Gerson Msigwa: Serikali tayari imeshanunua treni 10 za mchongoko, 8 zimeshawasili

Gerson Msigwa: Serikali tayari imeshanunua treni 10 za mchongoko, 8 zimeshawasili

Venus Star

JF-Expert Member
Joined
Dec 6, 2018
Posts
26,519
Reaction score
78,311
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, na Msemaji Mkuu wa Serikali Gerson Msigwa amesema Serikali tayari imeshanunua treni 10 za mchongoko ambapo treni 8 zimeshawasili na kati ya hizo 8, treni moja siku ya Jumamosi Januari 25, 2025 inakamilisha majaribio yake kutoka Morogoro kuelekea Dodoma ili ianze kutoa huduma rasmi

Msigwa ameyasema hayo mkoani Morogoro wakati akizungumza na wanahabari kabla ya kuelekea kwenye Hifadhi ya Taifa ya Mikumi na wanahabari hao ambapo Januari 25, 2025 atakuwa na mkutano wa kuelezea miradi mbalimbali ya kimkakati ya serikali.

Msigwa amesema kuwa hapo awali watu wengi waliongelea vibaya mradi huo wa Treni za SGR, kuwa Serikali imenunua treni zilizopitwa na wakati ambazo sio ‘mchongoko’ hata hivyo wao pia ni mashahidi wa treni zilizopo hivi sasa.

 
Tayari Serikali imelitatua. Vijana wenye nia mbaya na Tanzania walikuwa wanaiba vifaa vya SGR ya umeme.

Je, wewe unapenda maendeleo haya?
Hela za kununulia hizo treni pamoja na miundombinu yake mngejenga barabara za lami nchi nzima, halafu hayo matreni ya umeme mkawaachia sekta binafsi wajenge na kuyaendesha! Ndiyo ningependa.
 
Treni za mtumba siku zote hazina ubora.kila siku zitaendelea kufa njiani Kwa sababu zimetumika huko Asia miaka zaidi ya kumi na tano
 
Hela za kununulia hizo treni pamoja na miundombinu yake mngejenga barabara za lami nchi nzima, halafu hayo matreni ya umeme mkawaachia sekta binafsi wajenge na kuyaendesha! Ndiyo ningependa.
Hili wazo ni baya sana
 
Hayo majina kwenye treni JPM linawauma nini kulisema, hadiunakumbukakwashiiida aaaah Amani....vipi kuasisi wa treni JPM
 
Hela za kununulia hizo treni pamoja na miundombinu yake mngejenga barabara za lami nchi nzima, halafu hayo matreni ya umeme mkawaachia sekta binafsi wajenge na kuyaendesha! Ndiyo ningependa.
Fanya kazi acha uzembe.
Matrekta yapo mengi tu. Hii ni moja ya maonesho ya Nane nane 2024. Unashinda JF 24/7 ukitukana watu wanaofanya kazi 🤣 🤣 🤣 🤣

1737807308132.png


1737807336406.png


1737807359563.png
 
..SGR inapaswa kubeba MIZIGO ili iendeshwe kwa faida na kurudisha gharama za ujenzi.

..mradi kujikita ktk kusafirisha abiria kutasababisha serikali iwe inatoa ruzuku kwa shirika ili lijiendeshe.
 
Hela za kununulia hizo treni pamoja na miundombinu yake mngejenga barabara za lami nchi nzima, halafu hayo matreni ya umeme mkawaachia sekta binafsi wajenge na kuyaendesha! Ndiyo ningependa.
Mkuu sekta gani binafsi itawekeza $10b+ kwenye reli tz?
 
..SGR inapaswa kubeba MIZIGO ili iendeshwe kwa faida na kurudisha gharama za ujenzi.

..mradi kujikita ktk kusafirisha abiria kutasababisha serikali iwe inatoa ruzuku kwa shirika ili lijiendeshe.
Tayri Mabehewa ya kubeba mizigo yameshawasili awamu ya kwanza. Ubebaji wa mizigo utaanza. Au hujui hili?
 
..SGR inapaswa kubeba MIZIGO ili iendeshwe kwa faida na kurudisha gharama za ujenzi.

..mradi kujikita ktk kusafirisha abiria kutasababisha serikali iwe inatoa ruzuku kwa shirika ili lijiendeshe.
Ila mpaka sasa imeingiza hela kibao kwa kubeba abiria, miundombinu bora hurahisisha usafirishaji wa factors of production ambapo efficiency hukua, labour ni mojawapo ya factors of production
 
Ila mpaka sasa imeingiza hela kibao kwa kubeba abiria, miundombinu bora hurahisisha usafirishaji wa factors of production ambapo efficiency hukua, labour ni mojawapo ya factors of production

..imeingiza hela kibao relative to what?

..reli zote huingiza faida kwa kusafirisha MIZIGO sio abiria.

..sisi tunahimiza RATIBA na muda wa kukamilisha mradi izingatiwe ili SGR itimize lengo la kuwa reli ya MIZIGO.
 
Back
Top Bottom