Gharama za kupaua na kuezeka

abudist

JF-Expert Member
Joined
Oct 25, 2009
Posts
850
Reaction score
781
Habari wakuu.

Wakuu naomba watalaamu wa paa wanipe hesabu za kupaua na kuezeka nyumba ya ukubwa wa Sqm 400. Nataka hesabu za makadirio ya vifaa vinavyohitajika na za ufundi.

Vilevile nataka kuweka mabati ya (tiles shaped type). Nyumba ipo Dar es salaam na ramani ya paa ipo vilevile. I'm looking for realistic estimate please.
 
Inategemea na utaka tumia tiles gani. Mfano mimi nilitumia Nabaki na ni sqrm 250 tiles tuu ilikuwa 10M. Mbao 5M na fundi kutoka Nabaki 3M. Kwa ukubwa huo nadhani tiles peke yake ni 800 plus, mbao sio chini ya 8M. At least 30M inakatika kama unataka Nabaki (Decra Tiles). ukiweka migongo mikubwa unaweza kuwa kwenye 15-20M
 
Asante kwa ushauri mkuu! Kwanza sikujua kama Nabaki wanao mafundi wao wenyewe. Hicho ni kitu kizuri nafikiri mafundi wao watakua wazuri siyo wa ujanja ujanja.
 
Asante kwa ushauri mkuu! Kwanza sikujua kama Nabaki wanao mafundi wao wenyewe. Hicho ni kitu kizuri nafikiri mafundi wao watakua wazuri siyo wa ujanja ujanja.
Ukienda na raman yako pale nabaki wanakupa makadirio yote
Hata Alaf nao wana hiyo service tena bure kabisa
 
Mkuu ni apartments au? Tuambie. Watu tunatafuta nyumba. Kama ni nyumba ya kuishi utakuja potelea humo. 400 sq.m roughly ni kama 20m X 20m. Jumba kubwa mno, angalia usije over estimate vifaa kwa kuchanganya unit of measurement.
 
Mkuu ni apartments au? Tuambie. Watu tunatafuta nyumba. Kama ni nyumba ya kuishi utakuja potelea humo. 400 sq.m roughly ni kama 20m X 20m. Jumba kubwa mno, angalia usije over estimate vifaa kwa kuchanganya unit of measurement.

Mkuu ni nyumba ya kawaida. Ukubwa wa plot ni 1200 Sqm, sehemu ya mchoro ni about 400 sqm yaani ni 23M urefu x 17.5 upana umbo la mstatili. Lakini ramani ipo ndani ya hili eneo hivyo ni kweli jengo halisi sababu ya shape ya ramani na kona zake litakuwa chini kidogo ya 400 sqm
 
Mkuu,
Nenda FB jiunge na kundi la Ujenzi Zone. Kule kuna wanachama zaidi ya 10k. Utapata vyote unavyohitaji kujua kuhusu ujenzi including hao mafundi wa Nabaki.

Usisahau kuleta mrejesho ili na wengine wafaidike.

Barikiwa.
 
Mkuu,
Nenda FB jiunge na kundi la Ujenzi Zone. Kule kuna wanachama zaidi ya 10k. Utapata vyote unavyohitaji kujua kuhusu ujenzi including hao mafundi wa Nabaki.

Usisahau kuleta mrejesho ili na wengine wafaidike.

Barikiwa.

Tafanya hivyo mkuu. Shukrani!
 
Mkuu kupauwa hii nyumba ujiandae maana nina jamaa yangu yeye ana kama hiyo gharama za kupauwa tuu ni Million 48. Hii mijumba mikubwa mizuri kwenye picha tuu lakini gharama zake majanga.
 
Mkuu kupauwa hii nyumba ujiandae maana nina jamaa yangu yeye ana kama hiyo gharama za kupauwa tuu ni Million 48. Hii mijumba mikubwa mizuri kwenye picha tuu lakini gharama zake majanga.

Ni kweli mkuu nakubali gharama zake ni majanga. Until this level this house has cost me a fortune!
 
Ni kweli mkuu nakubali gharama zake ni majanga. Until this level this house has cost me a fortune!

Mkuu unaweza kutupatia mrejesho what did you opt last? Ulitumia nabaki Decra tyles au? How did it cost?

Nina nyumba ya sqm 210 ukubwa imefikia stegi hiyo ya kuezeka nahitaji ideas. Thanks
 
Mkuu unaweza kutupatia mrejesho what did you opt last? Ulitumia nabaki Decra tyles au? How did it cost?

Nina nyumba ya sqm 210 ukubwa imefikia stegi hiyo ya kuezeka nahitaji ideas. Thanks
Built up area ni ngapi mkuu? 210sqm ni nyumba kubwa
Unataka bati zipi?
 
Built up area ni ngapi mkuu? 210sqm ni nyumba kubwa
Unataka bati zipi?

Looking at actual roof plan dimensions ina 17.7X18M~~318SQM. Nyumba kubwa kidogo ni vyumba vinne

Nataka Decra ila naona bei itachangamka sana.
 
Looking at actual roof plan dimensions ina 17.7X18M~~318SQM. Nyumba kubwa kidogo ni vyumba vinne

Nataka Decra ila naona bei itachangamka sana.
Roofing dimension 17.7 x 18, je nyumba ni box? Nyumba yako ina umbo la mstatili? Yaan haina kona?
Tafuta eneo lote ambalo bati litagusa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…