Ngongo
Platinum Member
- Sep 20, 2008
- 20,654
- 35,887
Heshima sana wanajamvi,
Msemaji/Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu Mheshimiwa Gerson Msigwa hatimae kaondoka Ikulu.
Mheshimiwa Msigwa kapelekwa Idara ya Maelezo kama Mkurugenzi na Msemaji Mkuu wa Serekali. Sijui kama ndio kupanda cheo huko au kushuka,muhimu kaondoka Ikulu.
Mwanajamvi mwenzetu Pascal Mayalla ana sifa zote za kuongoza Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu.Ifahamike ndugu yetu kwa muda mrefu amekuwa ni mtu wa bahati mbaya kila nafasi ikijitokeza anasahaulika sijui kalogwa na nani,hata msukuma mwenzake hakumuona.
Wanajamvi wote wasiokuwa na husda na roho ya korosho tumweke katika maombi mwetu hasa kipindi hiki cha Pasaka akumbukwe katika uteuzi wa nafasi ambayo ipo wazi.
Iwapo Mayalla au njaa atateuliwa hakutakuwa na malalamiko ya ukabila wala udini.
Ngongo safarini Chake Chake,Pemba.
Msemaji/Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu Mheshimiwa Gerson Msigwa hatimae kaondoka Ikulu.
Mheshimiwa Msigwa kapelekwa Idara ya Maelezo kama Mkurugenzi na Msemaji Mkuu wa Serekali. Sijui kama ndio kupanda cheo huko au kushuka,muhimu kaondoka Ikulu.
Mwanajamvi mwenzetu Pascal Mayalla ana sifa zote za kuongoza Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu.Ifahamike ndugu yetu kwa muda mrefu amekuwa ni mtu wa bahati mbaya kila nafasi ikijitokeza anasahaulika sijui kalogwa na nani,hata msukuma mwenzake hakumuona.
Wanajamvi wote wasiokuwa na husda na roho ya korosho tumweke katika maombi mwetu hasa kipindi hiki cha Pasaka akumbukwe katika uteuzi wa nafasi ambayo ipo wazi.
Iwapo Mayalla au njaa atateuliwa hakutakuwa na malalamiko ya ukabila wala udini.
Ngongo safarini Chake Chake,Pemba.