Gereza la Hazwa

Gereza la Hazwa

STORY: GEREZA LA HAZWA
STORY WRITER: FEBIANI BABUYA
STORY TELLER: Bux the story teller
AGE: 18+

UKURASA WA KUMI NA SABA

TULIPO ISHIA UKURASA WA KUMI NA SITA

"Relax mimi sio mbaya wenu nipo hapa kuwasaidia" aliongea akiwa anashusha kitambaa usoni kwake machozi mengi yalikuwa yanamtoka.

"Wewe ni nani?" Aliuliza mwanamke mmoja ambaye alionekana kuwa shupavu miongoni mwao wale wanawake.

"Ni komando wa nchi hii nimekuja hapa kumaliza hili kundi lote la hawa magaidi na nyie kuanzia saivi mpo huru mnaweza kuondoka humu ndani" waliangaliana kwanza kila mtu alibaki anamshangaa hakuna aliye amini kwamba wanaweza kutoka kwenye sehemu ambayo wao kwao ilikuwa ni jehanamu kama hii eti leo walikuwa huru ilikuwa inashangaza sana.

ENDELEA........................
Wanawake wote mle ndani walikuwa wameamka tayari walibaki wanamshangaa sana Aariz kauli zake hawakuwa wakiziamini kabisa Kwa namna alivyokuwa ametapakaa damu ikabidi awasimulie kidogo namna alivyo fanikiwa kuingia ndani ya kambi hiyo mpaka muda huo ambao alikuwa mbele yao hapo, baadae walimuelewa vizuri tu hiyo ilimrahisishia kazi yake alianza kusaidiana na yule mwanamke ambaye alikuwa kiongozi kuwatoa wanawake hao humo ndani aliwaacha wakawa wanaelekea porini sehemu ambayo ilikuwa na miti mingi sana na huko kulikuwa na kiza kinene.

"Una uhakika utawafikisha wenzako salama?" Aariz alimuuliza mwanamke huyo akiwa anamalizikia kutoka mlangoni, aligeuka na kumwangalia mwanaume huyo.
"Nilikuwa miongoni mwa wafanyakazi wa humu ndani mpaka siku ambayo nilifanya jaribio la kutaka kuwasaidia hawa mateka nilikamatwa na kuwa mmoja wa mateka humu ndani kwahiyo hii kambi naijua mpaka nukta ya mwisho wake na kila aina ya ulinzi hapa naijua vizuri hawa nitawafikisha ila naomba nikushukuru sana kwa msaada wako mkubwa" Aariz alitabasamu Kwa mbali sana akiyafumba macho yake.

"Naomba unitajie jina lako ipo siku nitakuja nikutafute" sauti ya mwanamke huyo ilimshtua akafumbua macho yake na kumwangalia mwanamke huyo kwa umakini Sana alisikitika Kwa sababu wasingeweza kukutana tena kwenye maisha yao yote ila aliamua kumtajia tu jina lake.

"Aariz" dada wa watu alipotelea porini kuwaongoza wenzake ambao hawakuwa wakijua lolote kuhusu hiyo sehemu, dakika zilipita tatu tu Aariz alisikia alamu inapiga Kwa sauti kali sana akajua tayari ishajulikana humo ndani sio mahala salama sana, alicho kifanya alikaa chini akaweka silaha zake zote pembeni akaanza kusali akiwa amekaa amefumba macho yake mithili ya mashoulini wa kichina wanavyo fanya pale wanapokuwa kwenye imani zao na maombi mazito. Mboni za macho yake zilihisi uwepo wa vivuli vya watu humo ndani lakini hakuyafumbua macho yake mpaka ilipopita dakika nzima alinyanyuka ubavu wake wa kulia ukiendelea kuvuja damu aliokota silaha zake na kuziweka sehemu yake kwenye mwili mkononi alibakia na upanga mmoja tu ambao alikuwa akiuamini sana anapokuwa sehemu hatari kama hizo, alishtuka na kuguna watu ambao walikuwa mbele yake walikuwa ni tofauti kabisa na ambao alikuwa amekutana nao mwanzo hawa walikuwa watano tu walivaa nguo nyekundu ambazo zilikuwa ni safi mno lakini nyuso zao zilifunikwa na vitambaa vyeupe hiyo ni alama mbaya sana kwenye suala la mapigano watu wanaotumia nguo nyeupe huwa ni wa kutisha sana, nywele za mtu mmoja kati yao zilionyesha wazi alikuwa mtu wa Japan alilazimika kuukaza mkono wake alikuwa mbele ya viumbe vya ajabu na mmoja japo hakuwepo ilimpa mashaka makubwa mno hakuelewa huyo wa sita yuko wapi.

"You are the one who killed our guards right?" Hapa ndipo alipogundua kwamba hawa hawakuwa waarabu kwa sababu walikuwa wakiongea kiingereza ambacho kilikuwa kimechanganyika na lafudhi ya kikorea na kichina.

"I'm here to kill you all" ndiyo kauli ambayo ilitoka kwenye mdomo wake huku akiwanyooshea upanga wanaume hao watano lakini alishangaa mmoja mmoja anajigawa na kwenda kukaa mbele yake alibakia mwanaume mmoja tu ambaye huyo ndiye aliyetakiwa kusimama naye kwenye mapigano, nyota ndogo ndogo zilikuwa zinakuja kwa nguvu alizipangua tatu kwa upanga wake bahati mbaya sana moja ilimuingia pale pale palipokuwa na jeraha ubavuni ni wazi mwanaume huyo alikuwa ashajua sehemu hiyo yenye tatizo, Aariz aliishika sehemu hiyo baada ya damu kuongezeka alishtuka na kurudi nyuma baada ya kuona imeanza kutoka damu yenye rangi nyeusi hizo nyota zilikuwa na sumu kali kupita kiasi. Uwepesi wa ubongo wake ulimpa taarifa hizo silaha zilikuwa na sumu kali mno hapo alikuwa na dakika chache sana za kuwakimbia au kuwamaliza watu hao ili akatibiwe haraka vinginevyo alikuwa anakufa akiwa anajiona.

Upanga ulikuwa unakuja alifanikiwa kuukwepa ulipitiliza ukaenda kutoboa ukuta mjapan huyo alijipindua na kupiga kwenye kifua cha Aariz alidondoka chini na kutapika damu teke lililo ingizwa hapo lilikuwa na uzito wa tani kadhaa aliyakumbuka maneno ya mwanamke ambaye alikutana naye nje ya kambi wakati anaingia alivyo mwambia kwamba kama akifanikiwa kutoka salama basi atakuwa moja ya binadamu wenye bahati sana ambao waliishi kwenye kizazi hiki. Ilitakiwa atumie kila uwezo alio nao ili atoke humo ndani mlango ulikuwa umefungwa aliyafumba macho yake kwa hisia akiwa bado yupo chini mjapan alikuwa amemfikia alirusha upanga wake ili kuitenganisha shingo ya mwanaume huyo alijikuta amepiga hewa hapakuwa na kitu chochote alishtuka sana tumbo lake lilikuwa linamwaga damu Kwa wingi alijigusa na kugundua mtu huyo alinyanyuka Kwa kasi na kulikata tumbo lake alidondoka chini akiwa ameshikilia utumbo wake kitambaa kilimtoka usoni alikuwa ni kijana mdogo sana mpaka Aariz mwenyewe alishangaa inawezekanaje kijana kama huyo kuwa mtu wa kutisha hivyo.

Wenzake wote wanne walijikuta wakisimama Kwa mshangao hawakuwa na matarajio mwenzao angeuliwa kirahisi sana namna hiyo, walijikuta wanamshambulia mtu huyo kwa wepesi sana walitaka kumhusisha na uchawi lakini walikuwa vitani ungekuwa ni upotezaji wa muda nyota tano zilifanikiwa kutoka na nywele zake tu hakuna iliyo mpata alitishia kuingia kwatikati Kwa kasi halafu akasimama wanaume wawili walizamishiana panga zao wenyewe alikuwa amewachonganisha wakati wanashangaana alipita na shingo ya mmoja mpaka muda huo ambaye alikuwa amebaki salama alikuwa ni mmoja tu. Alijichanganya baada ya kutishiwa akakubali kwenye Aariz alidunda kwenye kifua cha mwanaume huyo ambaye alijizoa na kwenda kujibamiza kwenye moja ya kuta humo ndani alitaka kusimama kisu kilipita kwenye koromeo na kutokezea nyuma kwenda kukita ukutani, Aariz alidondoka chini na kupiga goti lake damu nyeusi ilikuwa inamtoka kwenye jeraha lake ilikuwa ni alama mbaya mwili ulianza Kwa mbali kupoteza nguvu yake ila bado alikuwa na kazi nzito mbele yake alielewa yule mmoja ambaye hakuwa hapo alikuwa ndiye anamlinda bosi wake na huenda ndiye huyo aliye ambiwa kwamba alikuwa ni mtoto wa bosi. Alitoka nje kwa kujivuta mpaka nje alitoa maji ambayo ilikuwa ni dawa ya kuongeza nguvu yalikuwa ya baridi mno alibugia nusu ya maji kidogo mwili ukawa na nguvu za kumuwezesha kutembea, alitukana baada ya kuona hata macho yanataka yaanze kumsaliti kuona.

Aliangalia saa yake Kwa umakini.

"I have remained only with ten minutes to get out of here damn" aliongea huku akiihisi maumivu makali sana alikuwa na dakika kumi za kumaliza kazi, aliliangalia lile ghorofa kubwa ambalo lilikuwa limezimwa taa zote kulikuwa na kiza sana, baada ya kuliangalia Kwa muda wa dakika mbili tu ramani nzima ilikuwa kichwani mwake hiyo ndiyo taaluma aliyo isomea Kwa miaka yake yote hivyo alikuwa akiijua kuliko hata jina lake, hakuwahi kuingia humo ndani ila Kwa aina ya nyumba ilivyojengwa haikumpa shida kabisa kuelewa namna nyumba hiyo ilivyokuwa imejengwa. Alijikongoja mpaka mlangoni mlango ulikuwa upo wazi kabisa hii ilimtia shaka sana Kwa mtu kama yeye hiyo ilikuwa ni ishara mbaya mno alitembea kwa hatua kumi alisimama baada ya moyo wake kudunda sana alisimama na kutulia mwanga mkali ulimfanya ayafumbe macho yake mkononi akiwa na upanga ambao ulikuwa unatoka damu nyingi sana hata yeye mwili ulitapakaa damu sana mkono wake mmoja wa kushoto aliutumia kushika kwenye ubavu wake wa kulia ambao ulikuwa unavuja damu nyeusi.

Wanaume wawili na wanawake kumi walikuwa wanamtazama, mmoja alikuwa amekaa na wanawake karibia wanne walimkalia wakiwa wapo nusu uchi huku wangine sita wakishindana kumpa huduma wakati mwanaume mwingine alikuwa amesimama pembeni ya mwanaume huyo akiwa ameikumbata mikono yake ni wazi waliutarajia ujio wake humo ndani ndio maana waliacha mlango wazi, aliyekuwa amekaa alikuwa anaitwa Bashiru Hazir huyu ndiye alikuwa mkuu wa hii kambi ya kigaidi na ndiye aliyekuwa chanzo cha mambo yote ambayo yalisababisha vita hili eneo la kusini mwa Libya pembeni yake alikuwa ni mwanae wa kumzaa na ndiye aliyekuwa mlinzi wake mkuu alijulikana kama Abushiri Hazir. Aariz aliliangalia kwa umakini hilo jengo bila kuongea chochote alikiangalia kidonda chake na kujisikitikia, hakufanya hivyo kwa bahati mbaya mtu ambaye alikuwa mbele yake ndiye aliyempa hofu ya kufanya hivyo angekuwa timamu ilikuwa ni kazi rahisi tu ila hali aliyokuwa nayo alihofia sana, Abushiri alikuwa kwenye mavazi meupe na usoni hakujifunika chochote ilikuwa ni bora na wale watano ambao walikuwa na vitambaa vyeupe tu vya usoni sasa huyu nguo zake zote zilikuwa nyeupe na usoni hakuwa na chochote alimtishia mno alielewa sio binadamu ambaye unaweza ukamgusa kiwepesi sana.

"Haya yote umeyafanya Kwa sababu tu ya pesa au kuna mengine nyuma ambayo hayajulikani?" Aariz alimuuliza mzee ambaye alikuwa yuko busy na wanawake wala hakujali kama humo ndani kulikuwa na mgeni.

"Ogopa sana neno pesa na nguvu kwenye maisha yako, kwanini umeamua kuyatoa maisha yako sadaka kirahisi sana namna hii unajua kabisa siwezi nikakuacha ukiwa hai kwa hicho ulicho kifanya" ni sauti zito na baya lilitoka Kwa mtu huyo alionekana kuwa mkatili sana.

"Hey ladies get out of here" aliongea kwa sauti ya kawaida tu lakini hakuna kilichotokea.

"Hey I say out" aliongea Kwa sauti ya ukali mpaka alitoa damu kwenye mdomo wake, wanawake hao waliogopa sana na kuanza kusogea nyuma, Aariz Alifanya shambulio la ghafla Sana kwa kurusha visu vyake viwili pale alipokaa yule mzee, alishuhudia kitu ambacho hata yeye mwenyewe kilimtisha sana visu hivyo vilidakwa Kwa vidole vinne tu vya yule mwanaume ambaye alikuwa pembeni vilirudishwa kwake alividaka lakini mkono wake ulipata maumivu vilitoka kwenye mikono ya mwanaume mwenye nguvu mno.

"Kill him" ni sauti moja tu ya mamlaka kutoka kwa yule mzee ambaye alionekana kuongea kawaida ila alikuwa na uchungu na hasira sana kambi yake ilikuwa imeharibiwa vibaya sana, alitaka kutoka humo ndani baada ya kuona wanawake wale wamekimbilia nje na kuanza kusambaa hovyo hovyo hayo mambo yalikuwa hayawahusu kabisa ya vita Aariz aliurusha upanga wake baada ya kupigwa mapigo makali kutoka Kwa mwanaume ambaye alikuwa amesimama nbele yake, upanga huo ulienda kuzama kwenye mgongo wa yule mzee alidondoka chini akianza kutapa tapa.

"Dadiiiiiiii" yule mwanaume aliita kwa uchungu sana na kuanza kumpiga Kwa hasira Aariz kwenye mbavu zake mwanaume alizidi kutapika damu ila ghafla alipotea yule mwanaume alianza kuhangaika kumtafuta huku akipiga kelele na kumtaka ajitokeze, hali yake ilikuwa mbaya sana alikuwa amesimama nyuma ya mwanaume huyo kiganja kizito kilitua kwenye shingo ya Abushiri na kumfanya apinde kidogo hata hivyo alirusha teke ambalo lilidakwa na mguu wake ulivunjwa alipiga kelele na kutoa bastola yake ambayo ilitoa risasi tano zote zilizama kwenye ubavu wa kulia ule ule ambao Aariz alikuwa ameharibiwa vibaya sana, maumivu makali mno yalitembea Kwa spidi kwenye mwili wake akiwa anatoa damu nyingi sana ubavuni na mdomoni alikunja vidole vyake na kuzamisha kwenye shingo ya Abushiri na kuikata mishipa ya shingoni mwanaume huyo alipiga kelele akiwa anajibamiza chini maumivu aliyo yapitia ni wazi yalimpa uchizi, Aariz naye alikuwa chini akiwa kwenye hali mbaya alimshuhudia mwanaume mwenzake akiwa anakata roho alijivuta mpaka alipokuwa anahangaika yule mzee aliuchomoa upanga wake Kwa nguvu hali iliyo mpa mzee yule maumivu makali sana.

"Huu sio mwisho huu ni mwanzo tu wa haya mambo hahahahahaha..." Aariz hakutaka kujisumbua kutaka kujua hiyo kauli za mzee huyo ilimaanisha nini aliamua kupita na shingo yake akanyanyuka kwa kuyumba yumba na kuanza kuondoka hilo eneo macho yake yalikuwa yamepoteza nuru alitoa saa ambayo aliichukua kwa yule mwanamke aliminya kwenye alama ya kijani milango yote ilikuwa wazi alitembea kwa muda kama dakika ishirini akiwa anaona Kwa mbali sana, alimshukuru MUNGU baada ya kuliona gari lake alikuwa tayari yupo nje ya pori alipanda na kutoa limoti ambayo aliichukua mle ndani Kwa wale wanaume sita wa mwanzo aliibonyeza ulisikika mlipuko mkubwa ambao hata yeye hakutegemea kuusikia tetemeko zito lilipita na kumfanya aondoe gari lake haraka hilo eneo lakini macho yake yalimsaliti alipapasa simu pembeni yake MUNGU alikuwa upande wake aliipata alitafuta kwa haraka namba moja na kupiga haikuchukua muda ilipokelewa.

"I'm dying" ni kauli yake moja tu aliitamka haikusikika sauti nyingine tena simu ikiwa bado ipo hewani.

"Kheeeee aliwezaje kuishi tena?" Takribani masaa 27 mpaka muda huo raisi na mzee huyo walikuwa wamekaa ndani ya chumba hicho kichafu sana cha GEREZA akiwa anasimuliwa historia ya huyo mtu aliingilia kati kuulizia aliweza vipi kupona kwenye hiyo hali, mzee huyo aliinama na kuinua uso wake na kuufungua tena.

"Huo ndio ulikuwa mwanzo wake wa kuwa binadamu ambaye ataishi miaka mingi sana akiwa bado yupo hai na itamchukua muda sana kuzeeka" raisi alishangaa mpaka akasimama alitamani kuondoka ila hilo lingemfanya asijue chochote kabisa kuhusu hadithi ambayo ni kama ilikuwa imefikia katikati hakuhitaji kuikosa hata nukta alirudi tena na kukaa chini ili apewe alicho hitaji kujua.

Kuna siri gani nyingine nzito sana kwenye historia ya mwanaume huyu? Ni kweli ataishi miaka mingi? Kivipi? GEREZA LA HAZWA naweka nukta ukurasa wa 17 tukutane wakati ujao.

Langu jina wananiita

Bux the story teller
 

Attachments

  • 319087090_138036052377551_8833566426369870948_n.jpg
    319087090_138036052377551_8833566426369870948_n.jpg
    44.6 KB · Views: 66
STORY: GEREZA LA HAZWA
STORY WRITER: FEBIANI BABUYA
STORY TELLER: Bux the story teller
AGE: 18+

UKURASA WA KUMI NA SABA

TULIPO ISHIA UKURASA WA KUMI NA SITA

"Relax mimi sio mbaya wenu nipo hapa kuwasaidia" aliongea akiwa anashusha kitambaa usoni kwake machozi mengi yalikuwa yanamtoka.

"Wewe ni nani?" Aliuliza mwanamke mmoja ambaye alionekana kuwa shupavu miongoni mwao wale wanawake.

"Ni komando wa nchi hii nimekuja hapa kumaliza hili kundi lote la hawa magaidi na nyie kuanzia saivi mpo huru mnaweza kuondoka humu ndani" waliangaliana kwanza kila mtu alibaki anamshangaa hakuna aliye amini kwamba wanaweza kutoka kwenye sehemu ambayo wao kwao ilikuwa ni jehanamu kama hii eti leo walikuwa huru ilikuwa inashangaza sana.

ENDELEA........................
Wanawake wote mle ndani walikuwa wameamka tayari walibaki wanamshangaa sana Aariz kauli zake hawakuwa wakiziamini kabisa Kwa namna alivyokuwa ametapakaa damu ikabidi awasimulie kidogo namna alivyo fanikiwa kuingia ndani ya kambi hiyo mpaka muda huo ambao alikuwa mbele yao hapo, baadae walimuelewa vizuri tu hiyo ilimrahisishia kazi yake alianza kusaidiana na yule mwanamke ambaye alikuwa kiongozi kuwatoa wanawake hao humo ndani aliwaacha wakawa wanaelekea porini sehemu ambayo ilikuwa na miti mingi sana na huko kulikuwa na kiza kinene.

"Una uhakika utawafikisha wenzako salama?" Aariz alimuuliza mwanamke huyo akiwa anamalizikia kutoka mlangoni, aligeuka na kumwangalia mwanaume huyo.
"Nilikuwa miongoni mwa wafanyakazi wa humu ndani mpaka siku ambayo nilifanya jaribio la kutaka kuwasaidia hawa mateka nilikamatwa na kuwa mmoja wa mateka humu ndani kwahiyo hii kambi naijua mpaka nukta ya mwisho wake na kila aina ya ulinzi hapa naijua vizuri hawa nitawafikisha ila naomba nikushukuru sana kwa msaada wako mkubwa" Aariz alitabasamu Kwa mbali sana akiyafumba macho yake.

"Naomba unitajie jina lako ipo siku nitakuja nikutafute" sauti ya mwanamke huyo ilimshtua akafumbua macho yake na kumwangalia mwanamke huyo kwa umakini Sana alisikitika Kwa sababu wasingeweza kukutana tena kwenye maisha yao yote ila aliamua kumtajia tu jina lake.

"Aariz" dada wa watu alipotelea porini kuwaongoza wenzake ambao hawakuwa wakijua lolote kuhusu hiyo sehemu, dakika zilipita tatu tu Aariz alisikia alamu inapiga Kwa sauti kali sana akajua tayari ishajulikana humo ndani sio mahala salama sana, alicho kifanya alikaa chini akaweka silaha zake zote pembeni akaanza kusali akiwa amekaa amefumba macho yake mithili ya mashoulini wa kichina wanavyo fanya pale wanapokuwa kwenye imani zao na maombi mazito. Mboni za macho yake zilihisi uwepo wa vivuli vya watu humo ndani lakini hakuyafumbua macho yake mpaka ilipopita dakika nzima alinyanyuka ubavu wake wa kulia ukiendelea kuvuja damu aliokota silaha zake na kuziweka sehemu yake kwenye mwili mkononi alibakia na upanga mmoja tu ambao alikuwa akiuamini sana anapokuwa sehemu hatari kama hizo, alishtuka na kuguna watu ambao walikuwa mbele yake walikuwa ni tofauti kabisa na ambao alikuwa amekutana nao mwanzo hawa walikuwa watano tu walivaa nguo nyekundu ambazo zilikuwa ni safi mno lakini nyuso zao zilifunikwa na vitambaa vyeupe hiyo ni alama mbaya sana kwenye suala la mapigano watu wanaotumia nguo nyeupe huwa ni wa kutisha sana, nywele za mtu mmoja kati yao zilionyesha wazi alikuwa mtu wa Japan alilazimika kuukaza mkono wake alikuwa mbele ya viumbe vya ajabu na mmoja japo hakuwepo ilimpa mashaka makubwa mno hakuelewa huyo wa sita yuko wapi.

"You are the one who killed our guards right?" Hapa ndipo alipogundua kwamba hawa hawakuwa waarabu kwa sababu walikuwa wakiongea kiingereza ambacho kilikuwa kimechanganyika na lafudhi ya kikorea na kichina.

"I'm here to kill you all" ndiyo kauli ambayo ilitoka kwenye mdomo wake huku akiwanyooshea upanga wanaume hao watano lakini alishangaa mmoja mmoja anajigawa na kwenda kukaa mbele yake alibakia mwanaume mmoja tu ambaye huyo ndiye aliyetakiwa kusimama naye kwenye mapigano, nyota ndogo ndogo zilikuwa zinakuja kwa nguvu alizipangua tatu kwa upanga wake bahati mbaya sana moja ilimuingia pale pale palipokuwa na jeraha ubavuni ni wazi mwanaume huyo alikuwa ashajua sehemu hiyo yenye tatizo, Aariz aliishika sehemu hiyo baada ya damu kuongezeka alishtuka na kurudi nyuma baada ya kuona imeanza kutoka damu yenye rangi nyeusi hizo nyota zilikuwa na sumu kali kupita kiasi. Uwepesi wa ubongo wake ulimpa taarifa hizo silaha zilikuwa na sumu kali mno hapo alikuwa na dakika chache sana za kuwakimbia au kuwamaliza watu hao ili akatibiwe haraka vinginevyo alikuwa anakufa akiwa anajiona.

Upanga ulikuwa unakuja alifanikiwa kuukwepa ulipitiliza ukaenda kutoboa ukuta mjapan huyo alijipindua na kupiga kwenye kifua cha Aariz alidondoka chini na kutapika damu teke lililo ingizwa hapo lilikuwa na uzito wa tani kadhaa aliyakumbuka maneno ya mwanamke ambaye alikutana naye nje ya kambi wakati anaingia alivyo mwambia kwamba kama akifanikiwa kutoka salama basi atakuwa moja ya binadamu wenye bahati sana ambao waliishi kwenye kizazi hiki. Ilitakiwa atumie kila uwezo alio nao ili atoke humo ndani mlango ulikuwa umefungwa aliyafumba macho yake kwa hisia akiwa bado yupo chini mjapan alikuwa amemfikia alirusha upanga wake ili kuitenganisha shingo ya mwanaume huyo alijikuta amepiga hewa hapakuwa na kitu chochote alishtuka sana tumbo lake lilikuwa linamwaga damu Kwa wingi alijigusa na kugundua mtu huyo alinyanyuka Kwa kasi na kulikata tumbo lake alidondoka chini akiwa ameshikilia utumbo wake kitambaa kilimtoka usoni alikuwa ni kijana mdogo sana mpaka Aariz mwenyewe alishangaa inawezekanaje kijana kama huyo kuwa mtu wa kutisha hivyo.

Wenzake wote wanne walijikuta wakisimama Kwa mshangao hawakuwa na matarajio mwenzao angeuliwa kirahisi sana namna hiyo, walijikuta wanamshambulia mtu huyo kwa wepesi sana walitaka kumhusisha na uchawi lakini walikuwa vitani ungekuwa ni upotezaji wa muda nyota tano zilifanikiwa kutoka na nywele zake tu hakuna iliyo mpata alitishia kuingia kwatikati Kwa kasi halafu akasimama wanaume wawili walizamishiana panga zao wenyewe alikuwa amewachonganisha wakati wanashangaana alipita na shingo ya mmoja mpaka muda huo ambaye alikuwa amebaki salama alikuwa ni mmoja tu. Alijichanganya baada ya kutishiwa akakubali kwenye Aariz alidunda kwenye kifua cha mwanaume huyo ambaye alijizoa na kwenda kujibamiza kwenye moja ya kuta humo ndani alitaka kusimama kisu kilipita kwenye koromeo na kutokezea nyuma kwenda kukita ukutani, Aariz alidondoka chini na kupiga goti lake damu nyeusi ilikuwa inamtoka kwenye jeraha lake ilikuwa ni alama mbaya mwili ulianza Kwa mbali kupoteza nguvu yake ila bado alikuwa na kazi nzito mbele yake alielewa yule mmoja ambaye hakuwa hapo alikuwa ndiye anamlinda bosi wake na huenda ndiye huyo aliye ambiwa kwamba alikuwa ni mtoto wa bosi. Alitoka nje kwa kujivuta mpaka nje alitoa maji ambayo ilikuwa ni dawa ya kuongeza nguvu yalikuwa ya baridi mno alibugia nusu ya maji kidogo mwili ukawa na nguvu za kumuwezesha kutembea, alitukana baada ya kuona hata macho yanataka yaanze kumsaliti kuona.

Aliangalia saa yake Kwa umakini.

"I have remained only with ten minutes to get out of here damn" aliongea huku akiihisi maumivu makali sana alikuwa na dakika kumi za kumaliza kazi, aliliangalia lile ghorofa kubwa ambalo lilikuwa limezimwa taa zote kulikuwa na kiza sana, baada ya kuliangalia Kwa muda wa dakika mbili tu ramani nzima ilikuwa kichwani mwake hiyo ndiyo taaluma aliyo isomea Kwa miaka yake yote hivyo alikuwa akiijua kuliko hata jina lake, hakuwahi kuingia humo ndani ila Kwa aina ya nyumba ilivyojengwa haikumpa shida kabisa kuelewa namna nyumba hiyo ilivyokuwa imejengwa. Alijikongoja mpaka mlangoni mlango ulikuwa upo wazi kabisa hii ilimtia shaka sana Kwa mtu kama yeye hiyo ilikuwa ni ishara mbaya mno alitembea kwa hatua kumi alisimama baada ya moyo wake kudunda sana alisimama na kutulia mwanga mkali ulimfanya ayafumbe macho yake mkononi akiwa na upanga ambao ulikuwa unatoka damu nyingi sana hata yeye mwili ulitapakaa damu sana mkono wake mmoja wa kushoto aliutumia kushika kwenye ubavu wake wa kulia ambao ulikuwa unavuja damu nyeusi.

Wanaume wawili na wanawake kumi walikuwa wanamtazama, mmoja alikuwa amekaa na wanawake karibia wanne walimkalia wakiwa wapo nusu uchi huku wangine sita wakishindana kumpa huduma wakati mwanaume mwingine alikuwa amesimama pembeni ya mwanaume huyo akiwa ameikumbata mikono yake ni wazi waliutarajia ujio wake humo ndani ndio maana waliacha mlango wazi, aliyekuwa amekaa alikuwa anaitwa Bashiru Hazir huyu ndiye alikuwa mkuu wa hii kambi ya kigaidi na ndiye aliyekuwa chanzo cha mambo yote ambayo yalisababisha vita hili eneo la kusini mwa Libya pembeni yake alikuwa ni mwanae wa kumzaa na ndiye aliyekuwa mlinzi wake mkuu alijulikana kama Abushiri Hazir. Aariz aliliangalia kwa umakini hilo jengo bila kuongea chochote alikiangalia kidonda chake na kujisikitikia, hakufanya hivyo kwa bahati mbaya mtu ambaye alikuwa mbele yake ndiye aliyempa hofu ya kufanya hivyo angekuwa timamu ilikuwa ni kazi rahisi tu ila hali aliyokuwa nayo alihofia sana, Abushiri alikuwa kwenye mavazi meupe na usoni hakujifunika chochote ilikuwa ni bora na wale watano ambao walikuwa na vitambaa vyeupe tu vya usoni sasa huyu nguo zake zote zilikuwa nyeupe na usoni hakuwa na chochote alimtishia mno alielewa sio binadamu ambaye unaweza ukamgusa kiwepesi sana.

"Haya yote umeyafanya Kwa sababu tu ya pesa au kuna mengine nyuma ambayo hayajulikani?" Aariz alimuuliza mzee ambaye alikuwa yuko busy na wanawake wala hakujali kama humo ndani kulikuwa na mgeni.

"Ogopa sana neno pesa na nguvu kwenye maisha yako, kwanini umeamua kuyatoa maisha yako sadaka kirahisi sana namna hii unajua kabisa siwezi nikakuacha ukiwa hai kwa hicho ulicho kifanya" ni sauti zito na baya lilitoka Kwa mtu huyo alionekana kuwa mkatili sana.

"Hey ladies get out of here" aliongea kwa sauti ya kawaida tu lakini hakuna kilichotokea.

"Hey I say out" aliongea Kwa sauti ya ukali mpaka alitoa damu kwenye mdomo wake, wanawake hao waliogopa sana na kuanza kusogea nyuma, Aariz Alifanya shambulio la ghafla Sana kwa kurusha visu vyake viwili pale alipokaa yule mzee, alishuhudia kitu ambacho hata yeye mwenyewe kilimtisha sana visu hivyo vilidakwa Kwa vidole vinne tu vya yule mwanaume ambaye alikuwa pembeni vilirudishwa kwake alividaka lakini mkono wake ulipata maumivu vilitoka kwenye mikono ya mwanaume mwenye nguvu mno.

"Kill him" ni sauti moja tu ya mamlaka kutoka kwa yule mzee ambaye alionekana kuongea kawaida ila alikuwa na uchungu na hasira sana kambi yake ilikuwa imeharibiwa vibaya sana, alitaka kutoka humo ndani baada ya kuona wanawake wale wamekimbilia nje na kuanza kusambaa hovyo hovyo hayo mambo yalikuwa hayawahusu kabisa ya vita Aariz aliurusha upanga wake baada ya kupigwa mapigo makali kutoka Kwa mwanaume ambaye alikuwa amesimama nbele yake, upanga huo ulienda kuzama kwenye mgongo wa yule mzee alidondoka chini akianza kutapa tapa.

"Dadiiiiiiii" yule mwanaume aliita kwa uchungu sana na kuanza kumpiga Kwa hasira Aariz kwenye mbavu zake mwanaume alizidi kutapika damu ila ghafla alipotea yule mwanaume alianza kuhangaika kumtafuta huku akipiga kelele na kumtaka ajitokeze, hali yake ilikuwa mbaya sana alikuwa amesimama nyuma ya mwanaume huyo kiganja kizito kilitua kwenye shingo ya Abushiri na kumfanya apinde kidogo hata hivyo alirusha teke ambalo lilidakwa na mguu wake ulivunjwa alipiga kelele na kutoa bastola yake ambayo ilitoa risasi tano zote zilizama kwenye ubavu wa kulia ule ule ambao Aariz alikuwa ameharibiwa vibaya sana, maumivu makali mno yalitembea Kwa spidi kwenye mwili wake akiwa anatoa damu nyingi sana ubavuni na mdomoni alikunja vidole vyake na kuzamisha kwenye shingo ya Abushiri na kuikata mishipa ya shingoni mwanaume huyo alipiga kelele akiwa anajibamiza chini maumivu aliyo yapitia ni wazi yalimpa uchizi, Aariz naye alikuwa chini akiwa kwenye hali mbaya alimshuhudia mwanaume mwenzake akiwa anakata roho alijivuta mpaka alipokuwa anahangaika yule mzee aliuchomoa upanga wake Kwa nguvu hali iliyo mpa mzee yule maumivu makali sana.

"Huu sio mwisho huu ni mwanzo tu wa haya mambo hahahahahaha..." Aariz hakutaka kujisumbua kutaka kujua hiyo kauli za mzee huyo ilimaanisha nini aliamua kupita na shingo yake akanyanyuka kwa kuyumba yumba na kuanza kuondoka hilo eneo macho yake yalikuwa yamepoteza nuru alitoa saa ambayo aliichukua kwa yule mwanamke aliminya kwenye alama ya kijani milango yote ilikuwa wazi alitembea kwa muda kama dakika ishirini akiwa anaona Kwa mbali sana, alimshukuru MUNGU baada ya kuliona gari lake alikuwa tayari yupo nje ya pori alipanda na kutoa limoti ambayo aliichukua mle ndani Kwa wale wanaume sita wa mwanzo aliibonyeza ulisikika mlipuko mkubwa ambao hata yeye hakutegemea kuusikia tetemeko zito lilipita na kumfanya aondoe gari lake haraka hilo eneo lakini macho yake yalimsaliti alipapasa simu pembeni yake MUNGU alikuwa upande wake aliipata alitafuta kwa haraka namba moja na kupiga haikuchukua muda ilipokelewa.

"I'm dying" ni kauli yake moja tu aliitamka haikusikika sauti nyingine tena simu ikiwa bado ipo hewani.

"Kheeeee aliwezaje kuishi tena?" Takribani masaa 27 mpaka muda huo raisi na mzee huyo walikuwa wamekaa ndani ya chumba hicho kichafu sana cha GEREZA akiwa anasimuliwa historia ya huyo mtu aliingilia kati kuulizia aliweza vipi kupona kwenye hiyo hali, mzee huyo aliinama na kuinua uso wake na kuufungua tena.

"Huo ndio ulikuwa mwanzo wake wa kuwa binadamu ambaye ataishi miaka mingi sana akiwa bado yupo hai na itamchukua muda sana kuzeeka" raisi alishangaa mpaka akasimama alitamani kuondoka ila hilo lingemfanya asijue chochote kabisa kuhusu hadithi ambayo ni kama ilikuwa imefikia katikati hakuhitaji kuikosa hata nukta alirudi tena na kukaa chini ili apewe alicho hitaji kujua.

Kuna siri gani nyingine nzito sana kwenye historia ya mwanaume huyu? Ni kweli ataishi miaka mingi? Kivipi? GEREZA LA HAZWA naweka nukta ukurasa wa 17 tukutane wakati ujao.

Langu jina wananiita

Bux the story teller
STORY: GEREZA LA HAZWA
STORY WRITER: FEBIANI BABUYA
STORY TELLER: Bux the story teller
AGE: 18+

UKURASA WA KUMI NA NANE

TULIPO ISHIA UKURASA WA KUMI NA SABA


"Kheeeee aliwezaje kuishi tena?" Takribani masaa 27 mpaka muda huo raisi na mzee huyo walikuwa wamekaa ndani ya chumba hicho kichafu sana cha GEREZA akiwa anasimuliwa historia ya huyo mtu aliingilia kati kuulizia aliweza vipi kupona kwenye hiyo hali, mzee huyo aliinama na kuinua uso wake na kuufungua tena.

"Huo ndio ulikuwa mwanzo wake wa kuwa binadamu ambaye ataishi miaka mingi sana akiwa bado yupo hai na itamchukua muda sana kuzeeka" raisi alishangaa mpaka akasimama alitamani kuondoka ila hilo lingemfanya asijue chochote kabisa kuhusu hadithi ambayo ni kama ilikuwa imefikia katikati hakuhitaji kuikosa hata nukta alirudi tena na kukaa chini ili apewe alicho hitaji kujua.
ENDELEA.....................

AVOCC STREET BARAKUDA TABATA DAR ES SALAAM

Mvua zilikuwa zinaendelea kunyesha ndani ya jiji hili Kama ilivyo kawaida huwa halitabiriki kabisa linapokuja suala la kushusha mvua, watu wachache walikuwa wanaonekana kuendelea na biashara zao kwenye kuutafuta mkate wa kila siku kwali ulikiwa ni usiku mzito lakini ilikuwa ni tofauti kwa mwanaume mmoja ambaye muda huo licha ya kuwa na mvua kali ambazo zlilileta halii ya ubaridi kwenye sehemu hii iliyokuwa na utajiri wa kutosha wa joto alikuwa akikimbizwa mithili ya mtu ambaye alikuwa amekula pesa za wanakijiji baridi lililokuwepo halikuwa na msaada wowote kwake alikuwa anavuja jasho ambalo lilisaidiwa kufutwa na maji ya mvua alikuwa akihema kwa nguvu mno. Hakuonekana mtu ambaye alikuwa anamfukuza maana alikuwa yupo pekeake ila alikuwa anakimbia kwa Kasi mno akikatiza chochoro nyingi kwa wepesi alionekana kuwa mwenyeji sana wa hii mitaa, hakuna mtu wa kawaida ambaye angeweza kuendana na kasi yake.

Alienda kusimama sehemu ambayo ilikuwa na uwanja mpana akiwa anahemeana kwa nguvu aliangaza kila upande hakuona mtu akaikunjua kola ya shati lake na kuanza kutembea alikuwa amechomekea vizuri sana kama ungekutana naye mchana basi usingesita kumpa vyeo vya ustaarabu hapa mjini ila bahati mbaya ilikuwa ni usiku wa manane ilikuwa ni ngumu sana kumpa hicho cheo bila kujua kilichokuwa kinamkimbiza ni nini. Alishtuka baada ya kusikia mtu anampigia makofi alisonya kwa hasira alikuwa amefanya kazi bure licha ya mbio zake zote bado aliishia kwenye njia za watu ambao ndio walimfanya usiku huo akurupuke sana na hizo mbio. Alitulia na kurudisha kumbukumbu zake nyuma namna alivyo wakimbia watu hao, dakika chache zilizopita alikuwa ndani ya ukumbi maarufu ujulikanao kama SMALL PLANET, huwa wanapaita TABATA KWA WALA BATA naye alikuwa mmoja wao mfuko ulituna angemhofia nani na Kodi kalipa alikuwa yupo na kimada mmoja ambaye aliona atamaliza naye safari yake ya starehe kwa siku hiyo.

Akiwa amekaa na mwanamke huyo ni zaidi ya dakika tano aliona kuna watu watatu wanamwangalia sana, alizuga kama anahama meza makusudi lakini bado watu hao macho yao yalikuwa kwake, alinyanyuka na kwenda chooni kuhakikisha kama je kweli walikuwa wanamfuatilia ni kweli mwanaume mmoja alinyanyuka naye na kuunga naye tera huko uani japo mtu huyo yeye hakuingia ndani alizuga mpaka mtu huyo alipotoka nje tena akawa anamfuata kwa nyuma. Mwanaume hakuwa Fala alielewa hiyo sehemu sio salama tena kwake alijifanya kama anaenda kaunta kulipia bili ambayo kiuhalisia alikuwa amelipa tangu anaagiza vinywaji hiyo ilikuwa nafasi ya kutoka nje, aligeuka na kuona watu hao wapo nae macho kwa macho aliingia kwenye uchochoro mmoja bila kujali mvua kali ambayo ilikuwa inaendelea kunyesha alishangaa nao wanamfuata, aliongeza mwendo nao waliongeza taa ya hatari ilizigusa sehemu za kichwa chake alianza kukimbia nao waliunga naye ila alishangaa wanatawanyika, mikimbio yao tu ilimpa tahadhali hawakuwa watu wa kawaida.

Alimaliza kutafakari kumbukumbu zake na sasa alikuwa anamshangaa mtu huyo ambaye alikuwa anampigia makofi alishangaa upande wa pili wake anatokea mtu mwingine na nyuma yake alitokea mwingine wote watatu walikuwa wamemuweka kati tayari.

"Mnataka nini kwangu?"

"Kwanini unatukimbia?"

"Nasimamaje nafuatiliwa kila nacho kifanya na watu ambao hata siwajui msinipotezee muda nina mambo mengi sana ya kufanya"

"Kwenye hayo maclub ndo una mambo mengi ya kufanya?"

"Fuata biashara zako yale sio maisha yako"

"Ok sawa, nifuate tuongozane kistaarabu tu tukifika mbele utaambiwa kwanini tumekuja kukuchukua hapa saivi"

"Hahahahahhaa yaani wewe hapo ndo unaongea kwa dharau kwamba unakuja kunichukua"

"Jiti Maalimu nadhani ndilo jina lako unatokea kwenye idara ya usalama wa taifa wa nchi ya Tanzania mpaka hapo inaonyesha nakujua kwahiyo usihitaji tukuchukue kwa nguvu bwana mdogo" mtu huyo ambaye kwa mara ya Kwanza tumemjua kama Jiti alipigwa na butwaa baada ya kutajiwa majina yake ya kweli ambayo alizaliwa nayo ukiachana na majina ambayo alikuwa anayatumia kwenye kazi yake hiyo ya usalama.

"Vipi tulishawahi kukutana kabla" alimuuliza mtu huyo ambayo kutokana na kiza hawakuwa wanaonana vizuri sura zao"

"Hilo jambo sio mhimu kwa sasa Ray ebu mchukueni tuondoke" mwanaume ambaye alijulikana kama Ray alipewa amri ya kumchukua mwanaume mwenzake kirahisi tu kama vile lililkuwa ni debe la karanga, Ray kama alivyokuwa ametajwa kwa jina lake moja tu alimsogelea mtu huyo mpaka alipokuwa alizungusha teke la chini ili kumzoa alimkosa, alizunguka teke lingine alijikuta anapiga hewa mtu huyo alikuwa mwepesi mno Ray aliyumba baada ya kukutana uso kwa uso na jabali la maana damu zilianza kumtoka mwanaume huyo alizunguka na double kick ambayo ilimpata Ray kifuani alizolewa mpaka ukutani mwa nyumba ambayo ilikuwa pembeni hapo, mwenzake alikuwa anakuja kwa spidi bila mpangilio alirusha ngumi alipitwa kwa juu na mtu huyo kwa sarakasi safi alipigwa ngumi ya mgongo iliyofuatiwa na teke zito alivyotaka kushuka kummalizia mtu huyo wa pili alijikuta yeye ndo anaenda chini aliishika shingo yake iliyokuwa na maumivu makali alikuwa amechomwa na sindano yenye sumu macho yake yalipoteza uangavu akaenda chini.

"Mbebeni tuondoke" aliongea yule mwanaume ambaye alionekana kuwa kiongozi wao tangu wanafika hapo, walimpakia kwenye mfuko mkubwa mmoja wao akamuweka begani wakapotelea vichochoroni.



KIBETA BUKOBA
Jua lililkuwa kali sana majira ya mchana wakati ni jua la utosi kabisa kama ilivyokuwa kawaida yao watu wastaarabu lakini wajivuni mno hawa Wahaya walikuwa wapo kwenye vigenge vyao vya kuufanya muda uende mbele kwenye hiki kijiji ambacho ni maarufu sana kwa maeneo yale watu walikuwa wako busy kuzielezea sarufi na visasili kwa sababu kwao darasa halikuwa shida kabisa kwenye vichwa vyao, ni siku ambayo ilikuwa ya ajabu japo wengine waliita ni siku ya bahati zaidi kwenye maisha yao, wakiwa hawana hili wala lile kwenye hicho kijiji chao lilitokea jambo la kushangaza ambalo kila mtu alikataa kabisa kuamini kwamba ni kweli limetokea hawakuwahi kuwa na kumbukumbu kwamba waliwahi kuwaza tukio kama hilo kufanyika kwenye kijiji chao. Ni kijiji ambacho kilijengwa mno na walio ishi hapo wengi walikuwa na ukwasi ambao haukuwafanya wawe na maisha ya kuombana chumvi.

"Hivi hili jambo ni la kweli au kuna namna watu wanatuchezea akili" aliuliza jamaa mmoja kwenye hiyo sehemu ambayo walikuwa na wenzake wakiwa wanapiga soga na kuongelea ishu za masomo nje ya nchi, alizubaa mpaka udenda ulimtoka na hakuna aliye mjali.

"Hope we are the luckiest generation ever" akiwa anamaanisha wao ndicho kizazi cha bahati zaidi kwenye historia, alikuwa ni mwingine ambaye yeye alionekana kuchekelea sana hilo jambo ila ilikuwa ni tofauti kwa mwenzao wa tatu yeye alikataa kabisa.

"Acheni upumbavu ninyi sio rahisi kama mnavyo fikiria acheni kuwa na akili za soda halafu mnalazimisha kunywa bia mtadhalilika wajinga nyie duniani watu ni wawili wawili unadhani mtu kama yule utamuona kama magazeti ya udaku namna hiyo hahahahha mnakuwa kama mitoto midogo nilishawahi kwenda huko SONGWE nikakutana na mtu ambaye nafanana naye kwa kila kitu mpaka namna ya kucheka acheni ushamba" yeye alijifanya ndiye aliwatani wa mji kila kitu alikijua yeye akiwapa na wenzake mifano kabisa.

"Sudi unavyozidi kukua naendelea kukushusha vyeo taratibu huwa unakurupuka tu bila mpangilio nadhani baba yako kutaka kukupeleka marekani kusoma hizo pesa ni bora tu akulipie mahali uoe hamna mtu hapo"

"Oya Maiko kuwa na heshima tusivuke mipaka kufikia hatua ya kutukanana nitakuzingua mwanangu heshima ikae mahala pake" palipita ukimya kwa sababu walionekana kuelekea kupigana juu ya kumbishania mtu. Mtu ambaye aliwafanya waache kila walichokuwa wanakifanya na kuanza kubishana alikuwa ni mtu ambaye alifanana sana na raisi wa nchi yao kwa kila kitu hata tukisema duniani wawili wawili jibu lilikiwa ni hapana walifanana mno ila kilicho wafanya wakatae kabisa kwamba huyo sio raisi wao ni namna alivyokuwa anazunguka mtaani walikuwa wapo wawili tu na wanajua raisi ndiye mtu anayelindwa zaidi ndani ya nchi hii isingewezekana akawa anazurula mtaani kiwepesi sana namna hiyo na tangu uchaguzi ufanyike hawakuwahi kutembelewa kabisa na raisi wao huyo japo walimpenda sana maana alikuwa mtu makini sana kwenye maendeleo ya taifa.

Fikra zao zilikuwa sahihi ila imani zao ziliwadanganya, huyo mtu ambaye walikuwa wanamfananisha ni kweli kwa asilimia zote alikuwa ni raisi wa nchi ya Tanzania mheshimiwa Alan Mwaiponela mtu wa Tukuyu Mbeya huyu kwa asili yake japo yeye aligoma kabisa kwamba hakuwa mtu wa mbeya haikueleweka kwanini anakataa kwao sababu alikuwa nazo yeye mwenyewe, leo alikuwa ndani ya kijiji hiki akiwa na mlinzi wake mmoja tu basi na alionekana kuwa na haraka mno, ilishangaza mheshimiwa aiache ikulu yake takatifu na kwenda sehemu kama hiyo tena akiwa na mlinzi wake tu ilikuwa ni hatari sana kwa usalama wake. Alivaa suti ya bei ghali mno pamoja na kiatu ambacho kilienda shule mtaji wa mtu wa Manzese ulikuwa umevaliwa kwenye mguu wa mtu huyo.

Alitoa kitambaa na kujifuta jasho alionekana kuwa na haraka mno walikunja kwenye uchochoro mrefu ambao ulikuwa una migomba mingi sana, mlinzi wake alimpa ishara ya heshima kumuonyesha raisi wake kwamba waendelee kusonga mbele. Mbele yao kulikuwa na jumba moja kubwa sana la kifahari ndipo ambapo walionekana kuelekea.

"Mamaaaaaaa" ni sauti ya mwanamke mmoja mmama mama hivi alipiga makelele kuelekea ndani alionekana kuwa mfanyakazi pale ndani, kelele hizo ni kwa sababu hakuamini alicho kiona, mtu ambaye alikuwa anamuonaga kwenye televisheni leo alikuwa yupo mbele yake alikimbia mno akiwa ameshika sehemu ya moyo wake, walitoka watu wanne humo ndani nayeye alikuwa wa tano japo mbele walitangulia wazee wawili Bibi na babu kiufupi kwa sababu umri wao ulikuwa upo dakika za jioni sana.

Baada ya kufika nje walipigwa na butwaa sana kiasi kwamba wale wengine wote walikimbia na kurudi ndani kila mtu akihema na kujificha, kulikuwa ni jambo la kutisha raisi wa nchi kufika kwao kirahisi namna hiyo tena bila taarifa.

"Shikamoo mzee wangu, wewe ndiye baba yake na SEKELAGA?" Ni swali ambalo lilitoka kwenye kinywa cha raisi wa nchi ya Tanzania, liliwashtua sana wazee hao, mzee huyo ambaye ndiye aliyeulizwa alikuwa akitetemeka sana, mdomo wake ulitaka kusema kitu ila uliishia kutetemeka tu alishuka chini na kukaa hakuwa na nguvu za kuendelea kusimama.

Heeeeeey kwamba huyu ndiye mzee Philebert baba wa SEKELAGA ambaye alikuwa mke wa Mansour Omran wa kipindi kile na raisi kayajua vipi mambo ya siri haya? nooooooooooo akili yangu bado inakataaa kabisa, raisi ana uhusiano upi na hawa binadamu mpaka ahatarishe maisha yake kwenda BUKOBA tena akiwa na mlinzi mmoja huku akitembea kwa miguu kabisa?.......na vipi kuhusu yule mwanaume ambaye ametekwa kule BARAKUDA walio mchukua ni akina nani?.............

Amka ndo Kwanza kunakucha natupa kalamu yangu ndani ya ukurasa wa 18 panapo majaaliwa tukutane tena sehemu inayofuata.

Langu jina wananiita

Bux the story teller

Chao.
 
STORY: GEREZA LA HAZWA
STORY WRITER: FEBIANI BABUYA
STORY TELLER: Bux the story teller
AGE: 18+

UKURASA WA KUMI NA NANE

TULIPO ISHIA UKURASA WA KUMI NA SABA


"Kheeeee aliwezaje kuishi tena?" Takribani masaa 27 mpaka muda huo raisi na mzee huyo walikuwa wamekaa ndani ya chumba hicho kichafu sana cha GEREZA akiwa anasimuliwa historia ya huyo mtu aliingilia kati kuulizia aliweza vipi kupona kwenye hiyo hali, mzee huyo aliinama na kuinua uso wake na kuufungua tena.

"Huo ndio ulikuwa mwanzo wake wa kuwa binadamu ambaye ataishi miaka mingi sana akiwa bado yupo hai na itamchukua muda sana kuzeeka" raisi alishangaa mpaka akasimama alitamani kuondoka ila hilo lingemfanya asijue chochote kabisa kuhusu hadithi ambayo ni kama ilikuwa imefikia katikati hakuhitaji kuikosa hata nukta alirudi tena na kukaa chini ili apewe alicho hitaji kujua.
ENDELEA.....................

AVOCC STREET BARAKUDA TABATA DAR ES SALAAM

Mvua zilikuwa zinaendelea kunyesha ndani ya jiji hili Kama ilivyo kawaida huwa halitabiriki kabisa linapokuja suala la kushusha mvua, watu wachache walikuwa wanaonekana kuendelea na biashara zao kwenye kuutafuta mkate wa kila siku kwali ulikiwa ni usiku mzito lakini ilikuwa ni tofauti kwa mwanaume mmoja ambaye muda huo licha ya kuwa na mvua kali ambazo zlilileta halii ya ubaridi kwenye sehemu hii iliyokuwa na utajiri wa kutosha wa joto alikuwa akikimbizwa mithili ya mtu ambaye alikuwa amekula pesa za wanakijiji baridi lililokuwepo halikuwa na msaada wowote kwake alikuwa anavuja jasho ambalo lilisaidiwa kufutwa na maji ya mvua alikuwa akihema kwa nguvu mno. Hakuonekana mtu ambaye alikuwa anamfukuza maana alikuwa yupo pekeake ila alikuwa anakimbia kwa Kasi mno akikatiza chochoro nyingi kwa wepesi alionekana kuwa mwenyeji sana wa hii mitaa, hakuna mtu wa kawaida ambaye angeweza kuendana na kasi yake.

Alienda kusimama sehemu ambayo ilikuwa na uwanja mpana akiwa anahemeana kwa nguvu aliangaza kila upande hakuona mtu akaikunjua kola ya shati lake na kuanza kutembea alikuwa amechomekea vizuri sana kama ungekutana naye mchana basi usingesita kumpa vyeo vya ustaarabu hapa mjini ila bahati mbaya ilikuwa ni usiku wa manane ilikuwa ni ngumu sana kumpa hicho cheo bila kujua kilichokuwa kinamkimbiza ni nini. Alishtuka baada ya kusikia mtu anampigia makofi alisonya kwa hasira alikuwa amefanya kazi bure licha ya mbio zake zote bado aliishia kwenye njia za watu ambao ndio walimfanya usiku huo akurupuke sana na hizo mbio. Alitulia na kurudisha kumbukumbu zake nyuma namna alivyo wakimbia watu hao, dakika chache zilizopita alikuwa ndani ya ukumbi maarufu ujulikanao kama SMALL PLANET, huwa wanapaita TABATA KWA WALA BATA naye alikuwa mmoja wao mfuko ulituna angemhofia nani na Kodi kalipa alikuwa yupo na kimada mmoja ambaye aliona atamaliza naye safari yake ya starehe kwa siku hiyo.

Akiwa amekaa na mwanamke huyo ni zaidi ya dakika tano aliona kuna watu watatu wanamwangalia sana, alizuga kama anahama meza makusudi lakini bado watu hao macho yao yalikuwa kwake, alinyanyuka na kwenda chooni kuhakikisha kama je kweli walikuwa wanamfuatilia ni kweli mwanaume mmoja alinyanyuka naye na kuunga naye tera huko uani japo mtu huyo yeye hakuingia ndani alizuga mpaka mtu huyo alipotoka nje tena akawa anamfuata kwa nyuma. Mwanaume hakuwa Fala alielewa hiyo sehemu sio salama tena kwake alijifanya kama anaenda kaunta kulipia bili ambayo kiuhalisia alikuwa amelipa tangu anaagiza vinywaji hiyo ilikuwa nafasi ya kutoka nje, aligeuka na kuona watu hao wapo nae macho kwa macho aliingia kwenye uchochoro mmoja bila kujali mvua kali ambayo ilikuwa inaendelea kunyesha alishangaa nao wanamfuata, aliongeza mwendo nao waliongeza taa ya hatari ilizigusa sehemu za kichwa chake alianza kukimbia nao waliunga naye ila alishangaa wanatawanyika, mikimbio yao tu ilimpa tahadhali hawakuwa watu wa kawaida.

Alimaliza kutafakari kumbukumbu zake na sasa alikuwa anamshangaa mtu huyo ambaye alikuwa anampigia makofi alishangaa upande wa pili wake anatokea mtu mwingine na nyuma yake alitokea mwingine wote watatu walikuwa wamemuweka kati tayari.

"Mnataka nini kwangu?"

"Kwanini unatukimbia?"

"Nasimamaje nafuatiliwa kila nacho kifanya na watu ambao hata siwajui msinipotezee muda nina mambo mengi sana ya kufanya"

"Kwenye hayo maclub ndo una mambo mengi ya kufanya?"

"Fuata biashara zako yale sio maisha yako"

"Ok sawa, nifuate tuongozane kistaarabu tu tukifika mbele utaambiwa kwanini tumekuja kukuchukua hapa saivi"

"Hahahahahhaa yaani wewe hapo ndo unaongea kwa dharau kwamba unakuja kunichukua"

"Jiti Maalimu nadhani ndilo jina lako unatokea kwenye idara ya usalama wa taifa wa nchi ya Tanzania mpaka hapo inaonyesha nakujua kwahiyo usihitaji tukuchukue kwa nguvu bwana mdogo" mtu huyo ambaye kwa mara ya Kwanza tumemjua kama Jiti alipigwa na butwaa baada ya kutajiwa majina yake ya kweli ambayo alizaliwa nayo ukiachana na majina ambayo alikuwa anayatumia kwenye kazi yake hiyo ya usalama.

"Vipi tulishawahi kukutana kabla" alimuuliza mtu huyo ambayo kutokana na kiza hawakuwa wanaonana vizuri sura zao"

"Hilo jambo sio mhimu kwa sasa Ray ebu mchukueni tuondoke" mwanaume ambaye alijulikana kama Ray alipewa amri ya kumchukua mwanaume mwenzake kirahisi tu kama vile lililkuwa ni debe la karanga, Ray kama alivyokuwa ametajwa kwa jina lake moja tu alimsogelea mtu huyo mpaka alipokuwa alizungusha teke la chini ili kumzoa alimkosa, alizunguka teke lingine alijikuta anapiga hewa mtu huyo alikuwa mwepesi mno Ray aliyumba baada ya kukutana uso kwa uso na jabali la maana damu zilianza kumtoka mwanaume huyo alizunguka na double kick ambayo ilimpata Ray kifuani alizolewa mpaka ukutani mwa nyumba ambayo ilikuwa pembeni hapo, mwenzake alikuwa anakuja kwa spidi bila mpangilio alirusha ngumi alipitwa kwa juu na mtu huyo kwa sarakasi safi alipigwa ngumi ya mgongo iliyofuatiwa na teke zito alivyotaka kushuka kummalizia mtu huyo wa pili alijikuta yeye ndo anaenda chini aliishika shingo yake iliyokuwa na maumivu makali alikuwa amechomwa na sindano yenye sumu macho yake yalipoteza uangavu akaenda chini.

"Mbebeni tuondoke" aliongea yule mwanaume ambaye alionekana kuwa kiongozi wao tangu wanafika hapo, walimpakia kwenye mfuko mkubwa mmoja wao akamuweka begani wakapotelea vichochoroni.



KIBETA BUKOBA
Jua lililkuwa kali sana majira ya mchana wakati ni jua la utosi kabisa kama ilivyokuwa kawaida yao watu wastaarabu lakini wajivuni mno hawa Wahaya walikuwa wapo kwenye vigenge vyao vya kuufanya muda uende mbele kwenye hiki kijiji ambacho ni maarufu sana kwa maeneo yale watu walikuwa wako busy kuzielezea sarufi na visasili kwa sababu kwao darasa halikuwa shida kabisa kwenye vichwa vyao, ni siku ambayo ilikuwa ya ajabu japo wengine waliita ni siku ya bahati zaidi kwenye maisha yao, wakiwa hawana hili wala lile kwenye hicho kijiji chao lilitokea jambo la kushangaza ambalo kila mtu alikataa kabisa kuamini kwamba ni kweli limetokea hawakuwahi kuwa na kumbukumbu kwamba waliwahi kuwaza tukio kama hilo kufanyika kwenye kijiji chao. Ni kijiji ambacho kilijengwa mno na walio ishi hapo wengi walikuwa na ukwasi ambao haukuwafanya wawe na maisha ya kuombana chumvi.

"Hivi hili jambo ni la kweli au kuna namna watu wanatuchezea akili" aliuliza jamaa mmoja kwenye hiyo sehemu ambayo walikuwa na wenzake wakiwa wanapiga soga na kuongelea ishu za masomo nje ya nchi, alizubaa mpaka udenda ulimtoka na hakuna aliye mjali.

"Hope we are the luckiest generation ever" akiwa anamaanisha wao ndicho kizazi cha bahati zaidi kwenye historia, alikuwa ni mwingine ambaye yeye alionekana kuchekelea sana hilo jambo ila ilikuwa ni tofauti kwa mwenzao wa tatu yeye alikataa kabisa.

"Acheni upumbavu ninyi sio rahisi kama mnavyo fikiria acheni kuwa na akili za soda halafu mnalazimisha kunywa bia mtadhalilika wajinga nyie duniani watu ni wawili wawili unadhani mtu kama yule utamuona kama magazeti ya udaku namna hiyo hahahahha mnakuwa kama mitoto midogo nilishawahi kwenda huko SONGWE nikakutana na mtu ambaye nafanana naye kwa kila kitu mpaka namna ya kucheka acheni ushamba" yeye alijifanya ndiye aliwatani wa mji kila kitu alikijua yeye akiwapa na wenzake mifano kabisa.

"Sudi unavyozidi kukua naendelea kukushusha vyeo taratibu huwa unakurupuka tu bila mpangilio nadhani baba yako kutaka kukupeleka marekani kusoma hizo pesa ni bora tu akulipie mahali uoe hamna mtu hapo"

"Oya Maiko kuwa na heshima tusivuke mipaka kufikia hatua ya kutukanana nitakuzingua mwanangu heshima ikae mahala pake" palipita ukimya kwa sababu walionekana kuelekea kupigana juu ya kumbishania mtu. Mtu ambaye aliwafanya waache kila walichokuwa wanakifanya na kuanza kubishana alikuwa ni mtu ambaye alifanana sana na raisi wa nchi yao kwa kila kitu hata tukisema duniani wawili wawili jibu lilikiwa ni hapana walifanana mno ila kilicho wafanya wakatae kabisa kwamba huyo sio raisi wao ni namna alivyokuwa anazunguka mtaani walikuwa wapo wawili tu na wanajua raisi ndiye mtu anayelindwa zaidi ndani ya nchi hii isingewezekana akawa anazurula mtaani kiwepesi sana namna hiyo na tangu uchaguzi ufanyike hawakuwahi kutembelewa kabisa na raisi wao huyo japo walimpenda sana maana alikuwa mtu makini sana kwenye maendeleo ya taifa.

Fikra zao zilikuwa sahihi ila imani zao ziliwadanganya, huyo mtu ambaye walikuwa wanamfananisha ni kweli kwa asilimia zote alikuwa ni raisi wa nchi ya Tanzania mheshimiwa Alan Mwaiponela mtu wa Tukuyu Mbeya huyu kwa asili yake japo yeye aligoma kabisa kwamba hakuwa mtu wa mbeya haikueleweka kwanini anakataa kwao sababu alikuwa nazo yeye mwenyewe, leo alikuwa ndani ya kijiji hiki akiwa na mlinzi wake mmoja tu basi na alionekana kuwa na haraka mno, ilishangaza mheshimiwa aiache ikulu yake takatifu na kwenda sehemu kama hiyo tena akiwa na mlinzi wake tu ilikuwa ni hatari sana kwa usalama wake. Alivaa suti ya bei ghali mno pamoja na kiatu ambacho kilienda shule mtaji wa mtu wa Manzese ulikuwa umevaliwa kwenye mguu wa mtu huyo.

Alitoa kitambaa na kujifuta jasho alionekana kuwa na haraka mno walikunja kwenye uchochoro mrefu ambao ulikuwa una migomba mingi sana, mlinzi wake alimpa ishara ya heshima kumuonyesha raisi wake kwamba waendelee kusonga mbele. Mbele yao kulikuwa na jumba moja kubwa sana la kifahari ndipo ambapo walionekana kuelekea.

"Mamaaaaaaa" ni sauti ya mwanamke mmoja mmama mama hivi alipiga makelele kuelekea ndani alionekana kuwa mfanyakazi pale ndani, kelele hizo ni kwa sababu hakuamini alicho kiona, mtu ambaye alikuwa anamuonaga kwenye televisheni leo alikuwa yupo mbele yake alikimbia mno akiwa ameshika sehemu ya moyo wake, walitoka watu wanne humo ndani nayeye alikuwa wa tano japo mbele walitangulia wazee wawili Bibi na babu kiufupi kwa sababu umri wao ulikuwa upo dakika za jioni sana.

Baada ya kufika nje walipigwa na butwaa sana kiasi kwamba wale wengine wote walikimbia na kurudi ndani kila mtu akihema na kujificha, kulikuwa ni jambo la kutisha raisi wa nchi kufika kwao kirahisi namna hiyo tena bila taarifa.

"Shikamoo mzee wangu, wewe ndiye baba yake na SEKELAGA?" Ni swali ambalo lilitoka kwenye kinywa cha raisi wa nchi ya Tanzania, liliwashtua sana wazee hao, mzee huyo ambaye ndiye aliyeulizwa alikuwa akitetemeka sana, mdomo wake ulitaka kusema kitu ila uliishia kutetemeka tu alishuka chini na kukaa hakuwa na nguvu za kuendelea kusimama.

Heeeeeey kwamba huyu ndiye mzee Philebert baba wa SEKELAGA ambaye alikuwa mke wa Mansour Omran wa kipindi kile na raisi kayajua vipi mambo ya siri haya? nooooooooooo akili yangu bado inakataaa kabisa, raisi ana uhusiano upi na hawa binadamu mpaka ahatarishe maisha yake kwenda BUKOBA tena akiwa na mlinzi mmoja huku akitembea kwa miguu kabisa?.......na vipi kuhusu yule mwanaume ambaye ametekwa kule BARAKUDA walio mchukua ni akina nani?.............

Amka ndo Kwanza kunakucha natupa kalamu yangu ndani ya ukurasa wa 18 panapo majaaliwa tukutane tena sehemu inayofuata.

Langu jina wananiita

Bux the story teller

Chao.
STORY: GEREZA LA HAZWA
STORY WRITER: FEBIANI BABUYA
STORY TELLER: Bux the story teller
AGE: 18+

UKURASA WA KUMI NA TISA

TULIPO ISHIA UKURASA WA KUMI NA NANE
Baada ya kufika nje walipigwa na butwaa sana kiasi kwamba wale wengine wote walikimbia na kurudi ndani kila mtu akihema na kujificha, kulikuwa ni jambo la kutisha raisi wa nchi kufika kwao kirahisi namna hiyo tena bila taarifa.

"Shikamoo mzee wangu, wewe ndiye baba yake na SEKELAGA?" Ni swali ambalo lilitoka kwenye kinywa cha raisi wa nchi ya Tanzania, liliwashtua sana wazee hao, mzee huyo ambaye ndiye aliyeulizwa alikuwa akitetemeka sana, mdomo wake ulitaka kusema kitu ila uliishia kutetemeka tu alishuka chini na kukaa hakuwa na nguvu za kuendelea kusimama.

ENDELEA......................

Aliomba Kwanza dawa zake mzee huyo alikuwa anahema sana alikumbushiwa jambo ambalo hakuwahi kuhitaji kulikumbuka kwenye maisha yake yote, alikumbuka namna alivyo hangaika kutafuta namna ya kupata mtoto wa kike kwa miaka mingi sana,Mungu huwa hamtupi mja wake alikuja kumpa zawadi hiyo kwa baadae akamtunuku mtoto huyo jina la SEKELAGA ndiye alikuwa binti pekee na mtoto wa mwisho kwenye familia hiyo, alikuwa ni mtoto ambaye alipendwa sana kuliko kitu chochote alilelewa mithili ya yai lakini stori yake ilikuja kubadilika baada ya kumpeleka kwenye chuo kikubwa duniani cha OXFORD UNIVERSITY ambako alikutana na mwanaume aliye itwa Mansour Omran walikuja kupendana sana kiasi kwamba aliwagomea wazazi wake walivyo mwambia wamemuandlia mwanaume wa kumuoa kutoka huko kwao na huo ndio ulikuwa mwisho wao wa kumuona mpaka pale walipo letewa taarifa za msiba napo mzee Philebert aliwafukuza watu hao kutoka Libya kwa sababu alidai hamjui binti huyo ila moyo ulikuwa unamuma mno leo raisi alikuja kukitonesha kidonda chake.

Alibugia dawa zake akiwa analia mno pale chini, alijifuta machozi na kwa msaada wa Yule mlinzi wa raisi alimnyanyua maana umri ulikuwa umemtupa sana mkono mzee huyo, yeye na mkewe waliongoza mpaka pembeni mwa nyumba hiyo ambako kulikuwa na sehemu safi sana yenyw hewa ya kutosha hapo ndipo walipohitaji kufanya mazungumzo na mheshimiwa raisi ili kidogo awape sababu ya kuhitaji kumjua binti yao na alimjuaje. Raisi alionekana kuvutiwa sana na mazingira hayo aliyaangalia vizuri na kuketi chini walikuwa watu watatu tu mzee Philebert, raisi pamoja na mkewe Philebert.

"Umenishtua sana mheshimiwa baada ya ujio wako wa bila taarifa unajua wewe ni mtu mkubwa sana na huwa tunaishia kukuona tu kwenye runinga zetu hizi lakini kilicho nichanganya zaidi ni swali ulilo niuliza nimeshangaa unahusikaje nalo na kwanini unauliza hayo mambo" aliongeza mzee huyo akiwa anamwangalia raisi kwa umakini ni kama bado alikuwa haamini kama aliyekuwa mbele yake alikuwa ni raisi wa nchi ya Tanzania.

Mheshimiwa aliguna kidogo
"Ni kweli Kwanza unisamehe sana kwa kuja ghafla bila taarifa lakini nimefanya hivi kutokana na uzito wa jambo hili nikawa sina namna ndio maana mpaka kufika hapa kwako nimekuja kwa dharura sana hata ikulu hawajui ila kuna kitu nitafanya hakuna atakaye kuwa na hisia mbaya za mimi kuja hapa maana nahisi kuna watu walisha niona" maneno hayo yalimuingia vizuri huyo mzee ila ni kama alishtuka.

"Mheshimiwa unasema kulingana na uzito wa jambo lenyewe jambo gani hilo ni zito" raisi alimwangalia mzee huyo kwa umakini machoni ni kama alikuwa anamsoma.

"Lakini bado haujanijibu swali langu mzee wangu"

"Ni stori ndefu sana mheshimiwa ila kweli huyo uliye mtaja ni binti yangu na ndiye alikuwa mtoto wa kike pekee kwenye hii familia nilimpenda kuliko hata nafsi yangu, nilimfanyia kila kitu kwenye maisha yangu ila najutia sana maamuzi ambayo niliyafanya sikubahatika hata kuuaga mwili wake" aliongea kwa uchungu sana mkewe ndiye ambaye alikuwa anafanya kazi ya kumfuta machozi ni wazi walikuwa wakipenda sana.

"Mhhhhhh kwamba alishakufa?" Raisi aliuliza kwa mshangao lakini ni kama alikuwa anawapima watu hao alionekana kulijua hilo jambo

"Ndiyo ni miaka mingi sana imepita sasa nadhani hata thelathini inapita"

"Poleni sana kwa hilo tatizo, nimekuja hapa kuna taarifa za mhimu sana nimezipata ndio maana nimekuja mwenyewe ujue hili jambo ni siriasi sana, nahitaji nijue historia nzima ya huyu mtoto wenu mpaka siku ya mwisho" hakukuwa na namna zaidi ya kumsimulia mheshimiwa raisi kila kitu mpaka siku ambayo uliletwa msiba huko na mzee huyo aliukataa kwa kumfukuza Mansour Omran na familia yake na kukana kwamba yeye hana mtoto.

"Pole sana mzee haukupaswa kufanya maamuzi magumu hivyo yule bado alikuwa ni mtoto wako ulitakiwa ubaki hata na alama ya kaburi lake ambalo lingekutengenezea kumbukumbu bora sana kwa wakati ambao uliishi na mwanao".

"Hilo ndilo kosa ambalo huwa nalijutia mpaka Kesho na sijui nitakuja kulilipa vipi kwenye maisha yangu"
"Baada ya kuletewa msiba uliwahi kuuliza chanzo cha kifo chake labda?"

"Hapana nilikuwa na hasira sana kwa wakati ule niliwafukuza bila kuhitaji kujua chochote kile"

"Wewe bado una damu yako kule" ni kauli ambayo iliwashtua sana wale wazee wawili walihisi pengine raisi alikuwa amechanganyikiwa walimtaka arudie tena kauli yake.

"Kwa taarifa chache ambazo nimezipata kuhusu binti yenu ni kwamba alikufa muda mchache tu baada ya kujifungua mtoto wa kiume ambaye alipewa jina la Zakaria Mansour, inasemekana ni mwarabu lakini ukimuangalia unaipata sura ya mama yake na huyo mtoto mpaka leo yupo hai na ni mzima wa afya kabisa ila kuna tatizo kwenye upatikanaji wake.

"Mjukuu wangu yupo na ni mzima? Tafadhali mheshimiwa naomba nisaidie niweze hata kuugusa uso wake tu mwanangu anaweza kunisamehe huko aliko, sikuwahi kujua kama kuna damu yangu ipo mbali namimi tafadhali naomba sana" hakuamini alipiga magoti mbele ya raisi akiomba kukutanishwa na huyo mjukuu wake ambaye anahisi ingekuwa faraja kwa mtoto wake ambaye alimkataa huko aliko, ilikuwa ni miaka mingi sana imepita kumaanisha mtu huyo alikuwa ni mtu mzima kwa sasa.

"Mzee sio kirahisi sana namna hiyo ndiyo maana nimekuja hapa kwako ili tuongee" raisi alijibu na kunyamaza kidogo na kuzama mfukoni akatoa picha ndogo na kuiweka mezani

"Jina lake kamili anaitwa Zakaria Mansour ila huku anajulikana kama Alen, kilicho nifanya niunyanyue mguu wangu kutoka Dar es salaam mpaka huku ni juu yake. Kupitia mkurugenzi wa usalama wa taifa siku moja nilipata taarifa kwamba kwa miaka kadhaa iliyopita kuna picha zilitumwa kwenye mamlaka yetu ya mawasiliano na nchi ya Libya na picha hizo ndizo zilizokuwa zimetumwa kwamba wanamhitaji sana huyo mtu kwa gharama yoyote ile ni gaidi( babu na bibi walibaki wanashangaana) hivyo kama wana usalama wenzao waliomba msaada kwamba kama tutafanikiwa kumuona huku basi tuwape taarifa waje wamchukue na kwa sababu huwa tunasaidiana kwenye masuala ya usalama wa nchi tuliwakubalia.

Baadae tena walikuja wakatusisitizia kwamba ni mhimu sana hilo jambo, lilianza kunipa mashaka kwamba kwanini wanasiaitiza sana namna hiyo basi ikanilazimu nianze kufuatilia kupitia majasusi wetu ambao walikuwa wapo ndani ya nchi ya Libya walifanikiwa kuiba taarifa za mtu huyo zilivyokuja kunifikia sikuamini japo zilikuwa ni taarifa za siri mno alikuwa na asili mbili Libya na Tanzania na hiki ndicho kilicho nivutia kuhitaji kumjua kiundani baada ya kuiona nchi yangu pale. Baadae tulikuja kugundua kwamba anatafutwa kwa kesi ya mauaji ya familia mbili zenye watu 50 pamoja na kuua wanajeshi wengi sana huko kwao ukijumlisha na baadhi ya viongozi wa nchi yao hivyo walimchukulia kama muasi.

Niliamua kulifuatilia hilo jambo baada ya kushangazwa na taarifa nilizo zipata ya kwamba huyo mtu alikuwa ni mmoja wao sasa nikajiuliza kama alikuwa ni mmoja wao kwanini afanye hayo yote na kutafutwa sana namna hiyo? Maana yake lazima kulikuwa kuna jambo nyuma yake. Ilivyo julikana kwamba ana uraia wa nchi mbili basi moja kwa moja kama alikimbia kwao wakati anatafutwa hesabu iliyokuwa imebaki ni Tanzania tu pekee ilikuwa ni kweli kamera zetu za ulinzi za siri sana zilifanikiwa kuinasa sura ya mtu ambaye alikuwa anafanana nae kwa kila kitu hapo ndipo tulipo amua kuanza kumfuatilia mtu huyo kwenye kumpekua pekua tulifanikiwa kuipata historia ya mama yake na kugundua kwamba kwao ni huku BUKOBA ambapo nipo hapa leo.
Mtu huyo alionekana ndani ya jiji la Arusha ikabidi niwatumie watu wangu wa usalama ambao wapo kule walitafuta taarifa sana za yule mtu hawakuwahi kuipata hata nukta yake hivyo tukawa tumekosa ushahidi wa kujiaminisha kwamba ni yeye moja kwa moja kwani ndani ya Arusha alikuwa na maisha magumu sana fikra zetu zikatwambia huenda ni kijana tu mtafutaji kama wengine ila walikuwa ni watu ambao walifanana tu. Kilichokuja kunipa majibu kwamba alikuwa ni yeye ni baada ya kupotea kwenye mazingira ya kutatanisha sana kwa huyo kijana huko Arusha na hapo ndipo nikaamini huenda mawazo yangu halikuwa sahihi huyo alikuwa ni yeye mwenyewe swali alipotelea wapi? Mpaka sasa hakuna mtu yeyote anayejua imepita miaka kadhaa hakuna taarifa yake yoyote. Mheshimiwa alimeza mate kidogo na kuendelea.

"Nilikuwa na sababu kubwa mbili za kutowapa taarifa serikali ya Libya kwamba kuna mtu ninamhisi ni huyo mtu wao, sababu ya Kwanza ni baada ya kujua huyo mtu mama yake ni mtanzania nisingeweza kumdumbukiza kwenye shimo raia wangu hata kama nchi yangu bado haijaruhusu uraia pacha ila kwa namna moja au nyingine bado atabaki kuwa kama raia wa nchi hii ndio maana nilitaka nijiridhishe, lakini sababu ya pili ambayo ndiyo kubwa zaidi taarifa zake zilikuwa na ukakasi sana nilitaka kujua kafanya nini hasa ukiachana na kuua hao watu mpaka atafutwe na kusakwa sana namna hiyo wakati alikuwa ni mtu wao? Hilo ndilo suala lililo nipa mashaka sana nayajua vizuri mambo yanayo fanyika pale viongozi wanapo hitaji kuyalinda maslahi yao huenda kuna jambo kubwa sana hapa kati kati ndio maana sikukurupuka.

Kwenye kulijua hilo lililo jificha nilihitaji nipate baadhi ya taarifa kutoa kwenu ili ikiwezekana mimi niwe mtu wa Kwanza kukutana naye ili tujue sababu kubwa hasa ni nini kwa mtu mwenye asili ya nchi yetu kutafutwa sana namna hiyo, kuna kitu nimekipata kwenu nadhani hapa inatakiwa nianzie uchunguzi kwenye maisha ambayo aliyaishi huyo mtu baada tu ya mama yake kufa" ni maelezo marefu kidogo ambayo yalimfanya kila mtu hapo abakie kimya kabisa hawakujua waongeze nini au wapunguze nini.

"Haitajalisha kama yeye kafanya nini ila naomba unisaidie nimuone hata mara moja tu kabla sijakata kauli yangu ya mwisho" walionekana kutojali kuhusu historia yake ila wao walitamani tu kumuona mjukuu wao angalau hata mara moja tu bas kwao ingekuwa faraja kubwa sana.

"Nitafanya kila ninalo liweza kuona namna gani mtu huyu anapatikana haraka kabla hajaingia kwenye mikono yao hao watu, ila hili jambo ambalo limetokea hapa leo asije akaambiwa mtu yeyote yule kama kuna mtu atakuuliza kuhusu ujio wangu hapa mwambie nimekuja kuangalia afya yako na kukupa msaada baada ya kuita na kuzindua ujenzi wa mradi wa maji usije ukasema kitu chochote tofauti utakuwa umeiweka familia yako kwenye matatizo makubwa sana" baada ya kumaliza maongezi yake mheshimiwa alimpa ishara mlinzi wake alikuwa na kibegi kidogo mkononi raisi alikifungua kilijaa noti nyekundu za kutosha aliwapa wazee hao ambao walimshukuru sana.

Mchezo unazidi kuingia kwenye mikono ya watu wengi, raisi anatamani kumpata mtu ambaye tayari ameingia kwenye mikono ya watu ambao alikuw hataki wamtangulie, alihitaji sana kumjua huyu mtu kiundani ni nani hasa bahati mbaya alikuwa amechelewa sana.

GEREZA LA HAZWA 19 sina la ziada tukutane wakati ujao.

Langu jina wananiita

Bux the story teller

Chao
 
STORY: GEREZA LA HAZWA
STORY WRITER: FEBIANI BABUYA
STORY TELLER: Bux the story teller
AGE: 18+

UKURASA WA KUMI NA TISA

TULIPO ISHIA UKURASA WA KUMI NA NANE
Baada ya kufika nje walipigwa na butwaa sana kiasi kwamba wale wengine wote walikimbia na kurudi ndani kila mtu akihema na kujificha, kulikuwa ni jambo la kutisha raisi wa nchi kufika kwao kirahisi namna hiyo tena bila taarifa.

"Shikamoo mzee wangu, wewe ndiye baba yake na SEKELAGA?" Ni swali ambalo lilitoka kwenye kinywa cha raisi wa nchi ya Tanzania, liliwashtua sana wazee hao, mzee huyo ambaye ndiye aliyeulizwa alikuwa akitetemeka sana, mdomo wake ulitaka kusema kitu ila uliishia kutetemeka tu alishuka chini na kukaa hakuwa na nguvu za kuendelea kusimama.

ENDELEA......................

Aliomba Kwanza dawa zake mzee huyo alikuwa anahema sana alikumbushiwa jambo ambalo hakuwahi kuhitaji kulikumbuka kwenye maisha yake yote, alikumbuka namna alivyo hangaika kutafuta namna ya kupata mtoto wa kike kwa miaka mingi sana,Mungu huwa hamtupi mja wake alikuja kumpa zawadi hiyo kwa baadae akamtunuku mtoto huyo jina la SEKELAGA ndiye alikuwa binti pekee na mtoto wa mwisho kwenye familia hiyo, alikuwa ni mtoto ambaye alipendwa sana kuliko kitu chochote alilelewa mithili ya yai lakini stori yake ilikuja kubadilika baada ya kumpeleka kwenye chuo kikubwa duniani cha OXFORD UNIVERSITY ambako alikutana na mwanaume aliye itwa Mansour Omran walikuja kupendana sana kiasi kwamba aliwagomea wazazi wake walivyo mwambia wamemuandlia mwanaume wa kumuoa kutoka huko kwao na huo ndio ulikuwa mwisho wao wa kumuona mpaka pale walipo letewa taarifa za msiba napo mzee Philebert aliwafukuza watu hao kutoka Libya kwa sababu alidai hamjui binti huyo ila moyo ulikuwa unamuma mno leo raisi alikuja kukitonesha kidonda chake.

Alibugia dawa zake akiwa analia mno pale chini, alijifuta machozi na kwa msaada wa Yule mlinzi wa raisi alimnyanyua maana umri ulikuwa umemtupa sana mkono mzee huyo, yeye na mkewe waliongoza mpaka pembeni mwa nyumba hiyo ambako kulikuwa na sehemu safi sana yenyw hewa ya kutosha hapo ndipo walipohitaji kufanya mazungumzo na mheshimiwa raisi ili kidogo awape sababu ya kuhitaji kumjua binti yao na alimjuaje. Raisi alionekana kuvutiwa sana na mazingira hayo aliyaangalia vizuri na kuketi chini walikuwa watu watatu tu mzee Philebert, raisi pamoja na mkewe Philebert.

"Umenishtua sana mheshimiwa baada ya ujio wako wa bila taarifa unajua wewe ni mtu mkubwa sana na huwa tunaishia kukuona tu kwenye runinga zetu hizi lakini kilicho nichanganya zaidi ni swali ulilo niuliza nimeshangaa unahusikaje nalo na kwanini unauliza hayo mambo" aliongeza mzee huyo akiwa anamwangalia raisi kwa umakini ni kama bado alikuwa haamini kama aliyekuwa mbele yake alikuwa ni raisi wa nchi ya Tanzania.

Mheshimiwa aliguna kidogo
"Ni kweli Kwanza unisamehe sana kwa kuja ghafla bila taarifa lakini nimefanya hivi kutokana na uzito wa jambo hili nikawa sina namna ndio maana mpaka kufika hapa kwako nimekuja kwa dharura sana hata ikulu hawajui ila kuna kitu nitafanya hakuna atakaye kuwa na hisia mbaya za mimi kuja hapa maana nahisi kuna watu walisha niona" maneno hayo yalimuingia vizuri huyo mzee ila ni kama alishtuka.

"Mheshimiwa unasema kulingana na uzito wa jambo lenyewe jambo gani hilo ni zito" raisi alimwangalia mzee huyo kwa umakini machoni ni kama alikuwa anamsoma.

"Lakini bado haujanijibu swali langu mzee wangu"

"Ni stori ndefu sana mheshimiwa ila kweli huyo uliye mtaja ni binti yangu na ndiye alikuwa mtoto wa kike pekee kwenye hii familia nilimpenda kuliko hata nafsi yangu, nilimfanyia kila kitu kwenye maisha yangu ila najutia sana maamuzi ambayo niliyafanya sikubahatika hata kuuaga mwili wake" aliongea kwa uchungu sana mkewe ndiye ambaye alikuwa anafanya kazi ya kumfuta machozi ni wazi walikuwa wakipenda sana.

"Mhhhhhh kwamba alishakufa?" Raisi aliuliza kwa mshangao lakini ni kama alikuwa anawapima watu hao alionekana kulijua hilo jambo

"Ndiyo ni miaka mingi sana imepita sasa nadhani hata thelathini inapita"

"Poleni sana kwa hilo tatizo, nimekuja hapa kuna taarifa za mhimu sana nimezipata ndio maana nimekuja mwenyewe ujue hili jambo ni siriasi sana, nahitaji nijue historia nzima ya huyu mtoto wenu mpaka siku ya mwisho" hakukuwa na namna zaidi ya kumsimulia mheshimiwa raisi kila kitu mpaka siku ambayo uliletwa msiba huko na mzee huyo aliukataa kwa kumfukuza Mansour Omran na familia yake na kukana kwamba yeye hana mtoto.

"Pole sana mzee haukupaswa kufanya maamuzi magumu hivyo yule bado alikuwa ni mtoto wako ulitakiwa ubaki hata na alama ya kaburi lake ambalo lingekutengenezea kumbukumbu bora sana kwa wakati ambao uliishi na mwanao".

"Hilo ndilo kosa ambalo huwa nalijutia mpaka Kesho na sijui nitakuja kulilipa vipi kwenye maisha yangu"
"Baada ya kuletewa msiba uliwahi kuuliza chanzo cha kifo chake labda?"

"Hapana nilikuwa na hasira sana kwa wakati ule niliwafukuza bila kuhitaji kujua chochote kile"

"Wewe bado una damu yako kule" ni kauli ambayo iliwashtua sana wale wazee wawili walihisi pengine raisi alikuwa amechanganyikiwa walimtaka arudie tena kauli yake.

"Kwa taarifa chache ambazo nimezipata kuhusu binti yenu ni kwamba alikufa muda mchache tu baada ya kujifungua mtoto wa kiume ambaye alipewa jina la Zakaria Mansour, inasemekana ni mwarabu lakini ukimuangalia unaipata sura ya mama yake na huyo mtoto mpaka leo yupo hai na ni mzima wa afya kabisa ila kuna tatizo kwenye upatikanaji wake.

"Mjukuu wangu yupo na ni mzima? Tafadhali mheshimiwa naomba nisaidie niweze hata kuugusa uso wake tu mwanangu anaweza kunisamehe huko aliko, sikuwahi kujua kama kuna damu yangu ipo mbali namimi tafadhali naomba sana" hakuamini alipiga magoti mbele ya raisi akiomba kukutanishwa na huyo mjukuu wake ambaye anahisi ingekuwa faraja kwa mtoto wake ambaye alimkataa huko aliko, ilikuwa ni miaka mingi sana imepita kumaanisha mtu huyo alikuwa ni mtu mzima kwa sasa.

"Mzee sio kirahisi sana namna hiyo ndiyo maana nimekuja hapa kwako ili tuongee" raisi alijibu na kunyamaza kidogo na kuzama mfukoni akatoa picha ndogo na kuiweka mezani

"Jina lake kamili anaitwa Zakaria Mansour ila huku anajulikana kama Alen, kilicho nifanya niunyanyue mguu wangu kutoka Dar es salaam mpaka huku ni juu yake. Kupitia mkurugenzi wa usalama wa taifa siku moja nilipata taarifa kwamba kwa miaka kadhaa iliyopita kuna picha zilitumwa kwenye mamlaka yetu ya mawasiliano na nchi ya Libya na picha hizo ndizo zilizokuwa zimetumwa kwamba wanamhitaji sana huyo mtu kwa gharama yoyote ile ni gaidi( babu na bibi walibaki wanashangaana) hivyo kama wana usalama wenzao waliomba msaada kwamba kama tutafanikiwa kumuona huku basi tuwape taarifa waje wamchukue na kwa sababu huwa tunasaidiana kwenye masuala ya usalama wa nchi tuliwakubalia.

Baadae tena walikuja wakatusisitizia kwamba ni mhimu sana hilo jambo, lilianza kunipa mashaka kwamba kwanini wanasiaitiza sana namna hiyo basi ikanilazimu nianze kufuatilia kupitia majasusi wetu ambao walikuwa wapo ndani ya nchi ya Libya walifanikiwa kuiba taarifa za mtu huyo zilivyokuja kunifikia sikuamini japo zilikuwa ni taarifa za siri mno alikuwa na asili mbili Libya na Tanzania na hiki ndicho kilicho nivutia kuhitaji kumjua kiundani baada ya kuiona nchi yangu pale. Baadae tulikuja kugundua kwamba anatafutwa kwa kesi ya mauaji ya familia mbili zenye watu 50 pamoja na kuua wanajeshi wengi sana huko kwao ukijumlisha na baadhi ya viongozi wa nchi yao hivyo walimchukulia kama muasi.

Niliamua kulifuatilia hilo jambo baada ya kushangazwa na taarifa nilizo zipata ya kwamba huyo mtu alikuwa ni mmoja wao sasa nikajiuliza kama alikuwa ni mmoja wao kwanini afanye hayo yote na kutafutwa sana namna hiyo? Maana yake lazima kulikuwa kuna jambo nyuma yake. Ilivyo julikana kwamba ana uraia wa nchi mbili basi moja kwa moja kama alikimbia kwao wakati anatafutwa hesabu iliyokuwa imebaki ni Tanzania tu pekee ilikuwa ni kweli kamera zetu za ulinzi za siri sana zilifanikiwa kuinasa sura ya mtu ambaye alikuwa anafanana nae kwa kila kitu hapo ndipo tulipo amua kuanza kumfuatilia mtu huyo kwenye kumpekua pekua tulifanikiwa kuipata historia ya mama yake na kugundua kwamba kwao ni huku BUKOBA ambapo nipo hapa leo.
Mtu huyo alionekana ndani ya jiji la Arusha ikabidi niwatumie watu wangu wa usalama ambao wapo kule walitafuta taarifa sana za yule mtu hawakuwahi kuipata hata nukta yake hivyo tukawa tumekosa ushahidi wa kujiaminisha kwamba ni yeye moja kwa moja kwani ndani ya Arusha alikuwa na maisha magumu sana fikra zetu zikatwambia huenda ni kijana tu mtafutaji kama wengine ila walikuwa ni watu ambao walifanana tu. Kilichokuja kunipa majibu kwamba alikuwa ni yeye ni baada ya kupotea kwenye mazingira ya kutatanisha sana kwa huyo kijana huko Arusha na hapo ndipo nikaamini huenda mawazo yangu halikuwa sahihi huyo alikuwa ni yeye mwenyewe swali alipotelea wapi? Mpaka sasa hakuna mtu yeyote anayejua imepita miaka kadhaa hakuna taarifa yake yoyote. Mheshimiwa alimeza mate kidogo na kuendelea.

"Nilikuwa na sababu kubwa mbili za kutowapa taarifa serikali ya Libya kwamba kuna mtu ninamhisi ni huyo mtu wao, sababu ya Kwanza ni baada ya kujua huyo mtu mama yake ni mtanzania nisingeweza kumdumbukiza kwenye shimo raia wangu hata kama nchi yangu bado haijaruhusu uraia pacha ila kwa namna moja au nyingine bado atabaki kuwa kama raia wa nchi hii ndio maana nilitaka nijiridhishe, lakini sababu ya pili ambayo ndiyo kubwa zaidi taarifa zake zilikuwa na ukakasi sana nilitaka kujua kafanya nini hasa ukiachana na kuua hao watu mpaka atafutwe na kusakwa sana namna hiyo wakati alikuwa ni mtu wao? Hilo ndilo suala lililo nipa mashaka sana nayajua vizuri mambo yanayo fanyika pale viongozi wanapo hitaji kuyalinda maslahi yao huenda kuna jambo kubwa sana hapa kati kati ndio maana sikukurupuka.

Kwenye kulijua hilo lililo jificha nilihitaji nipate baadhi ya taarifa kutoa kwenu ili ikiwezekana mimi niwe mtu wa Kwanza kukutana naye ili tujue sababu kubwa hasa ni nini kwa mtu mwenye asili ya nchi yetu kutafutwa sana namna hiyo, kuna kitu nimekipata kwenu nadhani hapa inatakiwa nianzie uchunguzi kwenye maisha ambayo aliyaishi huyo mtu baada tu ya mama yake kufa" ni maelezo marefu kidogo ambayo yalimfanya kila mtu hapo abakie kimya kabisa hawakujua waongeze nini au wapunguze nini.

"Haitajalisha kama yeye kafanya nini ila naomba unisaidie nimuone hata mara moja tu kabla sijakata kauli yangu ya mwisho" walionekana kutojali kuhusu historia yake ila wao walitamani tu kumuona mjukuu wao angalau hata mara moja tu bas kwao ingekuwa faraja kubwa sana.

"Nitafanya kila ninalo liweza kuona namna gani mtu huyu anapatikana haraka kabla hajaingia kwenye mikono yao hao watu, ila hili jambo ambalo limetokea hapa leo asije akaambiwa mtu yeyote yule kama kuna mtu atakuuliza kuhusu ujio wangu hapa mwambie nimekuja kuangalia afya yako na kukupa msaada baada ya kuita na kuzindua ujenzi wa mradi wa maji usije ukasema kitu chochote tofauti utakuwa umeiweka familia yako kwenye matatizo makubwa sana" baada ya kumaliza maongezi yake mheshimiwa alimpa ishara mlinzi wake alikuwa na kibegi kidogo mkononi raisi alikifungua kilijaa noti nyekundu za kutosha aliwapa wazee hao ambao walimshukuru sana.

Mchezo unazidi kuingia kwenye mikono ya watu wengi, raisi anatamani kumpata mtu ambaye tayari ameingia kwenye mikono ya watu ambao alikuw hataki wamtangulie, alihitaji sana kumjua huyu mtu kiundani ni nani hasa bahati mbaya alikuwa amechelewa sana.

GEREZA LA HAZWA 19 sina la ziada tukutane wakati ujao.

Langu jina wananiita

Bux the story teller

Chao
STORY: GEREZA LA HAZWA
STORY WRITER: FEBIANI BABUYA
STORY TELLER: Bux the story teller
AGE: 18+

UKURASA WA ISHIRINI

TULIPO ISHIA UKURASA WA KUMI NA TISA
"Haitajalisha kama yeye kafanya nini ila naomba unisaidie nimuone hata mara moja tu kabla sijakata kauli yangu ya mwisho" walionekana kutojali kuhusu historia yake ila wao walitamani tu kumuona mjukuu wao angalau hata mara moja tu bas kwao ingekuwa faraja kubwa sana.

"Nitafanya kila ninalo liweza kuona namna gani mtu huyu anapatikana haraka kabla hajaingia kwenye mikono yao hao watu, ila hili jambo ambalo limetokea hapa leo asije akaambiwa mtu yeyote yule kama kuna mtu atakuuliza kuhusu ujio wangu hapa mwambie nimekuja kuangalia afya yako na kukupa msaada baada ya kuita na kuzindua ujenzi wa mradi wa maji usije ukasema kitu chochote tofauti utakuwa umeiweka familia yako kwenye matatizo makubwa sana" baada ya kumaliza maongezi yake mheshimiwa alimpa ishara mlinzi wake alikuwa na kibegi kidogo mkononi raisi alikifungua kilijaa noti nyekundu za kutosha aliwapa wazee hao ambao walimshukuru sana.

ENDELEA............................
Mheshimiwa raisi alitoka hiyo sehemu na kuanza kuondoka hakuwa na kingine cha kusubiri tena
"Wanaonekana hawajui kitu chochote kile kinacho endelea na huenda wakaingia kwenye hatari kubwa sana fanya kila unalo liweza hakikisha unawatoa hapa mapema sana najua watajulikana muda sio mrefu hilo litakuwa tatizo kubwa kwa upande wao lakini pia nahitaji uchimbe kwa undani uniletee taarifa za kutosha kuhusiana na huyo mtu kwanini binadamu asakamwe namna hii kuliko hata taifa lake linavuowekeza kwenye uchumi wake huenda kuna mambo mazito ya kutosha yanayo husiana na hili jambo" Raisi alikuwa anaongea na mlinzi wake akimpaka maagizo aligeuka tena na kuiangalia nyumba hiyo kwa umakini sana.

"Sawa mkuu nitalifanyia Kazi mapema sana"

"Good" raisi alivyo maliza kujibu tu yaliibuka magari ya jeshi yapatayo kumi walishuka wanajeshi wakiwa na silaha kali sana walishuka kwa haraka, wote walitoa heshima kwa kiongozi wao wa nchi, kwenye gari la pili yake alishuka RPC pamoja na kamanda wa jeshi la wananchi mkoa walitoa heshima kwa kiongozi wao.

"Mheshimiwa ni jambo la hatari sana hili ambalo unajaribu kulifanya kumbuka unakuwa unaliingiza taifa kwenye matatizo mazito kufanya hivi, hapa sio muda mrefu nimepokea taarifa kutoka kwa viongozi wakubwa wa kiusalama baada ya kugundua kwamba haupo Ikulu na vifaa vya mawasiliano vikaonyesha upo huku ndiyo maana tumefanya kila namna tuwahi tunaomba sana usije ukarudia kufanya hili jambo unaziweka mashakani roho za watu pamoja na kazi za watu wanaweza kufukuzwa" RPC aliongea kwa unyenyekevu sana alichokuwa anakiongea alikuwa sahihi sio kawaida raisi kufanya jambo kama hilo bila taarifa. Alan mwaiponela raisi huyu wa jamhuri ya muungano wa Tanzania alijiangalia kwenye bega lake la kulia na kutabasamu hapo palikuwa na kifaa cha mawasiliano huwa ni lazima raisi na familia yake kwa ujumla kuwekewa aina hiyo ya ulinzi ili iwe ni rahisi kuwapata pale wanapo potea, kabla hajajibu chochote zilisikika chopa za kijeshi angani watu wa Ikulu walikuwa wamefika kuhakikisha usalama wa kiongozi wao.

"Nashukuru kwa umakini wenu RPC na mwenzako ni mambo ya mhimu sana yamenileta huku sikutaka mtu yeyote ajue basi kwa sababu ishajulikana hatakiwi mtu yeyote kujua kuhusu kilicho tokea hapa naenda kuzindua mradi wa maji wa kijiji hiki ambao alitakiwa kuniwakilisha mkuu wa mkoa mwishoni mwa mwezi huu, nitasema nimekuja kwa kuwashtukiza kwa sababu sikutaka mradi huo uchelewe, si kila kitu kipo tayari kule?" Aliongea kijasiri sana mheshimiwa ulinzi ulikuwa ni mkubwa sana.

"Ndiyo kila kitu kipo sawa kilichokuwa kinasubiriwa ni uzinduzi tu ili watu waanze kunufaika na mradi"

"Ok twende saivi". Raisi wakati anaanza kunyanyua hatua zake walisogea watu wa usalama kwa Kasi kuhakikisha kama bosi wao alikuwa yupo salama raisi alifurahi sana vijana wake walikuwa makini mno kwenye kuhakikisha usalama wake, alianza kuondoka na kuelelea ulipo mradi wa maji hakuna mwananchi ambaye aliamini kwamba kweli huyo alikuwa ni raisi mwenyewe na ndiye ambaye alikuwa anaenda kuuzindua huo mradi wao kwa niaba ya mkuu wa mkoa, watu walifurahi mno mradi ulizinduliwa rasmi na raisi aliongea kidogo na kuwapa ahadi za kutosha. Wakati anatoka kwenye kuzindua huo mradi mkuu wa mkoa alitoka anakimbia mbio mbio akihema sana alipewa taarifa muda mchache uliopita kwamba raisi alikuwa kwenye mkoa wake hivyo aliwahi sana kufika eneo la tukio alikuta ndo wanamaliza mheshimiwa alimtaka asiwe na wasiwasi aliamua tu kuja kuwatembelea raia wake akaamua na kuuzindua mradi huo yeye angempa majukumu mengine.

Mambo yaliisha na raisi alipanda kwenye helikopita ili kuwahishwa Ikulu, watu walifurahi sana ndani ya kijiji hicho cha KIBETA japo maswali ambayo yalibaki kwenye vichwa vyao ilikuwa ni raisi alikuwa anatafuta nini kwenye familia ya mzee Philebert? hakuna mtu ambaye alikuwa na uwezo wa kutoa majibu ya swali hilo hata walipo mfuata mzee huyo na kumuuliza jibu lake lililkuwa rahisi sana kwamba mheshimiwa alikuja kuzindua mradi wa maji basi katika pita pita yake yeye akabahatika kutembelewa na kiongozi huyo mkubwa zaidi wa nchi watu wengi waliishia kuguna tu kwa sababu familia zilikuwa ni nyingi sana kwanini iwe yeye tu bahati mbaya hakuna ambaye alikuwa ana uwezo wa kuubadilisha uhalisia watu waliamua kuyaacha mambo yawe kama yalivyo tu.



TABATA KWA WALA BATA (BARAKUDA)
Joto lililkuwa kali mno ilikuwa ni ngumu kulihimili kwa muda mrefu huenda ni kutokana na udogo wa chumba lakini haikuwa hivyo tu bali hata ukosefu wa rasilimali za kulipunguza joto hilo kama kiyoyozi na kukosekana kabisa kwa madirisha humo ndani, joto ndilo lililo mfanya mwanaume huyo aamke kutoka kwenye usingizi mzito sana maana alihisi kama vile mwili wake unachomwa kwa moto alikuwa amelowa jasho nguo zake zote zilikuwa hazitamaniki kabisa. Kichwa chake kilikuwa kizito pale alipojaribu kukinyanyua ili akae sawa alikirudisha tena chini shingo ilikuwa inamuma alimeza mate kwa shida akakiiunua tena wakati huu alifanikiwa kukiinua akayafumbua macho yake mbele hakuona chochote kile kutokana na kiza kinene ambacho kilikuwepo humo alijaribu kunyanyuka mikono ilimsaliti ndipo alipokuja kugundua kwamba alikuwa amefungwa kwenye kiti cha chuma alijitikisa aliishia kujiumiza tu ikabidi atulie Kwanza hakuelewa alifikaje hapo. Kumbukumbu zake zilimrejesha kutoka kwenye kuwakimbia wale watu kule mtaani baada ya kutoka ndani ya club ya Small PLANET hakuelewa muda huo alikuwa wapi maana hakukumbuka kilicho endelea baada ya yeye kuchomwa sindano ya shingo alilaani sana hicho kitu.
Alipiga makelele ili kama kuna mtu wa karibu yake aje amsikilize alishangaa baada ya kuona sauti inayotoka ni ndogo sana angemsikia mtu ambaye alikuw karibu sana kwa maana ilikuwa ni kama ananong'ona pekeyake, koo lililkuwa linamuua aligundua alikuwa na kiu kikali kutokana na joto la humo ndani alifanya maombi ili MUNGU amnusuru na kikombe ambacho kilikuwa mbele yake kugundulika kwamba yeye ni usalama wa taifa lilikuwa ni kosa kubwa. Zilipita dakika tano mlango ulifunguliwa mwanga wa taa za nje ya hicho chumba ulisaidia kidogo kupunguza hicho kiza lakini baadae tena ulipotea baada ya mlango kufungwa kwa ndani alikuwa ameingia mwanaume mmoja mrefu kiasi mweusi
"Humu ndani kuna joto sana unawezaje kuhimili hii hali na ukawa salama aisee" mwanaume huyo aliongea akiwa anawasha chemli ya mafuta ambayo nayo ilikuwa inaongeza joto sana Jiti kama alivyotambulika mwanzo alikua wazi leo ameingia cha kike, mwanga ulisambaa humo ndani ndipo alipopata bahati ya kukiona hicho chumba vizuri kulikuwa na mavyuma vyuma mengi sana na box ambalo lilikuwa na msalaba mwekundu alimeza mate baada ya kuliona alijua kazi yake vizuri sana, mwanaume huyo aliyekuwa mbele yake alimtazama sana aliona namna mwenzake alivyokuwa anaramba ramba midomo yake akiwa na kiu kikali alisikitika sana na kuinamia sehemu ambayo mwenzake huyo alifungwa hapo alitoa kikopo cha maji kwenye mfuko wa koti lake la kummiminia Jiti kwenye mdomo wake ambaye aliyafakamia kama fisi aliyepata mzoga bila kutegemea.

"Sikutakiwa kufanya hivi ila wewe ni kijana mwenzangu kuna muda mimi mwenyewe nina moyo wa kibinadamu pia imeniuma kukuona kwenye hiyo hali ndugu yangu ila sina namna haya ni maisha ambayo nilisha yachagua hivyo sina namna ya kufanya" alikuwa akiongea huku akikifunga kikopo chake cha maji na kukirudisha mfukoni kisha akasimama tena.

"Asante sana ndugu yangu sidhani kama nilikwua hata na dakika kumi za kuendelea kuwa hai nilikuwa na kiu kikali mno nashukuru sana, hivi hapa niko wapi na napaswa kufanya nini?" Kauli yake ilimfanya yuule mwanaume amwangalie sana kwa mara nyingine na kutikisa kichwa kuonyesha masikitiko yake kwa mwenzake huyo.

"Sina imani sana na safari ya maisha yako kuwa ndefu ila mdomo wako ndio utakao kuhakikishia wewe kuwa salama, mimi sihusiki na kuamua hatima ya maisha yako kwa sababu nilikuwa na kazi ya kukukamata tu na kukuleta hapa, ndani ya dakika kumi na tano zijazo anakuja kiongozi hapa huyo ndiye ameyashika maisha yako kwenye mkono wake" aliongea bila wasiwasi.

"Ina maana wewe ndiye uliyekuwa na wenzako wawili na kuamuru wanikamate?"

"Yes ndo mimi hapa hata hujakosea"

"Kwanini umeamua kuishi maisha ya namna hii na unaonekana ni mtu mwema kabisa?"

"Kuna mambo mengi sana kwenye maisha kabla ya kuwaza kwa uchache kulingana na ubongo wako unapofikia kufikiria, sio kila mwanadamu yupo kama akili yako inavyowaza maisha yana mambo mengi sana na ukiwa sehemu ambayo unapata kila kitu huwezi ukayaelewa mpaka siku uwe hauna namna ndo utaelewa kwamba ni kwanini binadamu huwa wanayachukua maamuzi magumu kwenye maisha na kuyaacha maamuzi mepesi" aliongea na kutoka humo ndani hakuhitaji tena stori maana mtu huyo alitaka kuleta kujuana sana kitu ambacho kulikuwa ni hatari kwenye maeneo kama hayo ambayo hayatakiwi kabisa watu kuaminiana.

Alishuhudia mlango ukifunguliwa tena raundi hii taa ziliwashwa chemli ilijizima yenyewe, mbele ya mlango alikuwa amesimama mwanaume mmoja ambaye alikuwa na asili ya kiarabu, alikuwa amevaa traki nyeupe kifua kilikuw wazi kilipasuka sana alikuwa ni mtu kazi haswa hata chini alikuwa peku licha ya sakafu kuwa na joto la kutosha kwake lilionekana kuwa la kawaida tu kichwani alikifunga kitambaa cheupe.

"Nilipokuwa na miaka nane ndiyo ilikuwa mara yangu ya kwanza kuua, ni siku ambayo kila muda huwa inapita kwenye kichwa changu kwangu ulikuwa ni usiku mzito sana siku ile ila sikuwa na namna kwa sababu tayari ilikuwa imeshatokea sikuwa na uwezo wa kuyarudisha mambo kama yalivyokuwa mwanzo ikabidi niukubali ukweli tu kwamba niliua, walikuwa watu ishirini niliwapiga wote risasi kwa mkono wangu nikiwa nalia na sababu kubwa ya kuwaua ni kwamba mdugu yao mmoja alikimbia na kete moja ya madawa ya kulevya ila aliyaponza maisha ya ndugu zake wote kumi na tisa nayeye akiwa wa ishirini. Nililia mno siku ile kwa sababu nililazimishwa kufanya vile na bosi wangu ndani ya nchi ile ya Morocco, tangu pale nimekuwa muuaji bora mno ambaye huwa sijiulizi hata mara mbili kuichukua nafsi ya mtu ni suala la sekunde tu na huwa najisikia vizuri sana napo itoa nafsi ya mtu(alimeza mate kidogo).

Jina langu naitwa Qader mimi sio mzaliwa wa nchi hii wala sikuwahi kutegemea kuja kuishi kwenye nchi hii hata kuzungumza lugha ya nchi hii ambayo ni Kiswahili sikuwahi kufikiria kabisa kuizungumza ila imetokea kwa sasa mimi ni miongoni mwa watu ambao wanaishi Tanzania kwa miaka zaidi ya mitano sasa nishakuwa mwenyeji mpaka lugha yenu naijua vizuri kiufupi mimi mwenyewe kwa sasa ni mswahili mzuri tu, sitaki mimi nawewe tufike mbali sana bado una nafasi ya kuwa mtu hai badala ya historia yako kuishia kwenye chumba hiki.

Mtu ambaye ulipewa kazi ya kuyafuatilia maisha yake na mpaka sasa unaifanya hiyo kazi ni mtu ambaye ninamhitaji kwa gharama yoyote ile na ni lazima nimpate, najua una baadhi ya taarifa za mhimu sana kumhusu mtu huyu hivyo sitataka uanze kupindisha jambo lolote lile kuhusu hizi taarifa nimekufuatilia kwa muda mrefu sana hivyo sijabahatisha kuja kwako kwahiyo kila neno ambalo utalitoa kwenye mdomo wako lipime kwanza na uelewe aina ya mtu ambaye unaongea naye sio muda mrefu nitageuka kuwa shetani humu ndani" mwanaume huyo aliongea bila kitetemeshi alikuwa anajiamini sana mkononi mwake alikuwa na sigara ambayo alipiga mafunda kadhaa na kuizima kwa mguu wake uliokuwa peku.

"Unahitaji taarifa za mtu gani?"

"Zakaria Mansour" Jiti alitoa macho hakuamini alichokuwa anaambiwa huyo mtu alikuwa anasakwa na kila mtu alifanya nini kwani? .......hata mimi nimebaki njiapanda kama wewe ulivyo achwa na mshangao.....

Binafsi 20 sina la ziada tena panapo majaaliwa tukutane wakati ujao.

Bye-bye

Bux the story teller
 
STORY: GEREZA LA HAZWA
STORY WRITER: FEBIANI BABUYA
STORY TELLER: Bux the story teller
AGE: 18+

UKURASA WA ISHIRINI

TULIPO ISHIA UKURASA WA KUMI NA TISA
"Haitajalisha kama yeye kafanya nini ila naomba unisaidie nimuone hata mara moja tu kabla sijakata kauli yangu ya mwisho" walionekana kutojali kuhusu historia yake ila wao walitamani tu kumuona mjukuu wao angalau hata mara moja tu bas kwao ingekuwa faraja kubwa sana.

"Nitafanya kila ninalo liweza kuona namna gani mtu huyu anapatikana haraka kabla hajaingia kwenye mikono yao hao watu, ila hili jambo ambalo limetokea hapa leo asije akaambiwa mtu yeyote yule kama kuna mtu atakuuliza kuhusu ujio wangu hapa mwambie nimekuja kuangalia afya yako na kukupa msaada baada ya kuita na kuzindua ujenzi wa mradi wa maji usije ukasema kitu chochote tofauti utakuwa umeiweka familia yako kwenye matatizo makubwa sana" baada ya kumaliza maongezi yake mheshimiwa alimpa ishara mlinzi wake alikuwa na kibegi kidogo mkononi raisi alikifungua kilijaa noti nyekundu za kutosha aliwapa wazee hao ambao walimshukuru sana.

ENDELEA............................
Mheshimiwa raisi alitoka hiyo sehemu na kuanza kuondoka hakuwa na kingine cha kusubiri tena
"Wanaonekana hawajui kitu chochote kile kinacho endelea na huenda wakaingia kwenye hatari kubwa sana fanya kila unalo liweza hakikisha unawatoa hapa mapema sana najua watajulikana muda sio mrefu hilo litakuwa tatizo kubwa kwa upande wao lakini pia nahitaji uchimbe kwa undani uniletee taarifa za kutosha kuhusiana na huyo mtu kwanini binadamu asakamwe namna hii kuliko hata taifa lake linavuowekeza kwenye uchumi wake huenda kuna mambo mazito ya kutosha yanayo husiana na hili jambo" Raisi alikuwa anaongea na mlinzi wake akimpaka maagizo aligeuka tena na kuiangalia nyumba hiyo kwa umakini sana.

"Sawa mkuu nitalifanyia Kazi mapema sana"

"Good" raisi alivyo maliza kujibu tu yaliibuka magari ya jeshi yapatayo kumi walishuka wanajeshi wakiwa na silaha kali sana walishuka kwa haraka, wote walitoa heshima kwa kiongozi wao wa nchi, kwenye gari la pili yake alishuka RPC pamoja na kamanda wa jeshi la wananchi mkoa walitoa heshima kwa kiongozi wao.

"Mheshimiwa ni jambo la hatari sana hili ambalo unajaribu kulifanya kumbuka unakuwa unaliingiza taifa kwenye matatizo mazito kufanya hivi, hapa sio muda mrefu nimepokea taarifa kutoka kwa viongozi wakubwa wa kiusalama baada ya kugundua kwamba haupo Ikulu na vifaa vya mawasiliano vikaonyesha upo huku ndiyo maana tumefanya kila namna tuwahi tunaomba sana usije ukarudia kufanya hili jambo unaziweka mashakani roho za watu pamoja na kazi za watu wanaweza kufukuzwa" RPC aliongea kwa unyenyekevu sana alichokuwa anakiongea alikuwa sahihi sio kawaida raisi kufanya jambo kama hilo bila taarifa. Alan mwaiponela raisi huyu wa jamhuri ya muungano wa Tanzania alijiangalia kwenye bega lake la kulia na kutabasamu hapo palikuwa na kifaa cha mawasiliano huwa ni lazima raisi na familia yake kwa ujumla kuwekewa aina hiyo ya ulinzi ili iwe ni rahisi kuwapata pale wanapo potea, kabla hajajibu chochote zilisikika chopa za kijeshi angani watu wa Ikulu walikuwa wamefika kuhakikisha usalama wa kiongozi wao.

"Nashukuru kwa umakini wenu RPC na mwenzako ni mambo ya mhimu sana yamenileta huku sikutaka mtu yeyote ajue basi kwa sababu ishajulikana hatakiwi mtu yeyote kujua kuhusu kilicho tokea hapa naenda kuzindua mradi wa maji wa kijiji hiki ambao alitakiwa kuniwakilisha mkuu wa mkoa mwishoni mwa mwezi huu, nitasema nimekuja kwa kuwashtukiza kwa sababu sikutaka mradi huo uchelewe, si kila kitu kipo tayari kule?" Aliongea kijasiri sana mheshimiwa ulinzi ulikuwa ni mkubwa sana.

"Ndiyo kila kitu kipo sawa kilichokuwa kinasubiriwa ni uzinduzi tu ili watu waanze kunufaika na mradi"

"Ok twende saivi". Raisi wakati anaanza kunyanyua hatua zake walisogea watu wa usalama kwa Kasi kuhakikisha kama bosi wao alikuwa yupo salama raisi alifurahi sana vijana wake walikuwa makini mno kwenye kuhakikisha usalama wake, alianza kuondoka na kuelelea ulipo mradi wa maji hakuna mwananchi ambaye aliamini kwamba kweli huyo alikuwa ni raisi mwenyewe na ndiye ambaye alikuwa anaenda kuuzindua huo mradi wao kwa niaba ya mkuu wa mkoa, watu walifurahi mno mradi ulizinduliwa rasmi na raisi aliongea kidogo na kuwapa ahadi za kutosha. Wakati anatoka kwenye kuzindua huo mradi mkuu wa mkoa alitoka anakimbia mbio mbio akihema sana alipewa taarifa muda mchache uliopita kwamba raisi alikuwa kwenye mkoa wake hivyo aliwahi sana kufika eneo la tukio alikuta ndo wanamaliza mheshimiwa alimtaka asiwe na wasiwasi aliamua tu kuja kuwatembelea raia wake akaamua na kuuzindua mradi huo yeye angempa majukumu mengine.

Mambo yaliisha na raisi alipanda kwenye helikopita ili kuwahishwa Ikulu, watu walifurahi sana ndani ya kijiji hicho cha KIBETA japo maswali ambayo yalibaki kwenye vichwa vyao ilikuwa ni raisi alikuwa anatafuta nini kwenye familia ya mzee Philebert? hakuna mtu ambaye alikuwa na uwezo wa kutoa majibu ya swali hilo hata walipo mfuata mzee huyo na kumuuliza jibu lake lililkuwa rahisi sana kwamba mheshimiwa alikuja kuzindua mradi wa maji basi katika pita pita yake yeye akabahatika kutembelewa na kiongozi huyo mkubwa zaidi wa nchi watu wengi waliishia kuguna tu kwa sababu familia zilikuwa ni nyingi sana kwanini iwe yeye tu bahati mbaya hakuna ambaye alikuwa ana uwezo wa kuubadilisha uhalisia watu waliamua kuyaacha mambo yawe kama yalivyo tu.



TABATA KWA WALA BATA (BARAKUDA)
Joto lililkuwa kali mno ilikuwa ni ngumu kulihimili kwa muda mrefu huenda ni kutokana na udogo wa chumba lakini haikuwa hivyo tu bali hata ukosefu wa rasilimali za kulipunguza joto hilo kama kiyoyozi na kukosekana kabisa kwa madirisha humo ndani, joto ndilo lililo mfanya mwanaume huyo aamke kutoka kwenye usingizi mzito sana maana alihisi kama vile mwili wake unachomwa kwa moto alikuwa amelowa jasho nguo zake zote zilikuwa hazitamaniki kabisa. Kichwa chake kilikuwa kizito pale alipojaribu kukinyanyua ili akae sawa alikirudisha tena chini shingo ilikuwa inamuma alimeza mate kwa shida akakiiunua tena wakati huu alifanikiwa kukiinua akayafumbua macho yake mbele hakuona chochote kile kutokana na kiza kinene ambacho kilikuwepo humo alijaribu kunyanyuka mikono ilimsaliti ndipo alipokuja kugundua kwamba alikuwa amefungwa kwenye kiti cha chuma alijitikisa aliishia kujiumiza tu ikabidi atulie Kwanza hakuelewa alifikaje hapo. Kumbukumbu zake zilimrejesha kutoka kwenye kuwakimbia wale watu kule mtaani baada ya kutoka ndani ya club ya Small PLANET hakuelewa muda huo alikuwa wapi maana hakukumbuka kilicho endelea baada ya yeye kuchomwa sindano ya shingo alilaani sana hicho kitu.
Alipiga makelele ili kama kuna mtu wa karibu yake aje amsikilize alishangaa baada ya kuona sauti inayotoka ni ndogo sana angemsikia mtu ambaye alikuw karibu sana kwa maana ilikuwa ni kama ananong'ona pekeyake, koo lililkuwa linamuua aligundua alikuwa na kiu kikali kutokana na joto la humo ndani alifanya maombi ili MUNGU amnusuru na kikombe ambacho kilikuwa mbele yake kugundulika kwamba yeye ni usalama wa taifa lilikuwa ni kosa kubwa. Zilipita dakika tano mlango ulifunguliwa mwanga wa taa za nje ya hicho chumba ulisaidia kidogo kupunguza hicho kiza lakini baadae tena ulipotea baada ya mlango kufungwa kwa ndani alikuwa ameingia mwanaume mmoja mrefu kiasi mweusi
"Humu ndani kuna joto sana unawezaje kuhimili hii hali na ukawa salama aisee" mwanaume huyo aliongea akiwa anawasha chemli ya mafuta ambayo nayo ilikuwa inaongeza joto sana Jiti kama alivyotambulika mwanzo alikua wazi leo ameingia cha kike, mwanga ulisambaa humo ndani ndipo alipopata bahati ya kukiona hicho chumba vizuri kulikuwa na mavyuma vyuma mengi sana na box ambalo lilikuwa na msalaba mwekundu alimeza mate baada ya kuliona alijua kazi yake vizuri sana, mwanaume huyo aliyekuwa mbele yake alimtazama sana aliona namna mwenzake alivyokuwa anaramba ramba midomo yake akiwa na kiu kikali alisikitika sana na kuinamia sehemu ambayo mwenzake huyo alifungwa hapo alitoa kikopo cha maji kwenye mfuko wa koti lake la kummiminia Jiti kwenye mdomo wake ambaye aliyafakamia kama fisi aliyepata mzoga bila kutegemea.

"Sikutakiwa kufanya hivi ila wewe ni kijana mwenzangu kuna muda mimi mwenyewe nina moyo wa kibinadamu pia imeniuma kukuona kwenye hiyo hali ndugu yangu ila sina namna haya ni maisha ambayo nilisha yachagua hivyo sina namna ya kufanya" alikuwa akiongea huku akikifunga kikopo chake cha maji na kukirudisha mfukoni kisha akasimama tena.

"Asante sana ndugu yangu sidhani kama nilikwua hata na dakika kumi za kuendelea kuwa hai nilikuwa na kiu kikali mno nashukuru sana, hivi hapa niko wapi na napaswa kufanya nini?" Kauli yake ilimfanya yuule mwanaume amwangalie sana kwa mara nyingine na kutikisa kichwa kuonyesha masikitiko yake kwa mwenzake huyo.

"Sina imani sana na safari ya maisha yako kuwa ndefu ila mdomo wako ndio utakao kuhakikishia wewe kuwa salama, mimi sihusiki na kuamua hatima ya maisha yako kwa sababu nilikuwa na kazi ya kukukamata tu na kukuleta hapa, ndani ya dakika kumi na tano zijazo anakuja kiongozi hapa huyo ndiye ameyashika maisha yako kwenye mkono wake" aliongea bila wasiwasi.

"Ina maana wewe ndiye uliyekuwa na wenzako wawili na kuamuru wanikamate?"

"Yes ndo mimi hapa hata hujakosea"

"Kwanini umeamua kuishi maisha ya namna hii na unaonekana ni mtu mwema kabisa?"

"Kuna mambo mengi sana kwenye maisha kabla ya kuwaza kwa uchache kulingana na ubongo wako unapofikia kufikiria, sio kila mwanadamu yupo kama akili yako inavyowaza maisha yana mambo mengi sana na ukiwa sehemu ambayo unapata kila kitu huwezi ukayaelewa mpaka siku uwe hauna namna ndo utaelewa kwamba ni kwanini binadamu huwa wanayachukua maamuzi magumu kwenye maisha na kuyaacha maamuzi mepesi" aliongea na kutoka humo ndani hakuhitaji tena stori maana mtu huyo alitaka kuleta kujuana sana kitu ambacho kulikuwa ni hatari kwenye maeneo kama hayo ambayo hayatakiwi kabisa watu kuaminiana.

Alishuhudia mlango ukifunguliwa tena raundi hii taa ziliwashwa chemli ilijizima yenyewe, mbele ya mlango alikuwa amesimama mwanaume mmoja ambaye alikuwa na asili ya kiarabu, alikuwa amevaa traki nyeupe kifua kilikuw wazi kilipasuka sana alikuwa ni mtu kazi haswa hata chini alikuwa peku licha ya sakafu kuwa na joto la kutosha kwake lilionekana kuwa la kawaida tu kichwani alikifunga kitambaa cheupe.

"Nilipokuwa na miaka nane ndiyo ilikuwa mara yangu ya kwanza kuua, ni siku ambayo kila muda huwa inapita kwenye kichwa changu kwangu ulikuwa ni usiku mzito sana siku ile ila sikuwa na namna kwa sababu tayari ilikuwa imeshatokea sikuwa na uwezo wa kuyarudisha mambo kama yalivyokuwa mwanzo ikabidi niukubali ukweli tu kwamba niliua, walikuwa watu ishirini niliwapiga wote risasi kwa mkono wangu nikiwa nalia na sababu kubwa ya kuwaua ni kwamba mdugu yao mmoja alikimbia na kete moja ya madawa ya kulevya ila aliyaponza maisha ya ndugu zake wote kumi na tisa nayeye akiwa wa ishirini. Nililia mno siku ile kwa sababu nililazimishwa kufanya vile na bosi wangu ndani ya nchi ile ya Morocco, tangu pale nimekuwa muuaji bora mno ambaye huwa sijiulizi hata mara mbili kuichukua nafsi ya mtu ni suala la sekunde tu na huwa najisikia vizuri sana napo itoa nafsi ya mtu(alimeza mate kidogo).

Jina langu naitwa Qader mimi sio mzaliwa wa nchi hii wala sikuwahi kutegemea kuja kuishi kwenye nchi hii hata kuzungumza lugha ya nchi hii ambayo ni Kiswahili sikuwahi kufikiria kabisa kuizungumza ila imetokea kwa sasa mimi ni miongoni mwa watu ambao wanaishi Tanzania kwa miaka zaidi ya mitano sasa nishakuwa mwenyeji mpaka lugha yenu naijua vizuri kiufupi mimi mwenyewe kwa sasa ni mswahili mzuri tu, sitaki mimi nawewe tufike mbali sana bado una nafasi ya kuwa mtu hai badala ya historia yako kuishia kwenye chumba hiki.

Mtu ambaye ulipewa kazi ya kuyafuatilia maisha yake na mpaka sasa unaifanya hiyo kazi ni mtu ambaye ninamhitaji kwa gharama yoyote ile na ni lazima nimpate, najua una baadhi ya taarifa za mhimu sana kumhusu mtu huyu hivyo sitataka uanze kupindisha jambo lolote lile kuhusu hizi taarifa nimekufuatilia kwa muda mrefu sana hivyo sijabahatisha kuja kwako kwahiyo kila neno ambalo utalitoa kwenye mdomo wako lipime kwanza na uelewe aina ya mtu ambaye unaongea naye sio muda mrefu nitageuka kuwa shetani humu ndani" mwanaume huyo aliongea bila kitetemeshi alikuwa anajiamini sana mkononi mwake alikuwa na sigara ambayo alipiga mafunda kadhaa na kuizima kwa mguu wake uliokuwa peku.

"Unahitaji taarifa za mtu gani?"

"Zakaria Mansour" Jiti alitoa macho hakuamini alichokuwa anaambiwa huyo mtu alikuwa anasakwa na kila mtu alifanya nini kwani? .......hata mimi nimebaki njiapanda kama wewe ulivyo achwa na mshangao.....

Binafsi 20 sina la ziada tena panapo majaaliwa tukutane wakati ujao.

Bye-bye

Bux the story teller
STORY: GEREZA LA HAZWA
STORY WRITER: FEBIANI BABUYA
STORY TELLER: Bux the story teller
AGE: 18+

UKURASA WA ISHIRINI NA MOJA

TULIPO ISHIA UKURASA WA ISHIRINI

Mtu ambaye ulipewa kazi ya kuyafuatilia maisha yake na mpaka sasa unaifanya hiyo kazi ni mtu ambaye ninamhitaji kwa gharama yoyote ile na ni lazima nimpate, najua una baadhi ya taarifa za mhimu sana kumhusu mtu huyu hivyo sitataka uanze kupindisha jambo lolote lile kuhusu hizi taarifa nimekufuatilia kwa muda mrefu sana hivyo sijabahatisha kuja kwako kwahiyo kila neno ambalo utalitoa kwenye mdomo wako lipime kwanza na uelewe aina ya mtu ambaye unaongea naye sio muda mrefu nitageuka kuwa shetani humu ndani" mwanaume huyo aliongea bila kitetemeshi alikuwa anajiamini sana mkononi mwake alikuwa na sigara ambayo alipiga mafunda kadhaa na kuizima kwa mguu wake uliokuwa peku.

"Unahitaji taarifa za mtu gani?"

"Zakaria Mansour" Jiti alitoa macho hakuamini alichokuwa anaambiwa huyo mtu alikuwa anasakwa na kila mtu alifanya nini kwani? .......hata mimi nimebaki njiapanda kama wewe ulivyo achwa na mshangao.....

ENDELEA........................
HAZWA GEREZANI
"Alikuwa kwenye dakika zake za mwisho za kuendelea kujihesabia kama binadamu ambaye bado alikuwa yupo hai, gari aliyokuwa amepanda ilipinduka vibaya na kwenda kujibamiza kwenye mti na kuanza kuvuja mafuta, mara ya mwisho kuongea alitamka kauli moja tu kwamba I'm dying simu ilibaki kuwa hewani muda wote. Zilipita dakika arobaini na tano tu wakati gari hiyo inaanza kuwaka moto alitokea mwanaume mmoja ambaye umri wake ulikuwa umeenda kiasi alikuwa amefika hapo na helikopita moja ya kijeshi ambazo huwa zinakimbia masaafa marefu kwa muda mfupi, alishuka haraka na kukimbilia lilipo gari hilo moto ulizidi kuwaka kiasi cha kuweza kulipuka muda wowote ule hata hivyo hakujali chochote kile maisha ya yule bwana mdogo kwake ilionekana ndiyo kila kitu alijitosa kwenye ule Moto ndani ya ile gari alimkokota Aariz mpaka nje ya gari na kumrushia pembeni naye alijirusha sehemu ile ambayo alimrushia Aariz na kwenda kuzuia kwa juu yake ulitokea mlipuko mzito sana kwenye ile gari na kufanya vyuma vyake viruke juu na kwenda kutua juu ya mgongo wa yule mzee ambaye alikuwa hapo kwa ajili ya kumuokoa Aariz, vyuma hivyo vilichomoka na baadhi ya nyama kwenye mgongo huo, aliuma meno kwa maumivu akambeba mwanaume huyo na kumpandisha kwenye helikopita aliyokuwa amekuja nayo akapotea nae.

Aariz aliyafumbua macho yake yalikuwa hayana nguvu za kutosha alijihisi mchovu sana, alikuwa kwenye chumba kimoja kisafi mno na hali yake ilikuwa bora kuliko kawaida mwili ulikuwa mwepesi tofauti na alivyokuwa anajijua mwanzo alinyanyuka taratibu na kusimama akajinyoosha mwili haukuwa na maumivu hata sehemu moja zaidi ya uchovu tu. Alikitazama chumba hicho kwa umakini hakuwa na kumbukumbu kama amewahi kukijua au aliwahi kuwepo mahala hapo kabla, alienda mpaka dirishani ilikuwa ni ghorofa aliangalia na kuona uzuri wa mandhali ya mji palikuwa panapendeza sana alijikuta akitabasamu watu wenye maisha ya kawaida bila shaka walikuwa wakifurahia sana maisha yao ya amani.

Alituliza kichwa chake alihitaji sana kujua kipi kilichotokea mpaka akafika hapo zilipita dakika mbili mbele alianza kuyakumbuka matukio yote tangu anafuatwa ili kwenda kufanya kazi na kufika kwenye ile kambi ambapo aliua watu wote na kuwaokoa wanawake wale miamoja, kumbukumbu ya mwisho iliishia akiwa kwenye gari hana hata uwezo wa kuona mbele alikumbuka vizuri alipiga simu mahali baada ya hapo hakujua kilichokuwa kinaendelea mpaka alipojikuta humo ndani. Alishtuka na kuvua shati lake ghafla sana alikumbuka vyema alikuwa amekatwa sehemu yake ya mbavu ya kulia na alikuwa akitoka damu nyeusi lakini alicho kiona kilimfanya yeye mwenyewe aanze kujiogopa hapakuwa na jeraha lolote lile palikuwa kama palivyokuwa mwanzo na hakuna mtu ambaye angeamini kwamba mtu huyo alikuwa amewahi kuguswa na kitu chenye ncha kali kwenye mbavu yake.

"Hapana, hapana hii haiwezi kuwa ndoto mimi nipo kwenye ukweli noooooooooooo" alipiga makelele ni kama alikuwa anachanyikiwa nafsi yake ni kama ilikuwa inamsaliti alichokuwa anakishuhudia kwenye mwili wake kilimfanya aanze kuukataa mwili mwenyewe japo hakuwa na uwezo wa kuukimbia alianza kutetemeka akiwa amefumba macho alijaribu kuwaza kila sayansi yenye uwezo wa kufanya hivyo alijikuta anaogopa mno. Akiwa ameyafumba macho yake kwa mbali alihisi kama mlango wa hicho chumba unafunguliwa hakujishughulisha kugeuka kwani moyo wake ulikuwa unamuenda mbio sana.

"Una mwili imara sana angekuwa mwanajeshi wa kawaida mpaka sasa tungekuwa tulishakuzika tumeanza na kukusahau, nimeamini kwanini ulichaguliwa kwa ajili ya hizi kazi wewe sio mwanadamu wa kawaida hata kidogo taifa hili limebahatika sana kuwa na mtu kama wewe" sauti aliyo isikia nyuma yake hakuwa hata na haja ya kugeuka aliijua kuliko kitu chochote kile na ndo sauti ambayo ameishi maisha yake yote akiwa anaiheshimu sana.

"Nimekaa humu ndani kwa muda gani?"

"Kesho ulikuwa unatimiza wiki ya pili ukiwa unaipambania hali yako kitandani ila MUNGU mkubwa umeamka mapema tofauti na nilivyokuwa nimetarajia" hapo aligeuka kumwangalia mtu huyo, alikuwa ni mwalimu wake ambaye ameishi naye tangu aanze kujielewa alikuwa ni mlezi pia ndiye ambaye amempa mafunzo mengi sana na ndiye mwanadamu pekee ambaye alikuwa anamwamini sana kwenye maisha yake.

"Are you a witch doctor or Wizard?" Alimuuliza mzee huyo akiwa anamaanisha yeye ni mchawi au mganga wa kienyeji? Mzee huyo alitabasamu tu alimwangalia Aariz kwenye ubavu wake ambapo hapakuwa na jeraha lolote lile alielewa hicho ndicho kilicho mchanganya mwanaume huyo.

"Wakati unasogea dunia inazidi kwenye mbali sana saivi hakuna kinacho shindikana hapa duniani kikubwa tu uwe na pesa za kutosha unaweza hata kuchelewesha mtu kufa kama unahitaji kujua kuhusu chochote ambacho kimetokea basi soma faili hili hapa lina maelezo yote ndani" alimalizia maelezo yake ambayo yalifuatiwa na kumkabidhi Aariz faili mkononi na mzee huyo akawa anaelekea mlangoni.

"How is my wife?(mke wangu anaendeleaje)" kauli hiyo ilimfanya mzee huyo atoe meno yake yote yatoke nje alionekana kufurahia swali hilo ambalo alilitarajia mapema sana kitu hicho kilimtoa mwanaume hofu moyoni.

"I'm a grandfather now( Mimi ni babu sasa)" Aariz alitamani ameze hata misumari baada ya kusikia mkewe kipenzi ameweza kujifungua alifurahi sana

"Are you serious?" Aliuliza akiwa analitafuta shati lilipo avae

"Soma kwanza hilo faili ukimaliza nenda kamuone mwanao wa kiume wiki ijayo nakuja kukukabidhi kazi yako ya mwisho" alimaliza mzee huyo na kutoka humo ndani. Aariz aliingia kwenye ulimwengu wa kuwa baba sasa ni jambo ambalo wanadamu wengi huwa wanaliishi kama ndoto zao, alifungua faili hilo na kuanza kulisoma mpaka analimaliza alikaa chini machozi yalimtoka alichukia na kuogopa sana.

"Why always me, why always me?" Aliongea kwa uchungu na hasira na kuanza kuvuruga vuruga vitu humo ndani alicho kisoma kilionekana kutokuwa cha kuvutia wala kupendeza kwake na kwa maisha yake kwa ujumla.

"NATAKA kuwa mwanadamu wa kawaida, NATAKA kuishi na kufa kama wanadamu wengine, kwanini wananifanyia hivi na kuwa jitu la kutisha namna hii mpaka mimi mwenyewe najiogopa alizunguka mpaka sehemu ambapo palikuwa na friji alikutana na pombe kali aliiweka mdomoni na kumaliza chupa nzima akiwa hajaweka kituo hata mara moja aliichukua sigara ambayo ilikuwa pembeni aliiwasha na kuivuta kwa mkupuo ni kitu ambacho kilionekana kutokuwa sehemu ya maisha yake ila alionekana kama kavurugwa alilewa sana akajitupa kitandani na kulala.

Siku ya pili yake alikuwa ndani ya suti maridadi sana na begi lake mkononi ambalo lilijaa pesa za kutosha, alionekana kama mfanya biashara mkubwa wala usinge amini kwamba kuna silaha akizishika kinakuwa kiumbe cha ajabu, gari moja zuri lilimfikisha kwake ambako aliamua kuishi maisha ya kawaida tu mbele ya mkewe ili mwanamke huyo asiishi kwa mashaka hata anavyopelekwa China aliwahi kuambiwa anakwenda kumtengenezea kijana huyo saikolojia yake baada ya kuondokewa na wazazi wake na baadhi ya ndugu zake kwa ajali alipoteza uwezo wa akili kabisa akawa ameathirika sana kisaikolojia mwisho wa siku wakajikuta wamependana kweli asiijue kazi ya huyo mwanaume alikuwa amedanganywa kila kitu kwenye maisha ya Zakaria au waweza kumuita Aariz. Mwanaume alifika nyumbani kwa kisingizio cha kutoka kwenye biashara nje ya nchi kumbe alikuwa kukata vichwa vya watu huko porini, mkewe alifurahi sana kumuona mumewe ambaye alimpatia zawadi ya mtoto wa kiume ilijaa furaha sana ndani ya familia mtoto alibadilisha kila kitu Aariz alianza kutamani sana kuwa mwanadamu wa kawaida asimame kama mume na baba ni jambo lililo onekana kumpa faraja sana ila alijipa moyo baada ya kukumbuka kwamba alikuwa na kazi ya mwisho kuifanya baada ya hapo wangemuacha na maisha yake aishi anakotaka yeye japo walimwambia itakuwa ni vyema zaidi kama ataishi ndani ya nchi ya Tanzania bila kupewa sababu akiahidiwa akimaliza kazi ataambiwa kwanini amechaguliwa kwenda Tanzania mpaka muda huo alikuwa hajui chochote cha maana kuhusu maisha yake.

Ilipita miezi kadhaa akiwa na furaha sana na familia yake. Usiku wa manane akiwa amelala alihisi nje ya nyumba yake kulikuwa na watu kwa sababu mwili ulimsisimka sana, akaamka na kuangalia pembeni alikuwa amelala mkewe na mtoto alitabasamu na kuwabusu kila mmoja kwa muda wake akavaa vizuri na kutoka nje akiwa hana hata hofu, mbele ya nyumba yake ilipaki gari moja ya kifahari nyeusi nje ya gari hiyo alikuwa amesimama yule mzee wa siku zote akiwa anavuta sigara kubwa, alivuta mafunda kadhaa na kuitupa kisha wakakumbatiana na Aariz mlinzi alifungua milango ya gari hilo wakaingia na kuondoka hiyo sehemu kwa Kasi sana usiku huo wa manane bila kuongea kitu chochote kile.

"AMADOU MBAYE, ni mfanya biashara mkubwa sana kwenye hili bara la Africa pia ni katibu mkuu wa umoja wa nchi za magaharibi mwa Africa ambao unajulikana kama ECOWAS ila kwa sasa yupo hapa nchini Libya kibiashara ila pia kuna makazi yake ya siri ambapo ana mkewe mdogo ambaye familia yake haijui kabisa kwamba huwa anafikia kwa mkewe anapokuwa huku. Amezaliwa ndani ya jiji la Dakar Senegal na kukulia kwenye familia ya kimaskini sana ambayo mpaka leo wote anaishi nao kwake lakini inasemekana familia nzima wana roho mbaya sana wakiwa wamerisi kwa baba yake AMADOU. Ni miaka kadhaa tangu ameingia ndani ya nchi ya Libya sasa kwa kisingizio cha kufanya biashara ya mafuta na hakuna mtu wa kumzuia kabisa kwa sababu kila anacho kifanya kipo sahihi kisheria na ana vielelezo vyote vya kumruhusu kufanya biashara.

Tangu ameingia kwenye nchi hii amekuwa miongoni mwa wawekezaji wakubwa sana ambao hata nchi inawategemea sana kiuchumi ila kwenye stori ya maisha yake kuna ukakasi mkubwa sana wa namna alivyoweza kuupata huo utajiri kuna matukio mengi sana amekuwa akihusishwa nayo hususani ya upoteaji wa watoto pamoja na biashaea zingine haramu ila hakuna ushahidi wa moja kwa moja ili kumkamata mtu huyo kwa sababu ana watu wengi sana serikalini na kupatikana kwake kunahitaji mtu uwe na ushahidi mzito sana vinginevyo wewe ndo unaweza kujikuta unaishia sehemu mbaya. Maaskari wapatao ishirini ambao waliwahi kupewa kazi ya kumpeleleza mzee huyu wamepoteaga kwenye mazingira ya kutatanisha sana ambayo mpaka leo huwa hawajulikani wako wapi na hakuna ufuatiliaji wowote ule ambao umefanywa na serikali mpaka sasa wa kuridhisha.

Kuna ushahidi mzuri tu wa kuhusu biashara haramu ambazo anazifanya huyu mtu ambazo ni hizi zifuatazo.
1.Ana mpango wa kutakatisha fedha za nchi ya Libya ambapo mpango huo mpaka sasa umefikia asilimia thelathini maana yake ukifika sitini tu mchezo umeisha hakuna mtu ambaye ataweza kuuzuia tena na stori ya utajiri wa Libya itabaki kuwa historia tu ya kusimulia.
2.Alikuwa anafanya na mpaka sasa anafanya biashara ya kuingiza mizigo kikubwa sana wa madawa ya kulevya ndani ya nchi ya Libya ambapo ni hatari saba kwa maendeleo ya nchi kwa sababu vijana wengi sana wanathirika sana na haya madawa mwisho wa siku wanakuwa hawana faida yoyote kwa nchi hivyo tunakuwa na kizazi ambacho ni kama kilishakufa wakati kipo hai hili linatakiwa kuisha mapema sana.
3.Anafanya biashara ya kuuza viungo vya binadamu ambavyo kwa kiwango kikubwa vimepelekea mauaji kuwa mengi sana ndani ya nchi hii kiholela mno ni jambo la hatari sana kuendelea kulivumilia na kuliacha liendelee kutokea Lina madhara makubwa sana kwa maendeleo ya nchi hii.
Ila kibaya sana mtu huyu ni mtu wa dini mno kiasi kwamba ni mhudhuriaji mzuri sana wa msikitini na watu wanamjua kama mtu safi kwa sababu anajitoa sana kwa jamii ndiyo maana mbele za sheria huwezi kumfanya lolote lile, kwahiyo kazi yako kubwa tunahitaji huyu mtu haya mambo yake yabainike hadharani kabisa kwamba anayafanya ili sheria ichukue mkondo wake haraka sana iwezekanavyo" picha kubwa ilikuwa mbele ya skrini na mwelekezaji alikuwa ameshika marking pen akiwa anachora chora kuonyesha msisitizo wa alichokuwa anakisema, ni maelezo marefu ambayo yalikuwa yanajitosheleza sana ya mlezi wake na Aariz akiwa anamueleezea mtu ambaye ndiye faili lake lililkuwa mezani kwa wakati huo na ndiyo aliambiwa itakuwa kesi yake ya mwisho baada ya hapo alikuwa anaachwa huru. Walikuwa ndani ya chumba kimoja cha siri sana chini ya ardhi na humo ndani walikuwa watu wanne tu waziri mkuu mheshimiwa Mr Khalfa, muidhini wa dawa za binadamu Profesa Ajeeb, Aariz mwenyewe pamoja na mwalimu wake ambaye pia alikuwa kama mlezi kwake na ndiye ambaye alikuwa mbele akielezea wakati wengine wote watatu macho yao yalikuwa mbele ya skrini hiyo kubwa wakiwa wanasililiza kwa umakini sana.

Aariz aligeuka na kuwaangalia watu hao wawili ambao walikuwa pembeni yake walitikisiana vichwa kuonyesha kukubaliana na maelezo yaliyo tolewa, alijifuta jasho usoni alijua ni kazi nyepesi sana ila kwa maelezo yaliyo tolewa kulikuwa kuna mlima mzito sana mbele yake, alirushiwa faili mbele yake ambalo lilikuwa na maelezo yote ya nini anacho takiwa kukifanya, wanaume hao watatu walitoka humo ndani kazi yao walikuwa wameimaliza sasa ilibakia juu yake aliachwa pekeyake kwenye hicho chumba mawazo yalikitawala sana kichwa chake aliwaza kuhusu familia yake hakuelewa hatima yake itakuwa ni nini.

Aariz waweza kumwita Zakaria kwenye kizingiti kingine je ndiyo sababu inayokwenda kumfanya awe binadamu ambaye anatafutwa sana? Kwanini na kivipi wakati kazi kapewa na serikali?.. Najua una hamu sana ya kujua aliponaje jeraha lake ubavuni na kwanini alivyosoma faili lenye maelezo yote alilaani sana.....21 nasema bye-bye.

Langu jina naitwa

Bux the story teller
 
STORY: GEREZA LA HAZWA
STORY WRITER: FEBIANI BABUYA
STORY TELLER: Bux the story teller
AGE: 18+

UKURASA WA ISHIRINI NA MOJA

TULIPO ISHIA UKURASA WA ISHIRINI

Mtu ambaye ulipewa kazi ya kuyafuatilia maisha yake na mpaka sasa unaifanya hiyo kazi ni mtu ambaye ninamhitaji kwa gharama yoyote ile na ni lazima nimpate, najua una baadhi ya taarifa za mhimu sana kumhusu mtu huyu hivyo sitataka uanze kupindisha jambo lolote lile kuhusu hizi taarifa nimekufuatilia kwa muda mrefu sana hivyo sijabahatisha kuja kwako kwahiyo kila neno ambalo utalitoa kwenye mdomo wako lipime kwanza na uelewe aina ya mtu ambaye unaongea naye sio muda mrefu nitageuka kuwa shetani humu ndani" mwanaume huyo aliongea bila kitetemeshi alikuwa anajiamini sana mkononi mwake alikuwa na sigara ambayo alipiga mafunda kadhaa na kuizima kwa mguu wake uliokuwa peku.

"Unahitaji taarifa za mtu gani?"

"Zakaria Mansour" Jiti alitoa macho hakuamini alichokuwa anaambiwa huyo mtu alikuwa anasakwa na kila mtu alifanya nini kwani? .......hata mimi nimebaki njiapanda kama wewe ulivyo achwa na mshangao.....

ENDELEA........................
HAZWA GEREZANI
"Alikuwa kwenye dakika zake za mwisho za kuendelea kujihesabia kama binadamu ambaye bado alikuwa yupo hai, gari aliyokuwa amepanda ilipinduka vibaya na kwenda kujibamiza kwenye mti na kuanza kuvuja mafuta, mara ya mwisho kuongea alitamka kauli moja tu kwamba I'm dying simu ilibaki kuwa hewani muda wote. Zilipita dakika arobaini na tano tu wakati gari hiyo inaanza kuwaka moto alitokea mwanaume mmoja ambaye umri wake ulikuwa umeenda kiasi alikuwa amefika hapo na helikopita moja ya kijeshi ambazo huwa zinakimbia masaafa marefu kwa muda mfupi, alishuka haraka na kukimbilia lilipo gari hilo moto ulizidi kuwaka kiasi cha kuweza kulipuka muda wowote ule hata hivyo hakujali chochote kile maisha ya yule bwana mdogo kwake ilionekana ndiyo kila kitu alijitosa kwenye ule Moto ndani ya ile gari alimkokota Aariz mpaka nje ya gari na kumrushia pembeni naye alijirusha sehemu ile ambayo alimrushia Aariz na kwenda kuzuia kwa juu yake ulitokea mlipuko mzito sana kwenye ile gari na kufanya vyuma vyake viruke juu na kwenda kutua juu ya mgongo wa yule mzee ambaye alikuwa hapo kwa ajili ya kumuokoa Aariz, vyuma hivyo vilichomoka na baadhi ya nyama kwenye mgongo huo, aliuma meno kwa maumivu akambeba mwanaume huyo na kumpandisha kwenye helikopita aliyokuwa amekuja nayo akapotea nae.

Aariz aliyafumbua macho yake yalikuwa hayana nguvu za kutosha alijihisi mchovu sana, alikuwa kwenye chumba kimoja kisafi mno na hali yake ilikuwa bora kuliko kawaida mwili ulikuwa mwepesi tofauti na alivyokuwa anajijua mwanzo alinyanyuka taratibu na kusimama akajinyoosha mwili haukuwa na maumivu hata sehemu moja zaidi ya uchovu tu. Alikitazama chumba hicho kwa umakini hakuwa na kumbukumbu kama amewahi kukijua au aliwahi kuwepo mahala hapo kabla, alienda mpaka dirishani ilikuwa ni ghorofa aliangalia na kuona uzuri wa mandhali ya mji palikuwa panapendeza sana alijikuta akitabasamu watu wenye maisha ya kawaida bila shaka walikuwa wakifurahia sana maisha yao ya amani.

Alituliza kichwa chake alihitaji sana kujua kipi kilichotokea mpaka akafika hapo zilipita dakika mbili mbele alianza kuyakumbuka matukio yote tangu anafuatwa ili kwenda kufanya kazi na kufika kwenye ile kambi ambapo aliua watu wote na kuwaokoa wanawake wale miamoja, kumbukumbu ya mwisho iliishia akiwa kwenye gari hana hata uwezo wa kuona mbele alikumbuka vizuri alipiga simu mahali baada ya hapo hakujua kilichokuwa kinaendelea mpaka alipojikuta humo ndani. Alishtuka na kuvua shati lake ghafla sana alikumbuka vyema alikuwa amekatwa sehemu yake ya mbavu ya kulia na alikuwa akitoka damu nyeusi lakini alicho kiona kilimfanya yeye mwenyewe aanze kujiogopa hapakuwa na jeraha lolote lile palikuwa kama palivyokuwa mwanzo na hakuna mtu ambaye angeamini kwamba mtu huyo alikuwa amewahi kuguswa na kitu chenye ncha kali kwenye mbavu yake.

"Hapana, hapana hii haiwezi kuwa ndoto mimi nipo kwenye ukweli noooooooooooo" alipiga makelele ni kama alikuwa anachanyikiwa nafsi yake ni kama ilikuwa inamsaliti alichokuwa anakishuhudia kwenye mwili wake kilimfanya aanze kuukataa mwili mwenyewe japo hakuwa na uwezo wa kuukimbia alianza kutetemeka akiwa amefumba macho alijaribu kuwaza kila sayansi yenye uwezo wa kufanya hivyo alijikuta anaogopa mno. Akiwa ameyafumba macho yake kwa mbali alihisi kama mlango wa hicho chumba unafunguliwa hakujishughulisha kugeuka kwani moyo wake ulikuwa unamuenda mbio sana.

"Una mwili imara sana angekuwa mwanajeshi wa kawaida mpaka sasa tungekuwa tulishakuzika tumeanza na kukusahau, nimeamini kwanini ulichaguliwa kwa ajili ya hizi kazi wewe sio mwanadamu wa kawaida hata kidogo taifa hili limebahatika sana kuwa na mtu kama wewe" sauti aliyo isikia nyuma yake hakuwa hata na haja ya kugeuka aliijua kuliko kitu chochote kile na ndo sauti ambayo ameishi maisha yake yote akiwa anaiheshimu sana.

"Nimekaa humu ndani kwa muda gani?"

"Kesho ulikuwa unatimiza wiki ya pili ukiwa unaipambania hali yako kitandani ila MUNGU mkubwa umeamka mapema tofauti na nilivyokuwa nimetarajia" hapo aligeuka kumwangalia mtu huyo, alikuwa ni mwalimu wake ambaye ameishi naye tangu aanze kujielewa alikuwa ni mlezi pia ndiye ambaye amempa mafunzo mengi sana na ndiye mwanadamu pekee ambaye alikuwa anamwamini sana kwenye maisha yake.

"Are you a witch doctor or Wizard?" Alimuuliza mzee huyo akiwa anamaanisha yeye ni mchawi au mganga wa kienyeji? Mzee huyo alitabasamu tu alimwangalia Aariz kwenye ubavu wake ambapo hapakuwa na jeraha lolote lile alielewa hicho ndicho kilicho mchanganya mwanaume huyo.

"Wakati unasogea dunia inazidi kwenye mbali sana saivi hakuna kinacho shindikana hapa duniani kikubwa tu uwe na pesa za kutosha unaweza hata kuchelewesha mtu kufa kama unahitaji kujua kuhusu chochote ambacho kimetokea basi soma faili hili hapa lina maelezo yote ndani" alimalizia maelezo yake ambayo yalifuatiwa na kumkabidhi Aariz faili mkononi na mzee huyo akawa anaelekea mlangoni.

"How is my wife?(mke wangu anaendeleaje)" kauli hiyo ilimfanya mzee huyo atoe meno yake yote yatoke nje alionekana kufurahia swali hilo ambalo alilitarajia mapema sana kitu hicho kilimtoa mwanaume hofu moyoni.

"I'm a grandfather now( Mimi ni babu sasa)" Aariz alitamani ameze hata misumari baada ya kusikia mkewe kipenzi ameweza kujifungua alifurahi sana

"Are you serious?" Aliuliza akiwa analitafuta shati lilipo avae

"Soma kwanza hilo faili ukimaliza nenda kamuone mwanao wa kiume wiki ijayo nakuja kukukabidhi kazi yako ya mwisho" alimaliza mzee huyo na kutoka humo ndani. Aariz aliingia kwenye ulimwengu wa kuwa baba sasa ni jambo ambalo wanadamu wengi huwa wanaliishi kama ndoto zao, alifungua faili hilo na kuanza kulisoma mpaka analimaliza alikaa chini machozi yalimtoka alichukia na kuogopa sana.

"Why always me, why always me?" Aliongea kwa uchungu na hasira na kuanza kuvuruga vuruga vitu humo ndani alicho kisoma kilionekana kutokuwa cha kuvutia wala kupendeza kwake na kwa maisha yake kwa ujumla.

"NATAKA kuwa mwanadamu wa kawaida, NATAKA kuishi na kufa kama wanadamu wengine, kwanini wananifanyia hivi na kuwa jitu la kutisha namna hii mpaka mimi mwenyewe najiogopa alizunguka mpaka sehemu ambapo palikuwa na friji alikutana na pombe kali aliiweka mdomoni na kumaliza chupa nzima akiwa hajaweka kituo hata mara moja aliichukua sigara ambayo ilikuwa pembeni aliiwasha na kuivuta kwa mkupuo ni kitu ambacho kilionekana kutokuwa sehemu ya maisha yake ila alionekana kama kavurugwa alilewa sana akajitupa kitandani na kulala.

Siku ya pili yake alikuwa ndani ya suti maridadi sana na begi lake mkononi ambalo lilijaa pesa za kutosha, alionekana kama mfanya biashara mkubwa wala usinge amini kwamba kuna silaha akizishika kinakuwa kiumbe cha ajabu, gari moja zuri lilimfikisha kwake ambako aliamua kuishi maisha ya kawaida tu mbele ya mkewe ili mwanamke huyo asiishi kwa mashaka hata anavyopelekwa China aliwahi kuambiwa anakwenda kumtengenezea kijana huyo saikolojia yake baada ya kuondokewa na wazazi wake na baadhi ya ndugu zake kwa ajali alipoteza uwezo wa akili kabisa akawa ameathirika sana kisaikolojia mwisho wa siku wakajikuta wamependana kweli asiijue kazi ya huyo mwanaume alikuwa amedanganywa kila kitu kwenye maisha ya Zakaria au waweza kumuita Aariz. Mwanaume alifika nyumbani kwa kisingizio cha kutoka kwenye biashara nje ya nchi kumbe alikuwa kukata vichwa vya watu huko porini, mkewe alifurahi sana kumuona mumewe ambaye alimpatia zawadi ya mtoto wa kiume ilijaa furaha sana ndani ya familia mtoto alibadilisha kila kitu Aariz alianza kutamani sana kuwa mwanadamu wa kawaida asimame kama mume na baba ni jambo lililo onekana kumpa faraja sana ila alijipa moyo baada ya kukumbuka kwamba alikuwa na kazi ya mwisho kuifanya baada ya hapo wangemuacha na maisha yake aishi anakotaka yeye japo walimwambia itakuwa ni vyema zaidi kama ataishi ndani ya nchi ya Tanzania bila kupewa sababu akiahidiwa akimaliza kazi ataambiwa kwanini amechaguliwa kwenda Tanzania mpaka muda huo alikuwa hajui chochote cha maana kuhusu maisha yake.

Ilipita miezi kadhaa akiwa na furaha sana na familia yake. Usiku wa manane akiwa amelala alihisi nje ya nyumba yake kulikuwa na watu kwa sababu mwili ulimsisimka sana, akaamka na kuangalia pembeni alikuwa amelala mkewe na mtoto alitabasamu na kuwabusu kila mmoja kwa muda wake akavaa vizuri na kutoka nje akiwa hana hata hofu, mbele ya nyumba yake ilipaki gari moja ya kifahari nyeusi nje ya gari hiyo alikuwa amesimama yule mzee wa siku zote akiwa anavuta sigara kubwa, alivuta mafunda kadhaa na kuitupa kisha wakakumbatiana na Aariz mlinzi alifungua milango ya gari hilo wakaingia na kuondoka hiyo sehemu kwa Kasi sana usiku huo wa manane bila kuongea kitu chochote kile.

"AMADOU MBAYE, ni mfanya biashara mkubwa sana kwenye hili bara la Africa pia ni katibu mkuu wa umoja wa nchi za magaharibi mwa Africa ambao unajulikana kama ECOWAS ila kwa sasa yupo hapa nchini Libya kibiashara ila pia kuna makazi yake ya siri ambapo ana mkewe mdogo ambaye familia yake haijui kabisa kwamba huwa anafikia kwa mkewe anapokuwa huku. Amezaliwa ndani ya jiji la Dakar Senegal na kukulia kwenye familia ya kimaskini sana ambayo mpaka leo wote anaishi nao kwake lakini inasemekana familia nzima wana roho mbaya sana wakiwa wamerisi kwa baba yake AMADOU. Ni miaka kadhaa tangu ameingia ndani ya nchi ya Libya sasa kwa kisingizio cha kufanya biashara ya mafuta na hakuna mtu wa kumzuia kabisa kwa sababu kila anacho kifanya kipo sahihi kisheria na ana vielelezo vyote vya kumruhusu kufanya biashara.

Tangu ameingia kwenye nchi hii amekuwa miongoni mwa wawekezaji wakubwa sana ambao hata nchi inawategemea sana kiuchumi ila kwenye stori ya maisha yake kuna ukakasi mkubwa sana wa namna alivyoweza kuupata huo utajiri kuna matukio mengi sana amekuwa akihusishwa nayo hususani ya upoteaji wa watoto pamoja na biashaea zingine haramu ila hakuna ushahidi wa moja kwa moja ili kumkamata mtu huyo kwa sababu ana watu wengi sana serikalini na kupatikana kwake kunahitaji mtu uwe na ushahidi mzito sana vinginevyo wewe ndo unaweza kujikuta unaishia sehemu mbaya. Maaskari wapatao ishirini ambao waliwahi kupewa kazi ya kumpeleleza mzee huyu wamepoteaga kwenye mazingira ya kutatanisha sana ambayo mpaka leo huwa hawajulikani wako wapi na hakuna ufuatiliaji wowote ule ambao umefanywa na serikali mpaka sasa wa kuridhisha.

Kuna ushahidi mzuri tu wa kuhusu biashara haramu ambazo anazifanya huyu mtu ambazo ni hizi zifuatazo.
1.Ana mpango wa kutakatisha fedha za nchi ya Libya ambapo mpango huo mpaka sasa umefikia asilimia thelathini maana yake ukifika sitini tu mchezo umeisha hakuna mtu ambaye ataweza kuuzuia tena na stori ya utajiri wa Libya itabaki kuwa historia tu ya kusimulia.
2.Alikuwa anafanya na mpaka sasa anafanya biashara ya kuingiza mizigo kikubwa sana wa madawa ya kulevya ndani ya nchi ya Libya ambapo ni hatari saba kwa maendeleo ya nchi kwa sababu vijana wengi sana wanathirika sana na haya madawa mwisho wa siku wanakuwa hawana faida yoyote kwa nchi hivyo tunakuwa na kizazi ambacho ni kama kilishakufa wakati kipo hai hili linatakiwa kuisha mapema sana.
3.Anafanya biashara ya kuuza viungo vya binadamu ambavyo kwa kiwango kikubwa vimepelekea mauaji kuwa mengi sana ndani ya nchi hii kiholela mno ni jambo la hatari sana kuendelea kulivumilia na kuliacha liendelee kutokea Lina madhara makubwa sana kwa maendeleo ya nchi hii.
Ila kibaya sana mtu huyu ni mtu wa dini mno kiasi kwamba ni mhudhuriaji mzuri sana wa msikitini na watu wanamjua kama mtu safi kwa sababu anajitoa sana kwa jamii ndiyo maana mbele za sheria huwezi kumfanya lolote lile, kwahiyo kazi yako kubwa tunahitaji huyu mtu haya mambo yake yabainike hadharani kabisa kwamba anayafanya ili sheria ichukue mkondo wake haraka sana iwezekanavyo" picha kubwa ilikuwa mbele ya skrini na mwelekezaji alikuwa ameshika marking pen akiwa anachora chora kuonyesha msisitizo wa alichokuwa anakisema, ni maelezo marefu ambayo yalikuwa yanajitosheleza sana ya mlezi wake na Aariz akiwa anamueleezea mtu ambaye ndiye faili lake lililkuwa mezani kwa wakati huo na ndiyo aliambiwa itakuwa kesi yake ya mwisho baada ya hapo alikuwa anaachwa huru. Walikuwa ndani ya chumba kimoja cha siri sana chini ya ardhi na humo ndani walikuwa watu wanne tu waziri mkuu mheshimiwa Mr Khalfa, muidhini wa dawa za binadamu Profesa Ajeeb, Aariz mwenyewe pamoja na mwalimu wake ambaye pia alikuwa kama mlezi kwake na ndiye ambaye alikuwa mbele akielezea wakati wengine wote watatu macho yao yalikuwa mbele ya skrini hiyo kubwa wakiwa wanasililiza kwa umakini sana.

Aariz aligeuka na kuwaangalia watu hao wawili ambao walikuwa pembeni yake walitikisiana vichwa kuonyesha kukubaliana na maelezo yaliyo tolewa, alijifuta jasho usoni alijua ni kazi nyepesi sana ila kwa maelezo yaliyo tolewa kulikuwa kuna mlima mzito sana mbele yake, alirushiwa faili mbele yake ambalo lilikuwa na maelezo yote ya nini anacho takiwa kukifanya, wanaume hao watatu walitoka humo ndani kazi yao walikuwa wameimaliza sasa ilibakia juu yake aliachwa pekeyake kwenye hicho chumba mawazo yalikitawala sana kichwa chake aliwaza kuhusu familia yake hakuelewa hatima yake itakuwa ni nini.

Aariz waweza kumwita Zakaria kwenye kizingiti kingine je ndiyo sababu inayokwenda kumfanya awe binadamu ambaye anatafutwa sana? Kwanini na kivipi wakati kazi kapewa na serikali?.. Najua una hamu sana ya kujua aliponaje jeraha lake ubavuni na kwanini alivyosoma faili lenye maelezo yote alilaani sana.....21 nasema bye-bye.

Langu jina naitwa

Bux the story teller
STORY: GEREZA LA HAZWA
STORY WRITER: FEBIANI BABUYA
STORY TELLER: Bux the story teller
AGE: 18+

UKURASA WA ISHIRINI NA MBILI

TULIPO ISHIA UKURASA WA ISHIRINI NA MOJA


Aariz aligeuka na kuwaangalia watu hao wawili ambao walikuwa pembeni yake walitikisiana vichwa kuonyesha kukubaliana na maelezo yaliyo tolewa, alijifuta jasho usoni alijua ni kazi nyepesi sana ila kwa maelezo yaliyo tolewa kulikuwa kuna mlima mzito sana mbele yake, alirushiwa faili mbele yake ambalo lilikuwa na maelezo yote ya nini anacho takiwa kukifanya, wanaume hao watatu walitoka humo ndani kazi yao walikuwa wameimaliza sasa ilibakia juu yake aliachwa pekeyake kwenye hicho chumba mawazo yalikitawala sana kichwa chake aliwaza kuhusu familia yake hakuelewa hatima yake itakuwa ni nini.

ENDELEA.......................

TABATA TANZANIA
Kilicho mshtua na kumshangaza sana Jiti Maalimu sio kwa sababu watu hao walifanikiwa kumjua yeye kama usalama wa taifa wala kuhitaji taarifa fulani alijua wazi vigogo wengi huwa wanawapenyeza watu wao ili kujinufaisha wao wenyewe hususani wanapo hitaji kufanya mambo yao ya siri bila kushtukiwa na mtu yeyote huwa wanawatumia sana watu hao ambao wengi kwao pesa huwa ni kipaumbele kikubwa sana ila kilicho mfanya abaki mdomo wazi mpaka muda huo ni mtu ambaye taarifa zake zilikuwa zinahitajika Zakaria Mansour, ilikuwa ni siri nzito sana kuhusu mtu huyo ambaye alionekana kuwa na dili sana sokoni, ni watu wachache mno ambao walikuwa na taarifa zake na ilikuwa ni siri yake pekeyake moyoni kwani kazi ya kumfuatilia mtu huyo hakupewa na mkurugenzi wa usalama wa taifa bali aliku amekabidhiwa na mheshimiwa raisi mwenyewe wa nchi ya Tanzania Mr Alan Mwaiponela sasa hawa watu walijuaje kuhusu hilo? aligundua kwamba ni lazima raisi kuna watu wengine ambao aliwashirikisha kwenye hiyo kazi hilo lilikuwa kosa la Kwanza kulifanya.

"Huyo Zakaria ndo nani?" Alikuwa siriasi sana kwenye uso wake alimaanisha kweli kwamba hana uelewa juu ya uwepo wa mtu ambaye jina lake lilikuwa likifahamika kama Zakaria.

"Mhhhhhh nimekuonya kwa mara ya Kwanza huwa sio mpiga stori mzuri sana ndio maana nimekupa tahadhari mapema sana" Qader aliyatamka maneno yake huku akilisogeza box la vifaa na kuchukua kiti akasogea karibu na alipokuwa amefungwa Jiti akakaa akiwa bado yupo kifua wazi.

"Nimefanya kazi kwa muda mrefu sana wenye hiyo idara sijawahi kusikia jina kama hilo hata siku moja ndiyo Kwanza nalisikia kwako leo" alionekana kukereka sana hivyo alikuwa anajibu kikakamavu ili asionekane mlaini sana mwarabu huyo alimwangalia kwa muda kwa hasira kisha akatamka kirahisi tu sawa.

"Sawa" alitoa koleo dogo na mkasi kwenye hilo box pamoja na waya, akasogeza mita ambayo ilikuwa inasoma umeme wa kutosha ambao usingeisha hata kwa bahati mbaya. Alizamisha koleo hilo kwenye kidole gumba cha mguu wa Jiti na kunyofoa ukucha ambao ulibanduliwa kwa lazima bila huruma licha ya Jiti kupiga makelele sana hakuna mtu ambaye alikuwa na muda naye wala kumuonea huruma, baada ya ukucha kunyofolewa mkasi ulipita na sehemu ya mbele ya kidole hicho damu nyingi ilikuwa inatoka mwanaume huyo alizamisha kwa nguvu waya mgumu ambao alikuwa ameushika kwa mkono wake wa kushoto ulitoboa na kuzama mpaka ndani waya ukiwa umezamishwa mwanaume huyo alichukua waya ya umeme ambayo iliunganishwa kwenye koleo la chuma akawa anagusisha kwenye waya ambao ulikuwa umezamishwa kwenye kidonda. Shoti ambayo ilikuwa inapita kwenye kidonda hicho hakuna binadamu mwenye moyo wa kawaida angeweza kuvumilia alitoa mkojo akiwa anaomba aongee kila kitu alikiri kumkosea sana mwanaume huyo, alilia sana uso wake ulichafuka kwa machozi na damu ambayo ilisababishwa na damu kutoka puani na mdomoni ni wazi alikuwa amekutana na shetani siku yake hiyo.

Baada ya dakika mbili mwanaume huyo alitoa vitu vyake na kuvirudisha kwenye box lake akalifunga na kulirudisha mahali lilipokuwa mwanzo bila kuongea kitu chochote kile kisha akarudi na kukaa akiwa anamwangalia Jiti ambaye bado alikuwa anatoa machozi kwa uchungu sana, Qader alisikitika sana kisha akainama chini kwa dakika moja na kuinua uso wake tena.

"Nadhani maelezo yangu uliyapuuzia wakati nakuelekeza kwa mara ya kwanza, nikiwa na miaka nane tu niliua watu 20 kwa risasi hivi unadhani leo nikiwa na miaka hii 28 nitashindwa kukuua mpumbavu mmoja kama wewe hapo ambaye hata sikujui kabisa?, Huwa nachukia sana kuongea jambo moja mara saba saba ambalo linaweza kuisha ndani ya dakika moja tuz hapo nimekuonjesha tu uwe unanijibu kwa nidhamu unapokuwa mbele yangu mimi sio mtu ambaye unaweza kunijibu vile unavyo jisikia wewe wala mimi sio mtu wa kuanza kukubembeleza pale ninapokuwa nazihitaji taarifa fulani kwako upo kwenye mikono yangu ni lazima useme ninacho kuuliza, hapa una sekunde thelathini tu za kuendelea kuwa na viungo vyako vyote kwenye mwili wako" Qader aliongea kiutulivu sana akiwa amemkazia macho Jiti lakini maneno yake yalikuwa kwenye msisitizo mkali sana.

"Naomba maji tafadhali nasema" Jiti aliongea kwa shida sana alihisi kama mwili wake umekauka ni dakika kadhaa alitoka kupatiwa maji lakini wakati huu alikuwa anahisi kama mwili wake haukuwahi kupata maji kwa miaka kadhaa, Qader alinyanyuka mwenyewe akatoka kwenye hicho chumba alirudi na ndoo nzima ya maji alimpa mtu huyo kikombe baada ya kumfungulia mkono mmoja alikunywa kwa pupa sana mengine yalikuwa ya baridi mno lakini ndoo nzima alimwagiwa mwilini kidogo mwili ulipata nguvu hata kidole maumivu yake yalipungua kiasi, alijifuta usoni akiwa anahema kwa nguvu.

"Una familia?" Qader alilisikia vizuri hilo swali lakini hakuelewa linamaanisha nini na Jiti hakuonekana kuwa na masiara maana alikaa vizuri akioekana wazi kwamba alikuwa anasubiri kwa umakini jibu kwa mtu huyo.

"Linahusiana vipi na maswali ambayo nimekuuliza hapa?" Aliuliza kwa sauti yake ya mgandamizo.

"Ni mhimu sana kunijibu hilo swali kabla haujaanza kujutia"

"Kwahiyo unanitisha"

"Sikutishi"

"Kwahiyo lengo lako ni lipi?

"NATAKA kukupa tahadhali"
"Ya nini"
"Ya huyo mtu ambaye wewe unamtafuta"
"Kuna kipi hicho cha kutisha ambacho unakijua kwake?"
"Nijibu swali lako ndani ya nchi hii mimi ndiye ninaye mjua yule mtu kuliko binadamu yeyote na hakuna ambaye analijua hili"
"Whaaaaaat"
"Nijibu nilicho kuuliza"

"Familia yangu ipo na ipo mahali salama sana" alijibu kwa kujiamini sana Qader

"Una uhakika na unacho kisema?" Jiti aliuliza kwa kujiamini sana kidogo mpaka Qader alishtuka
"Yes"

"Hahahahahahahahah unaitwa Taofic Mhamaduu, una watoto wawili mapacha ambao umewaficha ndani ya nchi ya Afrika ya kusini pembezoni mwa jiji la Johensberg u......" Qader moyo ulimuenda mbio alijikuta jasho linamtoka ikamlazimu kumkatisha mwanaume huyo mbele yake ambaye alikuwa kwenye maumuvu makali cha ajabu hakuwa na wasiwasi na alikuwa akiijua siri ambayo Qader hakuwahi kumwambia binadamu yeyote yule kwenye maisha yake.

"Weeee.wew..wew ni nani?" Aliuliza kwa kigugumizi Qader akiwa na hasira kali sana aliitoa bastola na kuiweka kwenye kichwa cha Jiti lakini mtu huyo aliishia kutabasamu tu.

"Halafu huwa sitishiwi na bastola kwenye maisha yangu kama unahitaji nikuue hapa hapa endelea kuniwekea hilo toi lako kichwani mwangu hebu kaka hapo chini nikufundishe maisha" Jiti alikuwa ni jeuri ambaye hata magaidi wasingeweza kwenda naye sawa chanzo cha ugaidi wake hakikueleweka ni nini, Qader alijikuta mwenyewe anaishusha bastola yake na kukaa chini nguvu zilimuishia alikuwa mtu katili sana ila leo alianza kumuogopa mtu ambaye yeye alimjua kama usalama wa taifa ila ilionekana mtu huyo alikuwa ni zaidi ya ambavyo yeye alikuwa anamfikria suala la kutajiwa familia yake ilipo lilimuogopesha sana mwanaume huyu aliogopa sana.

"Nitafutie sigara uniletee ili ujue kitu ambacho kinakupa jeuri kwenye maisha yako wakati huna chochote cha kukupatia jeuri" maneno mengine ya jeuri yalitoka kwenye kinywa cha Jiti yalimshtua sana Qader alitoka kwa mbio na kutoka nje ya hicho chumba alirudi akiwa na sigara za bei ghali tano alikumbuka amesahau kiberiti basi ilamlazimu kurudi teja akiwa anakimbia alitamani sana kujua kipi kilijificha nyuma mpaka mtu huyo alikuwa anayajua mambo mengi namna hiyo. Jiti alichukua aliiweka sigara mdomoni na kumpa ishara Qader amuwashie alifanya hivyo.

"Kwenye maisha yako huenda huwa unajidanganya kwamba wewe ni mtu mkatili na mwenye roho ngumu sana ila kwa mimi nakuona kama wewe ni mwanamke tu wewe bado ni kijana dhaifu sana hapo ulipo ambaye hadi kuua mtu mpaka ujisifie una roho nyepesi sana unajiuliza mara mbili mbili ndio maaana sikutaka uwe kijana wangu( aliongea na kuvuta funda lingine kwa mkono mmoja ambao ulikuwa umefunguliwa). Huyo mtu ambaye unamtafuta kwa nguvu na kufoka hivyo unamujua kwanza? Au kwa sababu tu umeagizwa ndo unakuja kwa pupa na mikwala mingi namna hiyo ushawahi kusikia wapi muwindaji akawa na makelele hivyo na akafanikiwa kupata windo lake?. Wewe sio mtu wa hatari kama unavyo jisifia wewe ni kijana wa kawaida saaaana tena saaana na huna jipya wanapo simama watu wanao itwa hatari, huyo mtu unaye mtafuta wewe mimi ndiye mtu ninaye mjua kuliko binadamu yeyote ndani ya nchi hii kupitia usalama wa taifa nimeweza kujua karibia robo tatu ya maisha ya huyo binadamu, yule sio binadamu wa kawaida kama unavyo msikia wewe wakikupa hadithi zake kwa ulivyo mlaini hivyo huwezi hata kumaliza dakika moja ukiwa umesimama mbele yake, una macho mazito mno, mikono yako mizito, hata kufanya maamuzi una kichwa kizito na unang'ang'ania kukutana na hilo dubwana hahahhahahahahahahahhahahah.

Kuna mambo ambayo bado wewe hapo huyaelewi Kwanza umefanya kosa kubwa sana kwenda kumbaka mkewe na kuwaua yeye na mtoto wake (Qader alishangaa hizi habari huyu mtu kazijuaje?) kosa kama hilo liliiponza familia moja miaka kadhaa iliyopita huko nyuma, kwa hicho ambacho umefanikiwa kukifanya kwa sasa ilitakiwa utafute sehemu ambayo hakuna binadamu atajua kwamba ulishawahi kutokeaga au kuzaliwaga kwenye hii dunia yaani upotee kabisa kwenye mifumo ya ulimwengu kwa sababu kwa namna yoyote ile hawezi kukuacha hai na hakuna sehemu utaweza kulikimbia lile dubwana kwenye hii dunia labda kama utajiua mwenyewe na ulivyo mjinga unafanya mawasiliano kabisa na watu wako ukiwa unajiachia unashindwa kuelewa kwamba mawasiliano yenu kuna watu wanayasikia moja kwa moja( alipiga funda lingine la sigara na kuendelea).

Huyo binadamu ambaye wewe unamtafuta ni bora hata ungeenda vijijini hapa Tanzania ukauze miwa na nyanya usijulikane uliko kuliko kulitafuta hilo dubwana una maisha mafupi sana kama ataamua kukutafuta wewe ni kama mtoto wa kike ambaye ilitakiwa ukae pembeni ukiwa unapika chakula nyumbani, hii michezo siyo ya watoto wadogo kama wewe, hauelewi chochote kile. Zakaria Mansour ni mtu ambaye mimi pekee ndiye mtu ninayeweza kumpiga kwenye dunia hii yote unayo ijua wewe" ni maelezo marefu ambayo yalimfanya Qader aanze kutetemeka hapo alikuwa hajauliza mtu huyo alijuaje familia yake ilipo alionekana kumjua sana Zakaria kuliko mtu yeyote yule, kauli yake ya kusema yeye pekee ndiye mtu ambaye alikuwa anaweza kumpiga Zakaria ilimfikirisha Qader na kuanza kujiuliza huyo mtu ni nani?. Baada ya maelezo hayo kwa kutumia mkono wake mmoja ambao ulikuwa umefunguliwa Jiti alitupa kipande cha sigara na kuingiza kwenye mfuko wake alitoa chupa moja ambayo ilikuwa ina maji maji ndani yalionekana kuwa makali mno kwa sababu chupa ilifungwa lakini bado ilikuwa inatoa mvuke, mwanaume alikifungua kwa mdomo akanywa kidogo kimiminika hicho kisha akajimwagia sehemu ambayo Qader alikuwa ameing'oa kucha hake na kukikata kidole.

Zilipita sekunde kumi na tano tu ile sehemu ilijiunga na kurudi kama ilivyokuwa mwanzo, mwanaume huyo alitabasamu sana alikaza mikono yake na miguu alikata vyuma ambavyo alikuwa amefungwa navyo Qader alibaki ameduwaaa, mwanaume huyo alisimama na kujinyoosha vizuri mifupa iliitikia alitabasamu na kuikunja sura yake alikuwa yupo huru, alitumia mkono wake wa kulia kuzamisha kucha yake kwenye shingo , alivuta kwa nguvu na kuitoa sura ambayo kila mtu alimjua kama anaitwa Jiti, aisee kitu alicho kiona Qader mbele yake alidondoka na kuzimia.

Naishiwa maneno ya kuongeza mambo yanatisha sana, huyu Jiti ni nani? Na kwanini sura yake ilivyoonekana kwenye uso wa Qader alizimia? Ameponaje sehemu yenye jeraha na kama yeye ndiye anaweza pekee kumpiga Zakaria ndani ya usalama wa taifa anatafuta nini?.....najua una maswali mengi sana ambayo hata mimi yananiumiza kichwa ila siku moja nikipata wasaa nitayajibu.

Kalamu ni yangu mwenyewe

Bux the story teller
 
Yeah huu ni moto tena si wa petrol bali wa gas, unawaka, unachoma na kugeuza majivu laini kile kichomachwo ndani ya sekunde kadhaa tu. Nimeikubali hii simulizi, big up sana mshika karamu FEBIANI BABUYA
 
Yeah huu ni moto tena si wa petrol bali wa gas, unawaka, unachoma na kugeuza majivu laini kile kichomachwo ndani ya sekunde kadhaa tu. Nimeikubali hii simulizi, big up sana mshika karamu @FEBIAN BABUYA
Shukrani sana mkuu kwa kuendelea kuifuatilia kalamu yangu, baadae kidogo tukaufunue ukurasa unao fuata tuone nini kinakuja. Ni hatari sana huko mbele.
 
STORY: GEREZA LA HAZWA
STORY WRITER: FEBIANI BABUYA
STORY TELLER: Bux the story teller
AGE: 18+

UKURASA WA ISHIRINI NA MBILI

TULIPO ISHIA UKURASA WA ISHIRINI NA MOJA


Aariz aligeuka na kuwaangalia watu hao wawili ambao walikuwa pembeni yake walitikisiana vichwa kuonyesha kukubaliana na maelezo yaliyo tolewa, alijifuta jasho usoni alijua ni kazi nyepesi sana ila kwa maelezo yaliyo tolewa kulikuwa kuna mlima mzito sana mbele yake, alirushiwa faili mbele yake ambalo lilikuwa na maelezo yote ya nini anacho takiwa kukifanya, wanaume hao watatu walitoka humo ndani kazi yao walikuwa wameimaliza sasa ilibakia juu yake aliachwa pekeyake kwenye hicho chumba mawazo yalikitawala sana kichwa chake aliwaza kuhusu familia yake hakuelewa hatima yake itakuwa ni nini.

ENDELEA.......................

TABATA TANZANIA
Kilicho mshtua na kumshangaza sana Jiti Maalimu sio kwa sababu watu hao walifanikiwa kumjua yeye kama usalama wa taifa wala kuhitaji taarifa fulani alijua wazi vigogo wengi huwa wanawapenyeza watu wao ili kujinufaisha wao wenyewe hususani wanapo hitaji kufanya mambo yao ya siri bila kushtukiwa na mtu yeyote huwa wanawatumia sana watu hao ambao wengi kwao pesa huwa ni kipaumbele kikubwa sana ila kilicho mfanya abaki mdomo wazi mpaka muda huo ni mtu ambaye taarifa zake zilikuwa zinahitajika Zakaria Mansour, ilikuwa ni siri nzito sana kuhusu mtu huyo ambaye alionekana kuwa na dili sana sokoni, ni watu wachache mno ambao walikuwa na taarifa zake na ilikuwa ni siri yake pekeyake moyoni kwani kazi ya kumfuatilia mtu huyo hakupewa na mkurugenzi wa usalama wa taifa bali aliku amekabidhiwa na mheshimiwa raisi mwenyewe wa nchi ya Tanzania Mr Alan Mwaiponela sasa hawa watu walijuaje kuhusu hilo? aligundua kwamba ni lazima raisi kuna watu wengine ambao aliwashirikisha kwenye hiyo kazi hilo lilikuwa kosa la Kwanza kulifanya.

"Huyo Zakaria ndo nani?" Alikuwa siriasi sana kwenye uso wake alimaanisha kweli kwamba hana uelewa juu ya uwepo wa mtu ambaye jina lake lilikuwa likifahamika kama Zakaria.

"Mhhhhhh nimekuonya kwa mara ya Kwanza huwa sio mpiga stori mzuri sana ndio maana nimekupa tahadhari mapema sana" Qader aliyatamka maneno yake huku akilisogeza box la vifaa na kuchukua kiti akasogea karibu na alipokuwa amefungwa Jiti akakaa akiwa bado yupo kifua wazi.

"Nimefanya kazi kwa muda mrefu sana wenye hiyo idara sijawahi kusikia jina kama hilo hata siku moja ndiyo Kwanza nalisikia kwako leo" alionekana kukereka sana hivyo alikuwa anajibu kikakamavu ili asionekane mlaini sana mwarabu huyo alimwangalia kwa muda kwa hasira kisha akatamka kirahisi tu sawa.

"Sawa" alitoa koleo dogo na mkasi kwenye hilo box pamoja na waya, akasogeza mita ambayo ilikuwa inasoma umeme wa kutosha ambao usingeisha hata kwa bahati mbaya. Alizamisha koleo hilo kwenye kidole gumba cha mguu wa Jiti na kunyofoa ukucha ambao ulibanduliwa kwa lazima bila huruma licha ya Jiti kupiga makelele sana hakuna mtu ambaye alikuwa na muda naye wala kumuonea huruma, baada ya ukucha kunyofolewa mkasi ulipita na sehemu ya mbele ya kidole hicho damu nyingi ilikuwa inatoka mwanaume huyo alizamisha kwa nguvu waya mgumu ambao alikuwa ameushika kwa mkono wake wa kushoto ulitoboa na kuzama mpaka ndani waya ukiwa umezamishwa mwanaume huyo alichukua waya ya umeme ambayo iliunganishwa kwenye koleo la chuma akawa anagusisha kwenye waya ambao ulikuwa umezamishwa kwenye kidonda. Shoti ambayo ilikuwa inapita kwenye kidonda hicho hakuna binadamu mwenye moyo wa kawaida angeweza kuvumilia alitoa mkojo akiwa anaomba aongee kila kitu alikiri kumkosea sana mwanaume huyo, alilia sana uso wake ulichafuka kwa machozi na damu ambayo ilisababishwa na damu kutoka puani na mdomoni ni wazi alikuwa amekutana na shetani siku yake hiyo.

Baada ya dakika mbili mwanaume huyo alitoa vitu vyake na kuvirudisha kwenye box lake akalifunga na kulirudisha mahali lilipokuwa mwanzo bila kuongea kitu chochote kile kisha akarudi na kukaa akiwa anamwangalia Jiti ambaye bado alikuwa anatoa machozi kwa uchungu sana, Qader alisikitika sana kisha akainama chini kwa dakika moja na kuinua uso wake tena.

"Nadhani maelezo yangu uliyapuuzia wakati nakuelekeza kwa mara ya kwanza, nikiwa na miaka nane tu niliua watu 20 kwa risasi hivi unadhani leo nikiwa na miaka hii 28 nitashindwa kukuua mpumbavu mmoja kama wewe hapo ambaye hata sikujui kabisa?, Huwa nachukia sana kuongea jambo moja mara saba saba ambalo linaweza kuisha ndani ya dakika moja tuz hapo nimekuonjesha tu uwe unanijibu kwa nidhamu unapokuwa mbele yangu mimi sio mtu ambaye unaweza kunijibu vile unavyo jisikia wewe wala mimi sio mtu wa kuanza kukubembeleza pale ninapokuwa nazihitaji taarifa fulani kwako upo kwenye mikono yangu ni lazima useme ninacho kuuliza, hapa una sekunde thelathini tu za kuendelea kuwa na viungo vyako vyote kwenye mwili wako" Qader aliongea kiutulivu sana akiwa amemkazia macho Jiti lakini maneno yake yalikuwa kwenye msisitizo mkali sana.

"Naomba maji tafadhali nasema" Jiti aliongea kwa shida sana alihisi kama mwili wake umekauka ni dakika kadhaa alitoka kupatiwa maji lakini wakati huu alikuwa anahisi kama mwili wake haukuwahi kupata maji kwa miaka kadhaa, Qader alinyanyuka mwenyewe akatoka kwenye hicho chumba alirudi na ndoo nzima ya maji alimpa mtu huyo kikombe baada ya kumfungulia mkono mmoja alikunywa kwa pupa sana mengine yalikuwa ya baridi mno lakini ndoo nzima alimwagiwa mwilini kidogo mwili ulipata nguvu hata kidole maumivu yake yalipungua kiasi, alijifuta usoni akiwa anahema kwa nguvu.

"Una familia?" Qader alilisikia vizuri hilo swali lakini hakuelewa linamaanisha nini na Jiti hakuonekana kuwa na masiara maana alikaa vizuri akioekana wazi kwamba alikuwa anasubiri kwa umakini jibu kwa mtu huyo.

"Linahusiana vipi na maswali ambayo nimekuuliza hapa?" Aliuliza kwa sauti yake ya mgandamizo.

"Ni mhimu sana kunijibu hilo swali kabla haujaanza kujutia"

"Kwahiyo unanitisha"

"Sikutishi"

"Kwahiyo lengo lako ni lipi?

"NATAKA kukupa tahadhali"
"Ya nini"
"Ya huyo mtu ambaye wewe unamtafuta"
"Kuna kipi hicho cha kutisha ambacho unakijua kwake?"
"Nijibu swali lako ndani ya nchi hii mimi ndiye ninaye mjua yule mtu kuliko binadamu yeyote na hakuna ambaye analijua hili"
"Whaaaaaat"
"Nijibu nilicho kuuliza"

"Familia yangu ipo na ipo mahali salama sana" alijibu kwa kujiamini sana Qader

"Una uhakika na unacho kisema?" Jiti aliuliza kwa kujiamini sana kidogo mpaka Qader alishtuka
"Yes"

"Hahahahahahahahah unaitwa Taofic Mhamaduu, una watoto wawili mapacha ambao umewaficha ndani ya nchi ya Afrika ya kusini pembezoni mwa jiji la Johensberg u......" Qader moyo ulimuenda mbio alijikuta jasho linamtoka ikamlazimu kumkatisha mwanaume huyo mbele yake ambaye alikuwa kwenye maumuvu makali cha ajabu hakuwa na wasiwasi na alikuwa akiijua siri ambayo Qader hakuwahi kumwambia binadamu yeyote yule kwenye maisha yake.

"Weeee.wew..wew ni nani?" Aliuliza kwa kigugumizi Qader akiwa na hasira kali sana aliitoa bastola na kuiweka kwenye kichwa cha Jiti lakini mtu huyo aliishia kutabasamu tu.

"Halafu huwa sitishiwi na bastola kwenye maisha yangu kama unahitaji nikuue hapa hapa endelea kuniwekea hilo toi lako kichwani mwangu hebu kaka hapo chini nikufundishe maisha" Jiti alikuwa ni jeuri ambaye hata magaidi wasingeweza kwenda naye sawa chanzo cha ugaidi wake hakikueleweka ni nini, Qader alijikuta mwenyewe anaishusha bastola yake na kukaa chini nguvu zilimuishia alikuwa mtu katili sana ila leo alianza kumuogopa mtu ambaye yeye alimjua kama usalama wa taifa ila ilionekana mtu huyo alikuwa ni zaidi ya ambavyo yeye alikuwa anamfikria suala la kutajiwa familia yake ilipo lilimuogopesha sana mwanaume huyu aliogopa sana.

"Nitafutie sigara uniletee ili ujue kitu ambacho kinakupa jeuri kwenye maisha yako wakati huna chochote cha kukupatia jeuri" maneno mengine ya jeuri yalitoka kwenye kinywa cha Jiti yalimshtua sana Qader alitoka kwa mbio na kutoka nje ya hicho chumba alirudi akiwa na sigara za bei ghali tano alikumbuka amesahau kiberiti basi ilamlazimu kurudi teja akiwa anakimbia alitamani sana kujua kipi kilijificha nyuma mpaka mtu huyo alikuwa anayajua mambo mengi namna hiyo. Jiti alichukua aliiweka sigara mdomoni na kumpa ishara Qader amuwashie alifanya hivyo.

"Kwenye maisha yako huenda huwa unajidanganya kwamba wewe ni mtu mkatili na mwenye roho ngumu sana ila kwa mimi nakuona kama wewe ni mwanamke tu wewe bado ni kijana dhaifu sana hapo ulipo ambaye hadi kuua mtu mpaka ujisifie una roho nyepesi sana unajiuliza mara mbili mbili ndio maaana sikutaka uwe kijana wangu( aliongea na kuvuta funda lingine kwa mkono mmoja ambao ulikuwa umefunguliwa). Huyo mtu ambaye unamtafuta kwa nguvu na kufoka hivyo unamujua kwanza? Au kwa sababu tu umeagizwa ndo unakuja kwa pupa na mikwala mingi namna hiyo ushawahi kusikia wapi muwindaji akawa na makelele hivyo na akafanikiwa kupata windo lake?. Wewe sio mtu wa hatari kama unavyo jisifia wewe ni kijana wa kawaida saaaana tena saaana na huna jipya wanapo simama watu wanao itwa hatari, huyo mtu unaye mtafuta wewe mimi ndiye mtu ninaye mjua kuliko binadamu yeyote ndani ya nchi hii kupitia usalama wa taifa nimeweza kujua karibia robo tatu ya maisha ya huyo binadamu, yule sio binadamu wa kawaida kama unavyo msikia wewe wakikupa hadithi zake kwa ulivyo mlaini hivyo huwezi hata kumaliza dakika moja ukiwa umesimama mbele yake, una macho mazito mno, mikono yako mizito, hata kufanya maamuzi una kichwa kizito na unang'ang'ania kukutana na hilo dubwana hahahhahahahahahahahhahahah.

Kuna mambo ambayo bado wewe hapo huyaelewi Kwanza umefanya kosa kubwa sana kwenda kumbaka mkewe na kuwaua yeye na mtoto wake (Qader alishangaa hizi habari huyu mtu kazijuaje?) kosa kama hilo liliiponza familia moja miaka kadhaa iliyopita huko nyuma, kwa hicho ambacho umefanikiwa kukifanya kwa sasa ilitakiwa utafute sehemu ambayo hakuna binadamu atajua kwamba ulishawahi kutokeaga au kuzaliwaga kwenye hii dunia yaani upotee kabisa kwenye mifumo ya ulimwengu kwa sababu kwa namna yoyote ile hawezi kukuacha hai na hakuna sehemu utaweza kulikimbia lile dubwana kwenye hii dunia labda kama utajiua mwenyewe na ulivyo mjinga unafanya mawasiliano kabisa na watu wako ukiwa unajiachia unashindwa kuelewa kwamba mawasiliano yenu kuna watu wanayasikia moja kwa moja( alipiga funda lingine la sigara na kuendelea).

Huyo binadamu ambaye wewe unamtafuta ni bora hata ungeenda vijijini hapa Tanzania ukauze miwa na nyanya usijulikane uliko kuliko kulitafuta hilo dubwana una maisha mafupi sana kama ataamua kukutafuta wewe ni kama mtoto wa kike ambaye ilitakiwa ukae pembeni ukiwa unapika chakula nyumbani, hii michezo siyo ya watoto wadogo kama wewe, hauelewi chochote kile. Zakaria Mansour ni mtu ambaye mimi pekee ndiye mtu ninayeweza kumpiga kwenye dunia hii yote unayo ijua wewe" ni maelezo marefu ambayo yalimfanya Qader aanze kutetemeka hapo alikuwa hajauliza mtu huyo alijuaje familia yake ilipo alionekana kumjua sana Zakaria kuliko mtu yeyote yule, kauli yake ya kusema yeye pekee ndiye mtu ambaye alikuwa anaweza kumpiga Zakaria ilimfikirisha Qader na kuanza kujiuliza huyo mtu ni nani?. Baada ya maelezo hayo kwa kutumia mkono wake mmoja ambao ulikuwa umefunguliwa Jiti alitupa kipande cha sigara na kuingiza kwenye mfuko wake alitoa chupa moja ambayo ilikuwa ina maji maji ndani yalionekana kuwa makali mno kwa sababu chupa ilifungwa lakini bado ilikuwa inatoa mvuke, mwanaume alikifungua kwa mdomo akanywa kidogo kimiminika hicho kisha akajimwagia sehemu ambayo Qader alikuwa ameing'oa kucha hake na kukikata kidole.

Zilipita sekunde kumi na tano tu ile sehemu ilijiunga na kurudi kama ilivyokuwa mwanzo, mwanaume huyo alitabasamu sana alikaza mikono yake na miguu alikata vyuma ambavyo alikuwa amefungwa navyo Qader alibaki ameduwaaa, mwanaume huyo alisimama na kujinyoosha vizuri mifupa iliitikia alitabasamu na kuikunja sura yake alikuwa yupo huru, alitumia mkono wake wa kulia kuzamisha kucha yake kwenye shingo , alivuta kwa nguvu na kuitoa sura ambayo kila mtu alimjua kama anaitwa Jiti, aisee kitu alicho kiona Qader mbele yake alidondoka na kuzimia.

Naishiwa maneno ya kuongeza mambo yanatisha sana, huyu Jiti ni nani? Na kwanini sura yake ilivyoonekana kwenye uso wa Qader alizimia? Ameponaje sehemu yenye jeraha na kama yeye ndiye anaweza pekee kumpiga Zakaria ndani ya usalama wa taifa anatafuta nini?.....najua una maswali mengi sana ambayo hata mimi yananiumiza kichwa ila siku moja nikipata wasaa nitayajibu.

Kalamu ni yangu mwenyewe

Bux the story teller
STORY: GEREZA LA HAZWA
STORY WRITER: FEBIANI BABUYA
STORY TELLER: Bux the story teller
AGE: 18+

UKURASA WA ISHIRINI NA TATU

TULIPO ISHIA UKURASA WA ISHIRINI NA MBILI

Zilipita sekunde kumi na tano tu ile sehemu ilijiunga na kurudi kama ilivyokuwa mwanzo, mwanaume huyo alitabasamu sana alikaza mikono yake na miguu alikata vyuma ambavyo alikuwa amefungwa navyo Qader alibaki ameduwaaa, mwanaume huyo alisimama na kujinyoosha vizuri mifupa iliitikia alitabasamu na kuikunja sura yake alikuwa yupo huru, alitumia mkono wake wa kulia kuzamisha kucha yake kwenye shingo , alivuta kwa nguvu na kuitoa sura ambayo kila mtu alimjua kama anaitwa Jiti, aisee kitu alicho kiona Qader mbele yake alidondoka na kuzimia.
ENDELEA.............................

Baada ya sekunde kadhaa za kuhesabu Qader alikurupuka kutoka kwenye usingizi mzito mbele yake bado mwanaume huyo alikuwa amesimama vile vile alimwangalia kwa hofu sana mwanaume huyo aliinama pale Qader alipokuwa amekaa aliinama kidogo na kuonyesha masikitiko, sura yake Qader hakuwahi kuiona kwenye maisha yake yote wala hakuwahi kuisikia stori ya mtu wa aina hiyo kwenye maisha yake yote ilimshtua baada ya kuona mbele yake alikuwa amesimama mtu mwenye asili ya kiarabu na sio sura ya kitanzania ambayo yeye alikuwa akiijua na kumjua mhusika kama Jiti Maalimu leo aliingizwa cha kike.

"How is this possible? (Hii inawezekanaje?)" Asingeshindwa kupata mshangao kwa kile ambacho kilikuwa kinatokea kwani kilikuwa kinatisha.

"Hii ndiyo dunia ambayo inabeba kila kitu, inabeba binadamu wanyonge wa kawaida tu, inabeba matukio ya kutisha, inabeba viumbe vya ajabu mara nyingi wanao kuwa hatari ni wale wenye upeo mkubwa wa akili na watu wenye pesa ila unapaswa kuwa makini kwa sababu unaweza kuwa na pesa ila ukikosa akili bado wenye akili zao watakutawala tu na hakuna kitu utaweza kukifanya na watakuendesha kadri watakavyo wao. Pale unapo jihisi kwamba unaijua sana dunia ndio muda sahihi wa kujifunza kwa sababu unakuwa ni mshamba sana kwenye baadhi ya maisha ya watu fulani. Hakuna mtu amewahi kulijua jambo hili kwamba mimi sio mtanzania wewe ndiye binadamu wa Kwanza kabisa ndiyo maana nilitaka nikutane nawewe mapema(aliguna kidogo) mimi kukamatwa na hao watoto sio kwamba walivyo nifuata walikuwa na uwezo wa kunikamata, hapana ile sindano na sumu ambayo walinichoma kwangu huwa hazifanyi kazi ila nilijifanya tu kudondoka ili nikutane nawewe.

Wale ni watoto wadogo sana ambao ningewaua kwa sekunde kadhaa tu, huyo mtu ambaye unamtafuta wewe nimetumia sio chini ya miaka minne kuweza kuzipata taarifa zake kwa sababu huwa hazipo na sio kila mtu anaweza kuzipata ndio maana mpaka leo hujawahi kumpata zaidi ya kubahatika kuipata familia yake napo ni baada ya yule mjinga rafiki yake kumsaliti alifanya kosa kubwa sana yule bwana mdogo usaliti ni kitu kibaya sana" alitulia na kumwangalia Qader ambaye ni dhahiri bado alikuwa na maswali mengi sana na ni kama alikuwa hamuelewi kabisa mtu huyo alishindwa kumsoma kwa namna yoyote ile.

"Miaka mitano iliyopita nilikuwa nimesambaza vijana wangu waweze kumtafuta sehemu yoyote ile ambayo wanaweza kumuona wanipe taarifa, nadhani kijiamini kuliwaponza sana walibahatika kukutana naye mara moja tu na ndicho kilicho nipa uhakika asilimia mia kwamba yupo kwenye nchi hii bahati mbaya sana aliwaua vijana wangu wawili na mmoja alifanikiwa kukimbia baada ya hapo haikuwahi kujulikana tena kuhusu uwepo wake mpaka pale alivyo potea na kuiacha familia yake ambayo wewe ulienda kufanya ujinga na mtu yule huwa hakubali kuacha familia nyuma lazima hapa katikati kuna tatizo ndiyo sababu amepotea kiwepesi namna hii" maneno mengine ni kama yalianza kumfungua kichwa Qader namna mtu huyo alivyo.

"Sasa wewe unasimama kama nani na unafanya kazi na nani kwa manufaa yapi na kwanini?" Maswali yalikuwa ni mengi sana kutoka kwa Qader yalimfanya Jiti acheke sana mpaka akashika mbavu zake kijana aliyekuwa mbele yake alikuwa ana wasiwasi mno.

"Nadhani umesema unanijua sana, mimi ni afisa usalama na ndo kazi yangu kama ulivyosema na nafanya kazi na Mr President"

"Noooooooo, usalama wa taifa na Mr President wapi na wapi?"

"Una kichwa cha hovyo na akili ya kijinga sana mambo huyajui na bado unakuwa na akili ya ubishi sana kiasi hicho sijajua ni kipi kinakupa jeuri hiyo, unajua nini wewe mpaka uwe na huo uwezo wa kunibishia?" Jiti aliongea kwa hasira na kumkazia macho Qader akimpiga piga shavuni ilibidi atulie tu ni wazi alionekana kudandia gari mbele.
"Mimi najulikana kama afisa usalama wa taifa halali wa Tanzania na kwa uadilifu wa kazi yangu ulinipa sana jina mpaka ikafikia sehemu nikaaminiwa na kuitwa na mheshimiwa raisi ambaye alinipa kazi ya kumsaidia kuifanya. Usiku mmoja nikiwa ndani ya nyumba yangu Osterbay nilipokea simu kutoka sehemu ambayo sikuijua kabisa alikuwa ni raisi wa nchi ya Tanzania ilinishtua sana kwa sababu sio kawaida raisi kukupigia simu mtu wa kawaida pasipo na sababu yoyote ya msingi basi ilinibidi nitulize akili vizuri ili nimsikilize kwa umakini

"Naongea na Jiti Maalimu?"
"Ndiyo wewe nani?"
"Alan Mwaiponela"
"You mean Mr President"
"Here you are" nilishtuka sana
"Welcome Mr President"
"I need you this time at the state house" nilikuwa na wasiwasi sana baada ya kuambiwa kwamba ananihitaji Ikulu muda huo nikiwa kwenye mawazo mazito nilisikia mlio wa gari nje ya nyumba yangu nikajua basi nimeisha, nilipanda kwa unyonge sana.

"Welcome Jiti" niliitikia salamu yake kwa kutoa heshima baada ya kuingia ndani ya Ikulu na ndio ilikuwa mara yangu ya Kwanza kupata bahati ta kukaa na raisi Ikulu asikudanganye mtu ile sehemu ni nzuri sana, ni ndoto ya kila mwananchi kuingia pale na ina ulinzi mkali wa kutisha nilijikuta naipenda mno na nilitamani siku moja ningekuwa miongoni mwa watu ambao wangeishi Ikulu bahati mbaya huo uwezo ilikuwa ni kazi sana kuufikia.
"Asante sana mheshimiwa"
"Lazima umeogopa sana raisi kukupigia simu tena usiku huu wa manane"
"Ndiyo mheshimiwa nimeshtuka sana kwa sababu sio rahisi raisi mwenye heshima kama wewe kumpigia simu mtu wa kawaida kama mimi imenitisha" alionekana kutabasamu sana
"Ni miongoni mwa vijana ambao mna mchango mkubwa sana kwenye taifa kwahiyo usijishushe sana chini"
"Lakini sioni kama nastahili heshima ya namna hii asante sana kiongozi"
"Sasa nimekuita hapa leo kwa sababu kuu moja, ufanyaji kazi wako kwa weledi, kujituma na kuwa na nidhamu na kile unacho kifanya ndicho kimefanya bahati hii ikudondokee wewe, i need to work with you (nahitaji kufanya kazi nawewe)" nilihisi sijasikia vizuri nilishangaa kivipi raisi atake kufanya kazi namimi, alitembea kwa mbele kidogo na kuvuta droo moja alitoa faili fulani ambalo lilikuwa na rangi nyeusi.
"Haya mafaili yana kazi tofauti hususani za utunzaji wa nyaraka na taarifa mhimu, yapo ya aina nyingi sana ila ukiona taarifa inatunzwa kwenye faili jeusi basi kuna mawili inawezekana taarifa hizo ni za kitu cha muhimu sana au ni taarifa za mtu mhimu sana. Ni siku kadhaa nyuma hapo nilikuwa natafuta mtu wa kufanya naye kazi ndani ya usalama wa taifa hivyo ilinilazimu niongee na mkurugenzi wa usalama wa taifa kwa sababu yeye ndo anaye wajua vizuri zaidi kuliko mimi, alinipa mafaili ya vijana kumi ambayo baada ya kuyapitia nilivutiwa sana na faili lako unaonekana unafanya kazi kwa weledi sana ndiyo sababu iliyo nifanya nikutafute tuifanye kazi hii" kidogo nilishusha pumzi maana nilihisi huenda nimesha shtukiwa.

"What do you think?(unafikiria nini?)" Hata sikusikia chochote kutokana na swali lake muda huo nilikuwa kwenye mawazo mazito sana nikiwa nakumbuka jinsi nikivyoweza kuingia ndani ya idara ya usalama huo, jina Jiti ni kweli ni jina ambalo alikuwa analitumia kijana mmoja ambaye alikuwa anaitwa Jiti Maalimu huyo kijana alikuwa ni usalama wa taifa muadilifu Saba na alijichukulia unaarufu sana ndani ya idara ya usalama wa taifa kutokana na uadilifu wake mkubwa kwenye kazi na ndiyo maana nilivutiwa naye sana. Nilianza kumfuatilia kwa umakini sana na baada ya muda nikazipata taarifa zake zote hivyo nikawa nahitaji kuichukua ile nafasi yake hiyo ilinilazimu kuyasoma maisha yake tangu anazaliwa mpaka siku hiyo, baada ya kuyajua mambo yote hayo ndipo nilipofanya maamuzi ya kumuua kisha sura yake ikabadilishiwa kwangu mambo ya utandawazi hayo hapo ndipo nilipo anza kuyaishi maisha ya kijana yule.

"Hey i asked what do you think(wewe niliuliza unafikiria nini?)" Sauti yake ndiyo iliyo nikurupua kutoka kwenye hayo mawazo nilishtuka sana.

"Oooh Mr President i accept it and I'm ready to work for you at any cost (ooh mheshimiwa raisi nimeikubali na nipo tayari kuifanya kwa ajili yako kwa gharama yoyote ile)" alitabasamu sana baada ya mimi kumjibu vile basi pale ndipo alipo anza kunipa mipango ya yeye kuzipata hizo taarifa za siri ambazo zilikuwa zinahusisha Zakaria kutafutwa sana alihitaji nichimbe kwa undani ili nijue kama kweli mtu huyu alikuwa ndani ya nchi hii na kama alikuwepo basi alitaka nijue yuko wapi na niitafute historia yake yote ya maisha ya nyuma na hapo ndipo nilipo anza kumjua vizuri Zakaria Mansour ni nani na ndivyo nilivyo ingia kwenye idara ya usalama wa nchi hii japo kuna taarifa siwezi kuzipata kutokana na nafasi ndogo ambayo niliyo nayo huko maana kufanya kazi na raisi imekuwa ni siri nzito sana" alijibu kwa macho makavu akiwa bado anamwangalia kwa umakini sana Qader.

"Then who are you na kwanini unayafanya haya yote? Kwa sababu unaonekana kabisa ulidhamiria kufanya haya ndiyo maana uliua mpaka mtu ili tu upate nafasi ya kuingia huko ndani ya usalama wa taifa" Qader aliuliza kinyonge sana.

"Yes upo sahihi sana, nilipania sana tena sana kuingia huko ili nipate urahisi wa kuzipata taarifa za mtu huyo ukiuliza kwanini swali ni moja na mtu kuniuliza mimi ni nani na kwanini namtafuta sana huyu mtu. Bado ni mapema sana kukutajia jina langu kwa sababu kuna asilimia nyingi kama ukilijua jina langu halisi nitakuua hapa hapa sasa chagua wewe nikutajie jina langu ufe hapa au tuache mambo kama yalivyo nikuache uendelee kula mema ya nchi?" Qader alifikiria sana hilo swali alitikisa kichwa kuonyesha kwamba hakuwa tayari kufa ni bora asilijue tu hilo jina lenyewe.

"Sasa mimi kuna kazi ambazo naenda kuzimalizia kwa sasa na najua una maswali mengi sana kuhusu mimi maana mpaka sasa hakuna chochote unacho kijua kuhusu mimi zaidi tu ya kuona kwamba mimi sio mtanzania na kupata historia fupi namna nilivyoweza kuingia ndani ya usalama wa taifa la Tanzania na kuanza kufanya kazi na mheshimiwa raisi. Najua hapa uliniita ili kupata taarifa za mtu huyo kwa kukusaidia tu familia yake ambayo imebakia inapatikana kwenye kijiji kimoja huko BUKOBA kinaitwa KIBETA panaitwa kwa mzee Philebert, huko ndiko aliko bibi, babu yake pamoja na anko zake na ndugu wengine na hajawahi kabisa kufika huko, unaweza ukawa na maswali mengi kama ni hivyo kwanini ni mtu wa Libya sasa hayo nakuachia mwenyewe utajiongeza.

Sikulazimishi wala sina ushauri wowote ule kwamba uende kufanya lolote huko ila kama unapahitaji basi ndo huko utajua mwenyewe kama utaenda au hautaenda sio biashara yangu kujua hilo. Ila nataka unisikilize vizuri sana na kwa umakini mno, kama unaweza kimbia na uende sehemu ambayo hakuna mtu atajua kuhusu uwepo wako hapa duniani, usitumie simu wala aina yoyote ya mtandao yaani usijulikane tena kama uliwahi kuwepo na ikiwezekana badilisha sura yako asikujue mtu yeyote yule hicho ndicho kinaweza kuifanya familia yako kuwa salama ila vinginevyo utakufa vibaya sana na ubaya wa yule jamaa huwa haachi mtu yaani kosa unafanya wewe ila anahakikisha familia yako yote inalipa hilo na nadhani ana sababu za msingi kufanya hivyo. Hii ni vita ya kisasi na wewe haikuhusu kabisa ni tamaa za pesa tu zinakuingiza huku hiyo itakupelekea upotee ukiwa bado kijana mdogo sana zingatia hilo kabla haujaanza kujuta nimekwambia mwanzo hata familia moja miaka kadhaa nyuma huko waliwahi kufanya mistake ya hivyo maumivu yaliyo tokea hakuna mwanadamu ambaye angeweza kuvumilia kuyaona kwa macho yake" Jiti aliitazama saa yake kwa umakini na kutoka nje alikuwa anaondoka hilo eneo kama ni kwake vile, aliletwa kama mateka ila aliondoka huru tena bila kuruhusiwa na mtu.

Qader hata hakushtuka wakati mwanaume huyo anaondoka kwenye kichwa chake ni mambo mengi sana yalikuwa yanamzunguka hakuelewa chochote kwani alihisi kama kichwa kinataka kupasuka alikaa chini na kulala huenda akili yake ingekaa sawa akiamka.

Bado hatujamjua Jiti ni nani anaonekana kuwa mtu wa kutisha sana, ipi sababu ya kumsaka sana Zakaria? Bado sana mchezo ndo Kwanza unaanza ebu twende sawa mpaka mwisho.

Langu jina naitwa

Bux the story teller
 
STORY: GEREZA LA HAZWA
STORY WRITER: FEBIANI BABUYA
STORY TELLER: Bux the story teller
AGE: 18+

UKURASA WA ISHIRINI NA TATU

TULIPO ISHIA UKURASA WA ISHIRINI NA MBILI

Zilipita sekunde kumi na tano tu ile sehemu ilijiunga na kurudi kama ilivyokuwa mwanzo, mwanaume huyo alitabasamu sana alikaza mikono yake na miguu alikata vyuma ambavyo alikuwa amefungwa navyo Qader alibaki ameduwaaa, mwanaume huyo alisimama na kujinyoosha vizuri mifupa iliitikia alitabasamu na kuikunja sura yake alikuwa yupo huru, alitumia mkono wake wa kulia kuzamisha kucha yake kwenye shingo , alivuta kwa nguvu na kuitoa sura ambayo kila mtu alimjua kama anaitwa Jiti, aisee kitu alicho kiona Qader mbele yake alidondoka na kuzimia.
ENDELEA.............................

Baada ya sekunde kadhaa za kuhesabu Qader alikurupuka kutoka kwenye usingizi mzito mbele yake bado mwanaume huyo alikuwa amesimama vile vile alimwangalia kwa hofu sana mwanaume huyo aliinama pale Qader alipokuwa amekaa aliinama kidogo na kuonyesha masikitiko, sura yake Qader hakuwahi kuiona kwenye maisha yake yote wala hakuwahi kuisikia stori ya mtu wa aina hiyo kwenye maisha yake yote ilimshtua baada ya kuona mbele yake alikuwa amesimama mtu mwenye asili ya kiarabu na sio sura ya kitanzania ambayo yeye alikuwa akiijua na kumjua mhusika kama Jiti Maalimu leo aliingizwa cha kike.

"How is this possible? (Hii inawezekanaje?)" Asingeshindwa kupata mshangao kwa kile ambacho kilikuwa kinatokea kwani kilikuwa kinatisha.

"Hii ndiyo dunia ambayo inabeba kila kitu, inabeba binadamu wanyonge wa kawaida tu, inabeba matukio ya kutisha, inabeba viumbe vya ajabu mara nyingi wanao kuwa hatari ni wale wenye upeo mkubwa wa akili na watu wenye pesa ila unapaswa kuwa makini kwa sababu unaweza kuwa na pesa ila ukikosa akili bado wenye akili zao watakutawala tu na hakuna kitu utaweza kukifanya na watakuendesha kadri watakavyo wao. Pale unapo jihisi kwamba unaijua sana dunia ndio muda sahihi wa kujifunza kwa sababu unakuwa ni mshamba sana kwenye baadhi ya maisha ya watu fulani. Hakuna mtu amewahi kulijua jambo hili kwamba mimi sio mtanzania wewe ndiye binadamu wa Kwanza kabisa ndiyo maana nilitaka nikutane nawewe mapema(aliguna kidogo) mimi kukamatwa na hao watoto sio kwamba walivyo nifuata walikuwa na uwezo wa kunikamata, hapana ile sindano na sumu ambayo walinichoma kwangu huwa hazifanyi kazi ila nilijifanya tu kudondoka ili nikutane nawewe.

Wale ni watoto wadogo sana ambao ningewaua kwa sekunde kadhaa tu, huyo mtu ambaye unamtafuta wewe nimetumia sio chini ya miaka minne kuweza kuzipata taarifa zake kwa sababu huwa hazipo na sio kila mtu anaweza kuzipata ndio maana mpaka leo hujawahi kumpata zaidi ya kubahatika kuipata familia yake napo ni baada ya yule mjinga rafiki yake kumsaliti alifanya kosa kubwa sana yule bwana mdogo usaliti ni kitu kibaya sana" alitulia na kumwangalia Qader ambaye ni dhahiri bado alikuwa na maswali mengi sana na ni kama alikuwa hamuelewi kabisa mtu huyo alishindwa kumsoma kwa namna yoyote ile.

"Miaka mitano iliyopita nilikuwa nimesambaza vijana wangu waweze kumtafuta sehemu yoyote ile ambayo wanaweza kumuona wanipe taarifa, nadhani kijiamini kuliwaponza sana walibahatika kukutana naye mara moja tu na ndicho kilicho nipa uhakika asilimia mia kwamba yupo kwenye nchi hii bahati mbaya sana aliwaua vijana wangu wawili na mmoja alifanikiwa kukimbia baada ya hapo haikuwahi kujulikana tena kuhusu uwepo wake mpaka pale alivyo potea na kuiacha familia yake ambayo wewe ulienda kufanya ujinga na mtu yule huwa hakubali kuacha familia nyuma lazima hapa katikati kuna tatizo ndiyo sababu amepotea kiwepesi namna hii" maneno mengine ni kama yalianza kumfungua kichwa Qader namna mtu huyo alivyo.

"Sasa wewe unasimama kama nani na unafanya kazi na nani kwa manufaa yapi na kwanini?" Maswali yalikuwa ni mengi sana kutoka kwa Qader yalimfanya Jiti acheke sana mpaka akashika mbavu zake kijana aliyekuwa mbele yake alikuwa ana wasiwasi mno.

"Nadhani umesema unanijua sana, mimi ni afisa usalama na ndo kazi yangu kama ulivyosema na nafanya kazi na Mr President"

"Noooooooo, usalama wa taifa na Mr President wapi na wapi?"

"Una kichwa cha hovyo na akili ya kijinga sana mambo huyajui na bado unakuwa na akili ya ubishi sana kiasi hicho sijajua ni kipi kinakupa jeuri hiyo, unajua nini wewe mpaka uwe na huo uwezo wa kunibishia?" Jiti aliongea kwa hasira na kumkazia macho Qader akimpiga piga shavuni ilibidi atulie tu ni wazi alionekana kudandia gari mbele.
"Mimi najulikana kama afisa usalama wa taifa halali wa Tanzania na kwa uadilifu wa kazi yangu ulinipa sana jina mpaka ikafikia sehemu nikaaminiwa na kuitwa na mheshimiwa raisi ambaye alinipa kazi ya kumsaidia kuifanya. Usiku mmoja nikiwa ndani ya nyumba yangu Osterbay nilipokea simu kutoka sehemu ambayo sikuijua kabisa alikuwa ni raisi wa nchi ya Tanzania ilinishtua sana kwa sababu sio kawaida raisi kukupigia simu mtu wa kawaida pasipo na sababu yoyote ya msingi basi ilinibidi nitulize akili vizuri ili nimsikilize kwa umakini

"Naongea na Jiti Maalimu?"
"Ndiyo wewe nani?"
"Alan Mwaiponela"
"You mean Mr President"
"Here you are" nilishtuka sana
"Welcome Mr President"
"I need you this time at the state house" nilikuwa na wasiwasi sana baada ya kuambiwa kwamba ananihitaji Ikulu muda huo nikiwa kwenye mawazo mazito nilisikia mlio wa gari nje ya nyumba yangu nikajua basi nimeisha, nilipanda kwa unyonge sana.

"Welcome Jiti" niliitikia salamu yake kwa kutoa heshima baada ya kuingia ndani ya Ikulu na ndio ilikuwa mara yangu ya Kwanza kupata bahati ta kukaa na raisi Ikulu asikudanganye mtu ile sehemu ni nzuri sana, ni ndoto ya kila mwananchi kuingia pale na ina ulinzi mkali wa kutisha nilijikuta naipenda mno na nilitamani siku moja ningekuwa miongoni mwa watu ambao wangeishi Ikulu bahati mbaya huo uwezo ilikuwa ni kazi sana kuufikia.
"Asante sana mheshimiwa"
"Lazima umeogopa sana raisi kukupigia simu tena usiku huu wa manane"
"Ndiyo mheshimiwa nimeshtuka sana kwa sababu sio rahisi raisi mwenye heshima kama wewe kumpigia simu mtu wa kawaida kama mimi imenitisha" alionekana kutabasamu sana
"Ni miongoni mwa vijana ambao mna mchango mkubwa sana kwenye taifa kwahiyo usijishushe sana chini"
"Lakini sioni kama nastahili heshima ya namna hii asante sana kiongozi"
"Sasa nimekuita hapa leo kwa sababu kuu moja, ufanyaji kazi wako kwa weledi, kujituma na kuwa na nidhamu na kile unacho kifanya ndicho kimefanya bahati hii ikudondokee wewe, i need to work with you (nahitaji kufanya kazi nawewe)" nilihisi sijasikia vizuri nilishangaa kivipi raisi atake kufanya kazi namimi, alitembea kwa mbele kidogo na kuvuta droo moja alitoa faili fulani ambalo lilikuwa na rangi nyeusi.
"Haya mafaili yana kazi tofauti hususani za utunzaji wa nyaraka na taarifa mhimu, yapo ya aina nyingi sana ila ukiona taarifa inatunzwa kwenye faili jeusi basi kuna mawili inawezekana taarifa hizo ni za kitu cha muhimu sana au ni taarifa za mtu mhimu sana. Ni siku kadhaa nyuma hapo nilikuwa natafuta mtu wa kufanya naye kazi ndani ya usalama wa taifa hivyo ilinilazimu niongee na mkurugenzi wa usalama wa taifa kwa sababu yeye ndo anaye wajua vizuri zaidi kuliko mimi, alinipa mafaili ya vijana kumi ambayo baada ya kuyapitia nilivutiwa sana na faili lako unaonekana unafanya kazi kwa weledi sana ndiyo sababu iliyo nifanya nikutafute tuifanye kazi hii" kidogo nilishusha pumzi maana nilihisi huenda nimesha shtukiwa.

"What do you think?(unafikiria nini?)" Hata sikusikia chochote kutokana na swali lake muda huo nilikuwa kwenye mawazo mazito sana nikiwa nakumbuka jinsi nikivyoweza kuingia ndani ya idara ya usalama huo, jina Jiti ni kweli ni jina ambalo alikuwa analitumia kijana mmoja ambaye alikuwa anaitwa Jiti Maalimu huyo kijana alikuwa ni usalama wa taifa muadilifu Saba na alijichukulia unaarufu sana ndani ya idara ya usalama wa taifa kutokana na uadilifu wake mkubwa kwenye kazi na ndiyo maana nilivutiwa naye sana. Nilianza kumfuatilia kwa umakini sana na baada ya muda nikazipata taarifa zake zote hivyo nikawa nahitaji kuichukua ile nafasi yake hiyo ilinilazimu kuyasoma maisha yake tangu anazaliwa mpaka siku hiyo, baada ya kuyajua mambo yote hayo ndipo nilipofanya maamuzi ya kumuua kisha sura yake ikabadilishiwa kwangu mambo ya utandawazi hayo hapo ndipo nilipo anza kuyaishi maisha ya kijana yule.

"Hey i asked what do you think(wewe niliuliza unafikiria nini?)" Sauti yake ndiyo iliyo nikurupua kutoka kwenye hayo mawazo nilishtuka sana.

"Oooh Mr President i accept it and I'm ready to work for you at any cost (ooh mheshimiwa raisi nimeikubali na nipo tayari kuifanya kwa ajili yako kwa gharama yoyote ile)" alitabasamu sana baada ya mimi kumjibu vile basi pale ndipo alipo anza kunipa mipango ya yeye kuzipata hizo taarifa za siri ambazo zilikuwa zinahusisha Zakaria kutafutwa sana alihitaji nichimbe kwa undani ili nijue kama kweli mtu huyu alikuwa ndani ya nchi hii na kama alikuwepo basi alitaka nijue yuko wapi na niitafute historia yake yote ya maisha ya nyuma na hapo ndipo nilipo anza kumjua vizuri Zakaria Mansour ni nani na ndivyo nilivyo ingia kwenye idara ya usalama wa nchi hii japo kuna taarifa siwezi kuzipata kutokana na nafasi ndogo ambayo niliyo nayo huko maana kufanya kazi na raisi imekuwa ni siri nzito sana" alijibu kwa macho makavu akiwa bado anamwangalia kwa umakini sana Qader.

"Then who are you na kwanini unayafanya haya yote? Kwa sababu unaonekana kabisa ulidhamiria kufanya haya ndiyo maana uliua mpaka mtu ili tu upate nafasi ya kuingia huko ndani ya usalama wa taifa" Qader aliuliza kinyonge sana.

"Yes upo sahihi sana, nilipania sana tena sana kuingia huko ili nipate urahisi wa kuzipata taarifa za mtu huyo ukiuliza kwanini swali ni moja na mtu kuniuliza mimi ni nani na kwanini namtafuta sana huyu mtu. Bado ni mapema sana kukutajia jina langu kwa sababu kuna asilimia nyingi kama ukilijua jina langu halisi nitakuua hapa hapa sasa chagua wewe nikutajie jina langu ufe hapa au tuache mambo kama yalivyo nikuache uendelee kula mema ya nchi?" Qader alifikiria sana hilo swali alitikisa kichwa kuonyesha kwamba hakuwa tayari kufa ni bora asilijue tu hilo jina lenyewe.

"Sasa mimi kuna kazi ambazo naenda kuzimalizia kwa sasa na najua una maswali mengi sana kuhusu mimi maana mpaka sasa hakuna chochote unacho kijua kuhusu mimi zaidi tu ya kuona kwamba mimi sio mtanzania na kupata historia fupi namna nilivyoweza kuingia ndani ya usalama wa taifa la Tanzania na kuanza kufanya kazi na mheshimiwa raisi. Najua hapa uliniita ili kupata taarifa za mtu huyo kwa kukusaidia tu familia yake ambayo imebakia inapatikana kwenye kijiji kimoja huko BUKOBA kinaitwa KIBETA panaitwa kwa mzee Philebert, huko ndiko aliko bibi, babu yake pamoja na anko zake na ndugu wengine na hajawahi kabisa kufika huko, unaweza ukawa na maswali mengi kama ni hivyo kwanini ni mtu wa Libya sasa hayo nakuachia mwenyewe utajiongeza.

Sikulazimishi wala sina ushauri wowote ule kwamba uende kufanya lolote huko ila kama unapahitaji basi ndo huko utajua mwenyewe kama utaenda au hautaenda sio biashara yangu kujua hilo. Ila nataka unisikilize vizuri sana na kwa umakini mno, kama unaweza kimbia na uende sehemu ambayo hakuna mtu atajua kuhusu uwepo wako hapa duniani, usitumie simu wala aina yoyote ya mtandao yaani usijulikane tena kama uliwahi kuwepo na ikiwezekana badilisha sura yako asikujue mtu yeyote yule hicho ndicho kinaweza kuifanya familia yako kuwa salama ila vinginevyo utakufa vibaya sana na ubaya wa yule jamaa huwa haachi mtu yaani kosa unafanya wewe ila anahakikisha familia yako yote inalipa hilo na nadhani ana sababu za msingi kufanya hivyo. Hii ni vita ya kisasi na wewe haikuhusu kabisa ni tamaa za pesa tu zinakuingiza huku hiyo itakupelekea upotee ukiwa bado kijana mdogo sana zingatia hilo kabla haujaanza kujuta nimekwambia mwanzo hata familia moja miaka kadhaa nyuma huko waliwahi kufanya mistake ya hivyo maumivu yaliyo tokea hakuna mwanadamu ambaye angeweza kuvumilia kuyaona kwa macho yake" Jiti aliitazama saa yake kwa umakini na kutoka nje alikuwa anaondoka hilo eneo kama ni kwake vile, aliletwa kama mateka ila aliondoka huru tena bila kuruhusiwa na mtu.

Qader hata hakushtuka wakati mwanaume huyo anaondoka kwenye kichwa chake ni mambo mengi sana yalikuwa yanamzunguka hakuelewa chochote kwani alihisi kama kichwa kinataka kupasuka alikaa chini na kulala huenda akili yake ingekaa sawa akiamka.

Bado hatujamjua Jiti ni nani anaonekana kuwa mtu wa kutisha sana, ipi sababu ya kumsaka sana Zakaria? Bado sana mchezo ndo Kwanza unaanza ebu twende sawa mpaka mwisho.

Langu jina naitwa

Bux the story teller
STORY: GEREZA LA HAZWA
STORY WRITER: FEBIANI BABUYA
STORY TELLER: Bux the story teller
AGE: 18+

UKURASA WA ISHIRINI NA NNE

TULIPO ISHIA UKURASA WA ISHIRINI NA TATU
Qader hata hakushtuka wakati mwanaume huyo anaondoka kwenye kichwa chake ni mambo mengi sana yalikuwa yanamzunguka hakuelewa chochote kwani alihisi kama kichwa kinataka kupasuka alikaa chini na kulala huenda akili yake ingekaa sawa akiamka.

ENDELEA.........................

TUNAENDELEA NA SIMULIZI YA GEREZANI
Aariz alitoka ndani ya hiyo nyumba yasiri kinyonge sana alinyong'onyea mno hakuelewa nini kilikuwa kinaendelea kwenye maisha yake Kila akimaliza mtihani huu basi ilikuwa ni lazima akutane na mtihani mwingine mpaka muda huo hakuijua kabisa historia ya maisha yake na hakuwahi kuulizia hata siku moja. Kulikuwa kunakaribia kupambazuka aliingia ndani kwake akiwa Hana amani hakutaka mkewe amshtukie kwamba hakuwepo humo ndani hivyo alipitiliza moja kwa moja kwenye chumba cha mazoezi ambacho ilikuwa kawaida yake kwenda kila asubuhi. Mkewe alikurupuka kutoka usingizini aliangalia pembeni hakumuona mumewe zaidi ya mtoto ambaye alikuwa bado amelala, alichanua tabasamu lake uso mzuri sana wenye nuru angavu ulionekana alifanya hivyo mwa sababu alikuwa anajua sehemu ya kumpata pale anapo mkosa kwenye kitanda, alinyoosha moja kwa moja mpaka kwnye chumba cha mazoezi huko alimkuta mwanaume akiwa kifua wazi anaruka kamba alikuwa na mwili wa kuvutia sana mwanamke huyo alimziba macho kwa nyuma, aligeuzwa na kudakwa akapigwa busu moja safi sana walipendana mno.

Hakukaa hapo alitoka kwenda kuandaa kifungua kinywa, Aariz alimwangalia mpaka anaishia ilimuuma sana huyo mwanamke alikuwa anamjali mno hakustahili kuweza kuyaishi hayo maisha yalikuwa yanasikitisha sana. Mchana wa jua kali Aariz alikuwa ndani ya chumba chake cha siri hiki kililkuwa chini ya gym ambayo alikuwa anafanyia mazoezi, chini ya chuma kimoja kizito sana ndipo paliluwa na mlango was siri wa kuweza kuingilia hapo chini. Kwenye dashboard yake ndogo ambayo Mara nyingi huwa anaitumia kuandikia mambo yake alikuwa ameibandika sura kubwa ya mtu ambaye alihitaji kwenda kumfanyia kazi haraka sana kwa sababu alionekana kuwa mtu hatari mno kwa upande wa nchi yao.

"Inawezekana vipi huyu mtu azaliwe Dakar na ni mwarabu kabisa kimwonekano nadhani kutakuwa na sababu ya msingi hapa" aliongea pekeake huki akiwaza sana ila alikosa jibu akaichukua simu yake na kuipiga mahali.

"Mzee nina swali kidogo hapa"
"Nakusikiliza"
"Huyu mtu mmesema asili yake ni Dakar Senegal sasa mbona ni mwarabu kabisa huyu kivipi mtu wa hivi atokee Senegal?
"Mhhhh hata mimi niliwahi kujiuliza sana hilo swali nilifuatilia sana ila nilikuja kuambiwa mambo yapo kama yalivyo basi nikaacha"
"Nani ambaye alikujibu hivyo"
"Wakubwa kazini"
"Ok silaha zangu ziko wapi?"
"Visu vyako viwili nadhani vililipuka na gari ila ule upanga upo chini ya kile kitanda ambacho ulikuwa umelazwa" simu ikakatwa, aliwaza sana mwanaume hakupata jibu kesho yake alitakiwa kuwepo eneo la tukio aliwaza namna ya kumuaga mkewe kwa mara nyingine lakini alifanikiwa kwa kisingizio cha biashara.

BENGHAZI RUMIO STREET HOUSE NO 734
Kwenye moja ya mtaa maarufu sana kwenye sehemu hiyo ambayo walikuwa wanaishi watu wenye ukwasi ulio pindukia ndipo alipokuwa ameshuka kwenye tax Aariz, alishuka na kuvua miwani yake alisimama na kuangaza akiwa kama vile anaufurahia uzuri wa jiji hilo la kitajiri ndani ya nchi ya Libya, kwa mbali ghorofa moja kubwa sana lililokuwa na maandishi makubwa lenye namba 734 palikuwa na maandishi makubwa sana ambayo yalisomeka kama MBAYE TRANSPORTATION, alitabasamu hilo ndilo lilikuwa lengo lake kubwa sana la kwenda kwenye ule mji. Akiwa na begi lake mkononi na suti ya bei ghali mno alinyoosha mpaka ng'ambo ya pili ambapo aliiona ile ghorofa na kutokezea mpaka mapokezi, alipokelewa kwa heshima kutokana na nguo ambazo alikuwa amezivaa.

"Hello bosi nikusaidie nini" ni sauti nzuri ya mrembo mmoja ambaye alikuwa amejisitiri sana juu mpaka chini ila bado urembo wake ulijidhihirisha wazi, Aariz alitabasamu.

"Ok Mimi ni mgeni hapa na nimevutiwa sana na kampuni yenu nadhani nahitaji kuonana na mmiliki wa kampuni kwa sababu nimetoka mbali sana nimechoka nahitaji kupumzika ila nadhani nikikutana naye kwanza litakuwa jambo la mhimu zaidi" Aariz alikuwa anaongea huku anashangaa sana mandhari kuonyesba mwamba alikuwa mgeni sana hiyo sehemu, mwanamke yule alimwangalia kwa umakini sana.

"Mhhhhhhh una ahadi naye" yule dada alimjibu akiwa amemkazia macho yake.

"Nadhani nimekwambia mimi ni mgeni sana hapa namaanisha hata simjui ila ni mhimu sana" alimjibu akiwa hana hata wasi wasi

"Samahani sana mmiliki wa hii kampuni hata mimi simjui huwa sio mtu wa kuonekana sana japo anasaidia sana watu cha kukusaidia nakukutanisha na mtendaji mkuu yeye atakusaidia na anaweza akakupa maelekezo namna ya kumpata" aliongea mwanamke huyo huku akiinyanyua simu yake ambayo aliipiga mahali baada ya dakika moja akamkabidhi Aariz kikadi kidogo mkononi ambacho kilikuwa na maelezo ya chumba kipi ambacho alikuwa anatakiwa kwenda, alipanda kwenye lifti na kupanda mpaka ofsi namba 107 humo ndimo alitakiwa kuingia, alivyofika mapokezi kwenye ofisi hilo la kifahari alikutana na mwanamke mwingine ambaye alimsalimia kwa heshima sana na kumuongoza ndani kwani taarifa yake ilikuwa imefika mapema

Ndani ya chumba ambacho mezani paliandikwa kwa maandishi makubwa kabisa TARIQ AMADOU MBAYE palimvutia sana Aariz ambaye baada ya kusoma alihisi huenda huyo kijana ni mmoja kati ya watoto wa tajiri huyo alifurahi sana kazi yake ilikuwa inaenda kuwa nyepesi sana ila alivyo yainua macho yake alishangaa alikuwa ni kijana mdogo sana hakuelewa ni kivipi anaweza kuongoza kampuni kubwa namna hiyo basi mpaka hapo aligundua huyu ni mtoto wa mhimu sana kwenye familia hiyo.

"Welcome Mr Josephat nadhani nimetambulishwa hivyo wakati napigiwa simu kutoka mapokezi" mwanaume huyo alimjibu hivyo akiwa anampa mkono Aariz waweza kumwita Josephat kwa sasa.

"Yes uko sahihi kabisa hilo ni jina langu, sasa nisizunguke sana niende moja kwa moja kwenye point ya msingi sana. Naitwa Mr Josephat ni mfanyabiashara wa madini kutoka ndani ya nchi ya Afrika ya Kusini kampuni yangu inaitwa Josephat mining company (JMC) nafanya biashara ya kusambaza dhahabu ndani ya nchi zote za ulimwengu mpaka kwenye visiwa pamoja na kuuza vito vya thamani, sasa kwenye kuuza kwangu hivyo vitu nikiwa kwenye safari yangu ya kwenda Marekani nilipita hapa Libya katika jiji la Tripoli kupitisha dhahabu nikawa nimevutiwa sana na kampuni yenu baada ya kuifuatilia na kugundua ni wasambazaji na wanunuzi wakubwa sana wa mafuta(alimeza mate). Kupitia kufuatilia biashara yenu nimegundua ni watu wenye soko kubwa sana ndani ya magharibi mwa Afrika, sasa kupitia kampuni yangu nahitaji tuingie ubia ili niwe nawasambazia ndani ya nchi zote zilizopo Kusini mwa jangwa la sahara na natumia pesa zangu mwenyewe halafu faida tunagawana ila kikubwa nahitaji tu mzigo wa kutosha na kila pesa inayo ingia kampuni yako inachukua asilimia 50 zinazobakia 50 ni zangu nadhani itakuwa ni biashara kubwa Sana na nitawasaidia pia kurahisisha upatikanaji wa dhahabu pamoja na utengenezaji wa vitu vya thamani kwenye kampuni yenu kuwa rahisi kwa kuwauzia madini kwa bei ya kawaida tofauti na ninavyo yauza kwa nchi zingine" ni mpango mzito wa kibiashara ambao mwanaume alituliza kichwa chake akauandaa ili aweze kukubaliwa na kupewa nafasi kwenye hiyo kampuni hakuona namna nyingine ya kupata ukaribu na watu hao zaidi ya kutoa ofa kunwa na kutumia pesa ambazo zingewasaodia kampuni hiyo kupata pesa nyingi ili wakubali kufanya naye kazi.

TARIQ kama alivyojulikana kwa jina lake aliinamia chini aliwaza sana ilikuwa imepita miaka kumi sasa walikuwa wanahangaika sana kutafuta namna ya kupenya kwenye masoko ya nchi ya kusini mwa Afrika kwa sababu wao walikuwa kaskazini ila biashara yao kubwa ilikuwa magharibi mwa Afrika, mwanaume aliyekuwa mbele yake alikuja na wazo kubwa sana ambalo amekuwa akilihangaikia kwa muda mrefu sana, ni kama alipata pumzuliko la akili bwana mdogo huyu mdogo alitabasamu na kuinua uso wake.

"Kama tukikubali unawekeza pesa kiasi gani ili nione kama tunaweza kufanya biashara au haiwezekani" aliongea akiwa amemkazia macho Mr Josephat ambaye alikuwa anaendelea kupata kahawa akimsubiri bwana mdogo aingie kwenye kumi na nane zake.

"Cash hapa kwenye begi kuna dola za kimarekani milioni 15 ambazo ni zaidi ya bilioni 30 na zaidi" kauli yake ambayo haikuwa na kitetemeshi ilifuatiwa na kulifungua begi lake bila wasiwasi, TARIQ aliliangalia begi hilo na kutabasamu.

"Ok i accept the deal lets do it" alitamka huku akitoka humo ndani, pesa zilikuwa ni nyingi mno asingeweza kuzikataa kiwepesi namna hiyo baada ya kutoka alimuacha mwanaume pekeyake akiwa ndani anaangaza macho huku na huku akiingalia ofisi hiyo kila kona hakuona kamera yoyote alitabasamu na kujiongelesha mwenyewe.

"Umejiingiza sehemu mbaya sana Tariq you are all dead" alitamka kwa msisitizo wakati huo TARIQ alirudi akiwa na makablasha mkononi ilikuwa ni mikataba ya kibiashara lakini pia aliongozana na mzee mmoja ambaye alikuwa ana mkoba mkononi.

"Huyu ni mwanasheria wa kampuni yetu nimemuita hapa ili tusaini rasmi mkataba na uwe mmoja wa kampuni yetu karibu sana Mr Josephat" ndio ubaya wa pesa unaweza ukakufanya akawaamini hata ambao unatakiwa kukaa nao mbali, kuona zile bilioni zaidi ya 30 zilimchanganya sana TARIQ alizitamani mno zile pesa ndio maana alihitaji mkataba usainiwe haraka haraka, Aariz hakuwa na papara alichukua kipande cha mkataba ule na kukisoma kwa dakika tano alikishusha chini akiwa na kalamu yake ya wino mkononi, akiiñama ili asaini lakini ni kama alighairi akainuka na kumuangalia TARIQ.

"Nimekubaliana na kila kitu kilichopo kwenye mkataba lakini nilihitaji kusaini mkataba mbele ya mmiliki wa kampuni hii kwa sababu ni muda mrefu huwa natamani sana kukutana naye nimfahamu pia kwa sababu ni mfanya biashara mkubwa sana na pia ni mtu anaye jitoa sana kwa watu nadhani kuna jambo kubwa tunaweza kulifanya pamoja nje ya biashara" aliongea kirahisi sana ila ni jambo ambalo liliwashtua wote hao wawili mwanasheria na TARIQ mwenyewe haikuwa kawaida mtu kuanza kumuulizia bosi.

"Unamaanisha unataka kuongea na baba?"

"Yes au mteja mkubwa ambaye nataka kuwekeza mabilioni kama mimi siruhusiwi kuonana na bosi wa kampuni endapo kuna vitu nataka kuongea naye yeye mwenyewe?"

"No sijamqanisha hivyo, ngoja nimpigie simu niangalie kama inawezekana kwa sababu huwa ni ngumu sana yeye kuja"

"Kwanini hawezi kuja kwenye kampuni yake mwenyewe?" Swali lake lilipuuziwa TARIQ aliinyanyua simu yake na kupiga mahali zilipita sekunde thelathini ilipokelewa.

"Nahitaji kuongea na baba ni mhimu sana" aliongea bila hata salamu ilionekana upande wa pili alipokea msaidizi.

"Baba Kuna dili kubwa sana la mabilioni ya fedha nahitaji kusaini na mfanya biashara mmoja kutoka kusini mwa Afrika lakini anahitaji akujue tu kwa sura ndo asaini kwa sababu anadai kwamba amekuwa akikuangalia kama mfano wake kwenye biashara zako Kuna vitu vingi anajifunza kwako na ulivyo na moyo wa kutoa kwa jamii hivyo anatamani sana akuone"

"Ndiyo"
"Ok sawa" simu ilikatwa haikueleweka upande wa pili mtu huyo alitamka nini, TARIQ alihema kwa nguvu.
"Amekubali hivyo Kesho asubuhi na mapema atakuwepo hapa naomba uwahi na tunakutafutia hoteli wenyewe kwa gharama zetu karibu sana ndani ya jiji la BENGHAZI" TARIQ aliongea kwa furaha wakipeana mikono na Mr Josephat, ilipigwa simu chini kabisa uliandaliwa usafiri kwa ajili ya kumpeleka Mr Josephat hotelini na hakukataa ofa hiyo hakutaka kumkwanza mwenyeji wake mwanaume alikuja kuchukuliwa na wafanyakazi akiahidi kurudi Kesho asubuhi na mapema, akiwa njiani kwenye lifti aliweka kiearphone chake kimoja cha kisasa kwenye sikio lake la kulia kilichokuwa kama pambo kisha akabonyeza kwenye batani ndogo kwenye saa yake.

"Bosi mbona kirahisi sana umekubali biashara hii bila hata kumjua kiundani mtu huyu?" Lilikuwa swali la mwanasheria kwenda kwa kijana TARIQ.

"I want to teach this idiot, this is BENGHAZI my city hahahaha, Mr Leone this is how i do business, huyu hakuna kitu atapata na nadhani leo ni siku yake ya mwisho kwenye hiyo hoteli ambayo wanampeleka usiku Kuna watu wanaenda na kuondoka na kila akicho nacho na hakuna mkataba unasainiwa" TARIQ aliongea kwa majigambo.

"Then after that? What follows?" You mean you want to killl him this night?" Aliuliza Mr Leone ambaye alikuwa ni mwanasheria wa kampuni hiyo.

"Nadhani umenielewa vizuri Mr Leone" aliongea kwa majigambo hakujua kama kila anacho kiongea ndani ya hiyo ofisi yake kilikuwa kinasikika ndani ya masikio ya mwanaume ambaye alikuwa anajulikana kama Josephat, alisikitika sana na kumsikitikia kijana huyo alikuwa amefanya moja ya makosa ambayo ilikuwa ni ngumu sana kusameheka. Alikumbuka vyema wakati TARIQ ameenda kumuita mwanasheria wa kampuni alichunguza kwa umakini sana kwenye ofisi hiyo hakuona kamera yoyote kuna kifaa kidogo mithili ya kiwaya ambacho alikibandika chini ya meza ya TARIQ hivyo alikuwa akisikia kila kilichokuwa kinaendelea humo ndani, walikuwa wamefika chini alitabasamu na kuingia kwenye gari safari ya kwenda hotelini ilianza.

Hii michezo wanaiweza wenye akili kubwa tu, cheza nikuchezee rasmi mwanaume ameanza kujiingiza kwenye mchezo ambao ulimfanya akaishia sehemu mbaya sana kwenye maisha yake, anaenda kuipoteza familia yake na kuishi kwa majuto mno, umoja ya nchi za magharibi unaenda kumsakama kwa gharama yoyote ikiwemo na nchi yake kivipi wakati ndio walio mtuma? Ngoja tuone Mr Josephat ni kosa gani kubwa anaenda kulifanya linalo mpekelea kote huko kwenye hii safari yake.

24 sina la nyongeza tena

Langu jina naitwa

Bux the story teller

Chao
 
STORY: GEREZA LA HAZWA
STORY WRITER: FEBIANI BABUYA
STORY TELLER: Bux the story teller
AGE: 18+

UKURASA WA ISHIRINI NA NNE

TULIPO ISHIA UKURASA WA ISHIRINI NA TATU
Qader hata hakushtuka wakati mwanaume huyo anaondoka kwenye kichwa chake ni mambo mengi sana yalikuwa yanamzunguka hakuelewa chochote kwani alihisi kama kichwa kinataka kupasuka alikaa chini na kulala huenda akili yake ingekaa sawa akiamka.

ENDELEA.........................

TUNAENDELEA NA SIMULIZI YA GEREZANI
Aariz alitoka ndani ya hiyo nyumba yasiri kinyonge sana alinyong'onyea mno hakuelewa nini kilikuwa kinaendelea kwenye maisha yake Kila akimaliza mtihani huu basi ilikuwa ni lazima akutane na mtihani mwingine mpaka muda huo hakuijua kabisa historia ya maisha yake na hakuwahi kuulizia hata siku moja. Kulikuwa kunakaribia kupambazuka aliingia ndani kwake akiwa Hana amani hakutaka mkewe amshtukie kwamba hakuwepo humo ndani hivyo alipitiliza moja kwa moja kwenye chumba cha mazoezi ambacho ilikuwa kawaida yake kwenda kila asubuhi. Mkewe alikurupuka kutoka usingizini aliangalia pembeni hakumuona mumewe zaidi ya mtoto ambaye alikuwa bado amelala, alichanua tabasamu lake uso mzuri sana wenye nuru angavu ulionekana alifanya hivyo mwa sababu alikuwa anajua sehemu ya kumpata pale anapo mkosa kwenye kitanda, alinyoosha moja kwa moja mpaka kwnye chumba cha mazoezi huko alimkuta mwanaume akiwa kifua wazi anaruka kamba alikuwa na mwili wa kuvutia sana mwanamke huyo alimziba macho kwa nyuma, aligeuzwa na kudakwa akapigwa busu moja safi sana walipendana mno.

Hakukaa hapo alitoka kwenda kuandaa kifungua kinywa, Aariz alimwangalia mpaka anaishia ilimuuma sana huyo mwanamke alikuwa anamjali mno hakustahili kuweza kuyaishi hayo maisha yalikuwa yanasikitisha sana. Mchana wa jua kali Aariz alikuwa ndani ya chumba chake cha siri hiki kililkuwa chini ya gym ambayo alikuwa anafanyia mazoezi, chini ya chuma kimoja kizito sana ndipo paliluwa na mlango was siri wa kuweza kuingilia hapo chini. Kwenye dashboard yake ndogo ambayo Mara nyingi huwa anaitumia kuandikia mambo yake alikuwa ameibandika sura kubwa ya mtu ambaye alihitaji kwenda kumfanyia kazi haraka sana kwa sababu alionekana kuwa mtu hatari mno kwa upande wa nchi yao.

"Inawezekana vipi huyu mtu azaliwe Dakar na ni mwarabu kabisa kimwonekano nadhani kutakuwa na sababu ya msingi hapa" aliongea pekeake huki akiwaza sana ila alikosa jibu akaichukua simu yake na kuipiga mahali.

"Mzee nina swali kidogo hapa"
"Nakusikiliza"
"Huyu mtu mmesema asili yake ni Dakar Senegal sasa mbona ni mwarabu kabisa huyu kivipi mtu wa hivi atokee Senegal?
"Mhhhh hata mimi niliwahi kujiuliza sana hilo swali nilifuatilia sana ila nilikuja kuambiwa mambo yapo kama yalivyo basi nikaacha"
"Nani ambaye alikujibu hivyo"
"Wakubwa kazini"
"Ok silaha zangu ziko wapi?"
"Visu vyako viwili nadhani vililipuka na gari ila ule upanga upo chini ya kile kitanda ambacho ulikuwa umelazwa" simu ikakatwa, aliwaza sana mwanaume hakupata jibu kesho yake alitakiwa kuwepo eneo la tukio aliwaza namna ya kumuaga mkewe kwa mara nyingine lakini alifanikiwa kwa kisingizio cha biashara.

BENGHAZI RUMIO STREET HOUSE NO 734
Kwenye moja ya mtaa maarufu sana kwenye sehemu hiyo ambayo walikuwa wanaishi watu wenye ukwasi ulio pindukia ndipo alipokuwa ameshuka kwenye tax Aariz, alishuka na kuvua miwani yake alisimama na kuangaza akiwa kama vile anaufurahia uzuri wa jiji hilo la kitajiri ndani ya nchi ya Libya, kwa mbali ghorofa moja kubwa sana lililokuwa na maandishi makubwa lenye namba 734 palikuwa na maandishi makubwa sana ambayo yalisomeka kama MBAYE TRANSPORTATION, alitabasamu hilo ndilo lilikuwa lengo lake kubwa sana la kwenda kwenye ule mji. Akiwa na begi lake mkononi na suti ya bei ghali mno alinyoosha mpaka ng'ambo ya pili ambapo aliiona ile ghorofa na kutokezea mpaka mapokezi, alipokelewa kwa heshima kutokana na nguo ambazo alikuwa amezivaa.

"Hello bosi nikusaidie nini" ni sauti nzuri ya mrembo mmoja ambaye alikuwa amejisitiri sana juu mpaka chini ila bado urembo wake ulijidhihirisha wazi, Aariz alitabasamu.

"Ok Mimi ni mgeni hapa na nimevutiwa sana na kampuni yenu nadhani nahitaji kuonana na mmiliki wa kampuni kwa sababu nimetoka mbali sana nimechoka nahitaji kupumzika ila nadhani nikikutana naye kwanza litakuwa jambo la mhimu zaidi" Aariz alikuwa anaongea huku anashangaa sana mandhari kuonyesba mwamba alikuwa mgeni sana hiyo sehemu, mwanamke yule alimwangalia kwa umakini sana.

"Mhhhhhhh una ahadi naye" yule dada alimjibu akiwa amemkazia macho yake.

"Nadhani nimekwambia mimi ni mgeni sana hapa namaanisha hata simjui ila ni mhimu sana" alimjibu akiwa hana hata wasi wasi

"Samahani sana mmiliki wa hii kampuni hata mimi simjui huwa sio mtu wa kuonekana sana japo anasaidia sana watu cha kukusaidia nakukutanisha na mtendaji mkuu yeye atakusaidia na anaweza akakupa maelekezo namna ya kumpata" aliongea mwanamke huyo huku akiinyanyua simu yake ambayo aliipiga mahali baada ya dakika moja akamkabidhi Aariz kikadi kidogo mkononi ambacho kilikuwa na maelezo ya chumba kipi ambacho alikuwa anatakiwa kwenda, alipanda kwenye lifti na kupanda mpaka ofsi namba 107 humo ndimo alitakiwa kuingia, alivyofika mapokezi kwenye ofisi hilo la kifahari alikutana na mwanamke mwingine ambaye alimsalimia kwa heshima sana na kumuongoza ndani kwani taarifa yake ilikuwa imefika mapema

Ndani ya chumba ambacho mezani paliandikwa kwa maandishi makubwa kabisa TARIQ AMADOU MBAYE palimvutia sana Aariz ambaye baada ya kusoma alihisi huenda huyo kijana ni mmoja kati ya watoto wa tajiri huyo alifurahi sana kazi yake ilikuwa inaenda kuwa nyepesi sana ila alivyo yainua macho yake alishangaa alikuwa ni kijana mdogo sana hakuelewa ni kivipi anaweza kuongoza kampuni kubwa namna hiyo basi mpaka hapo aligundua huyu ni mtoto wa mhimu sana kwenye familia hiyo.

"Welcome Mr Josephat nadhani nimetambulishwa hivyo wakati napigiwa simu kutoka mapokezi" mwanaume huyo alimjibu hivyo akiwa anampa mkono Aariz waweza kumwita Josephat kwa sasa.

"Yes uko sahihi kabisa hilo ni jina langu, sasa nisizunguke sana niende moja kwa moja kwenye point ya msingi sana. Naitwa Mr Josephat ni mfanyabiashara wa madini kutoka ndani ya nchi ya Afrika ya Kusini kampuni yangu inaitwa Josephat mining company (JMC) nafanya biashara ya kusambaza dhahabu ndani ya nchi zote za ulimwengu mpaka kwenye visiwa pamoja na kuuza vito vya thamani, sasa kwenye kuuza kwangu hivyo vitu nikiwa kwenye safari yangu ya kwenda Marekani nilipita hapa Libya katika jiji la Tripoli kupitisha dhahabu nikawa nimevutiwa sana na kampuni yenu baada ya kuifuatilia na kugundua ni wasambazaji na wanunuzi wakubwa sana wa mafuta(alimeza mate). Kupitia kufuatilia biashara yenu nimegundua ni watu wenye soko kubwa sana ndani ya magharibi mwa Afrika, sasa kupitia kampuni yangu nahitaji tuingie ubia ili niwe nawasambazia ndani ya nchi zote zilizopo Kusini mwa jangwa la sahara na natumia pesa zangu mwenyewe halafu faida tunagawana ila kikubwa nahitaji tu mzigo wa kutosha na kila pesa inayo ingia kampuni yako inachukua asilimia 50 zinazobakia 50 ni zangu nadhani itakuwa ni biashara kubwa Sana na nitawasaidia pia kurahisisha upatikanaji wa dhahabu pamoja na utengenezaji wa vitu vya thamani kwenye kampuni yenu kuwa rahisi kwa kuwauzia madini kwa bei ya kawaida tofauti na ninavyo yauza kwa nchi zingine" ni mpango mzito wa kibiashara ambao mwanaume alituliza kichwa chake akauandaa ili aweze kukubaliwa na kupewa nafasi kwenye hiyo kampuni hakuona namna nyingine ya kupata ukaribu na watu hao zaidi ya kutoa ofa kunwa na kutumia pesa ambazo zingewasaodia kampuni hiyo kupata pesa nyingi ili wakubali kufanya naye kazi.

TARIQ kama alivyojulikana kwa jina lake aliinamia chini aliwaza sana ilikuwa imepita miaka kumi sasa walikuwa wanahangaika sana kutafuta namna ya kupenya kwenye masoko ya nchi ya kusini mwa Afrika kwa sababu wao walikuwa kaskazini ila biashara yao kubwa ilikuwa magharibi mwa Afrika, mwanaume aliyekuwa mbele yake alikuja na wazo kubwa sana ambalo amekuwa akilihangaikia kwa muda mrefu sana, ni kama alipata pumzuliko la akili bwana mdogo huyu mdogo alitabasamu na kuinua uso wake.

"Kama tukikubali unawekeza pesa kiasi gani ili nione kama tunaweza kufanya biashara au haiwezekani" aliongea akiwa amemkazia macho Mr Josephat ambaye alikuwa anaendelea kupata kahawa akimsubiri bwana mdogo aingie kwenye kumi na nane zake.

"Cash hapa kwenye begi kuna dola za kimarekani milioni 15 ambazo ni zaidi ya bilioni 30 na zaidi" kauli yake ambayo haikuwa na kitetemeshi ilifuatiwa na kulifungua begi lake bila wasiwasi, TARIQ aliliangalia begi hilo na kutabasamu.

"Ok i accept the deal lets do it" alitamka huku akitoka humo ndani, pesa zilikuwa ni nyingi mno asingeweza kuzikataa kiwepesi namna hiyo baada ya kutoka alimuacha mwanaume pekeyake akiwa ndani anaangaza macho huku na huku akiingalia ofisi hiyo kila kona hakuona kamera yoyote alitabasamu na kujiongelesha mwenyewe.

"Umejiingiza sehemu mbaya sana Tariq you are all dead" alitamka kwa msisitizo wakati huo TARIQ alirudi akiwa na makablasha mkononi ilikuwa ni mikataba ya kibiashara lakini pia aliongozana na mzee mmoja ambaye alikuwa ana mkoba mkononi.

"Huyu ni mwanasheria wa kampuni yetu nimemuita hapa ili tusaini rasmi mkataba na uwe mmoja wa kampuni yetu karibu sana Mr Josephat" ndio ubaya wa pesa unaweza ukakufanya akawaamini hata ambao unatakiwa kukaa nao mbali, kuona zile bilioni zaidi ya 30 zilimchanganya sana TARIQ alizitamani mno zile pesa ndio maana alihitaji mkataba usainiwe haraka haraka, Aariz hakuwa na papara alichukua kipande cha mkataba ule na kukisoma kwa dakika tano alikishusha chini akiwa na kalamu yake ya wino mkononi, akiiñama ili asaini lakini ni kama alighairi akainuka na kumuangalia TARIQ.

"Nimekubaliana na kila kitu kilichopo kwenye mkataba lakini nilihitaji kusaini mkataba mbele ya mmiliki wa kampuni hii kwa sababu ni muda mrefu huwa natamani sana kukutana naye nimfahamu pia kwa sababu ni mfanya biashara mkubwa sana na pia ni mtu anaye jitoa sana kwa watu nadhani kuna jambo kubwa tunaweza kulifanya pamoja nje ya biashara" aliongea kirahisi sana ila ni jambo ambalo liliwashtua wote hao wawili mwanasheria na TARIQ mwenyewe haikuwa kawaida mtu kuanza kumuulizia bosi.

"Unamaanisha unataka kuongea na baba?"

"Yes au mteja mkubwa ambaye nataka kuwekeza mabilioni kama mimi siruhusiwi kuonana na bosi wa kampuni endapo kuna vitu nataka kuongea naye yeye mwenyewe?"

"No sijamqanisha hivyo, ngoja nimpigie simu niangalie kama inawezekana kwa sababu huwa ni ngumu sana yeye kuja"

"Kwanini hawezi kuja kwenye kampuni yake mwenyewe?" Swali lake lilipuuziwa TARIQ aliinyanyua simu yake na kupiga mahali zilipita sekunde thelathini ilipokelewa.

"Nahitaji kuongea na baba ni mhimu sana" aliongea bila hata salamu ilionekana upande wa pili alipokea msaidizi.

"Baba Kuna dili kubwa sana la mabilioni ya fedha nahitaji kusaini na mfanya biashara mmoja kutoka kusini mwa Afrika lakini anahitaji akujue tu kwa sura ndo asaini kwa sababu anadai kwamba amekuwa akikuangalia kama mfano wake kwenye biashara zako Kuna vitu vingi anajifunza kwako na ulivyo na moyo wa kutoa kwa jamii hivyo anatamani sana akuone"

"Ndiyo"
"Ok sawa" simu ilikatwa haikueleweka upande wa pili mtu huyo alitamka nini, TARIQ alihema kwa nguvu.
"Amekubali hivyo Kesho asubuhi na mapema atakuwepo hapa naomba uwahi na tunakutafutia hoteli wenyewe kwa gharama zetu karibu sana ndani ya jiji la BENGHAZI" TARIQ aliongea kwa furaha wakipeana mikono na Mr Josephat, ilipigwa simu chini kabisa uliandaliwa usafiri kwa ajili ya kumpeleka Mr Josephat hotelini na hakukataa ofa hiyo hakutaka kumkwanza mwenyeji wake mwanaume alikuja kuchukuliwa na wafanyakazi akiahidi kurudi Kesho asubuhi na mapema, akiwa njiani kwenye lifti aliweka kiearphone chake kimoja cha kisasa kwenye sikio lake la kulia kilichokuwa kama pambo kisha akabonyeza kwenye batani ndogo kwenye saa yake.

"Bosi mbona kirahisi sana umekubali biashara hii bila hata kumjua kiundani mtu huyu?" Lilikuwa swali la mwanasheria kwenda kwa kijana TARIQ.

"I want to teach this idiot, this is BENGHAZI my city hahahaha, Mr Leone this is how i do business, huyu hakuna kitu atapata na nadhani leo ni siku yake ya mwisho kwenye hiyo hoteli ambayo wanampeleka usiku Kuna watu wanaenda na kuondoka na kila akicho nacho na hakuna mkataba unasainiwa" TARIQ aliongea kwa majigambo.

"Then after that? What follows?" You mean you want to killl him this night?" Aliuliza Mr Leone ambaye alikuwa ni mwanasheria wa kampuni hiyo.

"Nadhani umenielewa vizuri Mr Leone" aliongea kwa majigambo hakujua kama kila anacho kiongea ndani ya hiyo ofisi yake kilikuwa kinasikika ndani ya masikio ya mwanaume ambaye alikuwa anajulikana kama Josephat, alisikitika sana na kumsikitikia kijana huyo alikuwa amefanya moja ya makosa ambayo ilikuwa ni ngumu sana kusameheka. Alikumbuka vyema wakati TARIQ ameenda kumuita mwanasheria wa kampuni alichunguza kwa umakini sana kwenye ofisi hiyo hakuona kamera yoyote kuna kifaa kidogo mithili ya kiwaya ambacho alikibandika chini ya meza ya TARIQ hivyo alikuwa akisikia kila kilichokuwa kinaendelea humo ndani, walikuwa wamefika chini alitabasamu na kuingia kwenye gari safari ya kwenda hotelini ilianza.

Hii michezo wanaiweza wenye akili kubwa tu, cheza nikuchezee rasmi mwanaume ameanza kujiingiza kwenye mchezo ambao ulimfanya akaishia sehemu mbaya sana kwenye maisha yake, anaenda kuipoteza familia yake na kuishi kwa majuto mno, umoja ya nchi za magharibi unaenda kumsakama kwa gharama yoyote ikiwemo na nchi yake kivipi wakati ndio walio mtuma? Ngoja tuone Mr Josephat ni kosa gani kubwa anaenda kulifanya linalo mpekelea kote huko kwenye hii safari yake.

24 sina la nyongeza tena

Langu jina naitwa

Bux the story teller

Chao
STORY: GEREZA LA HAZWA
STORY WRITER: FEBIANI BABUYA
STORY TELLER: Bux the story teller
AGE: 18+

UKURASA WA ISHIRINI NA TANO

TULIPO ISHIA UKURASA WA ISHIRINI NA NNE
"Nadhani umenielewa vizuri Mr Leone" aliongea kwa majigambo hakujua kama kila anacho kiongea ndani ya hiyo ofisi yake kilikuwa kinasikika ndani ya masikio ya mwanaume ambaye alikuwa anajulikana kama Josephat, alisikitika sana na kumsikitikia kijana huyo alikuwa amefanya moja ya makosa ambayo ilikuwa ni ngumu sana kusameheka. Alikumbuka vyema wakati TARIQ ameenda kumuita mwanasheria wa kampuni alichunguza kwa umakini sana kwenye ofisi hiyo hakuona kamera yoyote kuna kifaa kidogo mithili ya kiwaya ambacho alikibandika chini ya meza ya TARIQ hivyo alikuwa akisikia kila kilichokuwa kinaendelea humo ndani, walikuwa wamefika chini alitabasamu na kuingia kwenye gari safari ya kwenda hotelini ilianza.

ENDELEA...................
TANZANIA
Qader aliamka mchana wa jua kali baada ya kuhisi joto kali sana kwenye mwili wake, nguo zote zilikuwa zimelowa kwa jasho ambalo lilikuwa likimtoka kama maji, kichwa kilikuwa kinamuuma sana mpaka muda huo alitamani aendelee kulala ila hali ya ndani ya chumba hicho iliendelea kumsaliti sana hakuweza kuvumilia alisimama na kutulia. Kumbukumbu zilipita mbele ya ubongo wake alikumbuka vyema usiku wa jana yake alikuwa akimhoji mtu humo ndani lakini mambo ambayo baadae alikuja kuyasikia yalimtishia sana alibaki anashangaa ni kivipi mtu yule aliweza kuwa namna ile alijifuta jasho usoni kwa mkono wake mmoja alihema na kutoka humo ndani, alinyoosha moja kwa moja kwenye chumba chake cha kazi vijana wake walimshangaa inakuaje kiongozi wao amelowa namna hiyo na tangu asubuhi hawakuwa wamemuona kabisa ndani humo japo hawakuwa na haki ya kuuliza chochote walikuwa wanamjua akiwa na hasira kama Kuna mtu angemuongelesha hapo angeondoka na shingo yake muda huo huo.

Baada ya kuingia kwenye hiyo ofisi ambayo hakuna kijana wake hata mmoja ambaye alikuwa anaruhusiwa kuingia alifunga kila sehemu na kuelekea kwenye kabati moja kubwa sana ambalo lilikuwa ndani humo alilivutia pembeni kidogo na kukutana na ukuta mkubwa ambao ulikuwa na box dogo lilikuwa na namba nyingi sana, aliingiza namba kwa idadi ya 20 kwa kuzichanganya haraka haraka sana palifunguka ulikuwa ni mlango mkubwa sana kisha akaparudishia kama palivyokuwa mwanzo. Mbele yake ilikuwa ni ofisi moja nzuri sana na huko ndiko alikokuwa anayafanya mambo yake ya siri pasipo mtu yeyote yule kujua. Alifungua droo ya kwenye meza yake kulikuwa na pesa nyingi sana na bastola pamoja na passport nyingi zenye sura tofauti tofauti za kusafiria.

"Huyu mtu anasema nimekosea sana kufanya vile kwenye ile familia kwani hawa watu wawili ni akina nani hasa kati ya JITI MAALIMU na huyo ZAKARIA MANSOUR who are they? na huyu mtu amejua vipi kuhusu suala la familia yangu kitu ambacho hata bosi wangu hajawahi kukijua?" Alijiuliza maswali mengi majibu yake hayakuwezekana kabisa kuyapata kama alivyo hitaji yeye aliweza kuanza kuhesabu kwa umakini mkubwa kwamba ni wapi hasa amekosea hakuona kama kuna sehemu yoyote ile alienda vibaya bado alikuwa ana wasi wasi sana moyoni kila alipowaza kuhusu familia yake. Aliiwasha laptop yake ya humo ndani na Kuna namba aliipiga, ilionekana sura ya mwanamke mrembo akiwa karibu na watoto wawili mapacha wakike na wakiume, alitabasamu sana kuwaona watu hao watatu ndio walikuwa kila kitu kwake aliwapenda mno na hakuhitaji wapate matatizo yoyote yale kutokana na kazi zake ndio maana alienda kuwaficha mbali sana kwa siri.

"Mume wangu ni lini tutaanza kuishi maisha ya kawaida? Mimi nimechoka haya maisha kumbuka watoto wanahitaji malezi ya baba na mama kila siku wananisumbua wakitaka uje. Ni miaka kadhaa sasa unatuzungusha tu unadai kuna watu wanakufuatilia kwa usalama wetu tukae mbali hao watu umewakosea nini mpaka wawe na shida na sisi? I'm tired of this" mkewe aliongea kwa uchungu sana mwanaume alikata simu na kuzima laptop yake alijisikia vibaya sana kuona machozi ya mkewe hakuwa na kingine hicho ndicho kilichokuwa kimemleta humo ndani alikuwa akifanya nao mawasiliano kwa siri sana. Alitoka humo ndani na kuvaa suti ya bei, alitoka mpaka nje na kutoka ndani ya nyumba yake hiyo ya TABATA ambayo alikuwa akiitumia kwa mambo yake ya siri na kisha kurudi KIBO.

Safari yake iliienda kuishia NAMANGA karibu na kituo cha polisi cha OSTERBAY, aliliacha gari kwenye mgahawa mmoja akaanza kutembea kwa mguu alienda mpaka kwa mzee mmoja ambaye alikuwa anauza genge la vitu vya nyumbani na kashata, palikuwa panachangamka mno na watu wa mtaa huo walimzoea sana mzee huyo vivyo mida ya jioni kama hiyo walikuwa wanajaa hilo eneo ambapo hata kahawa ilikuwa inapatikana. Mzee huyo baada ya kumuona Qader alimuita kijana mmoja ambaye alimpa maagizo ya kumuacha pale kwenye kile kibanda yeye akaongozana na mwanaume huyo mpaka nyumbani kabisa kwa mzee huyo ambapo hapakuwa mbali kutoka pale na mzee huyo alikuwa anaishi mwenyewe kabisa bila mke ni ajabu kwa umri wake alitakiwa kuwa na mke pamoja na familia au watoto wa kutosha.

"Mhhhhhh vipi kuvamiana bila taarifa" ilikuwa ni sauti ta mzee huyo akiwa amekaa kwenye sofa la bei ghali ndani ya hiyo nyumba ambalo halikuendana kabisa na biashara ambayo alikuwa akiifanya, ndani ya nyumba yake ni watu wachache sana ambao walikuwa wanapata bahati ya kuingia alikuwa akiishi kwa siri sana kwa biashara ya kashata na genge mtaani na wengi walimjua hivyo. Qader hakujibu chochote alijibwaga kwenye sofa akionekana kuchanganyikiwa ni wazi hakuwa sawa, mzee huyo alinyanyuka na kwenda kutoa pombe kali sana kwenye vibati pombe hiyo ni maarufu sana ndani ya nchi ya Mexico pamoja na nchi zenye baridi kali kwa sababu inasadikika huwa ina joto kali sana na ni pombe ghali mno kwa mlala hoi hawezi kabisa kuzipata zaidi ya kuzishuhudia kwa watu wengine tu. Alimrushia moja akiwasha kiyoyozi alijua kinacho enda kutokea hata yeye alijichukulia moja na kuinywa taratibu akiwa anaikunja sura yake, Qader alipiga mafunda kadhaa na kuiweka mezani ilikuwa kali mpaka machozi yalimtoka.

"Hivi mzee ushawahi kukutana na wanadamu ambao ni kama majini?" Qader aliuliza swali ambalo lilimshtua mpaka mzee huyo.

"Una maanisha nini kusema hivyo?"
"Naomba unijibu kwanza"
"Kwa binadamu wa kawaida kuwa jini haiwezekani ila inasemekana majini yapo kutokana na nadharia nyingi za mambo ya ajabu ila kuna wanadamu ambao wanakuwa na uwezo ambao sio kawaida kwa mwanadamu kuwa nao na ndio hao ambao huwa wanaonekana viumbe vya ajabu baadae huwa wanafananishwa na majini" mzee huyo alimjibu Qader akiwa anamwangalia kwa umakini sana.

"Umekaa miaka mingapi kwenye hiyo idara yenu ya usalama wa taifa?" Aliuliza Qader akiwa anaigida tena hiyo pombe.

"Nina zaidi ya miaka 30 ndani ya idara ya usalama wa taifa nayajua mambo mengi sana ambayo binadamu wengi hawayajui, nimedumu na maraisi zaidi ya watatu mpaka sasa tofauti tofauti unahitaji nikusaidie kipi tena mimi nawewe tushamalizana labda kama utaongeza dau"

"Mzee pesa sio shida nipo hapa kwa sababu nilikulipa pesa nyingi sana uweze kunisaidia kupata taarifa za huyu kijana anaye itwa JITI MAALIMU ni kweli nilifanikiwa kumpata na kwenda naye kumhoji lakini bahati mbaya nimekuja kugundua yule mtu siye ambaye nilimdhania, nimekutana na mtu tofauti kabisa ambacho ni kiumbe cha ajabu sana mtu anaweza kuliunga jeraha likapona hapo hapo, anazijua siri nyingi mno mpaka maisha yangu yote, sasa nilitaka nikuulize haya mambo uliyajua mapema ukawa unaniingiza sehemu mbaya au nawewe hujui? Maana sikutaka nifanye kitu kibaya kwako bila kupata uhakika" aliongea kwa msisitizo sana alimwangalia mzee huyu ambaye alikuwa akimsikiliza kwa umakini sana.

"Mhhhhhh tangu nimejiunga ndani ya idara ya usalama wa taifa leo ndo kwa mara ya kwanza nasikia mtu ananitishia maisha yangu ni jambo la kushangaza sana na hili ndilo kosa kubwa ambalo vijana wengi huwa mnalifanya kwenye miaka hii ya leo halafu baadae huwa mnaanza kujutia sana uamuzi wenu. Kwa leo nitakuacha uende tu na hiyo kauli usije ukairudia tena mbele yangu unaweza usiwe na bahati ya kuishi tena" mzee huyo hakuwa na masiara tena na ule ulegevu ambao alikuwa nao ulikuwa umepotea kabisa mbele yake alikuwa imara sana.

"Mzee kwahiyo unanitisha mimi hahahahahhahahahah"
"Mimi sikutishi ila nakwambia ukweli usijisahau sana, kumbuka tulipo kutana siku ya kwanza nilikuwa kwenye misheni nzito ya kuwasaka watu ambao walikuwa wanavusha rasilimali za nchi kimagendo na kuingiza madawa ya kulevya ilitakiwa nikukamatishe siku ile tukaongea kikubwa yakaisha tangu siku ule umekuwa kama kijana wangu na tunafanya kazi pamoja. Uliomba nikusaidie kupata taarifa za huyo bwana mdogo ambaye sijui una kazi gani naye ipi mimi nilirisk kazi yangu nikaziiba taarifa hizo ndani ya idara na kukupatia kwa milioni miambili tu lakini Leo unakuja na kuanza kunipigia kelele hapa, ingekuwa ni vyema sana ungeeleza shida yako ila sio kuanza kunitisha itakuwa mbaya sana kwa upande wako hakuna unacho kijua chochote kuhusu mimi ndio maana kwenye maisha yangu huwa similiki simu" alijibu kistaarabu lakini kwa sauti nzito ambayo hata Qader aliishangaa, haikuwa ya yule babu ambaye alimjua kila siku ilikuwa inasikika sauti ya kiume tena yenye mamlaka makubwa sana.

"Huyo bwana mdogo JITI alishakufa muda mrefu sana na Kuna mwarabu mmoja ambaye anaivaa hiyo sura yake na kujifanya yeye ni huyo kijana hivyo anafanya kazi ndani ya usalama kwa kivuli cha yule mtoto, Jana nilifanikiwa kumteka baadae akaondoka kiwepesi tu baada ya kumjua kwa usahihi kwamba ni kiumbe cha ajabu sana na anajua karibia kila siri ya maisha yangu sikuwa na namna nilimuacha aende, nitakuongeza milioni miamoja ambazo zitaingia kwenye akaunti yako leo jioni naomba taarifa za mtu huyu kwa undani nimjue vizuri" Qader hakuongeza neno aliichukua hiyo pombe na kuinywa yote alitoka machozi yakiwa yanamtoka kwa ukali wa pombe hiyo hakuwajali watu ambao walikuwa wanamshangaa namna alivyokuwa analia, aliingia kwenye gari yake na kuondoka.
Aliingia kwenye makazi yake ya siku zote ambako mara nyingi alikuwa akiishi kwa starehe sana KIBO alifika hapo palikuwa kimya ni walinzi tu walikuwepo getini aliingia ndani na kuiwasha simu yake ambayo kwa muda mrefu sana aliizima aliingia kwenye uwanja wa meseji na kuandika kisha akatuma mahali na kuizima tena simu hiyo. Ndani ya nusu saa waliingia wanaume sita wakiwa na suti zao za bei kali.

"Jiandaeni watatu kati yenu muda huu tunaondoka na kwenda Bukoba huko" Leo alikuwa siriasi sana, saa moja baadae wanaume wanne walikuwa ndani ya AIR TANZANIA wakielekea BUKOBA ambako walifika salama, walichukua usafiri wa noa mpaka ndani ya kijiji cha KIBETA alikuwa analikumbuka jina la mtu ambaye alimfuata ndani ya kijiji hicho lakini hakumjua kabisa na hakuwahi kumuona kwenye maisha yake yote. Aliwaacha vijana wake sehemu wakiwa wanazuga baada ya kufika ndani ya kijiji hicho alinyoosha kwenye restaurant moja nzuri sana.

"Hello samahani naweza kuulizia kwa mzee Philebert?" Mhudumu ambaye alikuwa busy kuandaa chakula aliisikia sauti hiyo, huyo mzee alikuwa tajiri sana hivyo alifahamika sana kwenye hiyo mitaa.

"Zunguka huko nyuma hesabu hatua kumi mkono wako wa kulia utakutana na migomba imepandwa kwa mistali miwili katikati Kuna njia nzuri hivi nyoosha moja mwa moja jumba utakalo liona kwa mbele yako ndipo hapo hapo kwa mzee huyo. Alishukuru sana na kuondoka ulikuwa ni usiku sana tayari kila mtu alikuwa busy na kazi zake hakuna ambaye angewashtukia walijifunga vitambaa usoni na kusogea maeneo hayo palikuwa kimya sana taa za nje tu ndo zilikuwa zinawaka, walizunguka nyuma na kugawana madirisha walichomoa vioo kwa koleo zao ndogo na kutoa kistaarabu wakiwa wamegawana wawili wawili walizama ndani ila ilikuwa ni ajabu sana kwa Qader alishangaa humo ndani kulikuwa na kiza sana ila kioo ambacho walikitoa dirishani kilisaidia kuingiza mwanga kidogo. Mbele ya macho yake alifanikiwa kumuona mwanaume mmoja ambaye ni wazi alikuwa anawasubiri wafike alikuwa amevaa barakoa usoni kwake na nguo nyeusi, walikuwa wameingia cha kike.

Nyumbani kwa mzee Philebert Kuna wenyeji gani tena ambao wameongezeka hawa alio kutana nao Qader na team yake?, Atatoka hapa leo au ndo tunamsahau na hawa ni akina nani?

25 natupa kalamu chini tukutane tena wakati ujao

Langu jina naitwa

Bux the story teller

Chao.
 
Back
Top Bottom