singidadodoma
JF-Expert Member
- Nov 11, 2013
- 4,394
- 1,536
"MTWARA ya sasa ni tofauti na ile ya miaka ya 2011 na kurudi nyuma, kwani ilikuwa ikidharauriwa na haikuwa ikifikika kwa urahisi kutokana na miundombinu mibovu hususan barabara."Ilikuwa si ajabu mtu kulala njiani kwa muda wa siku tatu hadi wiki nzima ndipo ufike Mtwara lakini kwa sasa unahesabu saa tano na nusu hadi sita unakuwa tayari umefika.
"Halafu ukifika Mtwara unajisikia fahari kuwa nimefika kwani kumekuwa kunavutia na kunapendeza ukilinganisha na hapo zamani.
"Sasa kuna maghorofa mengi, hoteli nzuri, lami kwenye barabara za ndani ya manispaa na hali ya kibiashara kwa sasa ni nzuri kiasi kwamba unaweza ukafanya biashara yoyote bila wasiwasi wa kutopata wateja.
Hayo si maneno yangu bali ni ya mwenyeji wangu Mohamed Namkopa, ayezungumza nami baada ya kuwasili katika mkoa huo ambao wenyeji wake wanajinasibu kuwa umepiga hatua kiuchumi na kimaendeleo kutokana na kugundulika kwa gesi asilia, mafuta na uwekezaji wa viwanda vya saruji unaofanywa na mwekezaji maarufu Afrika, Alhaji Aliko Dangote.
Nami bila kusita naanza kwa kutaka kufahamu historia ya mkoa huo kwa undani hususan thamani ya ardhi kabla na baada ya ujio wa neema hiyo.Ikiwa ni takribani miaka mitatu imeshapita kutoka gesi ilipogunduliwa kwa mara ya kwanza mkoani Mtwara, hali imebadilika kwa kasi ya ajabu kiasi kwamba ardhi imegeuka na kuwa lulu kwa kila anayeihitaji.Hali hiyo inatokana na wamiliki wa ardhi ambao wengi wao ni wenyeji wa mkoa huo kubaini kuwa kuna uhitaji mkubwa wa ardhi kutoka kwa watu wanaotoka nje ya mkoa ambao wanataka waitumie kwa uwekezaji.
Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili umebaini jambo hilo la kupanda kwa thamani ya ardhi ambayo kabla ya kugundulika kwa gesi ilikuwa ikiuzwa kwa kiasi kidogo cha fedha ukilinganisha na baada ya ugunduzi huo.mKatika maeneo ya Kijiji cha Hiyari kilichopo takriban kilomita 20 kutoka katikati ya Manispaa ya Mtwara kilipo kiwanda cha saruji cha Dangote, ardhi kwa sasa inauzwa sh. milioni 2.5 kwa heka ukilinganisha na kipindi cha nyuma ambapo ukubwa huo ulikuwa ikiuzwa kwa bei ya sh. 100,000 hadi 200,000.
"Kabla ya kampuni hii ya Dangote kuanza ujenzi wa kiwanda chao hapa Hiyari, ardhi ilikuwa ikiuzwa kwa bei ya chini sana ambayo ilikuwa ni sh.50,000 hadi 100,000 au ukibahatika inafika 150,000 kwa heka moja."Sasa inauzwa zaidi ya sh. milioni 2. hadi 3. Wananchi wameona kuwa ardhi kwa sasa ni ‘dili' kubwa sana na ndiyo maana wameipandisha bei," anasema Namkopa ambae baadaye nilikuja kubaini kuwa ni Mwenyekiti wa Kijiji cha Hiyari.
Aidha, mwenyekiti huyo aliendelea kueleza kuwa ni vigumu sana kupata ardhi kwenye kijiji hicho kwani mara baada ya wajanja kuona ujenzi wa kiwanda hicho walikimbilia kijijini hapo kununua ardhi kabla ya wakazi wa Hiyari kushtuka lakini baada ya wao kufahamu umuhimu wa ardhi nao walianza kugoma kuwauzia kwa bei ya chini."Nakwambia ndugu yangu hapo wajanja walinunua ardhi kwa bei ya chini kabla ya wanakijiji kushtuka lakini baada ya kufahamu basi hali ikawa ni tofauti.
Wanataka wauze kwa bei wanayoitaka na ndiyo sababu ya kupanda hadi kufikia bei niliyoitaja hapo mwanzo, na kila siku inazidi kupanda thamani na usishangae ikapanda mpaka kufikia sh. milioni 10 au 20,"anasema. Hali ni tofauti kwenye vijiji vilivyopo kwenye mwambao wa Bahari ya Hindi hususan vile vya Mgao, Namgogori na Kisiwa ambavyo ndivyo mwekezaji Alhaji Aliko Dangote anatarajia kujenga bandari ambayo itakuwa msaada mkubwa kwa ukanda huo wa kusini kwani ardhi imekuwa ikiuzwa kati ya sh. milioni 8 mpaka 20 kwa ekari moja.
"Kuna Watanzania wenye asili ya Asia walikuja huku na kununua ardhi kubwa sana. Waliuziwa hekari moja kwa sh. milioni moja hadi mbili lakini kwa sasa bei hiyo imekufa na tumeizika zamani sana."Kwa sasa tunauza kati ya sh. milioni 8 hadi 20, inategemea na mtakavyoelewana na kitu unachotaka kuwekeza,"anasema mwanakijiji mmoja wa Mgao ambaye hakutaka kubainisha jina lake.
Gazeti hili lilipata shauku ya kufahamu undani wa kauli aliyoizungumza mkazi huyo wa Mgao hivyo liliamua kumtafuta Mwenyekiti wa kijiji hicho, Abdurahman Shah na ambaye bila kusita anasema hali ndivyo ilivyo."Ulichoelezwa ndugu yangu ndicho hicho hicho. Kabla ya Alhaji Dangote kubainisha adhma yake ya kujenga bandari kijijini hapa, kuna wahindi (Watanzania wenye asili ya kiasia) waliuziwa ardhi kwa bei ya chini sana lakini kwa sasa bila milioni 8 hadi 20 hupati kitu,"anasema Shah.
Vivyo hivyo mwenyekiti huyo anabainisha kuwa kuna mkazi mmoja ambaye alimpatia Alhaji Dangote eneo la hekari mbili kwenye mwambao wa pwani ya kijiji hicho alifanikiwa kukiuza kipande kingine cha ardhi hekari nne kwa sh. milioni 60.
Katika kuthibitisha kuwa hali ya sasa ni tofauti na ilivyokuwa zamani, Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro Mahamoud Kambona ambaye kabla ya kuwa DC wa wilaya hiyo, alikuwa ni Ofisa Tarafa wa Kata ya Mayanga, Wilaya ya Mtwara Vijijini anasema miaka ya 2010 hadi 2012 mwanzoni thamani ya ardhi ilikuwa ni ndogo ukilingana na sasa.
"Kabla ya kuja kwa mwekezaji huyu (Alhaji Dangote) thamani ya ardhi ilikuwa ndogo kupindukia, kipande cha hekari moja kilikuwa kinauzwa kuanzia sh.50,000 hadi 150,000, bado wanunuzi hawakuwepo.Ulikuwa ukiwa na shida ya kuuza ardhi inakupasa utafute mnunuzi hata kwa wiki mbili ama tatu lakini kwa sasa ukisema unauza ardhi dakika hiyo hiyo mnunuzi anafika,"anasema DC Kambona.
Aidha, DC huyo anaendelea kubainisha kuwa hali ya kiuchumi kwa mkoa huo ilikuwa mbaya na hususan vijiji vya Mgao, Namgogori, Kisiwa na Hiyari vilivyopo kwenye Wilaya ya Mtwara Vijijini ndiyo ilikuwa mbaya zaidi kutokana na wakazi wake kutokuwa na shughuli zozote za kuwaingizia kipato zaidi ya kilimo cha korosho ambacho nacho ni cha kusuasua na cha msimu.
"Hapo Hiyari hadi Mgao hapakuwa na shughuli zozote za kibiashara zaidi ya korosho tu. Wakazi wake walikuwa na maisha duni kwa kuwa uchumi wa mkoa ulivyokuwa mdogo lakini mara baada ya miradi ya Dangote kuwasili basi hali imebadilika na kuwa kama ulivyoiona. Biashara zipo hadi zile za fedha kupitia mitandao, uchumi umekua kwa kiasi kikubwa.
"Makazi mazuri pamoja na hoteli nzuri za hadhi ya juu zimejengwa mkoa mzima na hata kwenye vijiji hivyo kuna hoteli nzuri zinajengwa. Ni jambo la faraja kuona uchumi wa mkoa unapaa kwa kasi ya ajabu na si ajabu kuuona ukiwa kwenye safu ya mikoa yenye uchumi mkubwa nchini kutokana na kasi ya uwekezaji mkoani hapa,"anasema DC Kambona.Hali ya kupanda kwa thamani ya ardhi haipo kwenye Wilaya ya Mtwara Vijijini pekee bali hata kwenye Manispaa ya Mtwara Mikindani kwani hali ni hiyo hiyo. Bei ya viwanja iko juu tofauti na kabla ya ugunduzi wa gesi asilia mkoani humo.
Akida Zidikheri, mmiliki wa hoteli na nyumba za kulala wageni za Akida Appartments, anasema kabla ya ugunduzi wa gesi, bei za viwanja kwenye manispaa hiyo hazikuwa kubwa tofauti na ilivyo sasa.Mwandishi wa habari Mohamed Mwaya mkazi wa mkoa huo, akizungumzia jambo hilo anabainisha bila kusita kuwa hali ya maendeleo ni kubwa tofauti na zamani kabla ya ugunduzi huo na pia hata hadhi ya mkoa imepanda kwa kiasi kikubwa.
"Kipato cha mwananchi wa kawaida kwa sasa kimekua kwani hata bila ya kusubiri tafiti ziseme, unaweza ukaona kwa macho tu kwani wakazi wa mkoa huu sasa wanafanya biashara kwa wingi na zinatoka kwa kiasi cha kuridhisha. "Kwa upande wa maendeleo, miundombinu imeimarika na sehemu nyingi za mkoa kwa sasa zinafikika kwa urahisi zaidi tofauti na zamani. "Huduma za kijamii kama vile zile za afya, elimu, maji, benki na nishati zinapatikana kwa urahisi na kwa ukaribu zaidi kiasi kwamba unaweza ukafanya shughuli zako bila wasiwasi na hata ubadilishaji wa fedha za kigeni kwa sasa unafanyika kwa urahisi kupitia maduka ya kubadilishia fedha na benki,"anasema Mwaya.
chanzo jambo leo
"Halafu ukifika Mtwara unajisikia fahari kuwa nimefika kwani kumekuwa kunavutia na kunapendeza ukilinganisha na hapo zamani.
"Sasa kuna maghorofa mengi, hoteli nzuri, lami kwenye barabara za ndani ya manispaa na hali ya kibiashara kwa sasa ni nzuri kiasi kwamba unaweza ukafanya biashara yoyote bila wasiwasi wa kutopata wateja.
Hayo si maneno yangu bali ni ya mwenyeji wangu Mohamed Namkopa, ayezungumza nami baada ya kuwasili katika mkoa huo ambao wenyeji wake wanajinasibu kuwa umepiga hatua kiuchumi na kimaendeleo kutokana na kugundulika kwa gesi asilia, mafuta na uwekezaji wa viwanda vya saruji unaofanywa na mwekezaji maarufu Afrika, Alhaji Aliko Dangote.
Nami bila kusita naanza kwa kutaka kufahamu historia ya mkoa huo kwa undani hususan thamani ya ardhi kabla na baada ya ujio wa neema hiyo.Ikiwa ni takribani miaka mitatu imeshapita kutoka gesi ilipogunduliwa kwa mara ya kwanza mkoani Mtwara, hali imebadilika kwa kasi ya ajabu kiasi kwamba ardhi imegeuka na kuwa lulu kwa kila anayeihitaji.Hali hiyo inatokana na wamiliki wa ardhi ambao wengi wao ni wenyeji wa mkoa huo kubaini kuwa kuna uhitaji mkubwa wa ardhi kutoka kwa watu wanaotoka nje ya mkoa ambao wanataka waitumie kwa uwekezaji.
Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili umebaini jambo hilo la kupanda kwa thamani ya ardhi ambayo kabla ya kugundulika kwa gesi ilikuwa ikiuzwa kwa kiasi kidogo cha fedha ukilinganisha na baada ya ugunduzi huo.mKatika maeneo ya Kijiji cha Hiyari kilichopo takriban kilomita 20 kutoka katikati ya Manispaa ya Mtwara kilipo kiwanda cha saruji cha Dangote, ardhi kwa sasa inauzwa sh. milioni 2.5 kwa heka ukilinganisha na kipindi cha nyuma ambapo ukubwa huo ulikuwa ikiuzwa kwa bei ya sh. 100,000 hadi 200,000.
"Kabla ya kampuni hii ya Dangote kuanza ujenzi wa kiwanda chao hapa Hiyari, ardhi ilikuwa ikiuzwa kwa bei ya chini sana ambayo ilikuwa ni sh.50,000 hadi 100,000 au ukibahatika inafika 150,000 kwa heka moja."Sasa inauzwa zaidi ya sh. milioni 2. hadi 3. Wananchi wameona kuwa ardhi kwa sasa ni ‘dili' kubwa sana na ndiyo maana wameipandisha bei," anasema Namkopa ambae baadaye nilikuja kubaini kuwa ni Mwenyekiti wa Kijiji cha Hiyari.
Aidha, mwenyekiti huyo aliendelea kueleza kuwa ni vigumu sana kupata ardhi kwenye kijiji hicho kwani mara baada ya wajanja kuona ujenzi wa kiwanda hicho walikimbilia kijijini hapo kununua ardhi kabla ya wakazi wa Hiyari kushtuka lakini baada ya wao kufahamu umuhimu wa ardhi nao walianza kugoma kuwauzia kwa bei ya chini."Nakwambia ndugu yangu hapo wajanja walinunua ardhi kwa bei ya chini kabla ya wanakijiji kushtuka lakini baada ya kufahamu basi hali ikawa ni tofauti.
Wanataka wauze kwa bei wanayoitaka na ndiyo sababu ya kupanda hadi kufikia bei niliyoitaja hapo mwanzo, na kila siku inazidi kupanda thamani na usishangae ikapanda mpaka kufikia sh. milioni 10 au 20,"anasema. Hali ni tofauti kwenye vijiji vilivyopo kwenye mwambao wa Bahari ya Hindi hususan vile vya Mgao, Namgogori na Kisiwa ambavyo ndivyo mwekezaji Alhaji Aliko Dangote anatarajia kujenga bandari ambayo itakuwa msaada mkubwa kwa ukanda huo wa kusini kwani ardhi imekuwa ikiuzwa kati ya sh. milioni 8 mpaka 20 kwa ekari moja.
"Kuna Watanzania wenye asili ya Asia walikuja huku na kununua ardhi kubwa sana. Waliuziwa hekari moja kwa sh. milioni moja hadi mbili lakini kwa sasa bei hiyo imekufa na tumeizika zamani sana."Kwa sasa tunauza kati ya sh. milioni 8 hadi 20, inategemea na mtakavyoelewana na kitu unachotaka kuwekeza,"anasema mwanakijiji mmoja wa Mgao ambaye hakutaka kubainisha jina lake.
Gazeti hili lilipata shauku ya kufahamu undani wa kauli aliyoizungumza mkazi huyo wa Mgao hivyo liliamua kumtafuta Mwenyekiti wa kijiji hicho, Abdurahman Shah na ambaye bila kusita anasema hali ndivyo ilivyo."Ulichoelezwa ndugu yangu ndicho hicho hicho. Kabla ya Alhaji Dangote kubainisha adhma yake ya kujenga bandari kijijini hapa, kuna wahindi (Watanzania wenye asili ya kiasia) waliuziwa ardhi kwa bei ya chini sana lakini kwa sasa bila milioni 8 hadi 20 hupati kitu,"anasema Shah.
Vivyo hivyo mwenyekiti huyo anabainisha kuwa kuna mkazi mmoja ambaye alimpatia Alhaji Dangote eneo la hekari mbili kwenye mwambao wa pwani ya kijiji hicho alifanikiwa kukiuza kipande kingine cha ardhi hekari nne kwa sh. milioni 60.
Katika kuthibitisha kuwa hali ya sasa ni tofauti na ilivyokuwa zamani, Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro Mahamoud Kambona ambaye kabla ya kuwa DC wa wilaya hiyo, alikuwa ni Ofisa Tarafa wa Kata ya Mayanga, Wilaya ya Mtwara Vijijini anasema miaka ya 2010 hadi 2012 mwanzoni thamani ya ardhi ilikuwa ni ndogo ukilingana na sasa.
"Kabla ya kuja kwa mwekezaji huyu (Alhaji Dangote) thamani ya ardhi ilikuwa ndogo kupindukia, kipande cha hekari moja kilikuwa kinauzwa kuanzia sh.50,000 hadi 150,000, bado wanunuzi hawakuwepo.Ulikuwa ukiwa na shida ya kuuza ardhi inakupasa utafute mnunuzi hata kwa wiki mbili ama tatu lakini kwa sasa ukisema unauza ardhi dakika hiyo hiyo mnunuzi anafika,"anasema DC Kambona.
Aidha, DC huyo anaendelea kubainisha kuwa hali ya kiuchumi kwa mkoa huo ilikuwa mbaya na hususan vijiji vya Mgao, Namgogori, Kisiwa na Hiyari vilivyopo kwenye Wilaya ya Mtwara Vijijini ndiyo ilikuwa mbaya zaidi kutokana na wakazi wake kutokuwa na shughuli zozote za kuwaingizia kipato zaidi ya kilimo cha korosho ambacho nacho ni cha kusuasua na cha msimu.
"Hapo Hiyari hadi Mgao hapakuwa na shughuli zozote za kibiashara zaidi ya korosho tu. Wakazi wake walikuwa na maisha duni kwa kuwa uchumi wa mkoa ulivyokuwa mdogo lakini mara baada ya miradi ya Dangote kuwasili basi hali imebadilika na kuwa kama ulivyoiona. Biashara zipo hadi zile za fedha kupitia mitandao, uchumi umekua kwa kiasi kikubwa.
"Makazi mazuri pamoja na hoteli nzuri za hadhi ya juu zimejengwa mkoa mzima na hata kwenye vijiji hivyo kuna hoteli nzuri zinajengwa. Ni jambo la faraja kuona uchumi wa mkoa unapaa kwa kasi ya ajabu na si ajabu kuuona ukiwa kwenye safu ya mikoa yenye uchumi mkubwa nchini kutokana na kasi ya uwekezaji mkoani hapa,"anasema DC Kambona.Hali ya kupanda kwa thamani ya ardhi haipo kwenye Wilaya ya Mtwara Vijijini pekee bali hata kwenye Manispaa ya Mtwara Mikindani kwani hali ni hiyo hiyo. Bei ya viwanja iko juu tofauti na kabla ya ugunduzi wa gesi asilia mkoani humo.
Akida Zidikheri, mmiliki wa hoteli na nyumba za kulala wageni za Akida Appartments, anasema kabla ya ugunduzi wa gesi, bei za viwanja kwenye manispaa hiyo hazikuwa kubwa tofauti na ilivyo sasa.Mwandishi wa habari Mohamed Mwaya mkazi wa mkoa huo, akizungumzia jambo hilo anabainisha bila kusita kuwa hali ya maendeleo ni kubwa tofauti na zamani kabla ya ugunduzi huo na pia hata hadhi ya mkoa imepanda kwa kiasi kikubwa.
"Kipato cha mwananchi wa kawaida kwa sasa kimekua kwani hata bila ya kusubiri tafiti ziseme, unaweza ukaona kwa macho tu kwani wakazi wa mkoa huu sasa wanafanya biashara kwa wingi na zinatoka kwa kiasi cha kuridhisha. "Kwa upande wa maendeleo, miundombinu imeimarika na sehemu nyingi za mkoa kwa sasa zinafikika kwa urahisi zaidi tofauti na zamani. "Huduma za kijamii kama vile zile za afya, elimu, maji, benki na nishati zinapatikana kwa urahisi na kwa ukaribu zaidi kiasi kwamba unaweza ukafanya shughuli zako bila wasiwasi na hata ubadilishaji wa fedha za kigeni kwa sasa unafanyika kwa urahisi kupitia maduka ya kubadilishia fedha na benki,"anasema Mwaya.
chanzo jambo leo