Street brain
JF-Expert Member
- Oct 24, 2022
- 584
- 767
Tupe mzigo kaka tulale sasaShukrani sana mkuu, uwe na mwaka wenye baraka zaidi
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Tupe mzigo kaka tulale sasaShukrani sana mkuu, uwe na mwaka wenye baraka zaidi
Tupe mzigo kaka tulale sasa
Haahahhaha naweka mkuu, huko mbele tutaona namna ya kuongezaSema unatoa tudogo yaani unatuonjesha daaah yaani unasoma kdg tu eti kameish daaah
Daah apo mambo ni bambamHaahahhaha naweka mkuu, huko mbele tutaona namna ya kuongeza
Ndo natoka mishe mishe mkuu, inakujaFEBIANI BABUYA kaka umetusahau wanako huku
HahhahahahahaNipo nausikilizia pia
Utamu njooNOTE
HADITHI ZANGU ZOTE NI ZA KUBUNI TU HAZIHUSIANI NA MTU YEYOTE, TAASISI YOYOTE WALA MAMLAKA YOYOTE ILE WALA HAZILENGI KUMCHAFUA MTU, TAASISI AU MAMLAKA YOYOTE.
HADITHI: GEREZA LA HAZWA
UTANGULIZI....................
Mvua ilikuwa ni Kali sana majira haya ya usiku ikiambatana na upepo mkali ambao uliweza kuilaza chini miti yenye mizizi dhaifu, radi za kutisha ziliupamba masitu huo na kuufanya kuwa na mwanga kwa mbali majira hayo ya usiku wa manane. Ni ndani ya msitu Elnino upatikanao kusini mashariki mwa nchi ya Libya, ni msitu unao tisha sana hata ikiwa ni mchana una historia ya kupotezesha watu waliokuwa wanaingia humo hali iliyo pelekea watu kuanza kuogopa kuingia kwenye huo msitu, miti minene na iliyo shonana ilifanya giza muda wote hata muda wa mchana ndani ya msitu huo na ndiyo sababu ulimiliki viumbe vya kutisha sana kwa usalama wa maisha ya watu.
Majira haya ya usiku wa manane palitulia sana mvua na mjongeo wa maji ndicho kilichokuwa kinasikika sana na upepo mkali pamoja na radi zisizoisha zilizalisha mwanga ndani ya msitu huo, ndani ya tope zito mwanaume mmoja ambaye usoni kwake kulichafuka nywele za kutisha na ndevu zilizofanya hata sura yake isionekane alionekana akiwa anakimbia mno kuweza kuyaokoa maisha yake, hakuwa na namna angeweza kusimama alikuwa anakufa na hakuwa tayari hilo litokee, nyuma yake walikuwa wanakuja kwa kasi sana wanaume sita ambao wanne walivaa nguo za kininja hao walikuwa wanapotea na kurudi huku wawili wakiwa wamevaa magwanda ya jeshi ni wazi walikuwa ni makomando japo kwa lile giza ilikuwa ni ngumu kujua magwanda yao ni ya nchi gani.
Kisu kilikuwa kinakuja huku kikiwa kinajizungusha kilimkosa kichwa kikapita na nywele zake alihema kwa nguvu kisha hakuonekana tena, watu hao walifika hapo mmoja alijaribu kuvuta hisia kujua mtu huyo ameingia wapi lakini upepo ulikuwa unayapotezea utulivu masikio yake. Walipeana ishara ya kutawanyika wote wakionyesha alama ya kuua kwenye shingo kama wakimpata, baada ya kutawanyika hatua kumi na tano mbele yule komando mmoja ambaye alikuwa kwenye gwanda lake alihisi kuna tone limemdondokea lakini lilikuwa na harufu akajua wazi hilo ni jasho mkono wake ulikuwa kiunoni taratibu, ni kweli kuna mtu alitoka juu ya mti akishuka kwa kasi mithili ya paka kwenye kila kiganja kidole cha katikati kilikuwa na kitu kama pete ila haikuwa Pete kwa ajili ya mapenzi na mapambo bali Pete hizo zilikuwa na nyembe Kali sana tatu tatu kila upande na kufanya kuwa sita.
Komando aliikoki bastola yake mwa kisigino cha mguu wake aliirusha juu akiwa ameiachia kwa nguvu sana ikiwa inaelekea juu ya mti mrefu sana ambao ni wazi kwa juu kulikuwa na mtu anashuka kwa nguvu, bastola hiyo ilikuwa inajifyatua risasi yenyewe wakati huo komando alikuwa anapanda kwenye mti huo kama anatumia uchawi lengo alikuwa anamfuata mtu ambaye naye alikuwa anakuja aliko, bastola ilitoka risasi zote sita hakuna iliyo mgusa mtu huyo ikapigwa teke kwa nguvu wanaume walikuwa wamekutana Kati kati ya mti ilipigwa mikono kwa dakika moja kila mtu akiwa ameshikilia mti kwa miguu yake. Nywele za mtu huyo ambaye alionekana kuwa mchafu sana zilicheza upande wa jicho la kulia alijirusha kama anataka kupanda juu mpaka mti ulibonyea kwa nguvu alizotumia komando yule wakati anataka kumfuata alishangaa haoni chochote mbele yake alihisi mtu yupo nyuma yake wakati anageuka alikuwa amechelewa shingo yake ilikuwa inatoka damu nyembe zaidi ya sita ziliiharibu shingo yake, alijaribu kuchomoa bastola nyingine shingo yake ilikuwa tayari imevunjwa.
Baada ya kufanya hayo mauaji aligeuka nyuma mtu huyo mwenye nywele nyingi baada ya kutua chini kisu kilikuwa kimezama kwenye mgongo wake kilimlegeza sana lakini hakutaka kufia kwenye mikono ya hao watu wa kutisha ambao ni wazi aliwaogopa mno huenda alikuwa akiwajua namna walivyo, alianza kukimbia kwa nguvu wote watano waliobaki walikuwa wapo nyuma yake wanakuja kwa kasi ya ajabu, alisimama ghafla mbele yake kulikuwa na maporomoko makubwa na ya kutisha ambayo hayakuonekana hata yameishia wapi, alitoa damu mdomoni zaidi ya visu vidogo vitatu vingine vilikuwa vimezichana mbavu zake, hatua kumi kutoka hapo alipo kwa nyuma yake walisimama maninja wanne na mwanaume mwenye gwanda mmoja baada ya kujua hakuwa na sehemu ya kwenda, hakuhangaika hata kuwaangalia alijirusha huko chini ambako alikuwa anabeti maisha yake.
"He is not a human, he's completely a devil"
"But no survive, he is no more there"
"Let's go and take Donald's body"
Baada ya kumaliza mazungumzo yao kwa lugha ya kiingereza waliondoka hapo wakiwa kwenye tope zito ila kwao halikuwa na uzito wowote ule. Huyu mwanaume aliyekuwa anakimbizwa inasemekana alikuwa na miaka 10 ndani ya GEREZA na hakuwahi kutamka neno lolote lile mpaka siku anatoka ilikuwa ni lazima auawe kwa kufanya kosa la kutoroka kwenye gereza ambalo lilidumu kwa miaka 200 na hakuwahi kutoroka mwanadamu yeyote yule kwa aina ya ulinzi uliokuwepo na hakuna mfungwa hata mmoja ambaye alikuwa anajua wapi gereza hilo lipo, kuna binadamu leo yeye alikuwa nje ya GEREZA hili........what happens???? Nisikumalizie uhondo wako muda utaamua
Ni nini kilimpeleka gerezani? Hilo gereza liko wapi? Ni nani huyu binadamu hasa mpaka watu wamuandame sana kiasi hiki usiku wa manane na aliwezake kutoka huko? Je kwenye hayo maporomoko kuna kutoka kweli????????.......
GEREZA LA HAZWA.....na kalamu ya Bux the story tellerView attachment 2323516
Mkuu unatupandisha mzuka na kuweka karamu yako chini mapema sana. Uwe unatupia hata mbilimbili mkuu, ni ombi tuSTORY: GEREZA LA HAZWA
STORY WRITER: FEBIANI BABUYA
STORY TELLER: Bux the story teller
AGE: 18+
UKURASA WA THELATHINI NA TANO
ULIPO ISHIA UKURASA WA THELATHINI NA NNE
Akiwa anaendelea na swala yake kuna mwanaume ambaye alisogea mpaka mlangoni akapiga magoti na kumsubiri mtu huyo amalizie swala yake ndipo angeweza kumueleza shida yake, zilipita zaidi ya dakika ishirini tangu mtu huyo afike mlangoni na kupiga magoti ndipo mwanaume huyo ndani alipo nyanyuka na kukunja vitu vyake akaviweka sawa na kuanza kutoka humo ndani., alikabidhiwa simu yake ambayo mbele yake kulikuwa na video aliiangalia kwa muda kidogo ilikuwa inawaonyesha vijana zaidi ya sita wakiwa wamefungwa kwenye kamba miguu yao ikiwa chini na vichwa vikiwa juu.
“Wako wapi hawa”
“kwenye yard ya magari kule”
“Andaa gari nahitaji nikaonane nao wenyewe, na nahitaji unitumie picha ya huyo kijana mimi mwenyewe kwenye simu yangu nahitaji nikamuone mwenyewe”
“Sawa bosi nitafanya hivyo”
ENDELEA..........................
“The way she moves i come bro oooops (jinsi anavyo songa, nakuja oooohps ), nimetembea na wanawake wengi sana ile sijawahi kuona mwanamke mrembo kama yule kwa namna yoyote ile lazima nilale naye yule mwanamke nitakuwa mwanaume wa hovyo sana kama nitaacha kumfunua nguo yake yule mrembo hahahahaahhh i’m the master of this game” kijana Khelaif alikuwa akijinadi kwa rafiki zake watano akiwepo rafiki wake wa karibu sana aliye itwa Sharifu
“Hahahahahah nasikia kwao ni wana pesa sana yule mtoto huwezi kumpata kiboya sana kama unavyo fikiria kirahisi sana namna hiyo”
“Wana pesa gani wale nawewe acha kuyaishi maneno ya watu ya hovyo kwenye kichwa chako nawewe unayafuatisha yule demu anaishi hosteli na ana maisha ya kawaida tu ana pesa zipi yule sema tu anajipenda sana na anajua kupendeza by the way ni mzuri sana ila hana maisha yoyote yale ya ajabu namjua tangu anakuja kuanza kusoma hapa mwaka wa kwanza” ni maneno ambayo aliyatoa rafiki yao mmoja akiwa anamhakikishia mwenzake kwamba yeye alimjua binti huyo kuliko mtu yeyote yule kati yao. Hawa vijana walikuwa wanajuana sana kwa sababu tangu wapo high school waliwahi kusoma kwa pamoja hivyo walikuwa wanajuana sana na karibia wote akili zao zilikuwa ni sawa na zinafanana, Khelaif alikuwa anasoma chuo kingine kabisa lakini kutokana na baadhi ya tabia zake zilimfanya akafukuzwa chuo ambacho alikuwa anakisoma mwanzo mkono huwa unahusika sana unapokuwa ni mrefu mbele ya watu wenye njaa zao ndicho kilicho fanyika kwa kijana huyu ndipo akapata nafasi ndani ya hiki chuo. Baada ya kufika hapa alikuwa na siku kadhaa tu lakini macho yake yalikuwa na wepesi sana kwa kuona vitu vizuri mbele yake wakiwa kwenye uwanja wa kuchezea basketball aliweza kumuona binti mmoja ambaye alikaa upande wake mwenyewe na hakuonyesha kabisa kuchangamana na watu wengine alitabasamu kila alipokuwa anaangalia namna wachezaji walivyokuwa wanatumia vipawa vyao kwenye kuugombania mpira huo.
Alijikuta akinogewa sana kumwangalia binti huyo kwa matamanio makubwa ambayo ni miaka mingi yalikuwa kwenye moyo wake hasa pale anapokuwa anaona mwanamke mrembo asingeruhusu mwanamke huyo aweze Kwenda hivi hivi ni lazima ahakikishe kwanza anamvua nguo apate anacho kihitaji halafu anamtelekeza njiani tu.
“Ila rafiki yangu kwa ninavyo kujua kwa tabia yako ya kugusa kila sehemu na kuondoka hawezi kukukubali hapo ulipo una wanawake zaidi ya kumi unahisi yule duu atakuelewa?, kama unamhitaji kweli basi usionyeshe mazoea wala tamaa kwa mwanamke mwingine yeyote yaani badilika halafu ukimalizana naye ndo utajua ustaarabu wako japo bado sijui kama hata hivi atakukubali na kukuvulia nguo zake” rafiki yake mwingine aliongeza kwa sababu walimjua vizuri rafiki yao huyo kwa namna alivyokuwa na tamaa mbele ya wanawake. Alionekana kuupokea ushauri huo alichekelea na kutabasamu kwa pamoja alimgonga rafiki yake huyo kifuani kuonyesha ni ushauri bora sana kampa.
“Sasa nawahakikishieni kama mnasema anajifanya yeye mstaarabu sana na ana nata sana hapa wote tutapita naye baada ya mimi na nyie mnapita pale”
“Acha kujidanganya wewe huo uwezo wenyewe wa kumpata unao basi unajishaua tu ile mali hapa nipo ni mwaka wa pili huu sijawahi kuona kuna mtu kafanikiwa hata kukaa nayo hata kwa saa zima wakiwa wanacheka huwa ni mtu wa kujitenga tenga sana”
“Sasa nataka niwaonyesheeni kwamba mimi ni mtoto wa mjini hahhahah subirini hapa hapa leo leo naenda kulianza zoezi langu”
“Angalia sana yasije yakakutokea puani jiji kubwa hili vitu vinagharamikiwa ndugu yangu tusije tukakukosa ukiwa bado mdogo sana”
“Ndiyo maana huwa sipendi ukae kwenye michongo yangu Afidhu una mishe za kitoto sana kama sio mwanaume vile mpaka huwa napata wasiwasi sana ulikuwaje mshikaji wangu, mmesema jina anaitwa nani?”
“Aasia”
Ofcoz he has a good looking, handsome and so attractive alichokuwa amekosa kijana huyu ilikuwa ni nidhamu tu na mwelekeo bora wa maisha alibarikiwa na mvuto sana ndiyo sababu kubwa ambayo ilimfanya kuwa kipenzi cha wanawake wazuri ambao kwake walipishana kama magari yanavyo pishana stendi kubeba watu, kwa mwendo wa taratibu wenye nakshi ya mtu asiyekuwa na haraka miguu ilikuwa inajivuta kuelekea mahali alipokuwa Aasia ni kijana Khelaif ndiye aliyekuwa anafanya mjongeo huo, alifika karibu na lile eneo alilokuwa amekaa yule kisura ambaye kwa jina alitajiwa kuwa anaitwa Aasia.
“Hi Aasia” alitamka huku akitoa kitambaa cheupe na kukaa karibu na alipokuwa amekaa msichana huyo alimnyooshea hicho kitambaa akiwa na tabasamu zito sana kwenye uso wake, mwonekano wake na tabsamu lake lilimfanya huyo mrembo abaki amemkodolea macho akashindwa kabisa kufanya maamuzi alijikuta amekipokea kitambaa hicho bila kupenda alitamani akirudishe ila usin gekuwa ustaarabu kwa mtu ambaye aliamua kumsaidia japo hakuelewa kwanini amepewa kitambaa kisafi namna hiyo japo mwonekano wa kijana huyo ulimdhihirishia kwamba alikuwa ni kijana smart sana.
“Kitambaa hiki cha cha ni….ni” alibabaika mtoto wa watu asielewa anacho kifanya
“Unatoka sana jasho jifute kidogo” aliongeza kauli nyingine kijana huyo huku akitabasamu na kukaa mkabala na eneo ambalo alikaa mrembo huyo, alishindwa kabisa kufanya maamuzi na alijikuta hali ya kujiamini inampotea kabisa kwenye akili yake, alijikuta anajicheka mwenyewe ni kweli alikuwa anatoka jasho lakini hata yeye hakuwa amejua hiyo hali mapema.
“Ulijuaje kama natoka jasho?”
“Mwanamke mrembo kama wewe sura yako inakuwa inang’aa sana hata mtu anapokuwa mbali kwahiyo uangavu unapo pungua basi ujue kuna shida ndio maana nikagundua lazima kutakuwa na shida kwenye uso wako na isingekuwa kitu kingine zaidi ya joto tu”
“Asante sana kwa kunijali kwa hilo but im so sorry kwa sababu nimekichafua kitambaa chako basi nitakifua na siku nyingine tukikutana nitakupatia kikiwa bado kisafi kama ulivyokuwa umenikabidhi”
“Utanipatia wapi?”
“Nipe namba zako ili nikikamilisha nitakutafuta”
“0621567672”
“Unaitwa nani?”
“Asad” mtoto wa kiume alidanganya mpaka jina
“Asante sana Asad hata hivi mimi sio mkaaji sana hapa tutaonana siku nyingine” hakumjibu zaidi ya kutabasamu tu mtoto wa kike aliondoka akiwa anahema sana, sio kwamba kweli muda wa yeye kuondoka ulikuwa umefika kama alivyokuwa amesingizia lahasha ila alikosa kabisa kujiamini hivyo aliamua kujihami mapema kabla matatizo hayajampata anajua vizuri namna wanaume walivyo na wakizipata nafasi wanavyojuaga kuzitumia, hakutamani kauli ya majuto ni mjukuu iwe sehemu yake aliwahi mapema kukimbia hilo eneo”
“Kijana mdogo kama wewe unathubutu vipi kufanya kitu kama hiki?”
“Nisamehee nisameheee tafadhali naumia” hiki ndicho kilicho mshtua kijana huyo kwenye fikra zake ambazo zilikuwa mbali sana alikuwa analikumbuka vyema tukio la miezi kadhaa ambayo ilikuwa imepita bahati mbaya alishtuliwa na maumivu makali baada ya kuchapwa na mijeredi mikali kwenye mwili wake akiwa uchi wa mnyama mwili umelowa chapa kwa maji, alitoa machozi ya huruma sana lakini kwa wakati huo bahati mbaya sana hakukuwa na mtu ambaye angekuwa na muda wa kuweza kumuonea huruma ndani ya hiyo sehemu aliyokuwepo, maumivu ambayo alikuwa anayapitia ndiyo yaliyo msahaulisha kama humo ndani hakuwa pekeyake bali walikuwa wapo wengi ila kikubwa alikuwa anaangalia usalama wake alilia sana na kuujutia ulimwengu bahati mbaya kwake alikuwa amechelewa sana.
“Siku ya kwanza kumuona yule mwanamke ndiyo siku ambayo nilijiingiza kwenye matatizo mazito Sana im very stupid” alijiambia kimoyo moyo na kuilaani nafisi yake kwa kosa kubwa ambalo alilifanya
Alifeli wapi?
Baada ya kumkabidhi kile kitambaa ndipo mazoea yalipo anza he acted so gentle mbele ya yule mwanamke nadhani hata yeye aliamini hivyo kwamba mwanaume ambaye alikuwa mbele yake alikuwa ni mwanaume wa aina yake sana, baada ya siku mbili tu kupita alipigiwa simu, he was very excited baada ya kugundua alikuwa ni Aasia ndiye aliyekuwa anapiga, alijisogeza sehemu ambayo alielekezwa wakakutane ili akakabidhiwe kitambaa chake, kama kawaida yake hakuwahi kufanya makosa ya kuacha kunukia anapokuwa anaenda sehemu nyeti kama hiyo na ndicho kilimfanya awawim wanawake dhaifu kwa wepesi sana, ni sehemu ambayo alikuwa ameipania sana kuifanyia kazi. Baada ya kufika tu pale bila kutarajia alimkumbatia Aasia bila hata mrembo huyo kutegemea, alihitaji kujinasua kwenye mwili wa kijana huyo lakini alishikwa barabara hakuweza kufurukuta.
“Niachie” aliongea kwa ukali sauti yake haikufua dafu baada ya kijana huyo ambaye alionekana kuyajua mapenzi vizuri sana kumuinamia kidogo huku wamekumbatiana akiwa anayasikilizia mapigo ya moyo ya mtoto wa kike namna yalivyokuwa yanaenda kwa kasi isiyokuwa ya kawaida.
“Naomba nipumzike hapa walau kwa dakika moja tu, najihisi mpweke sana, nahisi nina mzigo mzito unanielemea kuegemia sehemu ya moyo wako imenifanya nafsi yangu itulie na kukaa vizuri naomba dakika moja tu kisha nitakuachia na nitaondoka hapa” alikuwa anaongea akiwa anamnong’oneza Aasia kwenye sikio lake, wakati huo yeye alikuwa amefumba macho yake akiwa anang’ata ulimi, alipigwa na shoti ambayo hajawahi kuisikia wala kuitegemea kwenye maisha yake baada ya kuguswa sehemu yake iliyokuwa imebeba maembe mawili kwenye kifua chake ukijumlisha na sauti ya hisia iliyo ongelewa karibu kabisa na sikio lake ambayo ilizalisha joto kwenye sehemu ya mwili wake ilimfanya asikumbuke kama yupo hapa kwenye dunia ya kawaida alijihisi kama yupo sehemu nyingine tofauti kabisa na huu ulimwengu wa kawaida, taratibi kijana Khelaif aliushusha mkono wake mmoja mpaka mlima kitonga ambao ulituna sana na kumpa hamu ya kuugusa Aasia alihema kwa shida sana. Alivyopata upenyo alikimbia sana akasahau hata kumkabidhi kijana huyo kitambaa ambacho ndicho alikuwa amekileta hapo Khelaif alibaki anacheka sana zoezi lake lilikuwa limebakia asilimia za kuhesabu tu aweze kuweka alama ya vema.
Aasia alikimbilia mpaka kwenye chumba ambacho alikuwa akiishi, alienda kwenye kitanda chake na kujifunika akiwa ameshika moyo wake she was so innocent, aliwaza kipi kimemfanya akimbie alibaki anajicheka mwenyewe baada ya kukumbuka hakuweza hata kumpatia yule kijana kile kitambaa chake.
“Ohhhh my God isiwe kwamba nimempenda yule kijana eeeh MUNGU wangu naomba niepushe na hili bado ni mapema sana sitaki kujiingiza kwenye haya mambo hususani kwa watu ambao siwajui oooh shiiiit” alijishauri mwenyewe lakini kwake ilikuwa ni kazi bure, kwenye maisha yake yote hakuwahi kabisa kukumbatiwa wala kuwa zero distance na mwanaume namna ile alianza kuhisi vitu vya tofauti sana kwenye mwili wake alihisi kama mwili unamuwasha sana baadae alianza kutabasamu mwenyewe kila akikumbuka namna kijana yule alivyokuwa amemkumbatia alitamani sana itokee tena moment nyingine kama ile akumbatiwe.
Mbele ya chai mikate yote huwa ni milaini sana ndicho kilicho mkuta bibie Aasia alijaribu sana kusahau lile tukio lakini ilishindikana kabisa akaamua kukubali matokeo kwamba the boy has stolen her heart, walikuwa karibu sana, Asad kama alivyoweza kujitambulisha kwake alimjali sana kila wakati ambao alimhitaji alikuwepo karibu nayeye, alimpatia furaha ambayo hakuwahi kuipata kwenye maisha yake yote, ule upweke sasa uliisha kabisa walizama kwenye penzi zito na kijana ambaye alihisi anamjua sana bahati ilikuwa siyo yake hakuwa akikijua chochote kwa yule kijana.
The night to remember (usiku ulio mfanya Aasia akaingia kwenye majuto ya maisha yake)
The night was so cool kulitulia na upepo mwanana, ilikuwa ni wikiendi moja bora sana ambayo walitumia siku nzima wakiwa pamoja kutembelea sehemu mbali mbali za kufurahi, jioni ya siku hiyo walikubaliana wakale chakula kwenye moja ya hoteli, it was a big mistake kwa Aasia to accept the arranged invitation unknowingly, yule boy hakufanya makosa kwa ushawishi ambao alikuwa nao kwa wakati ule na mapenzi mazito aliyokuwa amemteka nayo Aasia ndiyo siku ambayo aliondoka na bikra ya binti mrembo sana ambaye imani yake yote aliiwekeza kwa kijana Asad waweza kumuita Khelaif.
Kilitokea nini, nani anajuta na kwanini? Hiki kisa kimeingia vipi kwenye hii dunia ya kutisha ya Zakaria Mansour? Unahisi kuna mtu wa ziada kaingia kwenye huu msala? Hata mimi najiuliza swali kama lako huenda sehemu ijayo ikatufungua kichwa kwenye hili ingizo jipya humu ndani niseme tu 35 naweka nukta hapa tukutane tena wakati ujao.
Wako
Bux the story teller
Chao.
Massive broDah dadekiii alen a k.a zakaria amekutana mfupa mgumu wa AMEI asiyepigika si kwa mkono ule uliochukua masaa manner na hakuna mshindi
Nitajitahidi mkuu, twende sawa......inakuja nowMkuu unatupandisha mzuka na kuweka karamu yako chini mapema sana. Uwe unatupia hata mbilimbili mkuu, ni ombi tu