala la kucheza ilo ni jambo jingine kutokana na mipango ya mwalimu,ndo maana wachezaji wanauzwa timu mbalimbali.cha msingi ni kuangalia je maisha yake yatakuaje.Hao wachezaji uliowataja sidhani kama walivyoachwa simba na yanga walirudi majumbani kwao bila kutafuta timu zingine zakucheza ila pia sidhani kama waliondoka kama walivyokuja.Lazima kuna kitu walikiongeza.
 
Unataka umkumbuke uku akiwa maskini.Huu sio muda wakuishi kwakuangalia unapata sifa kiasi gani kwa watu.Anatakiwa aangalie maisha.Ajifunze kwa kaka zake walioimbwa sana wakaondoka kwenye soka wakiwa hawana kitu.inawezekana huu msimu ndo msimu wake pekee nyota kung'aa na ndo msimu wakujenga maisha yake ya badae.Mimi naamini ikija ofa nzuri ataitumia kwa busara.
Haya ndio mane o. Watu wanaweka million mia mezani na mshahara wa million nne unauachaje. Chukua chako mapema. Unaweza baki geita na usiwe na msimu bora.
Kama yeye ni quality anaweza enda yanga au simba na bado aka perform.
Kinachowamaliza wachezaji wakija mujini ni mbususu tuu kwa asilimia kubwa basi.
 
Kama uwezo anao kwanini asiende timu kubwa ili kuthibitisha uwezo wake?

Unaleta mawazo mgando ya kumdumaza mchezaji, muache akapambane na waliokomaa kama tayari ameweza kuwa mfungaji bora mbele yao.

Football ni mchezo wa muda mfupi sana, kuna injury na mengine, muache akajitafutie riziki yake penye malisho mema mapema akiwa bado mwenye nguvu.
 
Mwanangu George Mpole hongera sana kwa kuonyesha juhudi uwanjani katikati ya ligi iliyojaa wageni wengi, juhudi zako zinatamanisha wapenda soka wote duniani. Lakini lakini lakini bado unahitaji kuonekana tena tena kwa wadau wa mpira ukirudia kukifanya hiki ulichokifanya kwenye msimu huu ili kuwaaminisha wadau kuwa hivyo ndivyo ulivyo na sio mambo ya chance (bahati). Yaani watu wenye hela zao wananunua kipaji, juhudi, maarifa na nidhamu ndani na nje ya kiwanja. Na ili kuthibitisha kuwa unavyo hivyo vitu 4 kuna vitu wanaviangalia, kwa kimombo wanaviita precision, validity na specificity, KIFUPI wanaangalia consistence kwenye kufunga katika mazingira tofautitofauti ya mechi, aina ya wachezaji kwenye mechi, hali ya hewa, ukiwa na furaha, ukiwa na huzuni, nk. Hivyo lazima ubaki kwenye timu ambayo itakufanya ucheze mechi nyingi sana ili wadau wapate wasaa wa kutosha wa kukuangalia tena na tena na tena. Sehemu hiyo sio Simba na Yanga, lahsha.

Simba na Yanga ni timu ambazo hazina uvumilivu hata kidogo, zinataka matokeo leoleo. Ni timu ambazo zinasajili wachezaji wengi kutoka ligi nyinge kwa lengo la kupata matokeo viwanjani leoleo, hivyo kama utacheza mechi 3 mfululizo bila kufunga bao hawatakuvumila, utakaa benchi na kupisha wachezaji wenye majina yao na wanaolipwa pesa nyingi sana. Hivyo utarudi nyuma badala ya kwenda mbele. Kumbuka mle msemo maarufu wa makocha usemao "The wining team never change" kikosi kinachoshida uwanjani hakibadilishwi, hawataki kujaribu kumpunzisha mchezaji mwenye uhakika wa kufunga eti kwasababu ya kukupatia wewe uzoefu.

Kama malengo yako ni kupata hela kuliko unazopewa Geita Gold basi nenda Yanga na Simba, lakini kama malengo yako ni kupata hela nyingi zaidi kuliko utakazopewa na Yanga na Simba basi endelea kubaki Geita au kwenye timu nyingine ya kati angalau kwa msimu mwingine mmoja wa kucheza kikamilifu.

Tumia makosa ya wengine (Ayee, Yusufu Mhilu, Ali Yusufu, Waziri Juma, Adam Adam, Salamba, Raphael, Nkane, Ambundo, Ngushi, Ndemla.....) ambao walitoka kwao wakiwa heros na kuishia kuwa zeros walipofika Simba na Yanga.
Yaan kama Mpole kamshinda Manywele kwann acje Simba? Acha wivu mwanajangwani
 
Mimi nadhani akipata maslahi mazuri Azam, Kagera sugar au Namungo aende ila sio Simba wala Yanga...atasugua tu benchi apoteze makali.
 
Kati ya timu zote 3 kubwa zenye maslahi yenye unafuu, asijaribu kabisa kwenda simba au Azam! Akienda Yanga atacheza na kuendelea kufunga mengi zaidi. Ni bidii yake tu ya kumshawishi mwalimu Nabi, kama walivyofanya wenzake akina Sure Boy, nk.

Ila siyo simba ambayo kwa sasa haichezi kitimu! Isipokuwa uwezo wa mchezaji mmoja mmoja ndiyo unao amua matokeo. Akienda Azam, ataenda tu kuota kitambi! na kuishia kucheza kifather father. Azam kunawafaa wachrzaji wavivu kama Ibrahim Ajibu.
 
Ajifunze kwa ditram nchimbi
Huwezi kumfananisha Ditram Nchimbi na George Mpole. Labda ungemfananisha na Kibu Denis! Maana wote wanapenda kutumia muda wao mwingi kukimbia kimbia tu uwanjani. Ditram Nchimbi alipata nafasi ya kucheza Yanga mara nyingi, lakini aliishia kufunga magoli 2 tu msimu mzima!

Mpole akienda timu kama Yanga, ana uwezo wa kuingia moja kwa moja kwenye kikosi cha kwanza, na akafunga magoli. Kwa sababu aina ya mpira wanaocheza Yanga, wa uwepo wa viungo wengi wachezeshaji.
 
Back
Top Bottom