Geraruma: Sekta ya maji imefanya vizuri zaidi

Geraruma: Sekta ya maji imefanya vizuri zaidi

JUMA JUMA

JF-Expert Member
Joined
Jan 5, 2013
Posts
790
Reaction score
964
SEKTA YA MAJI IMEFANYA VIZURI ZAIDI - GERARUMA

Kiongozi wa mbio za mwenge Kitaifa, Sahili Geraruma amesema Kwa siku 195 Mwenge wa Uhuru umekagua na kuweka mawe ya msingi na kuzindua miradi ya Maendeleo 1293 yenye thamani ya Shilingi Bilioni 650.8

Geraruma amesema katika Sekta ambazo Mwenge wa uhuru umezifanyia kazi mwaka 2022 Sekta iliyofanya vizuri zaidi ni Sekta ya Maji

Geraruma amesema hayo katika Kilele cha Maadhimisho ya Mbio za Mwenge katika uwanja wa Kaitaba Bukoba Mjini Mkoani Kagera leo tarehe 14 Oktoba 2022

"Maji yanapatikana, Fedha zilizowekezwa Katika Sekta hiyo thamani yake inaonekana, Taratibu za manunuzi na mauzo zinafuatwa, nyaraka za utekelezaji wa miradi ya maji zinahifadhiwa vizuri watendaji wake wanatimiza wajibu wao wananchi wanashirikiana wanaridhika na huduma ya maji katika maeneo yote yenye miradi ya maji" - Amesema Geraruma.

 
Back
Top Bottom