Gerson Msigwa kaondoka Ikulu nafasi ipo wazi, Pascal Mayalla ana nafasi ya kulamba uteuzi

Mkuu mbona inaonekana una Chuki na Msigwa alikukwaza nini.?
 
Itifaki inaniambia kwa cheo chake, Gerson Msigwa shakua "mheshimiwa". Langu hilo tu
 
Mkuu mbona inaonekana una Chuki na Msigwa alikukwaza nini.?

Sina chuki hata kidogo,si vibaya akiwapisha na wengine waonje raha za Ikulu na mapochopocho yake.

Njaa akienda Ikulu ni faraja kubwa ya JF.
 
Mamam SSH anapita sana humu...hapo ndo njia nzuri sana ya kumwaribia Pascal Mayalla maana tunampigia debe kumwangamiza kimtindo
 
mayala hapana albda ikulu ya chato

Kwani Chato kuna Ikulu !.Yale ni makazi ya binafsi ya Magufuli.

Ikulu nyingi zipo makao makuu ya Mikoa.
 
Mayalla aende Maswa akachukue Ndagu ya Teuzi, naona wingu la mkosi wa teuzi likimuandama.
 
Pascal Mayalla pitia hapa Mkuu naomba Mungu upewe hii nafasi.
 
Namuombea Mzee Paschal Mayala Mungu wa Mbinguni amuwekee mkono apate uteuzi kabla ya mwaka huu kuisha
 
too late. mtu alieonyesha kujipendekeza ili apate cheo. huyo mtu ni MNAFIKI.
no qualification.
na kama una mpigia debe umefeli
Doooh! Toka lini ni marufuku mtu kueleza mawazo yake katika jukwaa hili huru?

Wengi humu tunatamani kuiona Tanzania yenye usawa lakini wengi wetu hatuamini katika usawa, maana mtu akifikiria tofauti na ufikiriavyo wewe unamtwisha rungu. Wapo madikteta wengi humu sema hawana mamlaka.

Easter Monday njema.
 
Kitendo Cha kumuanzishia Uzi tayari ushamharibia.ungenyamaza kimya.

Kama ipo ipo.

Kama hakuna hakuna.

Sent from my Infinix X5515 using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…