Gharama za kusoma masters vyuo vya Tanzania

Naibili

JF-Expert Member
Joined
Jan 24, 2011
Posts
1,878
Reaction score
1,060
Habari wadau, naomba msaada wenu, gharama za kusoma masters katika vyuo vyetu hapa nchini hasa evening zikoje?

Na Je? ni chuo gani chenye gharama nafuu na elimu yake ni bora? nimejaribu kucheki kwenye website za vyuo mbali mbali, hawajaweka fee structure kwa ajili ya masters bali wameweka kwa degree tuu.
 
Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Gharama Milioni 6.
 
Ndugu yangu acha uvivu nenda vyuoni kaulize mwenyewe, ndo maana mnatoa rushwa bila kuombwa sababu ya uvivu wenu.

Kwanza hujaeleza unataka kusoma kozi gani na chuo gani zuri kwako then uulize gharama sabu kila chuo inagharama zake na hata Kila kozi ina bei tofauti.

Samahani kama nimekuudhi ila ndo ukweli huo.
 

mkuu asante kwa ushauri, kumbuka huwezi kutembelea vyuo vyote nchini, nataka nisome mba
 
Naomba uingie kwenye kila web ya chuo na uangalie tuition fee zao .kila la kheri
 
Ni bora ungesema unataka kusom a kozi gani kwani kila kozi ina ada yake
 

Naomba nisaidiwe kufahamu, hivi Masters na degree ni vitu viwili tofauti? Maana hiyo sentensi ya mwisho imeniacha hoi!
 

Una hela we ya kusoma masters!!!
au kuna mtu amekutuma uulizie!!!
anyway, usiwe mvivu tembelea kila chuo fees structures zote zipo.

Goodluck
 
Wakuu, kwa chuo kama SUA na course zake za kilimo, gharama ya kusoma masters ni kiasi gani?

Binafsi nimevutiwa na course hizi katika idara ya kilimo:

1. Master of Science in Agricultural Economics (MSc. Agric Econ)
2. Master of Science in Agricultural and Applied Economics (MSc. Agric. and Applied Econ)
3. Master of Business Administration (Agribusiness) – MBA (Agribusiness)

namba mbili haswaa....

Kwa anaejua gharama tafadhali tusaidiane.

cc ze duduz na LORDVILLE kwa msaada zaidi.
 
Naomba nisaidiwe kufahamu, hivi Masters na degree ni vitu viwili tofauti? Maana hiyo sentensi ya mwisho imeniacha hoi!

nilivyo muelewa mtoa mada alitaka kusema degree ya awali, yaani first degree. Hata Masters ni degree japo inaitwa degree ya pili.

Usishangae, ndio elimu ya Mulugo ya Div 5 mtu anapata shahada lakini hajui kujieleza mwenyewe akaeleweka.
 
Serikali imeamua kuwapa second degree matajiri na kuwaacha maskini waliosoma kwa mikopo first degree wakipiga chaki vijijin
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…